Kaunara
JF-Expert Member
- Feb 4, 2013
- 258
- 540
Nimeumia sana ndani ya moyo wangu.
Dk 45 zilizopita nilikuwa na mke na mtoto wa miezi sita tumetoka pharmacy kuchukua dawa na gari. Sababu za kiusalama siwezi taja ni sehemu gani. Navyorudi nikapaki kwenye duka pembeni ya barabara nilikuwa na kiu.
Baada ya kupaki wife nae akawa ananiagiza vitu vingine nikawa sijazima gari na taa. Kumbe mbele yangu kulikuwa na polisi wawili wamevaa sare na wengine wanne hawana sare wapo na silaha. Hakaja mmoja mwenye sare akasema.
Hujui matumizi ya taa? Kwanini unatumulika? Nikabaki nimetahamaki. Maana hata dk 1 au mbili sidhani kama zilikuwa zimeisha. Nikamwambia samahani sikuwaona. Jamaa akaniambia shuka kwenye gari. Nikashuka, wakati nashuka wale jamaa wengine wakawa wamesogea wakaniambia piga magoti.
Kupiga magoti wakaanza kuniuliza unaenda kununua nini? Nikawajibu maji ya kunywa. Wakajibu unatumulika kisa unaenda kununua maji tu. Mwingine akasema hujasikia kwamba unatakiwa kukaaa ndani? Nikawaambia tena samahani maana watu wote pale wakawa wametawanyika.
Basi nikawa nimetulia ila hasira zimenipanda sana nikawa nimekaa kimya. Wakasema nenda. Kuingia kwenye gari jamaa kaja kasema mbona huendi kununua maji? Nikamwambia nimeghairi jamaa akajibu unasemaje?
Polisi akasema mmoja akasema kwanza huyu hatujamkagua mmoja akawa anakoki bunduki. Nikakaa kimya sijajibu kitu. Jamaa wa duka akaawa anafunga faster polisi mmoja akazunguka gari kamulika na torch kaenda hadi kwa wife kamkuta ametulia kamshika mtoto wala hatetereki hata simu hajashika jamaa akawaambia wenzake muacheni. Basi nikasepa.
Nimeumia sana sababu katika maisha yangu sijawahi kupigishwa magoti na polisi wala sijawahi kwenda hata kituo chochote. Nimeamini Watanzania hatupo salama kabisa.
Dk 45 zilizopita nilikuwa na mke na mtoto wa miezi sita tumetoka pharmacy kuchukua dawa na gari. Sababu za kiusalama siwezi taja ni sehemu gani. Navyorudi nikapaki kwenye duka pembeni ya barabara nilikuwa na kiu.
Baada ya kupaki wife nae akawa ananiagiza vitu vingine nikawa sijazima gari na taa. Kumbe mbele yangu kulikuwa na polisi wawili wamevaa sare na wengine wanne hawana sare wapo na silaha. Hakaja mmoja mwenye sare akasema.
Hujui matumizi ya taa? Kwanini unatumulika? Nikabaki nimetahamaki. Maana hata dk 1 au mbili sidhani kama zilikuwa zimeisha. Nikamwambia samahani sikuwaona. Jamaa akaniambia shuka kwenye gari. Nikashuka, wakati nashuka wale jamaa wengine wakawa wamesogea wakaniambia piga magoti.
Kupiga magoti wakaanza kuniuliza unaenda kununua nini? Nikawajibu maji ya kunywa. Wakajibu unatumulika kisa unaenda kununua maji tu. Mwingine akasema hujasikia kwamba unatakiwa kukaaa ndani? Nikawaambia tena samahani maana watu wote pale wakawa wametawanyika.
Basi nikawa nimetulia ila hasira zimenipanda sana nikawa nimekaa kimya. Wakasema nenda. Kuingia kwenye gari jamaa kaja kasema mbona huendi kununua maji? Nikamwambia nimeghairi jamaa akajibu unasemaje?
Polisi akasema mmoja akasema kwanza huyu hatujamkagua mmoja akawa anakoki bunduki. Nikakaa kimya sijajibu kitu. Jamaa wa duka akaawa anafunga faster polisi mmoja akazunguka gari kamulika na torch kaenda hadi kwa wife kamkuta ametulia kamshika mtoto wala hatetereki hata simu hajashika jamaa akawaambia wenzake muacheni. Basi nikasepa.
Nimeumia sana sababu katika maisha yangu sijawahi kupigishwa magoti na polisi wala sijawahi kwenda hata kituo chochote. Nimeamini Watanzania hatupo salama kabisa.