Baada ya mjadala kuvurugwa kwa hoja za madanguro kutoka kwa wenzetu waliokosa uvumilivu au ustaarabu, leo nimepita katika gazeti moja na kukuta habari ifuatayo ambayo inaunga mkono hoja niliyowahi kutoa. Inaunga mkono kwasababu imetolewa na mwana mapinduzi ambyae indirectly amikiri faida ya muungano. Soma.
Elias Msuya
MUASISI wa Mapinduzi ya Zanzibar, Hassan Nassoro Moyo, ameitaka serikali kuruhusu wananchi kujadili muundo wa muungano, ili waamue mustakabali wake.
Akizungumza kwenye mahojiano maalum nyumbani kwake jana, Fuoni Zanzibar, Moyo alionyesha kushangazwa na Muswada wa Marejeo ya Katiba ulioondolewa Bungeni hivi karibuni, akisema serikali inawabana wananchi kujadili mambo muhimu ya nchi yao.
Moyo anasema hayo wakati muungano huo ukiwa unatimiza miaka 47, huku kukiwa na malalamiko mengi yanayodhihirisha watu kutoridhishwa na muundo wake.
"Naunga mkono vijana wanaohoji muungano, muungano ni wao, sisi muda wetu umekwisha, wananchi wana haki ya kuhoji uhalali wa muungano," alisema Moyo.
Alionyesha kuguswa na ibara ya 9(2) ya muswada wa marejeo ya Katiba, inayokataza wananchi kuondoa mambo muhimu kama muungano, urais, uwapo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) na mengineyo na kwamba, wananchi wasizuiwe kujadili mambo hayo.
Moyo, alikuwa Naibu Waziri wa Mawasiliano katika Serikali ya Abeid Amani Karume mwaka 1964 na baadaye Waziri wa Sheria SMZ.
"Kwa sasa serikali inafanya jitihada za kurekebisha Katiba, pia muungano utaangaliwa. Lakini sasa wamezuia mambo muhimu kuzungumziwa," alisema Moyo na kuhoji:
"Kwanini uazuie watu kujadili muungano, kwanini wanasiasa wasishiriki kwenye mchakato wa Katiba? Nyerere hakuwa Askofu wala Karume hakuwa Mufti, wote walikuwa wanasiasa na ndio waliounda muungano, kwanini wanasiasa wa leo wasiruhusiwe?"
Alisema huu ni wakati wa wananchi kujadili muungano, kutoa mawazo yao na kwamba, muungano wa wakati ule ulikuwa ni wao na marehemu Karume, kizazi cha sasa kinataka kujua na kiachwe kiseme kinachokitaka.
Kuhusu mkataba wa Muungano, Moyo alisema awali ulikuwa na mambo 11, lakini yakaongezwa hadi kufikia 22, huku yote yakiwa yameingizwa na upande wa bara.
Akigusia kuondolewa madarakani aliyekuwa Rais wa SMZ, Aboud Jumbe mwaka 1983, alisema kilichomponza ni kutaka serikali tatu bila kushirikisha wenzake kwenyea Baraza la Mapinduzi.
"Mambo ya muungano yalikuwa 11, lakini yakaongezeka kufikia 22, juzi kwenye kongamano nimeambia kuwa yamefika 32 sasa na yote mmeyaleta ninyi wabara. Moja tu lililetwa na Mzanzibari na akafukuzwa kazi. Alikuwa Jumbe alipofasili mojawapo ya kifungu cha muungano," alisema na kuongeza:
"He was not wrong (Hakukosea), tatizo lake hakulishirikisha Baraza la Mapinduzi ili limtetee kwenye vikao."
Kuhusu mgawanyo rasilimali, Moyo alisema mkataba wa awali haukuzungumzia ushirikiano wa rasilimali, kama vile mafuta kuwa chini ya muungano, bali yaliwekwa na Bunge.
Pia, Moyo alisikitishwa na kitendo cha Serikali ya Muungano kulipisha kodi bidhaa zitokazo Zanzibar, akisema kimeua biashara visiwani humo
My Take
Suala la kujadili muungano kama lilivyowasilishwa katika muswada limepingwa na pande zote na wananchi wametaka kila kitu kijadiliwe bila masharti, hili si la Znz bali wote, tofauti ni kuwa huku bara limepingwa kwa hoja na Visiwani oops! Znz limehusisha tafrani na jazba.
Kilichomuondoa jumbe ni hicho cha serikali tatu, lakini Moyo ni mnafiki akisema baraza la mapinduzi halikushirikishwa! Si kweli, Jumbe nje ya madaraka amekaririwa akisema alisalitiwa na wenzake ndani ya baraza. Yeye kama kiongozi alikuwa anaongoza move, wenzake akiwemo Moyo wakamsaliti alipoitwa kuhojiwa. Kwa hasira za usaliti hajashiriki shughuli za baraza la mapinduzi na amesema hataki heshima siku mwenyezi akiamua vinginevyo.
Aliyevujisha habari za move ya Jumbe ni Mroho mmoja ambaye leo yupo madarakani.
Cha kushangaza ni huyu huyu msaliti ndiye amekuwa anapita duniani kusema muungano unawaonea Wznz. Nia yake ni kuwa rais na kukidhi haja yake na si muungano au serikali tatu kama alivyotaka Mzee Jumbe.
N.Moyo na msaliti mwenzie wote walimsaliti mzee Jumbe, asitake kusingizia kitu kingine.
Nassoro Moyo na Mzee Thabiiti Kombo Jecha wote walikuwa maswahiba wa Nyerere leo ushujaa wa kuongelea ubovu wa muungano anautoa wapi, aache kizazi kiamue bila kuingiza fitna akijua fika kilichotokea akiwa kiongozi.
Kuhusu rasilimali sijui kama mzee anajua maana yake halisi au anataka kujenga hoja kwa kutufanya mazuzu. Ujumbe anaotaka kuusema hapa ni kuwa mafuta kama yapo si ya muungano, lakini hajasema resource nyingine kwa kujua huenda zikaigusa Znz. Kama mafuta ni ya wznz ni haki yao lakini wawe wakweli na kwa rasilimali zingine pia.
Mkondo wa umeme kwenda ZNZ umegharamiwa kwa msaada na mkopo ambao Mtanganyika ameulipia bila manufaa,znz inapopata umeme rahisi na bila mgao ukilinganisha na mkazi wa kidatu wapi iliandikwa katika mambo 11 au 22 au 32. Angesema kama hayo mafuta yapo ni ya znz, period! asilete hoja kwa unafiki.
Mwisho, amekubali kuwa kuweka kodi tu kumeua biashara znz. Nimeeleza huko nyuma kuwa kwa vyovyote iwavyo Tanganyika ina impact kubwa sana katika uchumi wa ZNZ nikashambuliwa kwa kejeli na kashfa, sasa nauliza kama Tanganyika inaweka kodi kwanini wasifanye biashara na mauritius, Kenya, Uganda ili kukwepa kodi za bara kama wachangiaji wengi walivyosema huko nyuma.
Kama Nassoro Moyo amekubali hili basi namshukuru sana kwa kunitetea kuwa uchumi wa Znz based on the geo- position, social and cultural interaction una uhusiano mkubwa sana na Tanganyika na kwamba hata ikijitenga leo hilo halita epukika, ambaye anakataa ukweli huu asinijibu mimi amjibu Mzee Moyo, mwanampainduzi, waziri, na kiongozi.