Habari zenu. Ni mwaka wa tatu sasa niko kwenye mahusiano ya kimapenzi na mume wa mtu.nilikutana naye nikiwa nafanya dissertation kukamilisha mwaka wangu wa nne wa masomo chuoni, yeye alikuwa anamalizia masters yake, hivyo nilikuwa natumia muda mwingi library pale chuoni na yeye alikuwa anafika library kujisomea so katika harakati hizo ndipo tulipokutana na kufahamiana. Alinieleza ukweli kuhusu kuwa na mke na watoto na akaniomba tuwe wapenzi. Nami nilimweleza kuhusu kuwa na mpenzi aliye nje ya nchi kikazi. Sikumkubalia ombi lake nilimtaka tuwe marafiki tu,alikubali ila akanambia yuko tayari kunisubiri hadi hapo nitakapokuwa tayari kuwa mpenzi wake.tulispend some quality time pamoja kama friends hadi tulipograduate yeye akarudi kazini kwake nami nikapata ajira mapema kwa sapoti yake. Mwaka jana mwezi wa pili ndipo tulipo make love for the first time na tukawa wapenzi oficialy na ananipenda na kuniridhisha. Kadri muda ulivyokwenda nilijikuta nafall deeply in love na huyu mume wa mtu. Inshort nimepoteza mapenzi na boy wangu wa awali na nashindwa kumweleza ukweli nikihofia kumuumiza. Wandugu naombeni ushauri niko njiapanda.nimweleze ukweli mpenzi wangu ama nipotezee? NB:Kumwacha huyu mume wa mtu kwasasa haiwezekani.
kuwa na mume wa mtu inakuwa powa kama na wewe uko kwenye ndoa ambayo imeshakuchosha then mnapeana tu gudtime, sasa bibie huyu mwenzio ana ndoa na maisha yake, wewe unangangania eti unampenda. WHAT ABOUT YOU AND YOUR FUTURE?
au unadhani atamuacha wife akuoe wewe? Thubutuuuuuuuuuuu
inshort usimuache boyfriend wako, jitahidi kumsahau huyu mume wa mtu ili uweze kubuild future yako pia. trust me itafika wakati huyu mume wa mtu atakuchoka maana ur too available for him.
think of ur future, waume za watu tuachieni sie wake za watu tuliokinai ndoa zetu.