Nihamie wapi kati ya Arusha na Mbeya?

Nihamie wapi kati ya Arusha na Mbeya?

Chugga pagumu, Mwanza pako poa sana Kimaisha kuanzia watu wa kawaida mpaka wa Kati.

Bata unalokula kwa laki Arusha Mwanza ni elfu arobain hivi.

Hotel nzuri za Maana Arusha zinaanzia 80,000 wakati Mwanza ukiwa na 40,000 Hotel nzuri tu.

Siku maisha yakikubamba unaenda zako mwaloni hukosi kuja na Sato Sangara au Hata dagaa.

Mji unazungukwa na wakulima hasa Unga bei chee kabisa.
 
Arusha usije huku hata viwanja watu wanauza bei ghali kuliko mikoa mingine pia kodi za nyumba na frame bei ghali. Mbeya fursa nyingi sana kutoka itakua rahisi.
 
Upo msingi au sekondari?
Arusha ujue kukimbizana na noti,vinginevyo ubakie Dar
 
Matako bar
Unajua hilo jina ni waungwana tu waliwakatia wale individual wanayofanya kazi pale kwa kua huko nyuma sio masiara, ukimiliki demu wa pale ni sawa na unamiliki mzigo fulani hivi wa maana kwenye life lako
 
Unajua hilo jina ni waungwana tu waliwakatia wale individual wanayofanya kazi pale kwa kua huko nyuma sio masiara, ukimiliki demu wa pale ni sawa na unamiliki mzigo fulani hivi wa maana kwenye life lako
Hahaaaaaaa pale ni hatar sana mkuu
 
Mkuu hamia mbeya tena nakushauri nenda Tunduma.Nakushauri uende huko kwa sababu zifuatazo
1:Hakuna ukabila kwenye ile boda,watu hawashughuliki kujua wewe ni nani na umetoka wapi,wapo bize na kutafuta pesa.Arusha kuna ukabila kiaina,ikiwa wewe si mzawa wa kaskazini itakuchukua muda kutengeneza chaneli hususani za biashara.

2:Ukiwa Tunduma utakutana na watu wa mataifa mbalimbali ambao wanafanya ujasiriamali wa kuuza na kununua bidhaa kama vile samaki,mahindi,ulezi nk kwa mtaji mdogo unaweza ukaanza na baadaye ukakua taratibu.Arusha fursa kama hizo zimebanwa sana.

Ikiwa utakua kimtaji na ukawa unaishi mbeya ni rahisi ukanunua mazao ya chakula na kupeleka Arusha kuuza,ukiwa Arusha huwezi kununua mazao kule na kupeleka Mbeya.

4:Watu wa Mbeya ni wakarimu kuliko wale wa Arusha,ni rahisi kupokelewa Mbeya hata na watu wasiokujua na ukaishi nao na kufanya mambo yako.Arusha ni ngumu kupokelewa kirahisi hususani kama sio mwenye asili ya kaskazini mwa Tanzania

Bro si kweli kabisa,we mwambie tu arusha panaugumu lakini sio kwamba kuna ubaguzi..ktk mikoa ambayo haina ubaguzi ni Arusha,mwambie wajuaji ni wengi,wengi wanaijua hela vilivyo.ukiitoa Dar sehemu yenye mwingiliano wa makabila mengi ni Arusha.tatizo pale hata shilingi mia hakuachii kila mtu anaijua hela
 
Bro si kweli kabisa,we mwambie tu arusha panaugumu lakini sio kwamba kuna ubaguzi..ktk mikoa ambayo haina ubaguzi ni Arusha,mwambie wajuaji ni wengi,wengi wanaijua hela vilivyo.ukiitoa Dar sehemu yenye mwingiliano wa makabila mengi ni Arusha.tatizo pale hata shilingi mia hakuachii kila mtu anaijua hela
Ukweli asilimia mia moja ndugu yangu
 
Back
Top Bottom