sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,033
"USIPOTAJIRIKA TANZANIA HAKUNA SEHEMU UTAJA TAJIRIKA" Ni maneno niliyotamkiwa na moja ya rafiki yangu tuliesoma wote shule ya msingi leo hii tulipokutana na kupiga story zaidi ya lisaa, Yeye alipofika form 4 shughuli iliishia hapo.
Darasani na shuleni kiujumla nimewajua wahindi na waarabu kibao tu, nikiri wazi waarabu tulikuwa tunawaburuza "Sio Kitoto", uwezo wao ulikuwa mdogo mnooo, lakini leo hii sio wenzetu hata kidogo, ni story tu za kujuana nao lakini kimaisha tumepigwa gepu sio kitoto.
Wahindi angalau kulikuwa na upinzani ila tulikuwa tunaburuzana sana tu, vipanga wa kibongo waliburuzana na vipanga wa kihindi, huku wa kati nao walikuwepo tuliburuzana nao man to man, wengi wamesoma mpaka vyuoni lakini wanatumia elimu zao kwenye biashara zao hapa hapa Tz.
Tukija kwa upande wetu wabongo hali inatia huruma, tumesoma mpaka vyuoni + masters, mtu kapigiwa koneksheni na ndugu ama wazazi ama kapata ajira kivyake mshahra + posho vyote kwa jumla ni milioni 3 kwa mwezi yani hapo akiwa na gari na nyumba anaridhika kabisa cha kuwaza labda kuongeza mchepuko ama kuwahi viti virefu baada ya kazi, kwa wale wanaofanya biashara unakuta mtu akiingiza faida milioni around 8 kwa mwezi anajiona tayari mwamba.
Wenzetu hawa hawa tuliosoma nao suala la kuajiriwa hawataki kulisikia kabisa kwenye nchi hii, kuna muhindi moja aliniambia " Nchi hii ina untapped resources and oppurtunities kibao, hata elimu ya standard 7 inatosha kukutajirisha, Forest imejaa carrots ni wewe utaamua uwe punda ama mkulima" Sio siri nilihisi nimetupiwa dongo.
yani wao wanaunganisba nguvu kwenye timu zao (familia), kwa mwezi kulaza B na kuendelea ni kawaida.
MAPENDEKEZO
Nawajua matajiri wa hapa Tanzania wanataka watoto hawana exposure kabisa,yani mtoto maisha yake yote kasome Tz, matokeo yake mtoto anakuwa na akili za hapa hapa hata lugha inampiga chenga, hajui kumingle wala hana connections za watu wa mataifa mengine.
Fikra za 'KILA MTU AJITAFUTIE CHAKE' zimepitwa na wakati, unakuta tajiri anasubiria mpaka mtoto wake afikie miaka 25 ndio anampa mtaji akajitafutie chake, tena mtaji wenyewe unakuta ni milioni 20 wakati baba ni bilionea, NI UPUUZI!! hii ndio sababu kubwa biashara nyingi zinaanguka baba akifariki sababu watoto hawajui kuziendeleza, ukiona wenzetu mtoto hasubiriwi mpaka awe mkubwa, ni tangu akiwa mdogo anazoeshwa biashara maana hata kwa akili ya kawaida ukiwa na paka ama mbwa mdogo unaweza kumfunza vingi akiwa bado mdogo kuliko ukubwani, na hata mtoto akiwa mkubwa anaendeleza ama ku expand biashara za familia, hata baba akifariki biashara zinaendelea bila tatizo.
Darasani na shuleni kiujumla nimewajua wahindi na waarabu kibao tu, nikiri wazi waarabu tulikuwa tunawaburuza "Sio Kitoto", uwezo wao ulikuwa mdogo mnooo, lakini leo hii sio wenzetu hata kidogo, ni story tu za kujuana nao lakini kimaisha tumepigwa gepu sio kitoto.
Wahindi angalau kulikuwa na upinzani ila tulikuwa tunaburuzana sana tu, vipanga wa kibongo waliburuzana na vipanga wa kihindi, huku wa kati nao walikuwepo tuliburuzana nao man to man, wengi wamesoma mpaka vyuoni lakini wanatumia elimu zao kwenye biashara zao hapa hapa Tz.
Tukija kwa upande wetu wabongo hali inatia huruma, tumesoma mpaka vyuoni + masters, mtu kapigiwa koneksheni na ndugu ama wazazi ama kapata ajira kivyake mshahra + posho vyote kwa jumla ni milioni 3 kwa mwezi yani hapo akiwa na gari na nyumba anaridhika kabisa cha kuwaza labda kuongeza mchepuko ama kuwahi viti virefu baada ya kazi, kwa wale wanaofanya biashara unakuta mtu akiingiza faida milioni around 8 kwa mwezi anajiona tayari mwamba.
Wenzetu hawa hawa tuliosoma nao suala la kuajiriwa hawataki kulisikia kabisa kwenye nchi hii, kuna muhindi moja aliniambia " Nchi hii ina untapped resources and oppurtunities kibao, hata elimu ya standard 7 inatosha kukutajirisha, Forest imejaa carrots ni wewe utaamua uwe punda ama mkulima" Sio siri nilihisi nimetupiwa dongo.
yani wao wanaunganisba nguvu kwenye timu zao (familia), kwa mwezi kulaza B na kuendelea ni kawaida.
MAPENDEKEZO
Nawajua matajiri wa hapa Tanzania wanataka watoto hawana exposure kabisa,yani mtoto maisha yake yote kasome Tz, matokeo yake mtoto anakuwa na akili za hapa hapa hata lugha inampiga chenga, hajui kumingle wala hana connections za watu wa mataifa mengine.
Fikra za 'KILA MTU AJITAFUTIE CHAKE' zimepitwa na wakati, unakuta tajiri anasubiria mpaka mtoto wake afikie miaka 25 ndio anampa mtaji akajitafutie chake, tena mtaji wenyewe unakuta ni milioni 20 wakati baba ni bilionea, NI UPUUZI!! hii ndio sababu kubwa biashara nyingi zinaanguka baba akifariki sababu watoto hawajui kuziendeleza, ukiona wenzetu mtoto hasubiriwi mpaka awe mkubwa, ni tangu akiwa mdogo anazoeshwa biashara maana hata kwa akili ya kawaida ukiwa na paka ama mbwa mdogo unaweza kumfunza vingi akiwa bado mdogo kuliko ukubwani, na hata mtoto akiwa mkubwa anaendeleza ama ku expand biashara za familia, hata baba akifariki biashara zinaendelea bila tatizo.