Nikiwaambia msioe muwe mnasikia; kwa miezi 4 mwamba kaishi maisha magumu bila mshahara kumbe mkewe ana laki 8 ndani, na usaliti juu kaambulia

Eeeh bwana ehh ni Mimi Mr. Liverpool Tena.

Weekend hii tumempiga Manure na nyundo Kali sanaa mpaka kapoteana.!!
Sasa jiulize ile ilikua Old Traford, je wakija Anfield..!!!

Turudi kwenye mada ....

HIVI KWANINI HAMSIKII NIKIWAAMBIA MSIOE ??

Sasa Kuna mwenzenu yamemkuta huku ......

Nimemsikitikia sanaaa "Hiii BAGOSHAAAA" (in jiwe's voice)

Mr. Liverpool ni mfanyakazi na mkuu wa idara fulani katika moja ya Halmashauri nchini.

Ana rafiki yake nae ni mkuu wa Idara (kaimu) nyengine (tumuite John).

John kuna jambo alizingua mwezi wa 2 akapigwa SP (Due to Absentees - alisepa kazini wiki bila ruhusa Wala taarifa na aliondoka kiboya hasaa).

John aliishia miezi 4 bila mshahara (akipambana na nisamehe na kumbembeleza HR mpaka wakafungua mshahara, waliufungua mwezi wa 6).

Jana nikaona nipige na John story; "Alitoboa vipi maisha miezi 4 bila MSHAHARA" Tuliongea mambo mengii ila Kuna jambo kanisikitisha sanaaa.

Anasema ........

Kipindi hana mshahara ndio aliijua rangi halisi ya mkewe..!!
Kaishi na mkewe miaka 5 ila hakujua huyu mkewe yuko hivi..!!

Mwezi wa 4 ndio ulikua mwezi mgumu. Hali ilikua ngumu japo kwa nje hakuonyesha.

Alivyoona mambo magumu hasa ilibidi amshirikishe mkewe. Alimueleza kila kitu mkewe japo mkewe ana duka la mahitaji ya nyumbani ambalo alifunguliwa na John ila alimjibu hana kitu.

(John alioa mama wa nyumbani ila aliamua kumfungulia duka ili asiwe wa nyumbani kabisa..!!!)

Ikabidi John anyamaze tu "mtu gani kwenye biashara miaka miwili apati faidi ye kila siku anatangaza hasara?"
John alijiuliza mengi akaona anyamaze alale.

Maisha yalikua taiti, John alikosa hela ya bia na ya manhood (kulinda wallet).
Ye alikua ana hakikisha tu mwanae mmoja wa ndoa anakula na kufurahi.

Kumbe bana John alikua anapitia mengi kwa siri sanaa na hata kula alikua anakula mgahawa wa mbali ili tusimuone yule mzoea makuku ana kula maharage..!!!

Aliogopa aibu na maneno ya walimwengu.

Kuna siku hali ya ugumu ndio ilizidi alirudi home empty (kazini hakupata dili wala kaposho cha kikao).
Kukopa hataki (atalipa nini na hana mshahara?).

Kufika home akamshirikisha mkewe, mkewe akatoa jibu lile lile SINA HELA..!!!

Asubuhi ya siku ifuatayo ilifika aliwazaa akaona leo haendi kazini. Alimwacha mkewe aende dukani, John aliamua kufanya searching nyumba nzima.

Alikuta vifuatavyo:-

1. Kwenye begi la nguo lilikua limechanwa chini.
Alijiuliza begi jipya kuchanika..!! akakuta mule kwenye mchano Kuna vidonge vya uzazi na laki 3 kamili..!!!

2. Akainua godoro, kwa mwisho kwenye kono ya godoro akakuta kuna laki 5.

Akafanya searching kubwaa sanaa kwenye chumba chao cha kulala. Anakwambia alivyovigundua vilimfanya apate hasira hasaa.

Alitoka kwa hasira mpaka dukani kwa mkewe. Akamkuta mkewe anahudumia mteja, kuangalia simu akakuta haijajifunga (mkewe alikua akiangalia kitu YouTube)

John alizuga pale dukani akaiba ile simu akaenda kujificha ili aifanyie upekuzi.

Alivyoviona ........

1. Kumbe mkewe ana bwana ambae alikuaga mwanafunzi mwenzake chuo.

2. Na kwa kusoma sms, inaonyesha huyo jamaa ni X wa mke, na jamaa kapata Kazi mkoa huu huu tuliopo.

3. Mke wa John alimlipia jamaa kodi ya kuanzia maisha kazini na godoro alimnunulia.

3. Mke wa John anavyosemaga anaenda mjini kujumua vitu vya dukani huwa anashukia kwa mwamba ambacho ni chumba cha mke wa John na X..!!

4. Kwenye chatting ya WhatsApp inaonyesha X alimshauri mke wa John waache kutumia P2 ila mke awe anakula vidonge vya majira..!!!

Yaani John Ali screenshot kila chatting akajitumia WhatsApp.
Kwa kuonyesha ukatili hakufuta zile picha ili mkewe ajue kwamba John amejua.

Sasa haya yametokea Kati ya mwezi wa 4 mpaka wa 6.
John anasema anahitaji kuvunja ndoa.

Mke kuona John haitaki tena ndoa kakimbilia kanisani.
Mchungaji alimuita John, John alijibu "Mumewe huyo ni Michael (X)"

Mke akakimbilia kwa wazazi aombewe msamaha.
Wazazi wa mume na mke wamekaa, ila John anasema aliomba ili aelewe cha mtu basi yafanyike mazungumzo mengine na kwenye hayo mazungumzo Michael (X) awepo.

Ila Michael aligoma kabisaa kutimba kwenye usuluhishi na kwa taarifa ya mke pale alipokua anaishi Michael kahama na hajui kahamia wapi na namba za simu hazipatikani tena...!!!

John aligoma kumsikiliza yoyotee kwahiyo wazazi walisepa bila maelewano.

Nilichoshangaa sasa, anasema... Hajawahi kuongea na mtu juu ya hili ila Mimi kumuuliza mambo ya ku survive bila mshahara ndio kumemfanya animwagie yotee kama kushusha mzigo wa fikra..!!!

John haitaki tena ndoa na mpaka tunavyoongea hapa kasha file kesi ya talaka.

Kwake hajafika tokea mwezi wa 6 na nyumba haitaki tena.

John huenda kumchukua mwanae shule akitoka siku za Ijumaa huenda nae gheto lake jipya huku akimtaarifu mkewe "mtoto yupo kwangu".

Mshahara ulivyofunguliwa John kumbe kapanga chumba karibu kabisa na kwangu..!!

Kanunua vitu vichache vya kuanzia maisha.
Kaamua kumuachia mkewe nyumba tu aishi na mwanae.

Ye kaondoka na Shamba la Eka 10 na kiwanja chenye pagala..!! Hati ya nyumba kaacha kwa mkewe ye kaondoka na documents za kiwanja cha pagala na Shamba.

Kabla mahakama haijaamua John kashagawa mali na maisha yanasonga...!!!

Nilichofanya nilienda kupajua kwake alikopanga maana sasa Mimi ndio nimekua jirani yake..!!

Kwenye pagala lake anataka ajitahidi amalizie hata vyumba viwili ahamie maana maisha ya kupanga alishayasahau kabisaa.

TURUDI KWENU WANAUME WABISHI ......!!!!

Na hizi ndio ndoa zenu mnazokimbilia.

Mwamba alijifanya kupenda akamfungulia mpaka biashara kumbe POLE YAKE.

NIKIWAAMBIA MSIOE MUWE MNASIKIA.

Nani kakwambia kuwa wanakupenda?

Braza They love your wallet..!!

Huyu alimpenda John au alipenda pesa za John za kufungulia biashara??

Just hook with them halafu pita hivi kabla wallet haijaisha.

Ila man usisahau kuwezekeza kwenye Mali na akili (financial knowledge).

SECURE YOUR FINANCIAL FUTURE.

When You have ASSETS and FINANCIAL KNOWLEDGE, Then it's ENOUGH..!!!

PESA NDIO KILA KITU, Huoni ZILIVYOMUOKOA RAFIKI YANGU JOHN.

#YNWA
Hii ipo Sana Sana Kwa hawa wanawake ma-graduates. Ambao wanaolewa Kwa kigezo cha kupunguza ukali wa maisha mitaani baada ya kugraduate na kumaliza chuo na kukosa Ajira
 
Hii ipo Sana Sana Kwa hawa wanawake ma-graduates. Ambao wanaolewa Kwa kigezo cha kupunguza ukali wa maisha mitaani baada ya kugraduate na kumaliza chuo na kukosa Ajira
Sasa kwanini mnaoa kama mnaelewa hili...!??

#YNWA
 
Hawa wanawake wanatetea sana ndoa na kuzipigia promo kwa sababu wanajuaga tofauti na hapo hawana thaman nyingne yyte mbele ya mwanaume. Kiufupi ni kwamba "Marriage is a female institution, yu as a man you get nothing from it, yu have to sacrifice your dreams, ambition,time, etc"

Na ndo maa mwanaume akioa anaanza kukonda lakn mwanamke akiolewa anaaza kunenepa kwa sabab n kama kapata ajira/unafuu
📌📌📌

#YNWA
 
...Ubovu wa mwanamke mmoja haihalalishi kuwa watu wasioe
You need some kind of psychological treatment young boy! Got me??

Read this 👇👇

Jamaa yangu mmoja na yeye yamemkuta kama john... Hana hata mia ya kuacha home kila siku hadi aje town aunge unge ndio atume boda apeleke chochote home... Siku nyingine hola wanaishia kula viporo! Kumbe mke ana laki 5 kaficha kwenye begi hadi inakaribia kuoza...

#YNWA
 
Back
Top Bottom