Tanzania bila mageuzi hatutafika, tunawasomi wazuri sana lakini wanashindwa kutetea mabadiliko ya katiba badala yake wanakaa kimya eti kulinda nafasi zao au kuteuliwa kuwa wakuu wa mikoa na wilaya. Tuamke tukatae ujinga, baba wa Taifa hayati mwl Julius Nyerere alipiga vita maadui wakuu wa tatu wa taifa ambao ni ujinga, maradhi na umaskini. Kukaa kimya ni ujinga, watu kama kina Sitta wanakula jasho letu bila haya alafu tunakaa tunawasifia kuwa wanatutetea. Huo ni ujinga, bado hatujaweza kupambana na adui ujinga, wana CCM wanasema Nape Nauye anajitaidi kweli, siyo kweli ni hela za allowance anazopewa kila siku na magari anayosafiria yanamfanya kubwabwaja hovyo ili waliomtuma wamwone anafaa na kumuongezea safari.
Waziri Sitta amezeeka, hatufai tena, angehama kwenye nyumba ya spika akaishi kwake ili kuokoa gharama. Hizo milioni kumi na mbili kwa mwezi mara miaka mitano ni milioni 600 tungejenga hospital ata ya watoto kwenye kata mbili.