Huku mitaani naishi na wznz, hawa ni watu wa kawaida na wanaendesha maisha yao bila wasi wasi, wao muungano ni sehemu ya neema kwani wakienda bahari wanaleta pweza, wakirudi znz wamebeba viazi, watoto wanakwenda shule wanatibiwa n.k. kundi hili hawaoni Znz ya pepo yenye mito ya maziwa na asali bali Znz ya juhudi zao na fursa ya muungano.
Kuna kundi la wale waliosoma vitabu na kuamini kuwa Znz ya enzi hizo ilikuwa ni bora sana, znz ya sultani kwani tende, halua na mchele vilipatikana bure kutoka uarabuni. Kundi hili linaungwa mkono na wafanyabiashara kutoka uarabuni wanaotaka kurejesha usultan kwani nao wanatamani zama za usulatan wao a.k.a znz yao.
Wapeleke mswaada wa kura ya maoni ili warudishe nchi ya neema, nchi ya kusadikika, yenye mito ya asali, na mabwawa ya maziwa.
Mkuu.
Haya mambo ya muungano yanakugonga sana inaonekana. Maana yake lugha unayoiteremsha katika michango yako.... utafikiri Nyerere kafufuka!
Mkuu nguruvi3.
Tutalinda mapinduzi mpaka lini?
Bora jamaa warudishiwe sovereignty yao halafu wataamua wenyewe kama watachinjana au watatoana macho, au watakwenda baharini kutafuta pweza au kutafuta ng'ombe kukamua maziwa au kufuga nyuki ili wapate asali.
Mwanamapinduzi Gaddaffi si unamuona anavyolinda mapinduzi yake?
Sasa unataka ya Libya yaje TZ pia? Kuna kauli zinatolewa wajaribu wakione...kuna crime against humanity siku hizi ukiteleza wenye maliasili zao wanakuja na manoari za kivita na drones kukuletea demokrasi.
Mimi nafikiri wale wazee wa umri kama wako,nafikiri tu,kwa sababu unazungumza kama mwanamapinduzi.., au Jumbe, Ali hassan mwinyi, Nassor Moyo, Edwin mtei, Bomani, warioba, salim Ahmed salim, Seif sharif wakati wao umepita...sasa kuna vijana wa utandawazi, wa internet na twitter, wametembea ,wanaona mambo, wanasoma...kizazi kipya kina madai yake na si vyema kupuuzwa....wimbi la mageuzi limeshika kasi hata kama tutajaribu kulizuia litakuwa ni suala la muda tu.
Sisi tulipigana vita ya Kagera kuhakikisha Amin hachukui Ardhi yetu, sehemu ndogo tu...sasa kama wazanzibari wanaufananisha muungano na uvamizi au kutawaliwa basi hakuna lugha itakayowapoza mpaka watakapopata wanachokitaka.
Ni wazi wao wanataka ama shirikisho na sio unitary union au wanataka Zanzibar ya asali na maziwa kama unavyoiita.
Nafikiri mpira wameturushia sisi kaka viranja!
Mimi sifahamu kwa nini serikali inakataa mjadala wa wazi juu ya muungano na muundo wake? Muungano huu haujawahi kufanyiwa review, sisi tunauimarisha tu bila ya kujua wananchi wetu wanauonaje, faida na hasara zake.
muungano gani ambao hauna annual report? muungano ambao haujulikani mapato wala matumizi yake?kasoro au kero zipo zinajulikana sasa kwa nini iwe ni kosa kwa watu kutaka mjadala wa wazi wa muungano?
Mimi nazungumzia mjadala wa kitaifa sio kama hivi, mapinduzi, nywele za kimanga, visa za oman...Tanganyika haihitaji maoni.. serikali tatu mzigo...bajeti ya millioni 500.
Watu walio na Muungano fuctional, ambao wanaona faida yake hawalalamiki wala kupiga mayowe bana?
Nimesoma makala aliyoiweka Makaimati,kaimati....
Kama hata Mwanamapinduzi Moyo analalamika basi ameona kuwa mapinduzi yamepinduliwa!! Muungano unachakachuliwa!!!