Naombeni hekima zenu

Naombeni hekima zenu

Kashai

Member
Joined
May 12, 2024
Posts
30
Reaction score
69
Jana Rasmi Nimeachana na Mpenzi wangu, huyu Binti Tulipendana sana Wakati tupo Chuo, Mimi nikiwa Mwaka wa Pili, yeye wa kwanza, Sote Tumesoma Diploma.

Mimi ni introvert hivyo huwa napenda sana kutafakari Sana Mambo, Hivyo Jana Nikaona Nimuulize ikitokea sote Tukapata AJIRA Serikalini Mahusiano Yetu yatakuwaje !??

Maana huyu Binti nilipanga KumuOA, Sasaa Hofu yangu ikawa ni Umbali Maana Mmoja anaweza pata kazi Mkoa X Mwingine Mkoa Y, Na mimi siamini katika Mapenzi ya Mbali.

Akajibu yeye Lazima afanye kazi Serikalini kuhusu Ndoa sio Kipaumbele Chake Kwasasa,

Nami nikamwambia Sawa nimekuelewa Basi Tuishie Hapa... Aiseee Nilipomwambia Hivyo Akawaka sana, Amenitukana Sana Mara Mimi kiziwi, Mara Sintopata Mwanamke wa Kunipenda na Hali Yangu, Yaani kaongea Maneno Hayo Duuh !!!

Sasaa Naomba Kuwauliza Ndugu Zangu je, Nimekosea !?? Maana Nimejionea Ndoa Nyingiii Zikivunjika Kwasababu ya Umbali nami sikutaka kuona Watoto wangu Wanatangatanga... Nadhani sote Tunawafahamu TAMISEMI Na suala la Uhamisho Linavyosumbua.

NB; Sikumkataza Asifanye kazi ila nilimwambia Nikipata AJIRA Basi Tutatafuta Shule ya Private ili sote Tuwe Mkoa Mmoja ( Sisi sote ni Walimu wa Primary )

Niongeze Piaa Amesema Ataniroga Kisa kwao ni Shinyanga.

Wakuu Naombeni Hekima Zenu.
 
Kwa upande wangu naona umekosea sana,umejawa hofu kwasababu uzoefu au story nyingi ulizo sikia zimejaa matukio ya namna hiyo

Mbona ndoa zinachangamoto nyingi sana na watu bado kila leo wanaoa na kuolewa

Hata ajira bado hamjapata tayar umeiona hofu ambayo hujui hata kama itakuwepo kweli, tupunguze hofu ambazo hazina ulazima,huwezi jua huenda huyo ndio mwanamke ambaye atakuwa tofauti na story ambazo huwa tunazisika,don't over thinking
 
Jana Rasmi Nimeachana na Mpenzi wangu, huyu Binti Tulipendana sana Wakati tupo Chuo, Mimi nikiwa Mwaka wa Pili, yeye wa kwanza, Sote Tumesoma Diploma.

Mimi ni introvert hivyo huwa napenda sana kutafakari Sana Mambo, Hivyo Jana Nikaona Nimuulize ikitokea sote Tukapata AJIRA Serikalini Mahusiano Yetu yatakuwaje !??

Maana huyu Binti nilipanga KumuOA, Sasaa Hofu yangu ikawa ni Umbali Maana Mmoja anaweza pata kazi Mkoa X Mwingine Mkoa Y, Na mimi siamini katika Mapenzi ya Mbali.

Akajibu yeye Lazima afanye kazi Serikalini kuhusu Ndoa sio Kipaumbele Chake Kwasasa,

Nami nikamwambia Sawa nimekuelewa Basi Tuishie Hapa... Aiseee Nilipomwambia Hivyo Akawaka sana, Amenitukana Sana Mara Mimi kiziwi, Mara Sintopata Mwanamke wa Kunipenda na Hali Yangu, Yaani kaongea Maneno Hayo Duuh !!!

Sasaa Naomba Kuwauliza Ndugu Zangu je, Nimekosea !?? Maana Nimejionea Ndoa Nyingiii Zikivunjika Kwasababu ya Umbali nami sikutaka kuona Watoto wangu Wanatangatanga... Nadhani sote Tunawafahamu TAMISEMI Na suala la Uhamisho Linavyosumbua.

NB; Sikumkataza Asifanye kazi ila nilimwambia Nikipata AJIRA Basi Tutatafuta Shule ya Private ili sote Tuwe Mkoa Mmoja ( Sisi sote ni Walimu wa Primary )

Niongeze Piaa Amesema Ataniroga Kisa kwao ni Shinyanga.

Wakuu Naombeni Hekima Zenu.
Kama hekima za ukataji mauno ingekuwa vema dogo The Icebreaker aje atoe ufafanuzi mwanana je ina stahili?

secretarybird
 
Amenitukana Sana Mara Mimi kiziwi, Mara Sintopata Mwanamke wa Kunipenda na Hali Yangu, Yaani kaongea Maneno Hayo Duuh !!!
Kama ni kweli wewe ni kiziwi usimuache kirahisi hivyo(maana mshaanza kufanana), wanawake Kuna muda hua wanaropoka tu hilo la ndoa siyo kipaumbele chake lisikuumize kichwa cha msingi mnapendana.
 
japo sijui kwa nini imani yangu inaniambia mtakuja kurudiana ila hiyo sio ishu. Kwa sasa naomba uzingatie maswala ya mahusiano yako na Mungu. maana wachawi na walozi wapo asipo kuwa mkeo basi atakuwa jirani , asipokuwa jirani basi ofisini, isipokkuwa ofisini basi kwenye ukoo. so bila Mungu kila ukitishiwa kurogwa roho inatatarika kwa hofu na hofu ndio mlango mzuri sana kwa shetani kuutumia ili kukuibia,kukuharibu na kukuua. na mpaka mtu anakuambia nitakuroga huyo kuna vitu kajihakikishia rohoni kuwa anakumudu na pengine keshakuroga ufahamu tayari anainitiate hofu ili aje akupige dozi kubwa zaidi. maana ili dozi ikubali mlango lazima uwe wazi na hofu ndio mlango wenyewe. so kudhibiti hofu za maagenti ni kujenga imani na Mungu kwa kuhusiana nae.
 
Hujapata ajira tayari mnatengana, hamjaoana tayari malumbano. Ndugu yangu jipige kifua na useme mimi ni punda. After hapo fanya yafuatayo: uanze kusaka job ukiipata fanya kazi na umsahau. Ulitumia akili ulipo muuliza kuhusu ndoa na kama kweli alikujibu hivyo bro fanya yako mapema sana la sivyo mtakuja kukosana vibaya sana mtakapooana na kuajiriwa. Na ukwel tamisemi wana vitu once wakijua nyie ni wamoja watawafanyia mambo hadi mjishange. Nakushauri mim uachane nae utafute ambaye mtatumia akili zako yaan wewe uajiriwe na umfungulie kazi anayoipenda maisha yasonge.
 
Back
Top Bottom