Nikirudi katika kodi za Halmashauri, kwa mfano ile kodi ya Huduma/service levy, au kodi ya Hotel/hotel levy...
Je kwa Arusha kuna kampuni ngapi na hotel ngapi...?! Kumbuka pote huko wanapopita Halmashauri na TRA wanapita huko...
Je unaweza ukanipa sababu ni vigezo vipi vimefanya Kilimanjaro kuipita Mwanza kwenye ukusanyaji wa kodi kulingana na jedwali lako...?! Je ni wale watu wachache wa huko wanatoa sana kodi ama...?!
au labda nikuulize ni kwanini kwa mara ya kwanza kabisa walivyoingia serikali ya awamu hii ikaonekana kodi inakusanywa kubwa zaidi...?! Na kwenda kiwango kinapungua...
Nikuulize tena, mimi ninapoingia ziwani kwenda kuvua je kodi nitailipia wapi sababu hata sitokuwa na TIN, labda nikienda kuuza sokoni nitalipia ushuru wa soko ambayo ni 500 tu na wenyewe ni kwa ajili ya halmashauri tu...
Na Magufuli akiutoa huo ushuru sitolipa, wanaolipa kodi ni yale makampuni na viwanda vya samaki kitu kinasoma TRA na mimi sio ninaenda kuvua...
Wale watu wanaofanya shughuli ndogo ndogo pote Mwanza na Arusha hawalipi kodi TRA, kwa hiyo usiseme watu wa huku wanalipa sana kodi kuliko sehemu fulani, angalia vyanzo...