Nifanyeje ili niache kazi hii?

Nifanyeje ili niache kazi hii?

Wakuu habari.

Nataka kuacha kazi na niingie kwenye biashara. Kiufupi kazi hii imekuwa na majungu mengi. Imefika wakati nimeona nijiajiri

Naomba ushauri wako, nifanye biashara gani, na nianze vipi, na mtaji kiasi gani, kwa mtaji wetu wa tunaohustle

Cash ninayo 20M
Investment sio products or procedures it's PLANS. If you don't have PLANS, don't invest. Endelea kupambana na hayo majungu, huku yakikupa hasira kuweka plans ya kitu au vitu utakavyo kuwekeza.
 
Wakuu habari.

Nataka kuacha kazi na niingie kwenye biashara. Kiufupi kazi hii imekuwa na majungu mengi. Imefika wakati nimeona nijiajiri

Naomba ushauri wako, nifanye biashara gani, na nianze vipi, na mtaji kiasi gani, kwa mtaji wetu wa tunaohustle

Cash ninayo 20M
Habari!
Usiache kazi kwa sababu ya majungu, hata kama una mtaji.

Tumia mtaji wako kuanzisha biashara kulinhana na ulipo na interest uliyonayo. Mpaka pale biashara yako itakapokuwa na uzalishaji wenye kuaminika/unazalisha zaidi ya kazi yako na unahitaji muda zaidi kuisimamia ili kuiendeleza na kwenda kazini kunaonekana kukubana. Au biashara yako inaonyesha kuhimili ups and down za challenges ndani ya mdumo wake.

Hapo ndo uache au upumzike kwenye kazi yako ya mshahara.
 
Usithibutu kuacha hiyo kazi, piga mishe zako pembeni huku na kazi yako.. naongea kwa machungu mana nishawahi kuvaa viatu vyako!
 
Investment sio products or procedures it's PLANS. If you don't have PLANS, don't invest. Endelea kupambana na hayo majungu, huku yakikupa hasira kuweka plans ya kitu au vitu utakavyo kuwekeza.
Asante Sana
 
Huna sababu ya kua kuacha kazi ndugu yangu..... Unaogopa majungu?. "Are you not clean in your deeds?"
 
Ndugu kama uko seriously fanya chagua moja kati ya haya:

1. Tafuta sehemu ambayo mji unaanza kukua na uweke mashine ya kukoboa na kusaga mahindi alafu bakiza mtaji wa kununulia mahindi japo gunia hamsini ambazo utakuwa unauzia hapo mashineni.

2. Tafuta sehemu za mashamba kunako limwa maharage ya njano alafu nunua ekari tano chumba kisima cha kutosha kuhudumia hizo ekari na anza kulima. Kwa mwaka unalima mara tatu.

Kwa hayo niliyokueleza kama utafata huu ushauri na ukasimamia vizuri wewe mwenyewe hakika huta juta kuacha kazi. Maana pesa yako utakuwa unaiona na utakula faida mpaka ushangae.

NB. Biashara yoyote inahitaji committiment.
 
Ndugu kama uko seriously fanya chagua moja kati ya haya:

1. Tafuta sehemu ambayo mji unaanza kukua na uweke mashine ya kukoboa na kusaga mahindi alafu bakiza mtaji wa kununulia mahindi japo gunia hamsini ambazo utakuwa unauzia hapo mashineni.

2. Tafuta sehemu za mashamba kunako limwa maharage ya njano alafu nunua ekari tano chumba kisima cha kutosha kuhudumia hizo ekari na anza kulima. Kwa mwaka unalima mara tatu.

Kwa hayo niliyokueleza kama utafata huu ushauri na ukasimamia vizuri wewe mwenyewe hakika huta juta kuacha kazi. Maana pesa yako utakuwa unaiona na utakula faida mpaka ushangae.

NB. Biashara yoyote inahitaji committiment.
Asante
 
Hiyo Hela inaweza ikawa ndogo sana au pia ikawa kubwa sana,
Kwanza fikiria biashara unayoipenda na Anza kuifatilia kujua faida na changamoto zate epuka marafiki zako wa karibu watakuingiza Chaka wapate Cha kusema.
 
Hiyo Hela inaweza ikawa ndogo sana au pia ikawa kubwa sana,
Kwanza fikiria biashara unayoipenda na Anza kuifatilia kujua faida na changamoto zate epuka marafiki zako wa karibu watakuingiza Chaka wapate Cha kusema.
Asante Sana
 
Kama unaweza kufanya kazi na ku save hicho kiasi cha pesa.. nakusahuri uendelee kufanya kazi yako kwa moyo mmoja.

Asikudanganye mtu, bongo hakuna mfanyabiashara.. wapo wachuuzi tu..

Yaani ununue kitu 200 utafute wa kumgonga umuuzie 350.. ndo ujasiriamali wa wabongo huo... mwisho w siku ni pasua kichwa..

We endelea na kazi yako.. achana na habari za kuja kua mchuab

Boss biashara zinalipa sana
 
Kama unaweza kufanya kazi na ku save hicho kiasi cha pesa.. nakusahuri uendelee kufanya kazi yako kwa moyo mmoja.

Asikudanganye mtu, bongo hakuna mfanyabiashara.. wapo wachuuzi tu..

Yaani ununue kitu 200 utafute wa kumgonga umuuzie 350.. ndo ujasiriamali wa wabongo huo... mwisho w siku ni pasua kichwa..

We endelea na kazi yako.. achana na habari za kuja kua mchuuzi
Chamsingi pesa.

#MaendeleoHayanaChama
 
Wakuu habari,

Nataka kuacha kazi na niingie kwenye biashara. Kiufupi kazi hii imekuwa na majungu mengi. Imefika wakati nimeona nijiajiri.

Naomba ushauri wako, nifanye biashara gani, na nianze vipi, na mtaji kiasi gani, kwa mtaji wetu wa tunaohustle.

Cash ninayo 20M.
Kujiajiri lazima uhitimu "majungu"..
 
Back
Top Bottom