Ni uhaini - as simple as that!

Ni uhaini - as simple as that!

Tatizo la sasa hivi hatuna uongozi wa kitaifa.

Kikwete na genge lake ni watu ambao wapo kuangalia zaidi maslahi yao binafsi badala ya maslahi ya taifa letu.

Katiba inachezewa yuko kimya na kina makamba na Tambwe Hiza kuangalia namna gani ya kukabiliana na kimbunga cha Dr Slaa na vipi anaweza kusurvive katika uchaguzi ujao. It is a pity. His concern is his own survival and not the survival of Tanzania as a Nation. He is a week leader. hana uwezo wa kukabiliana na changamoto kama hizi za Wazanzibari kujitenga. Karume na seif are very strategic and they definitely know that at this time of election every one is bussy fighting for his political survival.

Kutokana na kukosekana kwa uongozi thabiti wa kitaifa mambo yataenda zanzibar kama yalivyopangwa na wazanzibari watapata kile walichokitaka. Ingekuwa ni wakati wa Nyerere Karume angechapwa viboko kama Jumbe alivyofanyiwa. Lakini sasa hakuna wa kufanya hivyo na imani yangu kuwa baada ya uchaguzi mkuu Zanzibar itaanda mpango rasmi wa kujitenga

Ni mwito wangu kwa watanzania tusirudie makosa ya nyuma kuchagua viongozi dhaifu. Hayo ndio madhara yake. Tusipoangalia hata huku bara wataanza kutugawa
 
Zanzibar ilianza kujitenga mapema tu pale walipo taka wimbo wao wa Taifa wakaja na bendera yao na hii nilihisi ingekuja kufikia hapa maana kipindi wanatengeneza wimbo wao wa Taifa (Zanzibar) ilitakiwa kpindi kile Mkapa akemee hilo but aliwaachia wakafanya kile watakacho ikaja wakatengeneza bendera ya Taifa (Zanzibar) sasa wamekuja na katiba kinachofuata itakuw ukitaka kwenda kwao (Zanzibar) unaomba visa halafu watadai nao wawekwe kwenye EA Community kama Kenya,Uganda, Rwanda na Burundi.
 
Mimi nadhani tatizo ni kwamba mfumo ulio wekwa kuendesha Muungano haukua sahihi. Wazo lilikua zuri. Wote tunajua Nyerere (R.I.P.) alikua na ndoto ya siku moja Africa kuwa nchi moja na ndiyo maana labda akaanza na jirani zetu kwa wakati huo. Sijui lini haswa mazungumzo nyuma ya pazia yalipo anza kuunganisha nchi hizo mbili lakini inaelekea ili harakishwa. Hata baada ya kuungana viongozi wetu sidhani kama wali jaribu kutengeneza mfumo permanent ambao unge dumu.

Kosa lakwanza lilikua katika nation building. Nyerere alifanya kazi nzuri ya kuondoa ukabila na udini (najua kuna watu wata pinga) lakini swala la sisi Wazanzibar na wao Wabara haliku fanyiwa kazi. Wakati Wabara wana jiona ni Watanzania kwanza Wazanzibari wengi wao wana jiona ni Wazanzibari kwanza. Ndiyo maana kuna tofauti za kihisia na kipaumbele na matokeo yake tunaona baadhi yetu tuki tetea Muungano wakati wengine wana tetea uwepo wa Zanzibar. Sisemi kuna mwenye kosa kwa kuwa hauwezi kulazimisha mtu loyalty na allegiance yake iko wapi. Simple we failed to keep every one on the same page.

Kosa la pili ni kuweka mfumo wa serikali mbili. Kwangu mimi hilo lilikua kosa kubwa sana na ndiyo iliyo sababisha point yangu ya kwanza hapo juu. Kwa vile Zanzibar wana serikali ni raisi kwao kudai maslahi ya Zanzibar na kwa vile Bara hakuna serikali ya Tanganyika hauwezi kuleta madai ya Tanganyika. Njia raisi ya kuepukana na hili ingekua kuwa na serikali moja tu ila labda kutokana na siasa labda hili swala lisinge wezekana (sijui). Kama kunge kuwa na serikali tatu basi Muungano ungesha vunjika kwa sababu "Watanganyika" wangedai haki yao na "Wazanzibar" wangedai haki yao. Sasa hivi ni upande mmoja tu unaovuta swala ambalo nalo lina madhara pia.

Miwsho kabisa ni kwamba viongozi wetu wame chelewa kudeal na hili swala. Nadhani kuna kipindi ambacho hili swala linge weza kutatuliwa hata na viongozi tu bila tatizo lolote na ndiyo maana nadhani katiba mpya is long over due na kama tuki tengeneza katiba mpya sasa hivi swala la Muungano lita kuwa very sensitive.

Sasa kwa vile tayari tupo hapa tulipo hamna haja ya kukazania sana mambo ya "what if". Sasa hivi ni muda wa kujiuliza "what now, what next". Zanzibar tayari ina move ahead na plans zake kwa hiyo hamna haja ya viongozi wa Muungano kukaa kimya. Viongozi wa pande mbili wakae chini na kila mmoja atoke na bill ya madai yake mwishoni wakae process ya debate and compromise ianze. Kama tuki shindwa kuelewana basi hatua za kuvunja huu uhusiano bila msuguano mkubwa uanze. Pamoja na kuupenda huu Muungano na kujivunia Utanzania wangu naamini kabisa kwamba hili swala halita malizwa kimabavu na lisipo tafutiwa ufumbuzi sasa ni bomu linalo ngojea kulipuka.
 
tatizo wanafikiri kuwa tunazungumza kutoka hewani tu ati tunaitakia Zanzibar mabaya; kama mazungumzo ya watu wawili leo hii (karume na seif) yamechukuliwa kuwa halali na kukumbatiwa yale ya wa Nyerere na Karume nayo yalikuwa na nguvu hiyo. Wazanzibar hawawezi kuwa na keki yao halafu waile huku wabakie nayo. Kama kuna watu Zanzibar wanataka kuwa nchi "nje" ya Muungano, waliseme hilo, kama ni kupigwa kura ipigwe na tuanze mahusiano baina ya nchi mbili.

But as long as we are a United Republic jaribio lolote la kuivunja ni uhaini - as simple as that.

Ni jukumu la kila Mtanzania (yes wapo watu wa taifa hilo) kulinda Muungano ulivyo. Hatupaswi na hatuwezi kuachii kikundi cha watu wachache kuivunja ati kwa sababu hawajisikii. Wazanzibari ambao wanajitambua kuwa ni Watanzania na wapo wengi ni lazima wakatae uhuni huu.

Kama Zanzibar haitaki kuwa ndani ya Muungano kwenye baraza la wawakilishi waseme hivyo mapema, wajitangaze kuwa wanataka kutoka nje ya Muungano na nina UHAKIKA Kikwete na uongozi wa CCM hakuna atakayeweza kujenga hoja za kuzuia kwani mashujaa hao hawapo tena. Basi watoke na kama nilivyosema tuanze uhusiano wa nchi mbili, binafsi wala sina tatizo kabisa. Lakini kama wanataka tuwe wamoja kama nchi ni lazima mpango wao wa kuitangaza Zanzibar kuwa ni nchi sijui madudu gani ukemewe mara moja na KILA MTANZANIA.

Si kwa sababu hatuwezi kuishi bila Zanzibar au wao bila sisi, bali kwa sababu MUUNGANO UPO na ni lazime utetewe kwa gharama yoyote. Kwanini Zanzibar wasipige kura ya maoni kutaka kujua kama wanataka kubakia ndani ya Muungano?

PIGENI HII KURA TUMALIZE MZIZI WA FITINA!!!

viNGINEVYO NI UHALIFU ULIOKUBUHU AMBAO ADHABU YAKE NI KIFO! Uhaini haurembuliwi macho.


Uhaini ni neno zito. Sidhani kama wamefanya yote haya bila wenzao wa Bara kuwa na habari. Kinachonitatiz mimi ni hii dhana ( ambayo kwa bahati mbaya na wewe unaiendeleza) kuwa Muungano ni sacrosant na wenye uamuzi nao ni wazanzibari peke yao. Naamini wakati umefika wa kufanya walichofanya wenzetu wa Canada na Czechoslovakia walipojikuta hapa tulipo. Ipigwe kura ya maoni (referendum) pande zote za Muungano (Bara na Zanzibar) na iwapo pande zote mbili zinataka Muungano uendelee basi uendelee kama ilivyokuwa Canada. Kama upande mmoja ( Bara au Zanzibar) ikipinga basi tutengane kwa amani kama ilivyokuwa Czechoslovakia. Kulazimishana kutaweza kutugeuza Yugoslavia nyingine.
Ni kwa referendum peke yake ndipo tutajua kama kweli kuna wazanzibari na watanzania bara wanaotaka Muungano uendelee. Huku kupulizia wakati wanauma lazima kuishe.

Hii nchi ni yetu sote na ni lazima sote tuulizwe. Tunaweza kushangaa hapo watakapokuta kuwa machogo nasi hatuutaki Muungano! Huku kutingisha kiberiti lazima kuwe na mwisho wake. Hii imani ya kuwa tuko tayari kuulinda Muungano kwa gharama yeyote ndiyo inayowapa kiburi. Watapojua kuwa hatuko tayari kumwaga damu kwa kitu ambacho ni figment ya imagination pengine watasita kabla ya kufanya upuuzi huu. Wasitugeuze Spain na Catalanya!

Amandla.......
 
of course.. hilo wala siyo hoja; wakitaka watangaze tu kuwa wanataka kutoka nje ya Muungano, wadai kile wanachokiita ni "uhuru". Kikwete awaruhusu kwa sababu sidhani kama ana uwezo wa kuzuia Zanzibar kutoka nje ya Muungano. Na ninaamini guess what will happen:

Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar watatoa hoja ya kutaka kutoka nje ya muungano na kupendekeza kura ya maoni kwa Wazanzibar wapige kaa wanataka kubakia ndani ya Muungano, hoja hiyo italetwa NEC (musoma au dodoma) CCM hawana watu wa kuutetea Muungano wetu na watasema endeleeni kupiga kura na mkishinda basi tunaachana "salama"..

Hili LITATOKEA! Kwani baada ya kuiweka Zanzibar kuwa ni nchi na mipaka yake kama ilivyo kwenye mabadiliko haya, kitakachofuata ni kujiuliza "je nchi yaweza kuwa sehemu ya nchi nyingine?". JIbu haliepukiki ni HAPANA.

OOH HOW I PITY THAT DAY!!

MMMJ,
Tukumbuke pia viongozi wengi wa CCM bara wana malengo yao 2015,ambapo kwa ukweli na haki ilipaswa Rais atoke Zanzibar hivyo wao watashangilia ZNZ kujitoa ili matakwa yao yatimie maana hakutakuwa na haja tena ya kuwa na mgombea toka ZNZ......UBINAFSI juu yao ni bora zaidi kuliko UMMA
 
Zanzibar ilianza kujitenga mapema tu pale walipo taka wimbo wao wa Taifa wakaja na bendera yao na hii nilihisi ingekuja kufikia hapa maana kipindi wanatengeneza wimbo wao wa Taifa (Zanzibar) ilitakiwa kpindi kile Mkapa akemee hilo but aliwaachia wakafanya kile watakacho ikaja wakatengeneza bendera ya Taifa (Zanzibar) sasa wamekuja na katiba kinachofuata itakuw ukitaka kwenda kwao (Zanzibar) unaomba visa halafu watadai nao wawekwe kwenye EA Community kama Kenya,Uganda, Rwanda na Burundi.

Nakubaliana na maelezo yako. Wahenga walishasema kuwa dalili za mvua ni mawingu. Dalili za hawa jamaa kujitenga zilianza siku nyingi. Walishatingisha kiberiti tangu enzi za comandoo na wakajua kuwa hakijajaa na sasa wanafanya kweli. Kinachoendelea ni utekelezaji wa mpango mkakati wa kujitoa kwenye huu muungano feki ambao unalindwa kwa mabavu zaidi kuliko mantiki.

Katiba ya muungano inaweza kusema inachotaka lakini ukweli unabaki kuwa muungano huu ulikuwa ni wa nchi mbili huru yaani Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar. Ila kwa mazingaombwe ya Nyerere Jamhuri ya Tanganyika iliuliwa kinyemela na kukabakia nchi ya zanzibar ikiwa na serikali yake na baraza lake la wawakilishi na raisi wake.

Kwa maoni yangu muundo wa huu muungano wetu ndiyo udhaifu wake mkubwa na bila kurekebisha huu muundo ni vigumu kutarajia kuwa muungano huu utadumu milele.
 


Uhaini ni neno zito. Sidhani kama wamefanya yote haya bila wenzao wa Bara kuwa na habari. Kinachonitatiz mimi ni hii dhana ( ambayo kwa bahati mbaya na wewe unaiendeleza) kuwa Muungano ni sacrosant na wenye uamuzi nao ni wazanzibari peke yao. Naamini wakati umefika wa kufanya walichofanya wenzetu wa Canada na Czechoslovakia walipojikuta hapa tulipo. Ipigwe kura ya maoni (referendum) pande zote za Muungano (Bara na Zanzibar) na iwapo pande zote mbili zinataka Muungano uendelee basi uendelee kama ilivyokuwa Canada. Kama upande mmoja ( Bara au Zanzibar) ikipinga basi tutengane kwa amani kama ilivyokuwa Czechoslovakia. Kulazimishana kutaweza kutugeuza Yugoslavia nyingine.
Ni kwa referendum peke yake ndipo tutajua kama kweli kuna wazanzibari na watanzania bara wanaotaka Muungano uendelee. Huku kupulizia wakati wanauma lazima kuishe.

Hii nchi ni yetu sote na ni lazima sote tuulizwe. Tunaweza kushangaa hapo watakapokuta kuwa machogo nasi hatuutaki Muungano! Huku kutingisha kiberiti lazima kuwe na mwisho wake. Hii imani ya kuwa tuko tayari kuulinda Muungano kwa gharama yeyote ndiyo inayowapa kiburi. Watapojua kuwa hatuko tayari kumwaga damu kwa kitu ambacho ni figment ya imagination pengine watasita kabla ya kufanya upuuzi huu. Wasitugeuze Spain na Catalanya!

Amandla.......

mzee kama Bara watataka ( na mimi ni mmoja wao ambao nataka tuendelee kuungana) na Zanzibar hawataki tutafuta matakwa ya nani na kwanini?
 
Halafu wakishajitenga (assuming ndiko tutakakoishia) uraia wa Zanzibar utakuwa vipi na wa Bara utakuwa vipi kuhusu Wazanzibari walioko Bara na wa Bara walioko Zanzibar?
 
mzee kama Bara watataka ( na mimi ni mmoja wao ambao nataka tuendelee kuungana) na Zanzibar hawataki tutafuta matakwa ya nani na kwanini?

Kama Bara watataka na Zanzibar wakikataa basi tutengane kwa vile Muungano hautakuwa na ridhaa ya wahusika. Kama Bara wakikataa na Zanzibar wakitaka basi napo tutengane kwa sababu zile zile. Tuendelee na Muungano pale tu watu wa Bara na Zanzibar wote wakonyesha kuwa wanautaka. Hatutakuwa nchi ya kwanza kutengana. Ikiwa USSR waliweza ( hata bila referendum) kwa nini sisi tuogope? Kuendelea na Muungano wakati upande mmoja hautaki utatufikisha kubaya. Mfano hai ni Yugoslavia. Mwingine ni Belgium ambayo mpaka sasa haitawaliki. Ni lazima tuwe majasiri kama walivyokuwa Canada na Czechoslovakia. Mbona pamoja na kelele zao Quebec walisita walipoambiwa kama unataka kuondoka nenda na RoC?

Amandla........
 
Halafu wakishajitenga (assuming ndiko tutakakoishia) uraia wa Zanzibar utakuwa vipi na wa Bara utakuwa vipi kuhusu Wazanzibari walioko Bara na wa Bara walioko Zanzibar?

Raia wa Tanzania ya sasa watachagua uraia wanaoutaka kutokana na makazi. Wenye asili ya Zanzibar walioko Bara watachagua kama wanataka uraia wa Bara au wa Zanzibar. Vile vile wenye asili ya Bara walioko Zanzibar nao wachague uraia wanaoutaka. Pande zote mbili zilazimishwe na jumuia za kimataifa kuhakikisha kuwa wananchi wake hawanyimwi haki ya kuchagua uraia wanaoutaka bila unyanyasaji wa aina yeyote. Masharti ya uraia yawekwe wazi na yafuate misingi ya haki za binadamu inayotambulika duniani kote.

Amandla........
 
Huu ni uhaini, unapoamuamua kuchora mipaka ya nchi ndani ya nchi, ni uhaini.

Lakini hebu tujiluize, chanzo cha chokochoko ya haya yote ni nini?

Ni uroho wa madaraka wa baadhi ya watu wachache wanaokandamizwa Dodoma?
Ni ubinafsi wa baaadhi ya wa Zanzibar ambao hawapendi kuishi kwa amani ama wanaona kuwa ndani ya Muungano wanshindwa kutimiza malengo yao?
 
Kama Bara watataka na Zanzibar wakikataa basi tutengane kwa vile Muungano hautakuwa na ridhaa ya wahusika.


Lakini Watanzania bara hatujafanya lolote kuonesha kuwa haturidhiki na Muungano. Hatujadai Tanganyika kwa namna yoyote ile. Kwa hiyo hili ni suala la Zanzibar tu.


Kama Bara wakikataa na Zanzibar wakitaka basi napo tutengane kwa sababu zile zile. Tuendelee na Muungano pale tu watu wa Bara na Zanzibar wote wakonyesha kuwa wanautaka.

NI asilimia ngapi ya kura za pande mbili zitahesabika kuwa watu wanataka? simple majority au absolute majority?


Hatutakuwa nchi ya kwanza kutengana. Ikiwa USSR waliweza ( hata bila referendum) kwa nini sisi tuogope?

Ingekuwa rahisi kutengana kila watu wanapotaka Quebec ingekuwa imeshatengana na US ingekuwa imeshatengana. Ninachoona ni woga na kutotaka kugonganisha vichwa watanzania kutetea misingi ya taifa lao. Kuna aibu fulani hivi inawakumba watu kusikia wanatetea Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Urusi ilitengana lakini unadhani ndio ulikuwa mwisho wa matatizo kati yao? remember masuala ya Chechyniya na Georgia, au kuvunjika kwa Yugoslavia na mambo ya Montenegro, Sebria, Slovakia na Macedonia, Albania na Kosovo. Kutengana si mwisho wa matatizo ya mahusiano.


Kuendelea na Muungano wakati upande mmoja hautaki utatufikisha kubaya.

Hadi hivi sasa sijaona hoja hasa za "upande mmoja haziutaki" ni viongozi wahuni tu wa CCM na CUF ndio wanafanya hivi. kama waliweza kuwauliza Wazanzibari kuhusu mfumo wa serikali yao kwa kura ya maoni kwanini wasiwaulize kama wanataka au hawataki. Na uamuzi watakaochukua sisi Bara tutauheshimu.


Mfano hai ni Yugoslavia. Mwingine ni Belgium ambayo mpaka sasa haitawaliki.

Belgium inatawalika; na Yugoslavia ndio kama nilivyosema hapo juu. Lakini miungano hiyo si sawa na Watanzania. Sisi hatukuunganishwa kwa nguvu. Muungano wetu unafanana sana na wa US kuliko sehemu nyingine.

Ni lazima tuwe majasiri kama walivyokuwa Canada na Czechoslovakia. Mbona pamoja na kelele zao Quebec walisita walipoambiwa kama unataka kuondoka nenda na RoC?

Thats my point. Mimi sina hofu, lakini pia simuumini wa urahisi rahisi wa kuvunjika kwa jamhuri ati kwa sababu sehemu fulani ya jamhuri "hawataki". Ni kitu gani kitazuia watu wa Kilimanjaro kujitenga wakiamini kuwa kwa kufanya hivyo wanatetea maslahi yao ambayo wanaona hayapatikani ndani ya Muungano? Hapo si tutaweza kutumia mfano wa Sudan na Sudani ya Kusini?
 
Hivi nini msimamo wa Dr. Bilal kwenye masuala ya muungano???/
 
Raia wa Tanzania ya sasa watachagua uraia wanaoutaka kutokana na makazi. Wenye asili ya Zanzibar walioko Bara watachagua kama wanataka uraia wa Bara au wa Zanzibar. Vile vile wenye asili ya Bara walioko Zanzibar nao wachague uraia wanaoutaka. Pande zote mbili zilazimishwe na jumuia za kimataifa kuhakikisha kuwa wananchi wake hawanyimwi haki ya kuchagua uraia wanaoutaka bila unyanyasaji wa aina yeyote. Masharti ya uraia yawekwe wazi na yafuate misingi ya haki za binadamu inayotambulika duniani kote.

Amandla........

Na suala la mali zao? Na wale ambao wako Zanzibar lakini wanataka kutambulika kuwa ni raia wa Bara watafanywa nini na vice versa? Isije ikaanza kampeni ya kusafisha safisha.. like somewhere we know..
 
Na suala la mali zao? Na wale ambao wako Zanzibar lakini wanataka kutambulika kuwa ni raia wa Bara watafanywa nini na vice versa? Isije ikaanza kampeni ya kusafisha safisha.. like somewhere we know..

Suala la mali zao litenganishwe na uraia. Kuvunjika kwa Muungano hakutakuwa na maana kuwa raia wa nchi moja hawawezi kuishi katika nchi nyingine. Raia wa Zanzibar ataweza kuishi, kufanya kazi au biashara Bara kama raia mgeni mwengine yeyote na haki zake zitakuwa hivyo hivyo. Wapemba wa namanga watakaotaka kutambulika kama raia wa Zanzibar wataendelea ni lazima waruhusiwe kuendelea kuishi Bara kama wanataka ili mradi wakitimiza masharti ya uhamiaji. Watakuwa kama raia wa Kenya n.k. wanaoishi Tanzania hivi sasa. Na wanyamwezi walio Zanzibar wanaotaka kubaki na uraia wa Bara navyo hivyo hivyo. Haki yao ya kuishi Zanzibar kama raia wageni ni lazima ilindwe. Na kama wakati huo tutakuwa na uraia wa nchi mbili basi wanaotaka wanaweza kuwa na uraia wa Bara na Zanzibar. Yote haya yawekwe wazi wakati wa kampeni kuhusu Muungano. Wananchi lazima waelewe maana ya kuvunja Muungano na namna gani itakavyo-affect maisha yao ya kila siku. Safisha safisha itatokea kama Muungano utavunjika kwa mabavu kama ilivyokuwa Yugoslavia. Mbona Czechoslovakia hapakuwa na hiyo safisha safisha?

Amandla.........
 
Suala la mali zao litenganishwe na uraia. Kuvunjika kwa Muungano hakutakuwa na maana kuwa raia wa nchi moja hawawezi kuishi katika nchi nyingine. Raia wa Zanzibar ataweza kuishi, kufanya kazi au biashara Bara kama raia mgeni mwengine yeyote na haki zake zitakuwa hivyo hivyo. Wapemba wa namanga watakaotaka kutambulika kama raia wa Zanzibar wataendelea ni lazima waruhusiwe kuendelea kuishi Bara kama wanataka ili mradi wakitimiza masharti ya uhamiaji. Watakuwa kama raia wa Kenya n.k. wanaoishi Tanzania hivi sasa. Na wanyamwezi walio Zanzibar wanaotaka kubaki na uraia wa Bara navyo hivyo hivyo. Haki yao ya kuishi Zanzibar kama raia wageni ni lazima ilindwe. Na kama wakati huo tutakuwa na uraia wa nchi mbili basi wanaotaka wanaweza kuwa na uraia wa Bara na Zanzibar. Yote haya yawekwe wazi wakati wa kampeni kuhusu Muungano. Wananchi lazima waelewe maana ya kuvunja Muungano na namna gani itakavyo-affect maisha yao ya kila siku. Safisha safisha itatokea kama Muungano utavunjika kwa mabavu kama ilivyokuwa Yugoslavia. Mbona Czechoslovakia hapakuwa na hiyo safisha safisha?

Amandla.........

kwa hiyo baada ya kuundwa kwa hii nchi ya Zanzibar kutakuwa na raia wa Zanzibar vile vile au watakuwa bado ni raia wa Tanzania? Hii nchi nyingine ndani ya nchi nyingine itaweza kutoa pasi za kusafiria au kama wakitaka kuna sababu ya wa kuwakatalia kuwa hawawezi?
 
Mzee Mwanakijiji umelonga. Hii si mara ya kwanza katiba kuwa tested. Imefanyika mara nyingi. Mwalimu na hata Ben ndio viongozi waliolinda katiba na hata muungano. Sasa hivi darasa halina kiranja.
On the other hand, muungano unatakiwa uwe na faida kwa pande zinazoungana. Mimi sioni faida ( za kiuchumi) kwa Watanganyika. Sijui twanunua nini kutoka upande wa pili. Faida za kisiasa hazitupunguzii njaa. Ndio maana mkulima wa kijini hana hata time na muungano huo.
Nakubaliana nawe kuwa, kufanya mbinu hizi za kujitengea "kijinchi" ndani ya muungano ni uhaini kwa kuwa inafanya hivyo wakati katiba hairuhusu. Isipoluwa wangeleta hoja ya kuuvunja na sioni taabu binafsi. Waanzishe kinchi chao, vipasport vyao kuja Dar, tufanye biashara.. safi. Isiwe choko choko.
 
Mwanakijiji,
Kwa OMBWE la sasa la UONGOZI tulilonalo kwenye serikali ya JMT, acha Wazanzibari walitumie "kuikomboa NCHI" yao. WM Pinda alijibu vizuri sana swali lile lililokuwa limekaa kimtego aliloulizwa na Mh Hamad Rashid kwa kutumia na kunukuu KATIBA ya JMT. Siku chache baadaye JK akalijibu kihuni kwenye moja ya hotuba zake za hovyo kabisa kwamba ndani ya Tanzania, Zanzibar ni NCHI!
Tuangalie hali ilivyo kwingineko Africa na hata duniani. Sudan miaka miwili ijayo itakuwa ni nchi mbili au tatu yaani Sudan ya Kusini, DaRFUR na Sudan yenyewe. Pale Somalia tayari kuna "nchi" tatu; Puntland, Somaliland na Somalia ya Mogadishu. Mnaoijua Yugoslavia ya zamani ya Joseph Bros Tito mnajua sasa hivi kuna nchi ngapi ikiwemo Kosovo ya juzi. Hivyohivyo Chekoslovakia na nyingine nyingi. Ni vigumu mno kulizuia wimbi hili hata kama Mwalimu angekuwepo.
Kinachoudhi sasa hivi ni Wazanzibari kuivunja KATIBA yetu ya JMT KIHUNI na JK anawatazama tu nadhani anataka apate zawadi ya Mo Ibrahim. WAlichopigia kura ya maoni sicho pekee kilichopelekwa kwenye Baraza la Wawakilishi.
 
Utaifa muutetee nyie, wakitetea wengine makosa! Ama kwa hakika nyani haoni makalio yake.

Binafsi napima hili suala la muungano ktk muono wa kiuchumi, achana na falsafa na hizo sarakasi za katiba, maana katiba yenyewe haimlindi yeyote zaidi ya tabaka twawala la mazuzu wa huko bara. Katiba inasema muizi akiiba apelekwa jela, kiongozi wenu Dr. Mkwere anasema walipe lakini wasiguswe..(na hakuna utrhibitisho kama wamelipa na hamna anayethubutu kuuliza)! sasa usitake kuniambia huoni priority hapa ni nini?

Muungano haujawasaidia lolote waznz kiuchumi na hali zao zinakuwa mbaya siku hadi siku, huku mazuzu wa huko bara wakizidi kujineemesha. Sasa sioni kwanini waendelee kuwakumbatia mawakala wa ukoloni kutoka bara wakati hawana msaada wowote. Its time to call the quits, and try something better.
Mkuu usirushe changa la macho mchana kweupe ili kuficha nia ya kuvunja muungano.
Bara hawakuiunguza karafuu.
In the contrary Pemba na Unguja wanategemea by over 80% vibarua toka bara.Si bara wanaowanyima nguvu ya kufanya kazi kwa bidii.
Ukisema ajenda ya kuuvunja muungano umekaa kiuchumi zaidi basi Mkuu Abdulhalim unakosa kuwa analytical juu ya suala la Zenj.
Vema , muungano utavunjika na Zenj itajitegemea , raha mustarehe.
Naomba mafuta yapatikane, tena Pemba, ndo sarakasi ya Mpemba na Muunguja litakavyo kolea utamu.Itabidi waBara tuchague sehemu ya kuegemea.

Vile vile si uongo kuwa nyie wenzetu mnauwezo mkubwa sana wa kufikiri zaidi kwa midomo kuliko vichwa.
Pamoja na ukweli kuwa nia ya kujitoa muungano ndo ajenda muhimu kwa wazanzibari, Bara tutakuwa tuna fanya makosa kuwazuia.Wao wanafikiri Bara tunafaidi sana na huu muungano, kitu ambacho si kweli-actually Zanzibar ni MZIGO.
Scenario inayofuata ni
MOSI, hisia kali za kurudisha UTANGANYIKA kwa Bara.
PILI, huuko Zanzibar Upemba na Uunguja utaanza kuleta mfarakano.Hamjui kwamba ni Bara ndio inayowapa amani na sehemu ya kukimbilia.
TATU,inabidi foreigners pande zote mbili warudishwe makwao na wavuke mipaka kwa makubaliano maalum.
Abdulhalim , nakutakia siku njema.
 
ukweli ni kwamba hamna muungano controversial duniani kama huu, haujulikani kama ni 'union' au 'federal'. mi nahani ni wakati muafaka wa kuuzungumza. Ila nakubaliana na Mwanakijiji kua knachofanyika sasa ni ukiukwaji mkubwa wa katiba
 
Back
Top Bottom