Niligombea NEC Na Nimeshindwa Kihalali - Le Mutuz!

Niligombea NEC Na Nimeshindwa Kihalali - Le Mutuz!

Status
Not open for further replies.
Wewe ni kubwa jinga, ulichoweza kuji sympathy nacho ni kusema umeshindwa kwa sababu huna uzoefu wa hapa, kisa umeishi 30 years abroad!! Very stupid sentence na njia ya kijinga ya kujitetea. Ulivyo waste 30 years kubeba mabox abroad hukujua bongo siasa tena chafu zinaendelea. Acha unafiki!! ushazeeka na ni bora uka step down kuliko kuendekeza kutumia mgongo wa jina la babako kudhani utapita kila mahala. soma alama za nyakati. Bichwa kubwa halina kitu hilo!! Rudi ukabebe mabox yakuvunje kiuno!! Ila mwisho wenu utakuwa mbaya sana nyie watoto wa vigogo!!! We are counting days!!
 
- Kamati Kuu ya CCM ilinipitisha kugombea NEC Viti 10 Bara, uchaguzi ulifanyika juzi Kizota Dodoma kura zangu hazikutosha, na nimeridhika sana na matokeo: Uchaguzi ulifanyika kihalali na haki na ninakubali kushindwa nitajipanga upya na kujikita tena next time zikitokea nafasi zingine za Chama changu CCM, chama Dume!!

-
I am proud na kushika nafasi ya 12, kati ya wagombea 31 ambao wote wengine ni wazoefu wa muda mrefu sana ndani ya CCM, kulinganisha na mimi niliyerudi Bongo Miezi 10 iliyopita, baada ya kuishi Miaka 30 Ulaya na USA, so leo kugombea na miamba hii ya CCM na kushika nafasi ya 12, na kuwapiga wengine 19 it is great honor to me I mean A Luta Continua yaani Mapambano Bado kabisaa yanaendelea, next time tutapigana mpaka kura zitoshe.

- Again, ninakishukuru Chama changu CCM kwa kutoa nafasi kwa kila mwananchi kushiriki kikamilifu bila kubagua wala kuonea, na pia ninawashukuru
CCM-WAZAZI kwa kunichagua kuwa Mjumbe wa Baraza Kuu la Taifa na pia kuiwakilisha kwenye Baraza Kuu la UV-CCM Taifa, na kesho kitakuwa ni kikao changu cha pili katika Baraza hapa Dodoma, I am grateful for that!!

- Ndugu zangu milioko nje rudini tujenge taifa letu, hakuna wa kutujengea huku tuje wenyewe, na pia tuchukue fomu za uongozi tujikite huko ndani kuleta mabadiliko badala ya kukaa kulia lia tu bila sababu na huku ni watuwazima na tuna akili timamu, tukazane tuingie wenyewe! KURUDI HOME SIO A DEATH SENTENCE!! HA! HA! HA! HA! HA!


RESPECT MUCH PEOPLE!!


LE MUTUZ - (KING OF ALL SOCIAL NETWORK MEDIA) & MJUMBE BARAZA KUU LA WAZAZI-CCM TAIFA & BARAZA KUU UVCCM TAIFA!!


Le Mutuz kweli unajua kujisifia, hapo kwenye rangi rangi umechakaza ile mbaya, kura hazikutosha bunge la afrika mashariki, kamati kuu pia, jipange upya. la sivyo watakupotezea mbali, ila nakusifu kwa kuwa mkweli muda wote siyo kama wengine wanaosingizia kuibiwa KURA. ukiona vipi karibu kwetuCDM.
 
Siasa za chama na nchi yetu ya Tanzania. We learn the hard way! Hongera sana William kwa kuwa muungwana na kukubali matokeo.
 
- WEll, nimeshindwa kwa sababu walioshinda ni wazoefu wakubwa zaidi yangu ndani ya chama, wameshinda Viongozi wa Taifa wote 10 naamin inajisema yenyewe ni kwa nini nimeshindwa, tatizo sio kushindwa ila ni ulipoangukia ni wapi!!

Le Mutuz!

Najua walioshindwa wana hasira hasa wanapoulizwa maswali, naomba hasira zako zisiniangukie ! Je, we hukujua kama unaoenda kushindana nao ni wazoefu wakubwa ?
 
- WEll, nimeshindwa kwa sababu walioshinda ni wazoefu wakubwa zaidi yangu ndani ya chama, wameshinda Viongozi wa Taifa wote 10 naamin inajisema yenyewe ni kwa nini nimeshindwa, tatizo sio kushindwa ila ni ulipoangukia ni wapi!!

Le Mutuz!
Uzoefu na ukubwa sio hoja ya msingi. Unaweza ukawa mzoefu wa kufanya madudu na kubwa jinga, wewe uzoefu wa mtu kama Wassira, Nchimbi, Kawambwa, Maghembe, IGP, Hosea, DPP, Idris Rashid na wababaishaji wengine unaweza sema unasaidia chochote kwenye maendeleo ya hili taifa???Hakuna asiyejua kuwa CCM uongozi ni pesa, hilo kundi lililokuja kukutendea haki wewe ndani ya uchaguzi wa CCM limetoka wap???Inaonekana wewe hukutoa pesa nyingi kwa wapiga kura.Jipange nxt time kopa bilioni uhonge utapata tu kijana.

Afu naona una dalili ya kuwa na zile ndimi mbili kama alivyosema JK, wewe unasema uchaguzi ulikuwa halali wenzako wa uchaguz huo huo wanalalama mitaani, nyumba kwenu, mama yako anasema chaguz za CCM zimetawaliwa na rushwa na hivyo c huru na wala si za haki. Hapo tushike lipi???Naweza sema Mama Kilango kasema ukweli coz alitaitiwa na nadhan hatokuja tena kuthubutu kugombea, wewe kwa kuwa unafkiria kugombea tena baadaye ndo mana unajifanya ulitendewa haki ili next time ufikiriwe tena au ili upewe ukuu wa wilaya kama pongezi kwa kuficha ukweli juu ya madudu ya chaguzi za ccm.

Ukiona kijana ameelimika anaenda CCM jua huyo ni mchumia tumbo, hakuna haki wala kweli ndani ya ccm, wote waendao huko ni njaa na uroho wa madaraka ila huwez sema unaenda ccm vile sera zake unazielewa vizur au zinasaidia ustawi wa nchi.
 
hahahaaa ..mods badilisheni title ya thread . naona le mutuz ameamka anaiota chadema kila baada ya sekunde. na huu ni mwanzo tu manake ukiingia ndani ya ccm ndio unapoyaona makali ya chadema. relax bro kukaa nje miaka milion sio kigezo hata sisi tumekaa europe miaka kibao na bado tupo huku . fight for your country narasilimali zake and not for your chama dude.

huyo le mutuz atuache tupumue.umekula vya kutosha kod za watz kupitia mdingi wako.mmekosa chama kingine mpaka+ukitaje chadema ndipo uridhike?.ati kina wanyima usingizi ee.iacheni chadema ipumue kwa kuporwa kur.. Mchana kweupe.
 
- Yaap katika miezi 10 niliyoishi bongo toka nirudi nimegombea:-

1- Ubunge EAC - Nimeshindwa
2. Katibu MWenezi na Elimu na Mazingira wa Wazazi Kata Kivukoni - Nikashinda
3. Ujumbe wa CCM Wilaya ya ILALA - Nikashinda
4. Ujumbe wa WAZAZI_CCM Mkoa wa Dar - Nikashinda
5. Katibu MWenezi CCM Mkoa wa Dar - Nikashindwa
6. Ujumbe Baraz la Wazazi-CCM Taifa - Nikashinda
7. NEC Viti 10 Bara - Nimeshindwa

- So haya yote in 10 months, ni supa sana na tupo vizuri sasa ni kutulia na kujipanga tena mapambano bado sana!!


Le Mutuz!!

una roho ya udikteta. Vyeo vyote vya nini!.
 
Le mutuz hongera kwa kukubali kushindwa na pia kupata hizo nafasi ulizozipata kwa chama chako. Kama kiongozi wa chama mwenye '30yrs ya Europe na US exposure' unapaswa kuwa na mawazo chanya hasa ya kujenga chama. Nimeona bado unafanya mipasho maana sijaona hapa Chadema na Dr Slaa umewaingizaje kwenye mjadala. Hizi ni zama za kufikiria namna ya kupambana na umaskini wa watanzania sio kufikiria mipasho.
 
- Ohh yeah nimeshindwa kama Chadema wanavyoshindwa Urais toka ianzishwe mpaka leo, maneno ya baba ni too low of argument ni simply waste of my time hata kujibu!!

Le Mutuz!

Hapo ndipo unapoharibu.Unaweza potezea hali ya kuwa looser ila unaweza ikomaza na kuikubali kama mchezo wako kwa kuwafanya wengine ni looser kama wewe ili ujipe esteem kuw ahaupo mwenyewe,na pengine katk looser ukawa bora zaidi.Cha kushangaza huijui CDM kama JK mwenyewe, CDM hawakuanza kwa kugombea urais moja kwa moja.Walpoanzia wamefanikiwa sana ndio maana sasa hivi CCM wasipo wataja kwa kuzunguka mbuyu saaana na baadaye wawataje kabisa majina ya viongozi na chama.

NI approach mbaya kudhani kuwa Wassira alifaidika sana kwa kuwa msatri wa mbele kujipitishapitisha kwa CDM, na wewe inaweza kupatia cha kujikomba.Kwanza ni mwoga, huwezi tazama in reality kwanini unachemsha kila kitu ktk siasa?Na ukubali kuwa kuna mengi sana ya kujifunza na kujikomaza.Pia usisahau CDM inaweza kuwa msaada sana kwako kisiasa au hata socially.Wana speaker kubwa sana zinaweza kuliwaza kuliko outing michosho za wanaokupamba halafu wanakunyima kura.

Le mutuz unaweka esteem yako ktk mambo usiyo na control nayo, wal kutoyajua, huku ni kutafuta kifo na huzuni kubwa.NA ccm wote wakiongozwa na presidaa kukubalika ni kuonyesha umahiri wa kuongea vitu vinaweza husishwa na CDM kwa nguvu.Wassira kapeat akw ahilo, presidaa naye, basi mamabo yanakuwa taabu kwelikweli.CCM haian auwezo wa kuzua kukbalika CDM na hivyo kujiweka ktk mfandhaiko mkubwa kama chama.

Mwisho nadhani ulipaswa jipambanua hivi.kama kweli unaamini au huamini ila bado you want to play safe(hoping some day mkono wa mafisadi utaanguka kukufungulia kama mangula),basi ulipaswa kukubali ushindi wa wengine, wapongeza kwa kushinda, wape ofa ya wao kuwa free kutaka msaada wako pale wanauona. Na ulipaswa achana na negative views kwa wengine hata maadui zako.Hapo ungeonyesha ukomavu.Otherwise tutaendelea kufurahia comedies za bure toka kwa mtoto wa kigogo.
 
Le mutuz
Hongera sana angalau unawapa darasa la demokrasia wanaJF; wengi wamegubikwa na vumbi la M4C wanapelekeshwa tu; CCM ni chama makini chenye mfumo huru wa kidemokrasia; sera ndio zinakufanya uchaguliwe; tuko pamoja usikate tamaa kwenye harakati; mkuu usiwe na wasiwasi taifa tunalijenga kutoka kila kona ya dunia; tunampiga adui umasikini ndani na nje!

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Hivi umesema umeishi miaka 30 US/Europe? Kama ni kweli, sa ndo kitu gani hichi ulichoki-post hapa pamoja na exposure yote hiyo???

jamaa bure kabisa! malecela alipata pigo kubwa kumpoteza marehemu Senyagwa akiwa bado kijana mdogo.
 
Ukichanganyikiwa na ukweli,utafuta sehemu ya kutolea stress zako.
Kichaa hakipigi hodi.
Wazee walilonga.
 
Ingawa mimi sio wa chama chenu, lakini sehemu yenye kustahili itabaki kustahili tu...Hongera sana...'Namkumbuka Mzee Malecela (Baba yako) siku moja aliniambia kijana kama umeshindwa sema tu nitakuelewa, ila usishindwe kirahisi kwani bado wewe ni kijana" mnisaidie wadau, Hivi naweza kum-pm mtu nika-attach na picha?..Lengo ni kuona ukweli wa mahali tulipokuwa halafu najua hapo utakuwa na kitu cha kuwaeleza wana JF...uwe na amani.
 
pole mkuu kujikwaa si kuanguka. Ila miaka 30 majuu bado unagombea UVCCM. halafu usikakandye CDM kimeshinwa kura lkn kimeshinda hoja nyingi amabazo zimelisaidia taifa letu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom