Amicus Curiae
JF-Expert Member
- Sep 12, 2012
- 5,352
- 7,662
- Thread starter
- #121
Nawashukuru sana wakuu kwa kunipa moyo, mmenitia nguvu sana.
Ha ha ha!
interesting! ujue 'Amicus Curiae' is a latin legal maxim which means "a
friend of the court", i am a lawyer ndio maana natumia hilo jina, huenda
nikikaita Amicus Curiae Jr katakua kanasheria kama mimi.
Utata sana...lakini kama ana miaka miwili si anaweza kuongea? - Anajijua jina lake? Ukimsikiliza kwa makini unaweza ukajua/kumuelewa akiongea. Au tafuta mtu mwenye mtoto wa umri huo akusaidie kumsikiliza! Unaweza pata some tips kumuhusu.
Kwa kumkadiria ni kama miaka 2 hivi
Vip mkuu nikuchagulie jina, kama vip ukimbatiza mi ntakua baba ubatizo.... kuhusu jina waweza Davion au Delmonte majina mazuri hayo....Asante mkuu, sikajui hata jina, sijui nikape jina lingine?
Nilikuja dar kikazi kwa takribani siku 4, sasa jana nikawa narudi mkoani kwangu. Wkt nipo Ubungo nimekaa kwenye dar express akaja mama mmoja mtu mzima mweupe amebeba mtoto, akaketi pembeni yangu, nikamsalimia nikapiga kimya.
Akaniomba nimbebee mtoto akajisaidie, nikakubali. Muda ukawa unazidi kwenda yule mama harudi! hadi basi linajaa hajarudi, mara kakaja kadem kamoja kakaketi kwenye ile siti ya yule mama nikapigwa na butwaa! nikamueleza kwamba ile siti ina mtu, akanionyesha tiketi yake ikabidi nimuamini kwamba kweli ile ni siti yake
Wkt basi linataka kuondoka ikabidi nimpe taarifa konda, tukashuka na konda na baadhi ya abiria hadi kituo kdg cha polisi ubungo, polisi hawakuniamini sana, wakadhani nafanya usanii nilipotaka kumuacha pale mtoto, ikabidi nipige copy vitambulisho vyangu na niache mawasiliano yangu niondoke na mtoto.
Wamama ndani ya basi wakawa wanapokezana kukabeba na kukalisha, ni katoto ka kiume, ka-handsome, baba, mama na girlfriend wangu nao hawaniamini, wanadhani ni mwanangu! Dah!
Kweli ameshakua wa kwangu huyu!
Nawashukuru sana wakuu kwa kunipa moyo, mmenitia nguvu sana.
Hahahahhahaha lol.....wotewote hunipi ati...ila akikataa kula niite nije kumuimbia😉😉😉😉
Mlee tu huwez jua huko mbele yatatokea nin
Ana afya njem kabisa? Lakini ni muhimu akapimwa vipimo vyote muhimu ili kujua afya yake kwa ujumla
kakubwa lakini, hivi ukimtangaza kwenye tv haiwezekani watu wakamtambua ni mtoto wa fulani? au ushaamua kubeba jukumu?
Umeona riziki hiyooo !! MashaAllah TZ bhanaa ina neema nyingi za ajabu kulikoni !!! ( Madini, Mazao, gesi, hifadhi ,hata watoto unapewa bila uchungu,nk ) Mungu mwema na atusamehe sana huyo mama ana roho ya jiweeee?