Le Mutuz, kwa kweli unastahili pongezi kwa 'DRIVE' uliyo nayo juu ya n
afasi ambazo huwa wagombea. Nashangaa sana kuwa all this has been in just ten months. Kimzaha zaha pamoja na kejeli zote hizi utafika tu mahala unataka ingawa bahati mbaya sana ukijulikana kwa tabia za kejeli, majidai, kujigamba kupenda watoto (most wanapenda lakini si kwa kujigamba) na kujiamini kupita kiwango stahili. However nina maswali kwako ambayo naomba ujibu kama hutajali;
1. Unadhani kuwa katika mchakato wote wa kupiga kura wanachama wapo huru kama inavyostahili? Kuwa kweli kabisa mtu anapiga kura vile anavyotaka na sio anavyo tarajiwa kupiga kura hasa kwa inapo husisha viongozi wakubwa katika hilo zoezi?
2. Mapungufu yepi unayaona yapo ambayo yanatakiwa kusimamiwa na kurekebishwa ili yasirudiwe tena uchaguzi ujao kama huo?
3. Chadema ni threat kiasi gani kwa kwa CCM?
4. Kuna interview uliwahi ongea na
Pascal Mayalla (sio
Pasco wa JF :smile
🙂 kuwa moja ya azma yako ni kuhakikisha CCM inaongioza miaka 50. Do you still believe CCM ina uwezo huo and why? (Nimeuliza sababu wewe mwenyewe ulijicheka saana hii kauli kana kwamba hukuwa na hakika na hii hoja yako).
5. BTW mara ya mwisho mkuu nilibahatika kuona mabandiko na maandishi yako kadhaa (na nje ya jf pia) jinsi gani huwezi kurudi mahala hapa, kwa maneno ya kejeli kana kwamba kweli huwezi thubutu na inaweza kuwa dhambi ukifanya hivyo (kurudi mahala hapa). Nini kimefanya change of heart?
Karibu tena mkuu..