Nimeamua kuwa Atheist

Nimeamua kuwa Atheist

Bado narudia kusema kwamba hatutoweza kuelewana ikiwa bado una mtazamo usio sahihi kuhusu uthibitisho.
Usahihi ni nini?

Una kipimo cha usahihi?

Unathibitisha vipi mtazamo wako ni sahihi na wangu sio sahihi?
 
Thibitisha kwa nini Mungu hayupo? Cc. Kiranga
Katika hili utakuwa una changamoto kwenye reasoning, mtu anayepinga uwepo wa kitu naturally anakuwa free ila anayesema kitu hicho kipo ndiye anapaswa kuthibitisha. Unamlazimishaje mtu kuthibitisha kiti ambacho yeye kashakwambia hakipo? Yaani akithibitisheje wakati hakipo?
 
Jinsi ulivyo hukujipangia, hukuanza tu kuwa mpenda sayansi na mawasiliano

Nyota yako ipo hivyo, you are a Gemini na una akili ya pekee kwa kuzaliwa (by nature), unaongozwa na sayari ya mawasiliano inaitwa mercury.

Najua huamini masuala ya Nyota na pengine unaweza hata kunitukana but I have studied you for so long huwezi kumaliza masaa 24 hujaingia Jf

You are in this way by natural design not by your will.

Pia kuna sehemu nimekuona unatetea mambo ya ubinadamu (mfano unakemea sana mauaji na unyanyasaji) hivi vitu havitokei tu they are in your DNA by the natural design (siyo kila mtu yupo hivi).

You are humanitarian by nature though sometimes you act as a gaidi it's all part of your design (ni mapacha wewe).

Kwahiyo my friend ni uwezo wako wa asili wa kuwa na akili nyingi sababu ya Nyota yako (gemini) ndiyo umekufanya kupenda sayansi na kuhoji kila kitu hadi kuhusu Mungu

Najua utanijibu >nonsense (I know you).

Umefanya vizuri sana kuandika hivi, kwa sababu kisayansi hapa umetupa a testabke theoey.

Theory yako ni kwamba mimi nyota yangu ni Gemini.

Test ni kuanhalia kama mimi nhota yangu ni Gemini.

Kwanza kabisa umekosea, hata kwa hiyo astrology yenu ya uongo, hata nikisema nataka kuiamini, naona kabisa ni uongo.

Mimi si Gemini.

Mpaka hapo tu ushakosea.
 
Nini umeelewa Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote?
Vipi unaweza kuzungumzia kuhusu hiari ya mwanadamu?
1. Mungu huyo hayupo, ni wa katika hadithi tu. Epicurean Paradox/ The Problem of Evil inaonesha hilo.

2. Hiyari hiyo haipo kama unavyofikiri. Wewe hata kunya tu mara nyingi unakunya bila hiyari yako kwa kulazimishwa na tumbo.Yani upo katikati ya safari hutaki kunya, tumbo linakubana na kukulazimisha kunya. Sasa unaongelea hiyari gani?
 
"kua mwema kwa viumbe hai hata visivyoonekana"

Sasa unakataa MUNGU hayupo kwasababu humuoni halafu hapo hapo unaamini kuna viumbe visionekana!
Hili kimantiki ni kosa linaitwa logical non sequitur.

Kwa sababu inawezekana vikawepo viumbe ambavyo havionekani, halafu pia Mungu asiyeonekana akawa hayupo.

Zaidi, pingamizi kubwa kuhusu kuwepo Mungu si kwa sababu haonekani, bali kwa logical inconsinstency iliyo katika hoja za kuwapo kwake.

Hata wewe sikuoni hapa, ila, hili halinifanyi niseme haupo kwa sababu huonekani.
 
Usahihi ni nini?

Una kipimo cha usahihi?

Unathibitisha vipi mtazamo wako ni sahihi na wangu sio sahihi?
Kwa sababu huo mtazamo wa kwamba uthibitisho ndio hufanya kitu kuwepo ni mtazamo ambao nakutana nao kwako tu, sijawahi kuona mtu mwengine ana mtazamo kama huo ndani na nje ya jamiiforums.

Na ni mtazamo ambao unapingana na uhalisia.
 
Kwa sababu huo mtazamo wa kwamba uthibitisho ndio hufanya kitu kuwepo ni mtazamo ambao nakutana nao kwako tu, sijawahi kuona mtu mwengine ana mtazamo kama huo ndani na nje ya jamiiforums.

Na ni mtazamo ambao unapingana na uhalisia.
Kitu kinaweza kuwepo bila kujulikana kama kipo.

Wewe tayari unajua Mungu yupo, Sasa thibitisha Mungu yupo, maana tayari unajua yupo.

Eleza ulijuaje yupo na thibitisha.
 
Twende kwa facts.

Fact 1.

Mpaka sasa, kufuatia miaka yote hii ya kusema Mungu yupo, hakuna aliyethibitisha Mungu yupo.
 
Kwa sababu huo mtazamo wa kwamba uthibitisho ndio hufanya kitu kuwepo ni mtazamo ambao nakutana nao kwako tu, sijawahi kuona mtu mwengine ana mtazamo kama huo ndani na nje ya jamiiforums.

Na ni mtazamo ambao unapingana na uhalisia.
Mkuu , jamaa wanataka uthibitisho ili waamini, wewe kuna namna yeyote unaona unaweza wasaidia kupata uthibitisho? Na hawa jamaa wasipopata uthibitisho na wakaendelea kukataa kuamini, kuna changamoto gani inawakabili hapo baadae?
 
Mkuu , jamaa wanataka uthibitisho ili waamini, wewe kuna namna yeyote unaona unaweza wasaidia kupata uthibitisho? Na hawa jamaa wasipopata uthibitisho na wakaendelea kukataa kuamini, kuna changamoto gani inawakabili hapo baadae?
Uthibitisho Upo kwenye vitabu tunavyoviamini na maisha yetu yote ni uthibitisho Mungu yupo.

Kama wewe huamini mpaka upate uthibitisho kuna shida gani? Wewe Endelea kutoamini na sisi tuache tunaoamini bila huo uthibitisho unaotaka, shida ipo wapi?

Mleta mada anadai haamini Mungu yupo sababu ya usaliti na dhiki lakini kwenye vitabu tumefundishwa dhiki na usaliti vitakuwepo na kwenye vitabu hata Yesu mwenyewe alisalitiwa, Yesu mwenyewe alipitia majaribu

Kwa mantiki hii mleta mada bado ni mtoto ambaye hajasoma na kuelewa vitabu vinasema nini kuhusu Mungu

Mimi nakuruhusu uendelee hivyo hivyo kutoamini lakini usitake na mimi nikufuate wewe.

Kila mtu yupo huru kuamini anachoamini na aishi maisha anayoona yanamfaa yeye
 
Umefanya vizuri sana kuandika hivi, kwa sababu kisayansi hapa umetupa a testabke theoey.

Theory yako ni kwamba mimi nyota yangu ni Gemini.

Test ni kuanhalia kama mimi nhota yangu ni Gemini.

Kwanza kabisa umekosea, hata kwa hiyo astrology yenu ya uongo, hata nikisema nataka kuiamini, naona kabisa ni uongo.

Mimi si Gemini.

Mpaka hapo tu ushakosea.
That was expected! Birthday yako ikifika nitakukumbusha!
 
Uthibitisho Upo kwenye vitabu tunavyoviamini na maisha yetu yote ni uthibitisho Mungu yupo.

Kama wewe huamini mpaka upate uthibitisho kuna shida gani? Wewe Endelea kutoamini na sisi tuache tunaoamini bila huo uthibitisho unaotaka, shida ipo wapi?

Mleta mada anadai haamini Mungu yupo sababu ya usaliti na dhiki lakini kwenye vitabu tumefundishwa dhiki na usaliti vitakuwepo na kwenye vitabu hata Yesu mwenyewe alisalitiwa, Yesu mwenyewe alipitia majaribu

Kwa mantiki hii mleta mada bado ni mtoto ambaye hajasoma na kuelewa vitabu vinasema nini kuhusu Mungu

Mimi nakuruhusu uendelee hivyo hivyo kutoamini lakini usitake na mimi nikufuate wewe.

Kila mtu yupo huru kuamini anachoamini na aishi maisha anayoona yanamfaa yeye

Mkuu unajibu comment ipi
 
Relax, nitakupa uthibitisho wa birthday yako soon...
Kinachokufanya usinipe sasa upige danadana ni kipi?

Umejuaje mimi ni Gemini?

Thibitisha kwa ushahidi usiopingika hapa.
 
Kitu kinaweza kuwepo bila kujulikana kama kipo.

Wewe tayari unajua Mungu yupo, Sasa thibitisha Mungu yupo, maana tayari unajua yupo.

Eleza ulijuaje yupo na thibitisha.
Kujua ni jambo moja na kuthibitisha ni jambo lengine, mimi naweza kuwa nimekuona wewe kabisa unaiba pesa na hivyo nikawa najua kwamba wewe ndio uliyeiba pesa ila kujua tu haifanyi kwamba lazima nitakuwa na uthibitisho wa wewe kuiba hizo pesa kama sikuweza kutengeneza ushahidi kuweza kuthibitisha kuwa wewe ndio uliyeiba pesa.
 
  • Thanks
Reactions: Lax
Back
Top Bottom