Tindikali
JF-Expert Member
- Mar 26, 2010
- 2,014
- 2,664
Kujaribu kuvunja Jamhuri ya Muungano kwa kisingizio chochote kile cha kisiasa ni uhaini.
Jaribio la upande mmoja kuirejesha kinyemela nchi iliyokwisha ungana na nyingine ni kutangaza secession kutoka kwa Muungano na viongozi wote wanaopanga kufanya hivyo ni wa kutiwa pingu.
of course.. hilo wala siyo hoja; wakitaka watangaze tu kuwa wanataka kutoka nje ya Muungano, wadai kile wanachokiita ni "uhuru". Kikwete awaruhusu kwa sababu sidhani kama ana uwezo wa kuzuia Zanzibar kutoka nje ya Muungano.
.... endeleeni kupiga kura na mkishinda basi tunaachana "salama"..
Mara uhaini, mara huwezi kuwazuia, mara watiwe pingu, mara waende na "salama," mara ni "secession," mara watangaze "uhuru," mara Kikwete awaruhusu (kana kwamba Kikwete mfalme wa Muungano), mara "Tanzania iliungana na Zanzibar ..."
Viongozi wa maoni wamechanganyikiwa na nini hasa watu wawili walikubaliana 1964.