Ni Zanzibar ipi wanaitaka?

Ni Zanzibar ipi wanaitaka?

yeah right hata historia ya Zanzibar mnataka tusahau! Hii Zanzibar ya pepo hiyo iliwahi kuwepo lini? Matatizo ya Kiuchumi, Kisiasa na Maendeleo ni nchi gani ambayo haina? Wengine tuliaminishwa kuwa nchi zote za Kiarabu ni pepo, maskini kina Khalid wametuonesha ile siri kuu. Tunaambiwa Oman ni pepo.. juzi tunaoneshwa kuwa ipo Pepo ya Wachache. Na hivi ndivyo mnavyotaka watu waamini kuwa Zanzibar ilikuwa Pepo kwa kila mtu, kumbe ilikuwa Pepo ya Wachache.

Kweli mnafikiri mkiwa nje ya Muungano ndio matatizo ya Kiuchumi, Kisiasa na Maendeleo yataondolewa? Really? SAudia na mafuta yake yote hayo imeweza vipi kuondoa matatizo yote ya Kijamii? Hata Libya, Iran, na Iraq zote ukiziangalia kwenye kipimo cha maendeleo zinaoneshwa ziko juu ya Tanzania lakini leo tunajua kuwa siyo vyote vinavyomeremeta dhahabu. Jamani msiwaadahe watu kuwa ati Zanzibar ikiwa nje ya Muungano basi pepo itarudi. Msije kujikuta mnabakia kuimbiana taarab za nyimbo za "iliyokuwa Zanzibar" huku watu wanatamani pepo isiyokuwepo.

Ushirikiano wetu unatuhakikishia sote na miye napendekeza zaidi Zanzibar a brighter future kuliko watu wanavyodanganyana.


Mkuu Mwanakijiji sijui wapi hayo ya pepo yameelezwa humu lakini wanachosema Wazanzibari, wanataka self determination na sio jengine. Hayo matatizo ya Zanzibar na Wazanzibari tangu lini kwenu kuwa ni issue?

Lugha hizi zenu ni vile tu mmenogewa na utamu wa kutawala na sio jengine. Kama sisi tuna matatizo na mzigo, si mtuache tu, ya nini kutung'ang'ania? Kwanini msiungane na Congo?

Ya Wazanzibari waachieni wenyewe watajua la kufanya.
 
Hivi ni nani anatakiwa kumuacha mwenzie?

Wanaitaka nchi yao na wakati huo huo mzimu wa mwalimu unawajia. Wanataka Tanzania ionekane imewatenga Tanzania nayo haiko tayari na wakati huo huo Tanzania inataka kuona wakijitenga lakini hawajitengi wanaishia kulalama tuuuu.

Wake up Zanzibarian, tengeneza mswada, pelekeni BWZ wapitishe, mupeleke kwa watu wenu ili wapige kura ya ama kuondoka ama kubaki. Baada ya hapo maamuzi yenu yataheshimiwa!!! Hivyo tuuuu. Mbwembwe nyiiiiiingi. Y?
 
yeah right hata historia ya Zanzibar mnataka tusahau! Hii Zanzibar ya pepo hiyo iliwahi kuwepo lini? Matatizo ya Kiuchumi, Kisiasa na Maendeleo ni nchi gani ambayo haina? Wengine tuliaminishwa kuwa nchi zote za Kiarabu ni pepo, maskini kina Khalid wametuonesha ile siri kuu. Tunaambiwa Oman ni pepo.. juzi tunaoneshwa kuwa ipo Pepo ya Wachache. Na hivi ndivyo mnavyotaka watu waamini kuwa Zanzibar ilikuwa Pepo kwa kila mtu, kumbe ilikuwa Pepo ya Wachache.

Kweli mnafikiri mkiwa nje ya Muungano ndio matatizo ya Kiuchumi, Kisiasa na Maendeleo yataondolewa? Really? SAudia na mafuta yake yote hayo imeweza vipi kuondoa matatizo yote ya Kijamii? Hata Libya, Iran, na Iraq zote ukiziangalia kwenye kipimo cha maendeleo zinaoneshwa ziko juu ya Tanzania lakini leo tunajua kuwa siyo vyote vinavyomeremeta dhahabu. Jamani msiwaadahe watu kuwa ati Zanzibar ikiwa nje ya Muungano basi pepo itarudi. Msije kujikuta mnabakia kuimbiana taarab za nyimbo za "iliyokuwa Zanzibar" huku watu wanatamani pepo isiyokuwepo.

Ushirikiano wetu unatuhakikishia sote na miye napendekeza zaidi Zanzibar a brighter future kuliko watu wanavyodanganyana.

Miaka 47 ya Muungano hakuna maendeleo...Kwahiyo wasubiri miaka 47 mengine? KUTATUA MATATIZO YA WATU MILIONI 1,000,000 NI RAHISI KULIKU MATATIZO YA WATU MILIONI 40... Zanzibar ilishakuwa nje ya Muungano ( kabla Muungano) na sasa ipo kwenye Muungano. Kwahiyo tayari wamesha experienced vipindi vyote na tofauti wanaziona sasa. Kuwa nchi masikini sio kitu kibaya kama kupoteza mamlaka ya nchi yako. Hiki ndio kilio cha wazanzibari wote.

Hayo unayoyasema kuhusu nchi za Kiarabu ndio yatakuja hapa Tanganyika na Zanzibar sio muda mrefu sana. Unless, mubadilike, muruhusu kura ya maoni, mjadala wa wazi kuhusu Muungano, Kuheshimu demokrasia ya kweli ( kuwaachia wazanzibari kuchagua viongozi wao wanao wataka). THERE IS NOTHING BETTER THAN BEING FREE...
HIZI SIO ZAMA ZA NYERERE, MPAKA KIELEWEKE.... Naomba kuwasilisha
 
Mi yangu macho. Muungano ukivunjika tutayaona mengi yaliyofichama chini ya uvungu. Moja ya kasheshe itakuwa ni madai ya kila upande kwamba kisiwa cha Latham kilichoko karibu na Mafia kusini mwa Zanzibar kwamba ni cha kwao. Kwa hivyo kutakuwa na kasheshe kwenye kugawana mipaka ya bahari (Territorial Sea na Exclusive Economic Zone) kati ya Tanganyika na Zanzibar. Kisiwa hiki ni strategic si tu kwa umuhimu wake wa kuwa kivutio cha utalii wa ndege, bali katika suala zima la rasilimali za bahari kuu wakiwemo samaki wa Magufuli na uwezekano wa kupatikana kwa gesi asilia na mafuta. Jihabarishe zaidi hapa kuhusu madai ya watu wa Zanzibar Ismail Jussa: Zanzibar tukilala hatutakuwa tofauti na Ukerew | Mzalendo.net
 
zanzibar ambayo wewe unaijua ndio Wazanzibari wanaitaka...

Kwaani kuna ubaya gani kwa mtu kuvunja urafiki kama kachoka kuendelea na urafiki na mtu? Au kuna ubaya ganin mtu kurejesha urafiki na adui yake? Nifahamuvyo mimi... There are no permanent friends or permanent enemies rather there is permanent interests. Kwa msingi huo basi, haijalishi Zanzibar ya namna gani... ya sultan sijui au ya nyerere (yeyote ile) bali iwe na mamlaka yake kamili kama awali, period.
 
Maadam wanaopiga kelee ni watu wa kuja mimi nadhani ndio maana WaZanzibar wataendelea kupata shida ndani ya nchi ya ugenini...Huku bara hao wa kuja, hutawasikia wala kuwaona wakipiga makelele tena hujificha wakati wa maandamano au mikutano, lakini zanzibar ndio wamekuwa wasemaji wakubwa sana na ukiwauliza watakwambia mimi sii Mzanznibar bali Myemen, Mu Oman. Mngazija na kadhalika.. Ni lini Wazanzibar mtakubali kuwa Wazanzibar kabla ya asili zenu?
 
Mnapenda kusafiria Pasi za Jamhuri ya Muungano wa TAnzania au mnataka Nchi ya Zanzibar iwe na pasi zake za kusafiria? ni swali rahisi ambalo halihitaji kumuitwa mtu mjinga au vyovyote vile.

Ndugu naona kama unaenda kando ya barabara. Issue hapa siyo pass ya kusafiria. Issue ni sovereignty ya nchi. Hebu niambie kwaani kuna tatizo gani kama mtu akivunja urafiki aliyo kuwa nao awali na rafikiye? Au kuna tatizo gani mtu kurejeshe urafiki na adui yake? Nifahamuvyo mimi...There are no permanent friends or permanent enemies rather there are permanent interests. Kwa msingi huo basi, haijalishi ni Zanzibar ya Sultan au ya Nyerere ... bali ni Zanzibar iliyo dola kamili ndiyo inayohitajika. Right?!


 
Maadam wanaopiga kelee ni watu wa kuja mimi nadhani ndio maana WaZanzibar wataendelea kupata shida ndani ya nchi ya ugenini...Huku bara hao wa kuja, hutawasikia wala kuwaona wakipiga makelele tena hujificha wakati wa maandamano au mikutano, lakini zanzibar ndio wamekuwa wasemaji wakubwa sana na ukiwauliza watakwambia mimi sii Mzanznibar bali Myemen, Mu Oman. Mngazija na kadhalika.. Ni lini Wazanzibar mtakubali kuwa Wazanzibar kabla ya asili zenu?

Jamani ketandawili ?Tega.... Kuna nchi moja ya Afrika, ina mlima mrufu sana kuliko nchi nyengine yeyote ya Afrka, ina mbuga , ina maadini ,ina natural gas , ina mwabao wa bahari, inazungumza kiswahili, Rais wao wa zamani (dikteta) wanamuita baba wa taifa, raia wake wengi ni masikini na wanaishi maisha duni sana, lakini wanataka kulazimisha kuitawala nchi nyingine....NCHI GANI HIYO ???
HIZI SIO ZAMA ZA NYERERE ....MPAKA KIELEWEKE... naomba kuwasilisha.
 
Mkuu Mwanakijiji , usipoteshe watu kwa falsafa zako za uongo na kweli... Kilio cha wazanzibari ni Matatizo ya ki-UCHUMI ,SIASA NA MAENDELEO. Hakuna mtu anabaguliwa Zanzibar eti mweusi ,sio kweli . Mimi nimeshi kote Tanganyika na Zanzibar sijaona hicho kitu. Ikienda Zanzibar ,halafu waambie hii sio nchi , kweli watakutenga hata uwe na rangi kama mzungu wa ulaya. Huo ndio ukweli wa mambao.

Nadhani hufuatilii post au uwezo wa kuzielewa unaleta tabu.
Kama Zanzibar hawabaguani kwanini wapemba wanasema si sehemu ya unguja na wamepeleka madai hadi UN. Hiyo unaiita nini kwa lugha yako. Pili, Kwanini waunguja wasema mapinduzi daima, wapemba waseme hayo ni ya Nyerere na Okello?
Tatu, kwanini Waunguja waseme Wapemba hawana elimu, wapemba waseme wao ni bora kwa rangi na nywele.
Kama si CCM kulazimisha wakati huu ni lini Pemba iliwahi kutoa kiongozi, na unadhani ni kwanini.
Mimi nimesihi kote huko najua vema kauli, kejeli na dharau, ni suala la muda tu utatambua haya tusemayo
 
yeah right hata historia ya Zanzibar mnataka tusahau! Hii Zanzibar ya pepo hiyo iliwahi kuwepo lini? Matatizo ya Kiuchumi, Kisiasa na Maendeleo ni nchi gani ambayo haina? Wengine tuliaminishwa kuwa nchi zote za Kiarabu ni pepo, maskini kina Khalid wametuonesha ile siri kuu. Tunaambiwa Oman ni pepo.. juzi tunaoneshwa kuwa ipo Pepo ya Wachache. Na hivi ndivyo mnavyotaka watu waamini kuwa Zanzibar ilikuwa Pepo kwa kila mtu, kumbe ilikuwa Pepo ya Wachache.

Kweli mnafikiri mkiwa nje ya Muungano ndio matatizo ya Kiuchumi, Kisiasa na Maendeleo yataondolewa? Really? SAudia na mafuta yake yote hayo imeweza vipi kuondoa matatizo yote ya Kijamii? Hata Libya, Iran, na Iraq zote ukiziangalia kwenye kipimo cha maendeleo zinaoneshwa ziko juu ya Tanzania lakini leo tunajua kuwa siyo vyote vinavyomeremeta dhahabu. Jamani msiwaadahe watu kuwa ati Zanzibar ikiwa nje ya Muungano basi pepo itarudi. Msije kujikuta mnabakia kuimbiana taarab za nyimbo za "iliyokuwa Zanzibar" huku watu wanatamani pepo isiyokuwepo.

Ushirikiano wetu unatuhakikishia sote na miye napendekeza zaidi Zanzibar a brighter future kuliko watu wanavyodanganyana.

Hawa wanaosema wanaonewa ni hawajui nyimbo wanazoimba. Maswali uliyoweka kuhusu Zanzibar ipi wanaitaka ni mtihani wa degree maana hawajui kuwa adui yao si Bara bali yumo miongoni mwao. Kuna kiongozi mmoja wa Znz anazunguka duniani kuungwa mkono na hoja yake si uchaguzi bali kuondoka ndani ya muungano. Asicho kijua ni kuwa yeye ana nywele za kimanga ambazo hazimruhusu kuwa kiongozi Unguja nyumbani kwa mapinduzi.

Huku mitaani naishi na wznz, hawa ni watu wa kawaida na wanaendesha maisha yao bila wasi wasi, wao muungano ni sehemu ya neema kwani wakienda bahari wanaleta pweza, wakirudi znz wamebeba viazi, watoto wanakwenda shule wanatibiwa n.k. kundi hili hawaoni Znz ya pepo yenye mito ya maziwa na asali bali Znz ya juhudi zao na fursa ya muungano.

Kuna kundi la wale waliosoma vitabu na kuamini kuwa Znz ya enzi hizo ilikuwa ni bora sana, znz ya sultani kwani tende, halua na mchele vilipatikana bure kutoka uarabuni. Kundi hili linaungwa mkono na wafanyabiashara kutoka uarabuni wanaotaka kurejesha usultan kwani nao wanatamani zama za usulatan wao a.k.a znz yao.

Na mwisho, ni kundi la hawa walioko nje. Wanaamini wana elimu sana ya kuweza kugeuza Znz kuwa kisiwa cha matunda, maziwa na asali. Wanaamini kuwa kwa vile wanaweza kuongea kiingereza hiyo ni elimu tosha inayoweza kuleta mabadiliko, na kuondoka katika muungano ni fursa yao kuwa mawaziri na makatibu wakuu. Ndio wanaoonekana katika internet, lakini waulize maswali mawili au matatu, hawana majibu ila matusi, kashfa(mzalendo.net), wao imani yao imejikita katika mafuta, misaada kutoka uarabuni na wanathubutu hata kusema Mzanzibar hahitaji visa kuingia Oman! yaani visa ya Oman ni kitu muhimu sana kwa maisha yao.

Wapeleke mswaada wa kura ya maoni ili warudishe nchi ya neema, nchi ya kusadikika, yenye mito ya asali, na mabwawa ya maziwa.
 
Nadhani hufuatilii post au uwezo wa kuzielewa unaleta tabu.
Kama Zanzibar hawabaguani kwanini wapemba wanasema si sehemu ya unguja na wamepeleka madai hadi UN. Hiyo unaiita nini kwa lugha yako. Pili, Kwanini waunguja wasema mapinduzi daima, wapemba waseme hayo ni ya Nyerere na Okello?
Tatu, kwanini Waunguja waseme Wapemba hawana elimu, wapemba waseme wao ni bora kwa rangi na nywele.
Kama si CCM kulazimisha wakati huu ni lini Pemba iliwahi kutoa kiongozi, na unadhani ni kwanini.
Mimi nimesihi kote huko najua vema kauli, kejeli na dharau, ni suala la muda tu utatambua haya tusemayo

Matatizo ya kifamilia yapo katika kila jamii...Hata watoto wa familia moja kila mmoja hua anapendelea apendwe zaidi kuliko mwengine. Pamoja na yote hayo , waunguja na wapemba wamekua wakiishi kwa amani miaka yote. Mbegu za chuki zimetokea Tanganyika, na huo ulikua ni mpango maalum wa kuwagawa wa Zanzibar ili watawaliwe kirahisi.

Familia za Kipemba na Unguja zinaowana na zinaendelea kufanya hivyo mpaka sasa. Dini moja ,mila na desturi moja , tofauti sana na mnanyo jaribu kupandikiza. Wazanzibari wanamjua nani adui yao leo, kile kipindi cha kupandikiza chuki kimepita. Katibu mkuu mpya wa CCM alikwenda Zanzibar majuzi, anawambia wana CCM kama watalinda mapinduzi...Hapo hapo,amesahau kama wazanzibari kama wamshachoka na kauli zisizo na manufaa kwao. Waandishi wa habari walitaka kumuliza masuala ya katiba na kuhusu kura ya maoni, amekimbia na kukwepa masuala. Hii ndio sura yenu. Kile cha moyoni mnakificha, lakini sio zama hizi tena. YOU CAN FOOL SOME PEOPLE SOMETIMES ,BUT CAN NOT FOOL ALL THE PEOPLE ALL THE TIMES...
Kuhusu kauli za nani ana elimu nani hana ...hayo ni maongezi ya mitaani hayana ugomvi wala chuki kama wewe unavyotaka tuamini. Ni sawa ya hapa Tanganyika ya mazaramo kumtania mnengereko kila mmoja anaona yeye mjanja lakini hapigani kwa hilo.
kuna THREAD MPYA , nadhani Makaimati ameiweka , jaribu kuipitia labda kama atapenda unaweza kuelewa kilio cha wazanzibar, Kuna maneno ya ambae sasa ni mwanasheria mkuu wa Zazibar. ALI OTHMAN MASOUD... NAOMBA MAONİ YAKO BAADA YA KUIPITIA.

Wanzibari wasasa sio wale wa zamani, sio muda mrefu mbivu na mbichi zitajulikana....HIZI SIO ZAMA ZA NYERERE...MPAKA KIELEWEKE.
 
Hawa wanaosema wanaonewa ni hawajui nyimbo wanazoimba. Maswali uliyoweka kuhusu Zanzibar ipi wanaitaka ni mtihani wa degree maana hawajui kuwa adui yao si Bara bali yumo miongoni mwao. Kuna kiongozi mmoja wa Znz anazunguka duniani kuungwa mkono na hoja yake si uchaguzi bali kuondoka ndani ya muungano. Asicho kijua ni kuwa yeye ana nywele za kimanga ambazo hazimruhusu kuwa kiongozi Unguja nyumbani kwa mapinduzi.

Huku mitaani naishi na wznz, hawa ni watu wa kawaida na wanaendesha maisha yao bila wasi wasi, wao muungano ni sehemu ya neema kwani wakienda bahari wanaleta pweza, wakirudi znz wamebeba viazi, watoto wanakwenda shule wanatibiwa n.k. kundi hili hawaoni Znz ya pepo yenye mito ya maziwa na asali bali Znz ya juhudi zao na fursa ya muungano.

Kuna kundi la wale waliosoma vitabu na kuamini kuwa Znz ya enzi hizo ilikuwa ni bora sana, znz ya sultani kwani tende, halua na mchele vilipatikana bure kutoka uarabuni. Kundi hili linaungwa mkono na wafanyabiashara kutoka uarabuni wanaotaka kurejesha usultan kwani nao wanatamani zama za usulatan wao a.k.a znz yao.

Na mwisho, ni kundi la hawa walioko nje. Wanaamini wana elimu sana ya kuweza kugeuza Znz kuwa kisiwa cha matunda, maziwa na asali. Wanaamini kuwa kwa vile wanaweza kuongea kiingereza hiyo ni elimu tosha inayoweza kuleta mabadiliko, na kuondoka katika muungano ni fursa yao kuwa mawaziri na makatibu wakuu. Ndio wanaoonekana katika internet, lakini waulize maswali mawili au matatu, hawana majibu ila matusi, kashfa(mzalendo.net), wao imani yao imejikita katika mafuta, misaada kutoka uarabuni na wanathubutu hata kusema Mzanzibar hahitaji visa kuingia Oman! yaani visa ya Oman ni kitu muhimu sana kwa maisha yao.

Wapeleke mswaada wa kura ya maoni ili warudishe nchi ya neema, nchi ya kusadikika, yenye mito ya asali, na mabwawa ya maziwa.

Huwezi kuwa na uwezo wa kumtawala mtu mwengine wakati wewe mwenyewe hujimudu...it is about time...harakati zinaendelea vizuri.
mwisho wa yote mtaelewa,gharama zitawashinda. ZANZIBAR MUST BE FREE....HIZI SIO ZAMA ZA NYERERE ...MPAKA KIELEWEKE.
 
Matatizo ya kifamilia yapo katika kila jamii...Hata watoto wa familia moja kila mmoja hua anapendelea apendwe zaidi kuliko mwengine. Pamaja na yote hayo , waunguja na wapemba wamekua wakiishi kwa amani miaka yote. Mbegu za chuki zimetokea Tanganyika, na huo ulikua ni mpango maalum wa kuwagawa wa Zanzibar ili watawaliwe kirahisi.

Familia za Kipemba na Unguja zinaowana na zinaendelea kufanya hivyo mpaka sasa. Dini moja ,mila na desturi moja , tofauti sana na mnanyo jaribu kupandikiza. Wazanzibari wanamjua nani adui yao leo, kile kipindi cha kupandikiza chuki kimepita. Katibu mkuu mpya wa CCM alikwenda Zanzibar majuzi, anawambia wana CCM kama watalinda mapinduzi...Hapo hapo,amesahau kama wazanzibari kama wamshachoka na kauli zisizo na manufaa kwao. Waandishi wa habari walitaka kumuliza masuala ya katiba na kuhusu kura ya maoni, amekimbia na kukwepa masuala. Hii ndio sura yenu. Kile cha moyoni mnakificha, lakini sio zama hizi tena. YOU CAN FOOL SOME PEOPLE SOMETIMES ,BUT CAN NOT FOOL ALL THE PEOPLE ALL THE TIMES...
Kuhusu kauli za nani ana elimu nani hana ...hayo ni maongezi ya mitaani hayana ugomvi wala chuki kama wewe unavyotaka tuamini. Ni sawa ya hapa Tanganyika ya mazaramo kumtania mnengereko kila mmoja anaona yeye mjanja lakini hapigani kwa hilo.
kuna THREAD MPYA , nadhani Makaimati ameiweka , jaribu kuipitia labda kama atapenda unaweza kuelewa kilio cha wazanzibar, Kuna maneno ya ambae sasa ni mwanasheria mkuu wa Zazibar. ALI OTHMAN MASOUD... NAOMBA MAONİ YAKO BAADA YA KUIPITIA.

Wanzibari wasasa sio wale wa zamani, sio muda mrefu mbivu na mbichi zitajulikana....HIZI SIO ZAMA ZA NYERERE...MPAKA KIELEWEKE.

Umesema Ukweli Mkuu nakuunga Mkono sasa kwa maelezo yako wataka iweje? Muungano uvunjike au La?
 
Hakuna Zanzibar nje ya Muungano! Nakumbuka kisa cha binti kumwambia mamaye kua "ungechelewa ningekuzaa"...
 
Umesema Ukweli Mkuu nakuunga Mkono sasa kwa maelezo yako wataka iweje? Muungano uvunjike au La?

Serikali tatu au Muungano na ufe....enough is enough...

HIZI SIO ZAMA ZA NYERERE....MPAKA KIELEWEKE
 
hakuna zanzibar nje ya muungano! Nakumbuka kisa cha binti kumwambia mamaye kua "ungechelewa ningekuzaa"...

hakuna tanzania nje ya muungano!!!wazanzibari wakifanikiwa kuvunja muungano jina la tanzania litakufa na mutabakia na jina lenu halisi la tanganyika...zanzibar itabakia kuwa jamhuri ya watu wa zanzibar DAIMA NA MILELE
 
images

Zanzibar Prime Minister Mohamed Shamte
at United Nation Conference in New York 1963

ZANZIBAR NATIONAL FLAG AFTER INDEPENDENT 1963
images



Hayo ndio Wazanzibar wanayoyataka,kurudisha hadhi ya nchi yao na dola yao huru...

Dont force them to support the fake Union, is their right to decide what to do on their country, let them free dont frightening them because of your
Military rule!!! Give them chance like South sudan...Peace
 
Ndugu yangu Mwanakijiji mimi najua unachokiuliza na jibu lake ni zile nchi mbili zilizoungana zinazoitwa Checkslovakia hili ndio jibu lako.
We cant wait to see Tahriri square ya Tanzania kama inayoanza kugonga mlango kule Kampala kusafiri ziwa Tanganyika to Tanganyika hii ndio nchi wanayo i dream wazanzibari for sure, Historia haifutiki kama tunavyojifunza historia nyengine duniani, kuanzia Russia to Yugoslavia na leo changes zimeingia Bara Arabia as well ingawa Western wanajaribu kuuzuia upepo wa magauzi kulinda Falme za warabu lakini historia zinabadilika kwani hata Falme za Kiafrika zilizobaki
huko Uswazi zimepata upepo japo kidogo na Mwambao wa Afrika Mashariki upepo wa mageuzi umeingia before bara Arabia Arabia ndio kuna mtu alisema no matter what CCM ikashinda uchaguzi wa 2010 upinzani wa Slaa hauzuliki utaendelea hata nje ya bunge na CCM watajivua magamba yote lakini upinzani hau8zuliki na tusbiri tuone CCM kama haitafikia kama ilivyo KANU leo kule Kenya.
 
hakuna tanzania nje ya muungano!!!wazanzibari wakifanikiwa kuvunja muungano jina la tanzania litakufa na mutabakia na jina lenu halisi la tanganyika...zanzibar itabakia kuwa jamhuri ya watu wa zanzibar DAIMA NA MILELE

Dah, napata taabu kidogo kujadili, nahisi kama nimeingia mzalendo.net.
Anyway, hivi jina lina uhusiano gani kiuchumi,kisiasa au kiutamaduni. Kwamfano Tanganyika ikibadili jina na kuwa Tanga then so what.
Burma wanajiita jina jipya inawasaidiaje. Hata sasa hivi Tanzania ni Tanganyika kwasababu Zanzibar haijiiti Tanzania ikiwa ni pamoja na ninyi wachangiaji.

Tafadhali kama huna hoja za kufikirisha, rejea mzalendo.net kwasababu JF inakuwa level ya juu kidogo. Usishushe hadhi ya mjadala kwa hoja rojo rojo. Please

Takashi
Serikali tatu au Muungano na ufe....enough is enough...

Serikali tatu zishughulikie nini? ni mambo gani unadhani seriakali ya shirikisho inapaswa kuyashughulikia, fafanua kwasababu neno tatu halijatusaidia kukuelewa.

My take: Post zilizopita nimewahi kusema wazanzibar wanataka Tanganyika irudi ili wajenge hoja kuwa tuwe na shirikisho tofauti na unafiki wa kusema eti wanataka Tangnayika kwani ndiyo inawashikilia. Sasa wanakuja na siri tuliyoijua mapema.
Tanganyika haihitaji maoni, mzigo wa muungano upo kwa Wznz, kuamua kunyoa au kusuka.
Serikali tatu hapana hadi watakaposema mambo gani yawe ya seriakali tatu kwanza.
Serikali tatu ni kubebesha mzigo bara kwasababu wao watachangia nini kwa bajeti ya bilioni 500.
Serikali tatu maana yake kuwasaidia kwa yale wanayonufaika ndani ya muungano.

Kura ya maoni ndiyo itaamua hatma ya nchi ya matunda, asali na maziwa Zanzibar.
 
Back
Top Bottom