Nimeamua kuwa Atheist

Nimeamua kuwa Atheist

Kinachokufanya usinipe sasa upige danadana ni kipi?

Umejuaje mimi ni Gemini?

Thibitisha kwa ushahidi usiopingika hapa.
Hapa tayari nimeondoka

Pia siyo sahihi kwangu kujihusisha na mada za kumkejeli Mungu

Nafsi yangu inachafuka kujibizana kwenye topic za namna hii.

Endeleeni kumkataa Mungu kwa sababu tu mmesalitiwa
 
Hapa tayari nimeondoka

Pia siyo sahihi kwangu kujihusisha na mada za kumkejeli Mungu

Nafsi yangu inachafuka kujibizana kwenye topic za namna hii.

Endeleeni kumkataa Mungu kwa sababu tu mmesalitiwa
Unakimbia tu kwa sababu umeshindwa kuthibitisha mimi ni Gemini.

Unaamini uongo kwamba mimi ni Gemini kama unavyoamini uongo kwamba kuna Mungu.
 
Mkuu , jamaa wanataka uthibitisho ili waamini, wewe kuna namna yeyote unaona unaweza wasaidia kupata uthibitisho? Na hawa jamaa wasipopata uthibitisho na wakaendelea kukataa kuamini, kuna changamoto gani inawakabili hapo baadae?
Sasa ukishakuwa na uthibitisho wa jambo, bado hilo jambo litabaki kuwa ni imani? Labda huo uthibitisho uwe ndani ya imani ila uthibitisho nje ya imani hakuwezi tena kuendelea kuwa imani.
Binafsi inanishangaza mtu anaposema anataka uthibitisho ndio ili aamini.

Kinachowafanya wasiamini Mungu sio kukosekana uthibitisho kwa sababu watu huwa hawaamini jambo kwa sababu ya uthibitisho na ndio maana hata kilichowafanya waache kuamini Mungu haikuwa kukosekana uthibitisho.

Huu wimbo wa uthibitisho unatumika tu kufanyia ubishi na kutetea madai yao ya kudai hakuna Mungu, ndio maana tunaona atheists wanaachana na atheism na kuamini Mungu pasina kuupata huo uthibitisho.

Sasa hao wenye kutaka uthibitisho ndio ili waamini hao bado wapo kwenye ubishani tu.
 
  • Thanks
Reactions: Lax
Kujua ni jambo moja na kuthibitisha ni jambo lengine, mimi naweza kuwa nimekuona wewe kabisa unaiba pesa na hivyo nikawa najua kwamba wewe ndio uliyeiba pesa ila kujua tu haifanyi kwamba lazima nitakuwa na uthibitisho wa wewe kuiba hizo pesa kama sikuweza kutengeneza ushahidi.
Unahamisha mada.

Usilete habari za Pesa kwenye Mungu.

Unafanya red herring fallacy.

You introduce irrelevant topic to distract the main topic.

Thibitisha Mungu yupo.

Habari za pesa, mahakama hazihusiani na Mungu.
 
Sasa ukishakuwa na uthibitisho wa jambo, bado hilo jambo litabaki kuwa ni imani? Labda huo uthibitisho uwe ndani ya imani ila uthibitisho nje ya imani hakuwezi tena kuendelea kuwa imani.
Binafsi inanishangaza mtu anaposema anataka uthibitisho ndio ili aamini.

Kinachowafanya wasiamini Mungu sio kukosekana uthibitisho kwa sababu watu huwa hawaamini jambo kwa sababu ya uthibitisho na ndio maana hata kilichowafanya waache kuamini Mungu haikuwa kukosekana uthibitisho.

Huu wimbo wa uthibitisho unatumika tu kufanyia ubishi na kutetea madai yao ya kudai hakuna Mungu, ndio maana tunaona atheists wanaachana na atheism na kuamini Mungu pasina kuupata huo uthibitisho.

Sasa hao wenye kutaka uthibitisho ndio ili waamini hao bado wapo kwenye ubishani tu.
mkuu sasa nimeanza kukupata mtizamo ulionao, najibu lako la swali la kwanza nimelipokea, nisaidie na hio kipande cha mwisho
Na hawa jamaa wasipopata uthibitisho na wakaendelea kukataa kuamini, kuna changamoto gani inawakabili hapo baadae?
 
Kujua ni jambo moja na kuthibitisha ni jambo lengine, mimi naweza kuwa nimekuona wewe kabisa unaiba pesa na hivyo nikawa najua kwamba wewe ndio uliyeiba pesa ila kujua tu haifanyi kwamba lazima nitakuwa na uthibitisho wa wewe kuiba hizo pesa kama sikuweza kutengeneza ushahidi.
mkuu unatumia mifano tata sana hapo, isiyo lingana uzito
 
Nimefanya tafiti yakinifu nimekuja kugundua Mungu hayupo. Ni story tu za kutupa matumaini hewa.

Nimeamua kuwa Atheist. Nitaupa muda nao ukizingua namrudia Yesu.

Dhulma, uonevu, usaliti na ukatili umetamalaki sana.

Bora kuamini nature na kuwa mwema kwa viumbe hai hata visivyonekana.

Ni maamuz yangu binafsi.
Ukifa hutawaona member wenzako kubeba kabati
 
Unahamisha mada.

Usilete habari za Pesa kwenye Mungu.

Unafanya red herring fallacy.

You introduce irrelevant topic to distract the main topic.

Thibitisha Mungu yupo.

Habari za pesa, mahakama hazihusiani na Mungu.
Wapi nilikwambia kuwa nipo hapa ili kuthibitisha Mungu yupo? Toka mwanzo nilikwambia kuwa hatuwezi kuelewana kuhusu suala la uwepo wa Mungu kutokana na mtazamo wako potofu kuhusu uthibitisho.

Unajua mkuu wewe hata hukupaswa kubishana kwenye hizi mada za Mungu kwa sababu wewe umeshafanya hitimisho kuwa kwa kukosekana uthibitisho wa kuwepo Mungu ni uthibitisho wa kutokuwepo Mungu.
 
mkuu sasa nimeanza kukupata mtizamo ulionao, najibu lako la swali la kwanza nimelipokea, nisaidie na hio kipande cha mwisho
Suala la nini kitawakuta wasipoamini ni suala la kiimani kwa wenye kuamini uwepo wa Mungu hivyo sioni haja ya kujadili hapa kwa watu ambao hawaamini hata huyo Mungu mwenyewe.
 
Wapi nilikwambia kuwa nipo hapa ili kuthibitisha Mungu yupo? Toka mwanzo nilikwambia kuwa hatuwezi kuelewana kuhusu suala la uwepo wa Mungu kutokana na mtazamo wako potofu kuhusu uthibitisho.

Unajua mkuu wewe hata hukupaswa kubishana kwenye hizi mada za Mungu kwa sababu wewe umeshafanya hitimisho kuwa kwa kukosekana uthibitisho wa kuwepo Mungu ni uthibitisho wa kutokuwepo Mungu.
Hakuna Mungu.

Ova.
 
Kuna mtu kathibitisha Mungu yupo?
Ila mkuu huwa ni uthibitisho wa aina gani hasa ambao huwa unautaka, maana watu walishatoa explanation mpaka za kisayansi kuhusu kuwepo kwa energy ambayo wanasayansi hawailewi na huenda inaweza kuwa ndio Creator, maelezo ya origin ya universe na mambo mengi tu
 
Ila mkuu huwa ni uthibitisho wa aina gani hasa ambao huwa unautaka, maana watu walishatoa explanation mpaka za kisayansi kuhusu kuwepo kwa energy ambayo wanasayansi hawailewi na huenda inaweza kuwa ndio Creator, maelezo ya origin ya universe na mambo mengi tu
1. Nataka uthibitisho wa kuwapo Mungu, ulio logical, unambiguous and undisputable. No bullshit explanation.

2. Uthibitisho wa kuwapo energy ambayo wanasayansi hawaielewi si uthibitisho wa kuwapo Mungu, ni uthibitisho wa kuwapo energy ambayo wanasayansi hawaielewi. Ukilazimisha huu uwe ni uthibitisho wa kuwapo Mungu, unafanya logical fallacy ya non sequitur. Google that. Huelewi wapi?

Ni sawa na kusema ukiwa na ushahidi kwamba humjui baba yako mzazi, basi jasusi wa Kiingereza James Bond 007 ndiye baba yako mzazi.

This is a bullshit explanation.

3. Ukiandika "Huenda inaweza kuwa creator" hapo wewe mwenyewe ushakubali huna uthibitisho. Ndiyo maana unapata kigugumizi na kuweka "huenda" na "inaweza". Yani hata "huenda" tupu umeona haitoshi ukaongeza na "inaweza" kuonesha huna uhakika na unachoandika.

This is a bullshit explanation.

4. Maelezo ya origin of the universe yapi? Yanathibitisha Mungu vipi? Unajua dunia hii ina maelezo mangapi ya the origin of the universe? Wewe unaongelea yapi? Maelfu na maelfu ya tamaduni na kabila za watu wa dunia yana maelfu na maelfu ya habari zao za the origin of the universe, mengi yanapingana, kila mtu ana maelezo tofauti yakuelezea ulimwengu umeanzaje, wewe unaongelea maelezo gani?

This is a bullshit explanation.

Mbona unaandika kivivuvivu na kizembezembe hivi?
 
Hakuna Mungu.

Ova.
Ilitakiwa ubaki na huo msimamo wako ila ukiuliza kuhusu uthibitisho kuhusu Mungu inakuwa kama hauna uhakika na msimamo wako na kuwa pengine Mungu anaweza kuwepo ndio maana unaulizia uthibitisho.

Sijakataza wewe kushiriki hizi mada ila nasemea tu kwamba tafsiri yake hauna uhakika na msimamo wako.
 
Suala la nini kitawakuta wasipoamini ni suala la kiimani kwa wenye kuamini uwepo wa Mungu hivyo sioni haja ya kujadili hapa kwa watu ambao hawaamini hata huyo Mungu mwenyewe.
kama hapa jamvini unaona noma nitumie hata pm, hilo jibu mimi ninashida nalo
 
kama hapa jamvini unaona noma nitumie hata pm, hilo jibu mimi ninashida nalo
Kuona noma tena? Kama una hoja mkuu ilete tuijadili hapa, kuliko kujizungusha kuuliza maswali sijui jibu una shida nalo. Haya mambo yote yanajulikana hapa tunayajadili tu mkuu.

Kwahiyo kuwa wazi mkuu kama una hoja yako wewe leta mkuu.
 
Kuona noma tena? Kama una hoja mkuu ilete tuijadili hapa, kuliko kujizungusha kuuliza maswali sijui jibu una shida nalo. Haya mambo yote yanajulikana hapa tunayajadili tu mkuu.

Kwahiyo kuwa wazi mkuu kama una hoja yako wewe leta mkuu.
Mkuu nimekuuliza swali very plain, ukanijibu lakini kuna kipande hukugusia, nikakukumbusha

Haya ndo majibu yako
Suala la nini kitawakuta wasipoamini ni suala la kiimani kwa wenye kuamini uwepo wa Mungu hivyo sioni haja ya kujadili hapa kwa watu ambao hawaamini hata huyo Mungu mwenyewe.

Mimi nimetafsiri labda unaona noma, kama hamna noma weka jibu tulione
 
Back
Top Bottom