Ni uhaini - as simple as that!

Kujaribu kuvunja Jamhuri ya Muungano kwa kisingizio chochote kile cha kisiasa ni uhaini.

Jaribio la upande mmoja kuirejesha kinyemela nchi iliyokwisha ungana na nyingine ni kutangaza secession kutoka kwa Muungano na viongozi wote wanaopanga kufanya hivyo ni wa kutiwa pingu.

of course.. hilo wala siyo hoja; wakitaka watangaze tu kuwa wanataka kutoka nje ya Muungano, wadai kile wanachokiita ni "uhuru". Kikwete awaruhusu kwa sababu sidhani kama ana uwezo wa kuzuia Zanzibar kutoka nje ya Muungano.

.... endeleeni kupiga kura na mkishinda basi tunaachana "salama"..

Mara uhaini, mara huwezi kuwazuia, mara watiwe pingu, mara waende na "salama," mara ni "secession," mara watangaze "uhuru," mara Kikwete awaruhusu (kana kwamba Kikwete mfalme wa Muungano), mara "Tanzania iliungana na Zanzibar ..."

Viongozi wa maoni wamechanganyikiwa na nini hasa watu wawili walikubaliana 1964.

 
tatizo wanafikiri kuwa tunazungumza kutoka hewani tu ati tunaitakia Zanzibar mabaya; kama mazungumzo ya watu wawili leo hii (karume na seif) yamechukuliwa kuwa halali na kukumbatiwa yale ya wa Nyerere na Karume nayo yalikuwa na nguvu hiyo. Wazanzibar hawawezi kuwa na keki yao halafu waile huku wabakie nayo. Kama kuna watu Zanzibar wanataka kuwa nchi "nje" ya Muungano, waliseme hilo, kama ni kupigwa kura ipigwe na tuanze mahusiano baina ya nchi mbili.

But as long as we are a United Republic jaribio lolote la kuivunja ni uhaini - as simple as that.

Ni jukumu la kila Mtanzania (yes wapo watu wa taifa hilo) kulinda Muungano ulivyo. Hatupaswi na hatuwezi kuachii kikundi cha watu wachache kuivunja ati kwa sababu hawajisikii. Wazanzibari ambao wanajitambua kuwa ni Watanzania na wapo wengi ni lazima wakatae uhuni huu.

Kama Zanzibar haitaki kuwa ndani ya Muungano kwenye baraza la wawakilishi waseme hivyo mapema, wajitangaze kuwa wanataka kutoka nje ya Muungano na nina UHAKIKA Kikwete na uongozi wa CCM hakuna atakayeweza kujenga hoja za kuzuia kwani mashujaa hao hawapo tena. Basi watoke na kama nilivyosema tuanze uhusiano wa nchi mbili, binafsi wala sina tatizo kabisa. Lakini kama wanataka tuwe wamoja kama nchi ni lazima mpango wao wa kuitangaza Zanzibar kuwa ni nchi sijui madudu gani ukemewe mara moja na KILA MTANZANIA.

Si kwa sababu hatuwezi kuishi bila Zanzibar au wao bila sisi, bali kwa sababu MUUNGANO UPO na ni lazime utetewe kwa gharama yoyote. Kwanini Zanzibar wasipige kura ya maoni kutaka kujua kama wanataka kubakia ndani ya Muungano?

PIGENI HII KURA TUMALIZE MZIZI WA FITINA!!!

viNGINEVYO NI UHALIFU ULIOKUBUHU AMBAO ADHABU YAKE NI KIFO! Uhaini haurembuliwi macho.


Mwanakijiji ni nini unazunguka zunguka, Msimamo wa Maalim Seif ambae ni katibu mkuu wa CUF unajulikana kuwa wao wanataka serikali tatu... mazungumzo yake na Rais wa zanzibar Aman Karume yamepelekea kukubaliana kuundwa kwa serikali ya kimseto, ambayo inaonekana kama ni faraja kwa raiya wa Unguja na Pemba... Inawezekana pia may be wamezungumza kuhusu kuwa na serikali tatu, kwani kuna kila dalili ya CUF kushinda visiwani, je wakishinda tutawagomea kuwa na serikali tatu?

Pili Watanganyika ndio ambao hatuna serikali kama ilivyo Zanzibar, sisi Watanganyika ambao tunategemea serikali ua muungano. Kwa maana hiyo basi wao wana uwezo wa kukaa kwenye baraza lao la wawakilishi na kupitisha kile ambacho wanaona ndio mustakabali wa nchi yao ya Zanzibar.

Kitacho Amuliwa uko baadae ndio kitapelekwa kwenye bunge la Tanzania kwa maamuzi ya mwisho... Lakini wakiamua kulipekeka ili suhala kwa wananchi na kulipiga kura hakuna wa kuwazuiya na si uhaini, kwa nini kulazimika kuwa ni uhaini kwani wanataka kupindua serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania? Unaposisitiza kuwa muungano utetewe kwa gharama yoyote una maana gani? Unataka kupeleka vifaru Unguja na Pemba kutishia wananchi si ndio utawapa cha kusema kuwa Watanganyika tumeigeuza Zanzibar kuwa ni koloni la Tanganyika?
 
Hivi wakuu kuna uwezekano wa kuangalia tena ile articles of Union inasemaje?

Mwenye access nayo aitume hapa tuangalie.
 
Tatizo viongozi wetu wame liachia hili swala mpaka lime kua a controversial issue. Itafika kipindi kudiscuss Muungano ita kuwa kama kudiscuss dini. Mkuu Mwanakijiji maybe this is a wake up call that something should be done now. Tuta fika kipindi tuta kuwa kwenye point of no return. But mambo mengi nalaumu mfumo ulio wekwa kuendesha Muungano na nita rudi baadae kuelezea kwa nini (kwa maoni yangu).
 
Sijawahi kufikiria kusema JWTZ liangalia ulinzi wa Katiba lakini wakati huu endapo mabadiliko yanayopendekezwa Zanzibar yatafanyika ni wakati wa kuwaangalia hawa "maadui wa ndani".

I couldn't be more blunt than that.
Nashindwa kushangaa kuona celebrity wa JF kama MKKJ unaongea pumba kama hizi kama Yussuf Makamba vile! MKKJ wakati unafikiria (endelea kufikiria maana Nyerere hafufuki tena) kuwa jeshi lilinde katiba, you sound like Hitler...Mussolin...Idd Amin and the likes.

Ujuwe hilo jeshi unalosema ni la wananchi wa Tanzania-Zanzibar, limeundwa kwa katiba ya Tanzania ambayo wawakilishi wa zanzibar inadaiwa wameshiriki. Uelewe kuwa BLW lipo kwa mujibu wa katiba na maamuzi yake yananguvu ya katiba zote mbili...chombo kingine chochote kitakachoingilia maamuzi yake kitakuwa kinavunja katiba...nakushangaa uonavyo wewe jeshi litakuwa linalinda katiba badala ya kuwa linavunja kwa fikra zako.

Kama katiba inavunjwa...Mkuu remedy yake ndiyo nguvu za kijeshi?
MKkJ, unamkumbuka mwalimu Paul Mhozya..na kesi ya OIC? kenda kumshitaki rais Mwinyi mahakamani na mahakama ikamsikiliza...MKKJ, you are suggesting military intervention for your alleged treason?

Unashindwa kujenga hoja ya maana hata kwenye jambo jepesi kama hili..unakuwa kama mtu wa maskani vile!! Post hii ikiendelea kuwapo hapa utaendelea kujishushia hadhi na heshima yako uliyojijengea kwenye mitandao...you can't talk pumbaz and nonsense like these MkkJ...you are not of such type!

Leo kama wazanzibar wataandika petition kupeleka bungeni au BLW kuwa hawataki tena muungano...katika akili yako unadhani ndiyo JWTZ litaweza kuondoa matakwa ya Wazanzibar kwenye nyoyo zao kwa nguvu za kijeshi...? Angalia tu wakati tunapiga kura ya maoni macho ya ulimwengu mzima yalihamia Zanzibar, leo unavyofikira huo 'uvamizi wa kijeshi' Zanzibar dunia itafunga mikono kukutazameni tu...?

Unadhani iwapo jeshi linavamia Zanzibar, wazanzibar tutafunga mikono tukutazameni mnfavyofanya uhuni wenu...kama mlivyowafanyia Uganda...unajidanganya? au unadhani hilo jeshi lenyewe litabaki kama lilivyo baada ya kitendo hicho...kumbuka vijana wetu wazalendo, wapenda na wenye uchungu wa nchi yao ya Zanzibar pia wamo humo humo JWTZ, so unazungumzia CIVIL WAR THEN not military intervention any more...?

Mkkj, kama bado unafikiria hivyo basi ujuwe unaishi na mzimu wa Nyerere "zidumu fikra zake" kwa kuwa kama hivyo ingekuwa ndivyo leo kusingekuwa na nchi kama Eritrea, Bosnia-Hetzegovina, East Timor na karibuni tu Cosovo...and I strongly believe that Zanzibar will, one day, not be the exception..whatever comes may.

Sitaki kusema MKKJ, unakosa heshima, adabu na busara ya kiutu uzima unapoashiria kuwaita Wazanzibar "maaduwi wa ndani", sijuwi ndani ipi! uaduwi upi! wakati walioamua mabadiliko hayo kwa mustakbali wa nchi yao ni wananchi wenyewe wa Zanzibar tena kwa wingi tu na kwa njia halali ya kidemokrasia...nakushangaa unawatangazia uaduwi...sitaki kuanzia leo nikuone kama aduwi wa Zanzibar...unless unafafanuwa ulikusudia nini unaposema "maaduwi wa ndani?"

So mabadiliko ya 10 ya katiba are there to stay...whether you like it or not...ZANZIBAR NI NCHI...tunasubiri jeshi lije...maana wanaoshindwa kwa hoja hutumia nguvu...na hii ndiyo sifa ya tawala za kidhalimu...mfano wa CCM.
 
KWA HILI TUMEMALIZA...NEXT IS.....

House of Representatives endorse GNU Bill

MEMBERS of the Zanzibar House of Representatives discussed and overwhelmingly endorsed the island's 10th constitutional amendment on Monday, that paves the way for the formation of the Government of National Unity (GNU) after the October general elections.

"This timely amendment of the constitution is necessary for our country," most of the legislators were heard saying in the House as they poured praise on President Amani Abeid Karume and CUF's Secretary General Seif Sharif Hamad.

Said Ali Mbarouk (CUF- Gando) said the two leaders had moved the Zanzibar people from tension to happiness and unity, suggesting the Nobel Prize organizers to consider nominating the two for it.

Almost all members of the House including legislators who performed poorly in their constituencies in the referendum, joined together to support all the proposed constitutional amendment including clauses not directly related to GNU. In the referendum held on July 31, this year, majority 66.4 per cent voted 'yes' and 33.6 per cent voted ‘no.'

Mr Mustapha Ibrahim, the regional commissioner argued that those who voted ‘no' expressed their concern and fear about the consequences of GNU particularly by deleting the word ‘Mapinduzi' (revolution) from Zanzibar history through GNU and also the opposition sabotaging the government after elections.

"These doubts must be cleared to get 100 per cent support of the GNU," he said.

Some ministers, Mr Mansour Yussuf Himid (Water and Land), Mr Sultan Mohamed Mugheiry (Health), Mr Machano Othman Saidi (Communication), Mr Haroun Ali Suleiman (Education) raised their voices in support of the Bill, as they praised the House Committee of six led by Mr Ali Mzee Ali (CCM- nominated), for educating people prior to referendum day.

Mr Ali Suleiman Ali (CCM- Kwahani) and Mzee Ali Ussi (CCM-Chaani), strongly supported the re-defining of Zanzibar as stipulated in the constitution, "Zanzibar is state" formally known as ‘people's republic of Zanzibar' with its territory of Unguja, Pemba and all other surrounding small islands, as identified before merging with Tanganyika.

"I think the use of Republic of Zanzibar should remain, since republic means a country led by a president like Zanzibar. It should remain ‘revolutionary republic of Zanzibar," Mbarouk suggested as Mr Ussi said "the new clarification of Zanzibar clears doubts about whether Zanzibar is a state or not."

Moving the ‘constitutional amendment bill' motion, the State Minister (Constitution and good governance), Mr Ramadhani Abdallah Shaabani said a new clause in the amendment include that "Zanzibar is among two countries that form the United Republic of Tanzania." Section 1, & 2 of the Zanzibar constitution, which has been identifying Zanzibar as "part of the United Republic of Tanzania," will be deleted from the constitution.

It is on record that between late 2008 and early last year, a heated debate emerged among Union and Zanzibar politicians over whether Zanzibar was a ‘state' or not. The majority Zanzibaris led by members of the House were unhappy with statements that Zanzibar was ‘not a ‘state' but only part of Tanzania.'

Other amendment in the 1984 constitution include increasing women special seats from the current 30 per cent to 40 per cent; abolishing Regional Commissioners (RCs) becoming members of the House.
SOURCE: DAILY NEWS
 
Ni vema waZnz wangefanya vitu one at a time..serikali ya mseto ni jambo jema zaidi kulifuatilizia utekelezaji wake kabla ya kuchokoa mambo ya muungano (ambao ni kama haupo).
 
Hii "Nchi Mpya ya Zanzibar Ndani ya Muungano" itaenda kutangazwa UN au kipi kitaendelea jamani?
 
Tatizo la Zanzibar sio Muungano kama muungano. Ni watu kama 'hapa pangu' wanaowafanya Wazanzibari wasione unyonyaji wao bali waone Watanganyika kama wanyonyaji wao. Wazanzibari wanahaki ya kupambana na unyonyaji wa ndani na nje. Naamini Wazanibari wakiweza kusimama kidete na kuiwajibisha SMZ mbona mambo mswano tu... ni kijimtazamo changu tu
 
Mwanakijiji unaota endelea kuota tu...!
Mkuu inaelekea wewe ndo unaishi katika mazingira ya kusadikika.You cannot eat your cake and yet have it!
Matokeo ya kuvunja muungano yataonekana muda si mrefu tokea sasa.Ni dhahiri Zenj wametupa jiwe la kwanza sasa subirini response ya bara.
Kwa angalizo tu fuatilia position ya Karume baada ya uchaguzi
 
Kwani hii ndoa ya muungano ni ngumu kama ya Roma? Wanaotaka muungano wana maslahi yao, na kinyume chake
 
Naona watu humu mnataka tu kutengeneza tatizo ambalo halipo, huu muungano whether unavunjwa au hauvunjwi na waznz, wabara u have better things to do, mbona kuna watu tena mnawajua kwa majina wamekwiba mabilioni na mnajifanya hamuwaoni? nashangazwa sana na logic ya miafrika. Kwanini msieke effort kwenye ku-recover hiyo pesa iliyoibiwa mkajenge mashule, barabara na mahsopitali? what r u waiting for? mnasubiri uchaguzi eehh? endeelini hivohivo mtakula siasa zenu uchwara!ur misguided patriotism lacks logic.totally.huwa mnakawaida ya kuilaumu serikali kwa kukosa priority, ile nyie zenu ni zipi?

Znz inachopaswa kufanya ni kujiondoa kwene makucha ya hawa masukule CCM. Whether kwa kuvunja muungano au la, i do support them 100%. It is time waznz kufanya mambo yao na kuangalia future yao..hawa mazuzu wa bara wasiwababaishe, ya kwao yanawashinda seuze yenu?
 
Naona watu humu mnataka tu kutengeneza tatizo ambalo halipo, huu muungano whether unavunjwa au hauvunjwi na waznz, wabara u have better things to do, mbona kuna watu tena mnawajua kwa majina wamekwiba mabilioni na mnajifanya hamuwaoni? nashangazwa sana na logic ya miafrika. Kwanini msieke effort kwenye ku-recover hiyo pesa iliyoibiwa mkajenge mashule, barabara na mahsopitali? what r u waiting for? mnasubiri uchaguzi eehh? endeelini hivohivo mtakula siasa zenu uchwara!ur misguided patriotism lacks logic.totally.huwa mnakawaida ya kuilaumu serikali kwa kukosa priority, ile nyie zenu ni zipi?

Znz inachopaswa kufanya ni kujiondoa kwene makucha ya hawa masukule CCM. Whether kwa kuvunja muungano au la, i do support them 100%. It is time waznz kufanya mambo yao na kuangalia future yao..hawa mazuzu wa bara wasiwababaishe, ya kwao yanawashinda seuze yenu?
Watch this space mkuu na muwe consistent.You cannot eat your cake and yet have it.
Wazenj wametamka kinaga ubaga nia ya kujitoa muungano,tuheshimu matakwa yao.
Patriotism na wizi masuala mbali mbali. Hata majambazi ya mafia walisupport utaifa wao wakati wa vita kuu ya pili
 
Nashindwa kushangaa kuona celebrity wa JF kama MKKJ unaongea pumba kama hizi kama Yussuf Makamba vile! MKKJ wakati unafikiria (endelea kufikiria maana Nyerere hafufuki tena) kuwa jeshi lilinde katiba, you sound like Hitler...Mussolin...Idd Amin and the likes.

Ujuwe hilo jeshi unalosema ni la wananchi wa Tanzania-Zanzibar, limeundwa kwa katiba ya Tanzania ambayo wawakilishi wa zanzibar inadaiwa wameshiriki. Uelewe kuwa BLW lipo kwa mujibu wa katiba na maamuzi yake yananguvu ya katiba zote mbili...chombo kingine chochote kitakachoingilia maamuzi yake kitakuwa kinavunja katiba...nakushangaa uonavyo wewe jeshi litakuwa linalinda katiba badala ya kuwa linavunja kwa fikra zako.

Kama katiba inavunjwa...Mkuu remedy yake ndiyo nguvu za kijeshi?
MKkJ, unamkumbuka mwalimu Paul Mhozya..na kesi ya OIC? kenda kumshitaki rais Mwinyi mahakamani na mahakama ikamsikiliza...MKKJ, you are suggesting military intervention for your alleged treason?

Unashindwa kujenga hoja ya maana hata kwenye jambo jepesi kama hili..unakuwa kama mtu wa maskani vile!! Post hii ikiendelea kuwapo hapa utaendelea kujishushia hadhi na heshima yako uliyojijengea kwenye mitandao...you can't talk pumbaz and nonsense like these MkkJ...you are not of such type!

Leo kama wazanzibar wataandika petition kupeleka bungeni au BLW kuwa hawataki tena muungano...katika akili yako unadhani ndiyo JWTZ litaweza kuondoa matakwa ya Wazanzibar kwenye nyoyo zao kwa nguvu za kijeshi...? Angalia tu wakati tunapiga kura ya maoni macho ya ulimwengu mzima yalihamia Zanzibar, leo unavyofikira huo 'uvamizi wa kijeshi' Zanzibar dunia itafunga mikono kukutazameni tu...?

Unadhani iwapo jeshi linavamia Zanzibar, wazanzibar tutafunga mikono tukutazameni mnfavyofanya uhuni wenu...kama mlivyowafanyia Uganda...unajidanganya? au unadhani hilo jeshi lenyewe litabaki kama lilivyo baada ya kitendo hicho...kumbuka vijana wetu wazalendo, wapenda na wenye uchungu wa nchi yao ya Zanzibar pia wamo humo humo JWTZ, so unazungumzia CIVIL WAR THEN not military intervention any more...?

Mkkj, kama bado unafikiria hivyo basi ujuwe unaishi na mzimu wa Nyerere "zidumu fikra zake" kwa kuwa kama hivyo ingekuwa ndivyo leo kusingekuwa na nchi kama Eritrea, Bosnia-Hetzegovina, East Timor na karibuni tu Cosovo...and I strongly believe that Zanzibar will, one day, not be the exception..whatever comes may.

Sitaki kusema MKKJ, unakosa heshima, adabu na busara ya kiutu uzima unapoashiria kuwaita Wazanzibar "maaduwi wa ndani", sijuwi ndani ipi! uaduwi upi! wakati walioamua mabadiliko hayo kwa mustakbali wa nchi yao ni wananchi wenyewe wa Zanzibar tena kwa wingi tu na kwa njia halali ya kidemokrasia...nakushangaa unawatangazia uaduwi...sitaki kuanzia leo nikuone kama aduwi wa Zanzibar...unless unafafanuwa ulikusudia nini unaposema "maaduwi wa ndani?"

So mabadiliko ya 10 ya katiba are there to stay...whether you like it or not...ZANZIBAR NI NCHI...tunasubiri jeshi lije...maana wanaoshindwa kwa hoja hutumia nguvu...na hii ndiyo sifa ya tawala za kidhalimu...mfano wa CCM.

Junius, kwanini msiende mbele tu muitishe kura ya maoni ili mchague kutoka katika Muungano kabisa ili tuwe na undugu na ushirikiano wa nchi na nchi? Kwanini mnataka kama hamtaki? Too bad, kwa kuwa Katiba ya sasa iko ilivyo tutaitetea sisi wengine. Kinachofanyika kama siyo uhaini kamili basi kimepakana kabisa na uhaini. It is as simple as that.
 
Watch this space mkuu na muwe consistent.You cannot eat your cake and yet have it.
Wazenj wametamka kinaga ubaga nia ya kujitoa muungano,tuheshimu matakwa yao.
Patriotism na wizi masuala mbali mbali. Hata majambazi ya mafia walisupport utaifa wao wakati wa vita kuu ya pili

Utaifa muutetee nyie, wakitetea wengine makosa! Ama kwa hakika nyani haoni makalio yake.

Binafsi napima hili suala la muungano ktk muono wa kiuchumi, achana na falsafa na hizo sarakasi za katiba, maana katiba yenyewe haimlindi yeyote zaidi ya tabaka twawala la mazuzu wa huko bara. Katiba inasema muizi akiiba apelekwa jela, kiongozi wenu Dr. Mkwere anasema walipe lakini wasiguswe..(na hakuna utrhibitisho kama wamelipa na hamna anayethubutu kuuliza)! sasa usitake kuniambia huoni priority hapa ni nini?

Muungano haujawasaidia lolote waznz kiuchumi na hali zao zinakuwa mbaya siku hadi siku, huku mazuzu wa huko bara wakizidi kujineemesha. Sasa sioni kwanini waendelee kuwakumbatia mawakala wa ukoloni kutoka bara wakati hawana msaada wowote. Its time to call the quits, and try something better.
 
Nashindwa kushangaa kuona celebrity wa JF kama MKKJ unaongea pumba kama hizi kama Yussuf Makamba vile! MKKJ wakati unafikiria (endelea kufikiria maana Nyerere hafufuki tena) kuwa jeshi lilinde katiba, you sound like Hitler...Mussolin...Idd Amin and the likes.


Haijibu hoja zaidi ya kuita majina kulazimisha hoja. dismissed!

Ujuwe hilo jeshi unalosema ni la wananchi wa Tanzania-Zanzibar, limeundwa kwa katiba ya Tanzania ambayo wawakilishi wa zanzibar inadaiwa wameshiriki. Uelewe kuwa BLW lipo kwa mujibu wa katiba na maamuzi yake yananguvu ya katiba zote mbili...chombo kingine chochote kitakachoingilia maamuzi yake kitakuwa kinavunja katiba...nakushangaa uonavyo wewe jeshi litakuwa linalinda katiba badala ya kuwa linavunja kwa fikra zako.

Ulivyojichanganya hapo itachukua muda kukufungua; kama Katiba unayosema inawalinda na waliapa kuilinda ndiyo katiba wanayoivunja wakati kuna chombo kingine kimepewa jukumu la kuilinda Katiba basi ni jukumu la chombo hicho kingine. Viapo vya Jeshi na vya wawakilishi si sawasawa. Nashukuru wapo Wazanzibar kwenye Jeshi ambao wanajua waliapa kulinda nini.


Kama katiba inavunjwa...Mkuu remedy yake ndiyo nguvu za kijeshi?

Kwa jibu la haraka ni "YES".


MKkJ, unamkumbuka mwalimu Paul Mhozya..na kesi ya OIC? kenda kumshitaki rais Mwinyi mahakamani na mahakama ikamsikiliza...MKKJ, you are suggesting military intervention for your alleged treason?

Kama Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar anapeleka mswada huu na Mwanasheria wa Muungano anarembua macho nani atailinda Katiba?

Unashindwa kujenga hoja ya maana hata kwenye jambo jepesi kama hili..unakuwa kama mtu wa maskani vile!! Post hii ikiendelea kuwapo hapa utaendelea kujishushia hadhi na heshima yako uliyojijengea kwenye mitandao...you can't talk pumbaz and nonsense like these MkkJ...you are not of such type!

Bahati nzuri baada ya miaka kadhaa humu utakuwa unajua kabisa kuwa hakuna kitu ambacho hakiniingii akilini kama "hadhi, na heshima" ya kwenye mtandao au mahali popote pale. Sifanyi kitu kwa kutafuta heshima, ujiko, upendo au sifa ya aina fulani. Havinisaidii kwa namna yoyote na kuvikosa hakunipunguzii kitu. So, vyote huja na kuondoka kama ukungu wa alfajiri.


Leo kama wazanzibar wataandika petition kupeleka bungeni au BLW kuwa hawataki tena muungano...katika akili yako unadhani ndiyo JWTZ litaweza kuondoa matakwa ya Wazanzibar kwenye nyoyo zao kwa nguvu za kijeshi...? Angalia tu wakati tunapiga kura ya maoni macho ya ulimwengu mzima yalihamia Zanzibar, leo unavyofikira huo 'uvamizi wa kijeshi' Zanzibar dunia itafunga mikono kukutazameni tu...?

Kuandika petition au kulalamika wala si tatizo ndio uzuri wa siasa.. tatizo linakuja watu wanapochukua hatua za kihaini.. hapo ni tatizo. Hilo tumaini la "dunia" liko njozini aisee. Hii dunia iliyoka kimya wakati Ahmedinajad anawaua watu wake kisa uchaguzi na wakabakia kukaa mbali wanaangalia tu. Msifanye mambo kwa kisingizio cha dunia; kuna vingine dunia inatambua kuwa ni necessary evil. Msivunje Muungano wetu kinyemela. Mkitaka takeni ipigwe kura ya maoni mtoke au mbakie siyo muimong'onyoe nchi yetu pole pole.

Unadhani iwapo jeshi linavamia Zanzibar, wazanzibar tutafunga mikono tukutazameni mnfavyofanya uhuni wenu...kama mlivyowafanyia Uganda...unajidanganya? au unadhani hilo jeshi lenyewe litabaki kama lilivyo baada ya kitendo hicho...kumbuka vijana wetu wazalendo, wapenda na wenye uchungu wa nchi yao ya Zanzibar pia wamo humo humo JWTZ, so unazungumzia CIVIL WAR THEN not military intervention any more...?

Na sisi wengine ndiyo hatutavumilia uhuni unaofanywa sasa na baadhi ya Wazanzibari; uhuni wa kujaribu kuiua Tanzania huku wakijifanya wanaipenda! NI uhaini.

Mkkj, kama bado unafikiria hivyo basi ujuwe unaishi na mzimu wa Nyerere "zidumu fikra zake" kwa kuwa kama hivyo ingekuwa ndivyo leo kusingekuwa na nchi kama Eritrea, Bosnia-Hetzegovina, East Timor na karibuni tu Cosovo...and I strongly believe that Zanzibar will, one day, not be the exception..whatever comes may.

Ndiyo hiyo nasema kwanini tufikie huko; si mwende tu sasa ili tumalize hili jinamizi la kutishana tishana. Kama mnataka Zanzibar iwe nje ya Muungano mnaogopa nini kusema, kuandamana na kudai kwa nguvu zenu. Hamuwezi kuanzisha nchi ndani ya nchi! Ni uhaini!


Sitaki kusema MKKJ, unakosa heshima, adabu na busara ya kiutu uzima unapoashiria kuwaita Wazanzibar "maaduwi wa ndani", sijuwi ndani ipi! uaduwi upi! wakati walioamua mabadiliko hayo kwa mustakbali wa nchi yao ni wananchi wenyewe wa Zanzibar tena kwa wingi tu na kwa njia halali ya kidemokrasia...nakushangaa unawatangazia uaduwi...sitaki kuanzia leo nikuone kama aduwi wa Zanzibar...unless unafafanuwa ulikusudia nini unaposema "maaduwi wa ndani?"

Sina heshima adabu wala busara kwa wahaini; I DON'T.


So mabadiliko ya 10 ya katiba are there to stay...whether you like it or not...ZANZIBAR NI NCHI...tunasubiri jeshi lije...maana wanaoshindwa kwa hoja hutumia nguvu...na hii ndiyo sifa ya tawala za kidhalimu...mfano wa CCM.


Ni mabadiliko ya kuelekea kuiua Tanzania na tutayapinga kwa nguvu zetu zote. Si kwa sababu tunapenda hali iliyopo sasa bali ni kwa sababu mnataka kuiua Tanzania.
 
Baada ya kufanikiwa Azma ya kuunda Serikali ya Kitaifa ,Zanzibar sasa wanataka kujitoa kwenye Muungano,haya mabadiliko yaliyozungumzwa kwenye BLW yanaondoa dhumuni la awali la Muungano.Watanzania tu wepesi sana kusahau,lakini wale wanaojua vyema wanamjua vyema Maalim Seif na misimamo yake kuhusu Muungano,mmekwishasahau siku Seif aliyoondoka kwa hasira Dodoma baada ya ubishi mkubwa kuhusu serikali Tatu? Mmesahau kuundwa kwa G-55 baada ya vurugu zile za Dodoma zilizomuondolea Seif U-waziri Kiongozi wake?

Kwa hali ilipofikia ni bora kwenda "solo" kuliko karaha hizi za kuwabeba/lea watu wanaoona wananyanyaswa na kumezwa na Tanzania Bara.Jazba hazitosaidia kitu.Tujadili hatma ya Muungano kwa Uwazi bila Uoga katika ngazi zote.Udhaifu wa Viongozi wa Bara ndio matokeo ya hali hii ya leo.Kikwete,Karume,Seif na Pinda hawatoshi kuwaamulia watanzania karibu millioni 45 wenye misimamo tofauti.Tuwaulize Wananchi wa Bara na Visiwani wao ndio watupe maamuzi ya mwisho kuhusu hatma ya Muungano.
 
Baada ya kufanikiwa Azma ya kuunda Serikali ya Kitaifa ,Zanzibar sasa wanataka kujitoa kwenye Muungano,haya mabadiliko yaliyozungumzwa kwenye BLW yanaondoa dhumuni la awali la Muungano.Watanzania tu wepesi sana kusahau,lakini wale wanaojua vyema wanamjua vyema Maalim Seif na misimamo yake kuhusu Muungano,mmekwishasahau siku Seif aliyoondoka kwa hasira Dodoma baada ya ubishi mkubwa kuhusu serikali Tatu? Mmesahau kuundwa kwa G-55 baada ya vurugu zile za Dodoma zilizomuondolea Seif U-waziri Kiongozi wake?

Kwa hali ilipofikia ni bora kwenda "solo" kuliko karaha hizi za kuwabeba/lea watu wanaoona wananyanyaswa na kumezwa na Tanzania Bara.Jazba hazitosaidia kitu.Tujadili hatma ya Muungano kwa Uwazi bila Uoga katika ngazi zote.Udhaifu wa Viongozi wa Bara ndio matokeo ya hali hii ya leo.Kikwete,Karume,Seif na Pinda hawatoshi kuwaamulia watanzania karibu millioni 45 wenye misimamo tofauti.Tuwaulize Wananchi wa Bara na Visiwani wao ndio watupe maamuzi ya mwisho kuhusu hatma ya Muungano.


Mwawado, bara wala hatuhitajiki kuulizwa; hili ni suala la Zanzibar..sisi tumelalamika lini kuidai Tanganyika? Kumbuka hata hoja ya G55 ilitokana na Zanzibar na OIC (rejea kitabu cha Mwalimu). Hilii ni suala la Zanzibar TU. Ndio maana miye ningependa twende mbele kabisa (kama Nyerere anavyosuggest kwenye UWHT). Zanzibar waulizwe kama wanataka kuwa sehemu ya NCHI MOJA YA TANZANIA au KUWA NCHI HAKIMIYA Nje ya Muungano? Hili ndilo swali pekee wanalotakiwa kuulizwa Wazanzibar.

Tatizo ni kuwa wao wenyewe Zanzibar hawana ujasiri wa kusema wazi wanachotaka; kama wanataka kutoka nje ya Muungano waseme na kwa vile inaonekana kabisa wana uwezo wa kuendesha kura ya maoni hadi kubadili muundo wa serikali yao, miye naomba waitishe kura ya maoni kama wanataka kubakia sehemu ya Jamhuri ya Muungano au kuwa Nchi nje ya Muungano. Jibu lao litaamua wafanye nini. Tanzania Bara tutabakia kuwa Tanzania na ni matumaini yangu hata jina letu haturudii la Mkoloni. Tutaitwa TAnzania.
 
Back
Top Bottom