MKKJ,
Nina wasi wasi kuna mtu kavamia ID ya Mwanakijiji, na anaongea kama mlevi, anapayukwa payukwa tu, hatujuwi hasa anasimama na hoja ipi na ipi ana kataa. Tunaomba kama kuna mtu kaivamia ID ya Mwanakijiji atupe nafasi...asimtie aibu...mwenyewe kwa maongezi yasiyoeleweka eleweka.
Hapo juu kwenye post 113 unakataa kuwa hujawahi kusema Zanzibar lazima iwe kwenye muungano...wakati thread yako inakusuta kwa kauli za "tutaulinda kwa gharama yoyote", "jeshi lichukuwe hatua" n.k...na jazba,chuki na nongwa kwa Wazanzibar unaiyonesha wazi wazi kwa sababu tu kwa umoja wao wamekubali mabadiliko ya muundo wa serikali yao na hadhi yake katika muungano.
Mkuu unayejiita Mwanakijiji(siye yule ninayemfahamu kuwa mtu muelewa wa mambo), inaonyesha neno "jamhuri ya muungano" kwa kiswahili cha kusini ya Tanzania linamaanisha siku zote "nchi moja", unasahau neno kama 'muungano' linaashiria kitu zaidi ya kimoja, kwa muktadha wetu ni nchi/jamhuri mbili ambazo ni Tanganyika na Zanziabar.
Mabadiliko tuliyoyafanya wazanzibar wengi wetu (wahuni, maadui kama ulivyotuita) ni kuainisha tafsiri sahihi ya neno "jamhuri ya muungano" ambao ni wa nchi mbili ambazo kabla ya 1964 kila moja ilikuwa na "jamhuri" yake.
Kinachokufanya uwashwe sijuwi nini tena. Acha jazba na chuki zako kwa wazanzibar, sisi si mazuzu kama nyinyi sisi tuna njaa ya mabadiliko ya kweli si ya vitabuni, nyinyi endeleeni kuabudu CCM na mizimu ya muasisi wake,sisi tushatoka huko,hatutaki kurudi tena...mnaibiwa rasilimali zenu, mnanyanyaswa na kudharauliwa na watawala halafu hao hao mnawachaguwa kwa kishindo.
Sisi hatuyataki hayo na hatua za kuyaondoa ndiyo hizo tushaanza kuzichukuwa...CUF ipo ikulu...we do'nt have to wait for another saviour...he has already come. Mda huu tunahisabu tarehe tu kuifutilia mbali CCM Zanzibar, inayolea muungano wa kidhalimu...ambao hatuutaki.