Wana jamvi naandika hapa nikiwa na hofu na mashaka juu yangu mwenyewe..
hili jambo limekua likinitatiza sana..mwaka 2006,nikiwa shule niliota nyumbani tunalia,tumefiwa,haikuchukua hata wiki mbili..nikapigiwa simu kujulishwa msiba,bibi yangu mzaa mama amefariki..
Mwaka uliofuata nikaota mjomba wangu kafariki..wiki kadhaa baadae mtoto wa mjomba wangu nlomuota (binamu yangu sasa)alifariki kwa kupigwa na radi..nikaanza kujistukia lakini sikumuambia mtu..Mwaka jana niliota kuna msiba umetokea kwao my best frnd kabisa wa toka utoto (tumekua kama ndugu sasa)..haukupita muda,kaka yake akafariki..miezi miwili baada ya huo msiba,nikaota tena msiba tena..baba yake na my best huyo huyo akafariki..
Leo usiku,nimelala usingizi wa mang'amu ng'amu..nimeota niko msibani nalia..sasa hivi tuu nimepata ujumbe wa simu mjomba wa rafiki yangu (sio alofiwa na kaka na baba) amefariki..
Jamani ni nini hii?..wengine husema wakiota msiba maana yake ni jambo la heri mbona mm sio hivo?
Hapa sina amani..