Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Tupe ushahidi. Mkuki kwa nguruwe.
 
Atupe ushahidi vinginevyo "Ataqualify kuitwa muongo, mzandiki, mzushi,mpekupeku, majitaka" na yote zaidi ataqualify pia kuitwa "mtumwa" wa mafisadi wanaomuona kuwa Sitta ni mwiba kwa agenda zao.

Akitoa ushahidi tu basi mimi ntakuwa nyuma yake kumsapoti anayoongea.
 
1. Atupe ushahidi vinginevyo "Ataqualify kuitwa muongo, mzandiki, mzushi,mpekupeku, majitaka"

2. Akitoa ushahidi tu basi mimi ntakuwa nyuma yake kumsapoti anayoongea.

- Mkuu hoja yako nzito ingeeleweka sana kama ungetumia maneno ya mstari chini tu ya mstari pili, hakukuwa na sababu ya kuandika yale ya mstari wa kwanza maana ni demeaning kwa member mwenzio,

- Labda unazo dataz zenye ukweli kuliko zake uziweke hapa, au uzipime alizokwisha zitoa kama zina nguvu ya ukweli, tusikubaliane kwa kuheshimiana, huku tukiendelea kukubaliana kutokubaliana, lakini kwa heshima, maana wote hapa ni bin-adam wenye mapungufu na tunaojitegema.

Ahsante.

William.
 
Nimesoma habari hapa kwenye website ya BBC na kukuta kwamba Speaker wa UK amejiuzuru kutokana na kashfa ya fedha iliyolikumba bunge lao. Najiuliza Samwel Sitta naye si atangaze kuwa anajiuzuru kwa sababu alisema ushahidi wa Slaa kuhusu EPA ni uwongo na wa kuokoteza mtandaoni?
 

Utamaduni huu utachukua miaka kuingia kwenye akili na ufahamu wa viongozi wetu wa kibongo. Kwani wengi hawaongei kutoka ndani ya dhamiri zao bali kwa ajili ya maslahi ya waliowaweka madarakani. Ukifuatilia kauli za namna hiyo za kukanusha vitu wakati ni kweli na ushahidi upo sidhani kama kuna kiongozi aliye madarakani atapona, haswa wa SISIEMU.

Kumbuka issue ya Mh. Zitto, wakati mambo yalikuwa kweli na jamaa wamewajibishwa, nini kimetokea kwa waliokanusha na kumchukulia hatua jamaa?? Wamejaa uongo, unazi na ufisadi mtupu kuanzia kiranja mkuu mpaka wafagiaji wasiochoka kusema kusema hata pumba kule kwenye kiota chao Dodoma!.
 
Last edited:
upuuzi mwingine huu,hivi kuwa na hawara na ukawa mtendaji mzuri,na kutokua na hawara lakini mbabaishaji kipi bora?nadhani spika wetu hakuupata uspika kutokana na kuwa ******* ama cheo chake sio uaskofu.hii ni vita ya kina RA inahamishiwa huku
 
Mjomba, this is a day dream kwetu wabongo! Nasikia itaanza mara baada ya sirikali yetu yooote kuhamia Dodoma.
 
Last edited:
Umeuliza swali jema sana.
Ila ujue grounds za kujiuzuli jamaa wa commons zina kauwiano na mjadala wa sasa unaoendelea kuhusu mapato ya wabunge. Jamaa alikamatwa pabaya naamini Sitta atajifunza hapo na kuacha kutetea uroho wa wabunge wengi kukamua hazina ya nchi......
 

Jamani, mbona huo siyo utaratibu wetu. mnataka kila kitu tuige kwa wazungu?! Acha na wao waanze kuiga kwetu bwana. utaratibu wetu ni kama ilivyokuwa kwa Pro. Mbilinyi na Prof. Kigoma Malima. Sisi huwa hatujiuzuru hivyo kwa makelele yenu wadanganyika msio na meno, tunajiuzuru kwa heshima tukitakiwa kufanya hivyo na jumuia za kimataifa kwa kuzuia misaada.
 
Mjomba, we vp.. unaongelea msamiati wa KIYUNANI kwa watumishi wa SIRIKALI yetu?

We hukusikia aliyekuwa 'mwenye nchi' wa awamu ya tatu jinsi alivyoipokea kwa MASIKITIKO MAKUBWA taarifa ya kujiuzulu kwa waziri wa fedha wa enzi hizo, prof.Mbilinyi?

We hujamsikia mtu juzi anawaambia wananchi 'wazowee milipuko ya mabomu'? Je hizo ni kauli za uwajibikaji? Kungekuwa na kujiuzulu nchi hii, si angeshaachia ngazi?

Hebu nikumbusheni mie, nilishasahau, hivi ishu hii ya kuwajibika inaongelewa wapi vile kwenye dokomenti zetu?
Ni kwenye katiba, sera, miongozo, au vision 2025? Au ilikuwemo kwenye lileeee Azimio la Kaloleni Arusha? Nisaidieni...!!!
 
babu sitta si majuzi kaadhimisha miaka 40 ya ndoa...kumbe anapenda chini namna hii.....alafu si alikula kona kupima UKIMWI bungeni?
 
Si umesikia yaliyotokea juzi Mbagala, hakuna yoyote anakubali kutake responsibility. Wameishia kuunda tume ya kufunika aibu!
 
Jamani hii sasa ni nafasi nzuri kwetu hasa wana JF pamoja na vyombo vya habari kumshinikiza SPIKA wetu aachie ngazi. Alichokisema Dk. Slaa kuhusu marupurupu ya wabunge yanavyowakaba walalahoi yafanyiwe kazi. Jamani nchi inaendeshwa kihuni hivi mpaka lini? Tutaendelea kullalamika mpaka lini? Wakati ni huu tusimame kidete kupigania maisha bora kwa walalahoi wa nchi hii na si maisha bora kwa makabwela kama kina Spika Martin. Tazama huko Tarime watu wanakunywa maji yenye sumu kwa expense ya utajiri wetu wa madini na hamna tunachofaidi !!!!! Huu ndio wakati wa kutumia nguvu ya umma kuwaondoa hawa mafisadi!!!!! ALUTA CONTINUA!!!! NIGER DELTA WAMEANZA TUNASUBIRI NINI?
 
Hii yote na namna ya kukwepesha mashambulizi kwa mafisadi, GT nimeitambua janja yako. Hoja ulizotoa si ngeni, zilishajadiliwa hapa sana, magazeti uliyonukuu ni ya mwaka jana (2008). Hiyo yote ni janja tu, siku zote unaibua shutuma kwa wanaoongoza vita dhidi ya ufisadi kama akina Mengi, Mwakyembe, Sitta nk. Huko ukiwa kimya juu ya ufisadi wa akina Rostam and his group.
 
babu sitta si majuzi kaadhimisha miaka 40 ya ndoa...kumbe anapenda chini namna hii.....alafu si alikula kona kupima UKIMWI bungeni?

heheheeh hata Yo Yo hula kona kupima Ngoma...acheni bwana kama mzee huwa anauza mechi inaonyesha!
 
heheheeh hata Yo Yo hula kona kupima Ngoma...acheni bwana kama mzee huwa anauza mechi inaonyesha!
wazee akma hawa waanuza sana game....na si unajua hawana viwango vya kucheza kama Pele hao mademu wakizidaka ndio wanakuja kwa wakian Zidane wapate skills....si hatari hio shem na skills ujuavyo ni kavu bin kavu.....
 
kama kuna ukweli ktk hili,

Ni serious abuse of resouces za Ofisi ya Bunge!

Ni vema akashikiwa bango ili ajiuzulu!
 
Na bado anadai wabunge wa Tanzania wanalipwa kidogo kulinganisha na wabunge wa Kenya na hata South africa! anacheza huyu mbona halinganishi kima cha chini cha watanzania na hizo nchi?

Huyu ananuka ufisadi its time to go....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…