Ni uhaini - as simple as that!

Ni uhaini - as simple as that!

nadhani I will be the last person kusapoti muungano uliojaaa malalamiko yaliyopitiliza .....ht mke/mume akionekana haridhishwi na ndoa mliyofinga bora umuache tuu..maana ukijifanya kumbembeleza anakupotezea muda wa kufanya majukumu yako mengine...kila siku mtajadili kero..ukisovu moja anakuja na mpya..ooops .....kuungana na mlalamishi ni KERO Na upotevu wa muda......nadhani hkukufanyika research kabla ya maamuzi haya....ooops naboreka sana
mix with yours

Sidhani kama kuna mtu anaungangania Muungano, na hata ukiforce uwepo, unakuwa hujawatendea haki wasio utaka, hapa kinachozungumzwa, haki ifuatwe, maana isije ikawa wasitaka muungano ni wachache kuliko wengi wanaoutaka, hapa hoja ilikuwa iende kwenye bunge la JMT na hapo ndio wangeamua ama kuitisha kura ya maoni ama njia yoyote nyingine inayofaa kuupima huu Muungano na kama haiwezekani basi uvunjwe

hapo juu naona unazungumzia habari za ndoa, nadhani hata wewe ukitaka kuachana na mkeo/mmeo kuna utaratibu wa kufuata ili ijuliknae kuwa mmeachana, uwezi kukurupuka na kusema umemwacha mtu bila kufuata utaratibu (Usuruhishi na mwisho taraka)
 
Sidhani kama kuna mtu anaungangania Muungano, na hata ukiforce uwepo, unakuwa hujawatendea haki wasio utaka, hapa kinachozungumzwa, haki ifuatwe, maana isije ikawa wasitaka muungano ni wachache kuliko wengi wanaoutaka, hapa hoja ilikuwa iende kwenye bunge la JMT na hapo ndio wangeamua ama kuitisha kura ya maoni ama njia yoyote nyingine inayofaa kuupima huu Muungano na kama haiwezekani basi uvunjwe

hapo juu naona unazungumzia habari za ndoa, nadhani hata wewe ukitaka kuachana na mkeo/mmeo kuna utaratibu wa kufuata ili ijuliknae kuwa mmeachana, uwezi kukurupuka na kusema umemwacha mtu bila kufuata utaratibu (Usuruhishi na mwisho taraka)

Mie nafikiri ni non sense kuitisha kura za maoni kwa pande zote, Hata hiyo sheria ya kwamba inayosema 2/3 ya wabunge wa bara na 2/3 ya wawakilishi ndo muungano uvujike kwa akili ya kawaida kabisa ni kipengele ni hicho ni mufuuuu wala hakina mshiko wa kuki kilejea na kukiita kilejeo mama.

Binafsi sina uelewa na sheria hata kidogo , lakini kwa kweli nimewashangaa sana wanasheria wetu waliobobea kujenga hoja zao kulingana na kifungo hicho.
 
Sidhani kama kuna mtu anaungangania Muungano, na hata ukiforce uwepo, unakuwa hujawatendea haki wasio utaka, hapa kinachozungumzwa, haki ifuatwe, maana isije ikawa wasitaka muungano ni wachache kuliko wengi wanaoutaka, hapa hoja ilikuwa iende kwenye bunge la JMT na hapo ndio wangeamua ama kuitisha kura ya maoni ama njia yoyote nyingine inayofaa kuupima huu Muungano na kama haiwezekani basi uvunjwe

hapo juu naona unazungumzia habari za ndoa, nadhani hata wewe ukitaka kuachana na mkeo/mmeo kuna utaratibu wa kufuata ili ijuliknae kuwa mmeachana, uwezi kukurupuka na kusema umemwacha mtu bila kufuata utaratibu (Usuruhishi na mwisho taraka)[/QUOTE]

hoja ya kukurupuka inatoka wapi?
mix with yours
 
Huu muungano ni suala la muda tu kuvunjika. La sivyo gharama za kuug'ang'ania zitakuwa kubwa. Kilichopo sasa hivi ni kutegeana tu nani aanzishe move za kuuvunja na kuuvunja kikweli.a

Hahahaahaaa na kwa sheria ya dual citzenship sijui itakuwaje ukivunjika Wazenj wataqualify kuwa watanganyika lakini watanganyika hawataqualify kuwa wazenj?
 
Endapo marekebisho haya ya Katiba ya Zanzibar yatapitishwa na Baraza la Wawakilishi, basi ndiyo sauti ya Wazanzibari. Cha msingi hapa ni kuiangalia Katiba ya Jamhuri ya Muungano ifanyiwe marekebisho stahili ikiwa ni pamoja na kuitambua Tanganyika kama nchi iliyoungana na Zanzibar kuunda JMT. Wanasheria mchemke.
 
Hakuna mtu yeyote anayetaka kuwa mhaini. There is the Union of Tanganyika and Zanzibar. And there was also the Soviet Union. But what happenned to the Soviet Union? It disintegrated. Did it disintergrate because of Ronald Reagan? No,it disintergrated because The Russians were trying to be too clever for themselves. It disintergrated because of the Stalinist policies of arresting 1000 people every day to safeguard the Union.
Kwa hiyo mazungumzo yoyote ya kusema ya kutaka kudumisha Muungano bila kuzingatia Justice,hayafai. Kweli,we should be diplomatic in our dealings with other countrries,but ruthless in dealing with Kilimanjaro Region if it wants to secceed,but there must be Justice.
 
correction,

If Kilimanjaro Region wants to secede[ not secceed],we should use force.
 
"As President of Tanzania it is my duty to safeguard the integrity of the United Republic. But if the mass of the people of Zanzibar should, without external manipulation, and for some reason of their own, decide that the Union was prejudicial to their existence, I could not advocate bombing them into submission. To do so would not be to defend the Union. The Union would have ceased to exist when the consent of its constituent members was withdrawn. I would certainly be one of those working hard to prevent secession, or to reduce its disintegrating effects. But I could not support a war on the people whom I have sworn to serve - especially not if the secession is preceded by a rejection of Zanzibaris by Tanganyikans.

Similarly, if we had succeeded in the 1963 attempt to form an East African Federation, or if we should do so in the future, Tanzania would be overjoyed. But if at some time thereafter the vast majority of the people of any one of the countries should decide - and persist in a decision - to withdraw from the Federation, the other two countries could not wage war against the people who wished to secede. Such a decision would mark a failure by the Federation. That would be tragic; but it would not justify mass killings." - (Julius K. Nyerere, "Why We Recognised Biafra," in The Observer, London, April 28, 1968; reproduced in Colin Legum and John Drysdale, eds., Africa Contemporary Record: Annual Survey and Documents 1968 - 1969, London: Africa Research Ltd., 1969, pp. 651 - 652. Nyerere's entire article in The Observer is also reprinted in Godfrey Mwakikagile, Nyerere and Africa: End of an Era, pp. 276 - 278).
 
Kwani shida iko wapi?
Waacheni wajipangie ya kwao.
Hakuna lenye mwanzo lisilo na mwisho!
tuliungana na waganda,wakenya na kikawaka,kila mmoja akaishi kivyake na tena poa kabisa.
Iweje hawa wameanza mchakato wa mambo zao mnaanza, ooh wahaini,katiba na makorokocho kibao.
kwani EAC haikuwepo KATIBA????????
Tuache basi liende limesha waka hilo! watarudi kama tulivyorudi EAC japo nayo ina mizengwe.

Goo ZNZ gooooooooooooooooo
 
tunahitaji viongozi smart kama wakina Lincolin huko Marekani maana kama Lincolin angekuwa na hulka za Kikwete, i swear today Texas ingekuwa nchi huru! Nashangaa Kiwete yuko kimya!

GU mbona unalinganisha tembo na sungura?? Kikwete si mtu wa kulinganishwa na hata dharimu Mgabe, yeye ni yes man ni mtu anayeogopa kuchukua maamuzi magumu (unpopular decisions). Mtu yeyote ambaye hawezi kuchukua maamuzi ambayo ni unpopular hafai kuwa kiongozi, inapotokea mtu huyo ni Rais wa nchi basi ujue ni tatizo kubwa kuliko tunavyoweza kuamini... Leo hii Wasukuma wakisema wanataka wawe na serikali yao ya jimbo (Mwanza, Shy, Tbr, na baadhi ya maeneo ya Mara na Kagera) Kikwete anaweza kuridhia kwa kuogopa kuwakosea!
 
Tuliwahi kuishi na vyama viwili hapa ( TANU na ASP) huku Katiba ya JMT ikitamka kwamba Tanzania ni NCHI ya CHAMA KIMOJA hadi mwaka 1977 tuliporekebisha kadhia hiyo. Sasa ni zamu ya kuishi na "NCHI" mbili ndani ya Katiba ya JMT.
Viongozi wetu wa kitaifa wanaapa huku wameshika Quran au Biblia badala ya KATIBA. Nadhani ndio maana wanashindwa kuilinda na kuitetea kikamilifu ingawa wanatamka hivo. Tunao pia wanasiasa wengi tu wanaoteuliwa/chaguliwa huku hawaijui kabisa ya JMT.
 
"Mtazamaji
Huu muungano ni suala la muda tu kuvunjika. La sivyo gharama za kuug'ang'ania zitakuwa kubwa. Kilichopo sasa hivi ni kutegeana tu nani aanzishe move za kuuvunja na kuuvunja kikweli"

Hatua ya kwanza katika safari ya kuvunja muungano imechukuliwa na baraza la wakilishi na inaonekana serikali ya muungano imestukizwa na hii inadhibitisha dhamira ya viongozi wa zanzibari .Ni jukumu la serikali ya muungano kusoma alama za nyakati na kutowabembeleza wazanzibari waache waende na safari yao na tubaki tanganyika yetu ambayo ni kubwa sana na hatuna sababu ya kuking'ang'ania kisiwa cha zanzibari.
 
Mengi yamesemwa hapa jamvini kuhusu huu Muungano na Katiba,
mimi nafikiri sehemu kubwa ya Watanzania walikuwa hawajazaliwa
wakati Muungano huu ulipoasisiwa tarehe 24 April, 1964.

Wengi wetu tumesoma katiba na maandishi kadhaa kuhusu Muungano
huu, wananchi wanahaki ya kujadili na kukarabati kwa kutumia wawakilishi
wao kwenye vyombo vya kutunga sheria kama wanaona kuna jamabo
la kurekebishwa kwa manufaa ya wengi.

Sioni tatizo kama wawakilishi walitumia nia ya dhati kurekebisha vifungu
vya katiba ya Zanzibar kama itawaletea manufaa Watanzania.
Tafsiri isitupotoshe muungano utakuwepo tu kwa miaka mingi ijayo, kwa
sababu huu haukuanzia tarehe 24 April 2010. ukisoma historia utaona jamii
ya Tanganyika na Zanzibar ilikuwa pamoja hata kabla mipaka kuwekwa
na wakoloni.

Tatizo jengine wengi humu jamvini hawajaisoma katiba ya Jamhuri ya muungano wa
Tanzania na ile ya Zanzibar lakini wanashabikia kiupofu upofu tu kama mchezo ambao
unachezwa lakini huelewi kanuni za huo mchezo iwe football, baseball, basketball, tennis,
golf kama huelewi nini kinachezwa huwezi hata kujua magoli au points zinapatikana vipi.

Tutenge wakati wa kusoma katiba zetu ili tukichangia tuwe na vitu vya maana vya kujadili.
 
Ilianza bendera, ikaja shirikisho la mpira, ikaja rasilimali za mafuta, ikaja hoja toka pemba kuhoji uhalali wa muungano wao na unguja...... listi inaendelea....
 
Mengi yamesemwa hapa jamvini kuhusu huu Muungano na Katiba,
mimi nafikiri sehemu kubwa ya Watanzania walikuwa hawajazaliwa
wakati Muungano huu ulipoasisiwa tarehe 24 April, 1964.

Wengi wetu tumesoma katiba na maandishi kadhaa kuhusu Muungano
huu, wananchi wanahaki ya kujadili na kukarabati kwa kutumia wawakilishi
wao kwenye vyombo vya kutunga sheria kama wanaona kuna jamabo
la kurekebishwa kwa manufaa ya wengi.

Sioni tatizo kama wawakilishi walitumia nia ya dhati kurekebisha vifungu
vya katiba ya Zanzibar kama itawaletea manufaa Watanzania.
Tafsiri isitupotoshe muungano utakuwepo tu kwa miaka mingi ijayo, kwa
sababu huu haukuanzia tarehe 24 April 2010. ukisoma historia utaona jamii
ya Tanganyika na Zanzibar ilikuwa pamoja hata kabla mipaka kuwekwa
na wakoloni.

Tatizo jengine wengi humu jamvini hawajaisoma katiba ya Jamhuri ya muungano wa
Tanzania na ile ya Zanzibar lakini wanashabikia kiupofu upofu tu kama mchezo ambao
unachezwa lakini huelewi kanuni za huo mchezo iwe football, baseball, basketball, tennis,
golf kama huelewi nini kinachezwa huwezi hata kujua magoli au points zinapatikana vipi.

Tutenge wakati wa kusoma katiba zetu ili tukichangia tuwe na vitu vya maana vya kujadili.


Sipendi kupoteza saaana muda na kusoma jambo ambalo halina tija tena....hawataki ndoa hii basi! inatosha tugange yetu jamani
mix with yours
 
Mkjj,

..toka 9th Dec 1961 na kabla hatujaungana na Zenj tulikuwa na Tanganyika yetu.

..wa-Tanganyika hatukuwa na tatizo kabisa kujivua utaifa wetu na kuungana na wenzetu wa-Zenj. tatizo ni kwamba ndugu zetu wa-Zenj wamegoma.

..kwa hali ilipofikia sasa hivi na huko tunakoelekea hatuna jinsi isipokuwa tu kukubaliana nao na kurudisha Tanganyika yetu.

..kama kuna wanaoona kuitwa wa-Tanganyika ni matusi na dharau, basi wapendekeze jina jipya la nchi yetu, lakini wa-Zenj wameamua kwamba hawatakuwa na sisi.

Kwa vile sisi hatujaukana utanzania basi hata Muungano ukivunjika tubaki na jina letu Tanzania na wenzetu Zanzibar. Itatupunguzia usumbufu.

Amandla........
 
Waliobadilisha Katiba mwaka 1977 wakati huo wakiongozwa na Nyerere hawakuwa WAHAINI???????
 
Kujaribu kuvunja Jamhuri ya Muungano kwa kisingizio chochote kile cha kisiasa ni uhaini. Mnaweza kutafuta kura na support ya wapiga kura lakini ukweli ni kuwa kuna nchi moja ambayo ni Jamhuri ya Muungano ambayo imetokana na kuungana kwa nchi mbili huru za Tanganyika na Zanzibar.

Jaribio la upande mmoja kuirejesha kinyemela nchi iliyokwisha ungana na nyingine ni kutangaza secession kutoka kwa Muungano na viongozi wote wanaopanga kufanya hivyo ni wa kutiwa pingu.

Sijawahi kufikiria kusema JWTZ liangalia ulinzi wa Katiba lakini wakati huu endapo mabadiliko yanayopendekezwa Zanzibar yatafanyika ni wakati wa kuwaangalia hawa "maadui wa ndani".

Ati wenyewe wamekaa kupitisha mabadiliko ya Katiba ya Zanzibar ili kipengele kimojawapo kisomeke hivi:

Wenyewe wanashangilia!! Lakini wanasahau kabisa waliapa kulinda Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayosema (msisitizo wangu):
na Magenius wetu hawaoni tatizo hapo: Je hii ni chemsha Bongo? Hivi ukisoma katiba hizo mbili utaelewa kuna nchi "ngapi"? Hivi hata hesabu za seti hawazielewi masikini wa Mungu au somo la mantiki linahitaji kufundishwa kuanzia darasa la kwanza?

Kama a. Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo "LOTE" la Tanzania bara na eneo "LOTE" la TAnzania Zanzibar, sasa Zanzibar ina ENEO GANI ambalo si sehemuya Eneo la Jamhuri ya Muungano? Kama seti moja inahusisha wanyama wote wa mwituni na seti nyingine inauhusisha simba na chui ambao nao ni wanyama wa mwituni, inakuwaje mtu anaanzisha seti nyingine inayosema "wanyama wa mwituni"?


Wanachezea maneno lakini maneno yana maana. Na miye natumia nasema kinachofanyika ni uhaini... (mnaweza kutafuta namna nyingine ya kulikwepa neno hilo). Lakini wataalamu wetu hawa hawa wanasahau Ibara ya 28:3 ya Katiba (waliyoapa kuilinda) inasema nini:

(

Halafu kama watu wasiojua Katiba wanasahau Katika ya Muungano inasemaje kuhusu wakuu wa mikoa. Katiba inasema hivi:



sasa magenius wetu wa Zanzibar wameamua kumnyang'anya madaraka Rais wa Muungano ya kushiriki uteuzi wa wakuu wa mikoa ya Zanzibar kama Katiba ya Muungano inavyotaka na kina Werema wamekaa na tai zao wanachekelea!


Sasa hawa wahuni wa Zanzibar wamepata wapi ujasiri wa kuridhia kuligawa taifa na kutengeneza nchi nyingine nje ya hii NCHI moja? Kuna njia moja tu ya kuunda Nchi ya Zanzibar- KUJITOA kwenye MUUNGANO. Nje ya hapo ni UHAINI!!!



I couldn't be more blunt than that.

Labda nikumbushie sehemu kidogo tu ya hotuba ya Baba wa Taifa kwenye Bunge lililoridhia Muungano Aprili 25, 1964 (msisitizo wangu):

Ooh how prophetic!!!

I'm standing on guard, by CHOICE!
Wazanzibari muda mrefu wamekua wakitaka muungano ufanyiwe marekebisho na kero za muungano zitafutiwe ufumbuzi, lakini Watanganyika wemekuwa wakiwapuuza wazanzibari kwa muda wote ...Sasa mimi si shangai kuona wameanza kufanya yale ambayo wao wana weza bila ya Tanganyika... Hii kasumba tuliyokuanayo sisi ya kuwaona waZanzibari vijitu kidogo kwahiyo sisi ndio tuamue kila kitu mapaka nani awe Rais wa Zanzibar...Vukuto la kisiasa liko muda mrefu Zanzibar, mimi sishangai kuano tumefikia hapa... na kama tunataka ukweli ni kwamba option ya kujitoa katika muungano kwa upande mmoja wa muungano ilikuwapo tangu kuanzishwa kwa huu muungano...Sina haja ya kunukuua kauli za Nyerere nyinyi mnazielewa... Senegal na Gambia ziliungana na baadaya Gambia kuona inakandamizwa walijitoa katika muungano wao na Senegal aliokua ukiitwa SENEGAMBİA.... Hizi kasumba zimeshapitwa na wakati na mwenyewe Nyerere hayupo tena hapa... Kwanini tuishikilie Zanzibar wakati hapa Tanganyika hatuna lolote, Mtwara kunahitaji maendeleo na ni sehemu ya Tanganyika sio Zanzibar...:confused2:
 
GU mbona unalinganisha tembo na sungura?? Kikwete si mtu wa kulinganishwa na hata dharimu Mgabe, yeye ni yes man ni mtu anayeogopa kuchukua maamuzi magumu (unpopular decisions). Mtu yeyote ambaye hawezi kuchukua maamuzi ambayo ni unpopular hafai kuwa kiongozi, inapotokea mtu huyo ni Rais wa nchi basi ujue ni tatizo kubwa kuliko tunavyoweza kuamini... Leo hii Wasukuma wakisema wanataka wawe na serikali yao ya jimbo (Mwanza, Shy, Tbr, na baadhi ya maeneo ya Mara na Kagera) Kikwete anaweza kuridhia kwa kuogopa kuwakosea!
Zanzibar sio sehemu ya Tanganyika na haitokua sehemu ya Tanganyika milele.... usitoe mifano ya kulinganisha Mbwa na paka...
 
Back
Top Bottom