Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

MAMBO YA KATIBA YA UVCCMM

18. Ni mwiko kwa kiongozi:-
(1) Kutumia madaraka aliyopewa ama kwa ajili
ya manufaa yake binafsi au kwa
upendeleo, au kwa namna yoyote ambayo
ni kinyume cha lengo lililokusudiwa
madaraka hayo.
(2) Kupokea mapato ya kificho, kutoa au
kupokea rushwa, kushiriki katika mambo
yoyote ya magendo au mambo mengine
yaliyo kinyume cha lengo lililokusudiwa
madaraka hayo.
 
http://www.klhnews.com/index.php/headlines/agenda-21-yaundwa.php

Pamoja na mada hii kuwa tamu, hebu tujikumbushe hii habari ya Mwanakijiji hapa na kama JF nayo ni sehemu ya mkakati

husika.

http://www.klhnews.com/index.php/headlines/agenda-21-yaundwa.php


Wakati habari hii ya KLHN inaandikwa tayari Kikwete, Dk. Slaa, Mengi na Zitto walikwisha kuguswa na kuchafuliwa, sasa kaja

Mbowe na baadaye Sitta. Nakumbuka mtu mmoja alimwambia Mbowe, "nitakujibu kwa staili yangu" baada ya mtu huyo kuguswa na mapigo ya wabunge wa Chadema hasa siku ile ilipotolewa kwa mara ya kwanza orodha ya MAFISADI. Kwa wanaokumbuka orodha ile hata hapa JF ilitolewa ikiwa na majina manane (8) likiwamo jina la Kikwete lakini bila ya majina ya Lowassa, Karamagi na Rostam,katika kipindi ambacho BoT (EPA) na Richmond na TICS zilikua zimepamba moto.

SINA hakika na hii hapa ya web ya Chadema

http://www.chadema.net/habari/2007/orodha1/ukurasa2.php

Majina hayo ya kina EL, Karamagi na RA ambayo yaliongezwa baadaye, yaliwakera wahusika. Sina hakika kama hili lilikua BAHATI MBAYA katika maandalizi ya orodha kwani wananchi waliwajua hawa kuwa ndio vinara wa UFISADI.

Ndipo mtu mmoja akawaambia watu, "atajibu kiaana" na kwamba hana haraka na hilo, kwani ni SUALA LA MUDA TU.

Kabla sijahoji USAHIHI wa TAARIFA ya SITTA na kwamba pamoja na kuwa HOJA ya SITTA ni sehemu ya mapambano yetu ya kuhakikisha
nchi inakua SAFI, kuna maswali ya kujiuliza, maswali ambayo nilijiuliza alipoanza kushambuliwa Slaa, Zitto na hata Mengi.

-Nilitoa mfano wa polisi (SITTA,SLAA, ZITTO, KILANGO, MWAKYEMBE, MENGI,MBOWE) ambaye 'tunamtuhumu' kwamba hana maadili ambaye AMESHIKA SILAHA na mbele yetu tuna MAJAMBAZI (LOWASSA, ROSTAM, KARAMAGI, CHENGE) yenye silaha yanaua WATANZANIA WENZETU, sasa tutaanza kumshughulikia huyo POLISI kwanza!!? ama tutampa nafasi ayadhibiti majambazi?!!!

Hapa lazima tuzingatia kipindi tulichonacho, kwamba sasa ndicho ambacho wanaibuka watu wanaojifanya wana uchungu na nchi, watu ambao awali hawakua wenzetu kabisa, sasa wametoka nje eti ndio wanaona maovu, kuzuia wasishughulikiwe ama kuwatisha POLISI wetu wasipambane nao. KWanza tujue kwamba polisi (WAZALENDO) tulionao ni wachache mno na hawana SILAHA (uwezo) na vyombo vya usafiri (MEDIA) vilivyopo ni vichache (JF, MWANAHALISI, RAIAMWEMA, THISDAY, KLHN) na tunapoanza kugeukana na kugeuza mashambulizi upande wetu, tunampa adui nafasi ya kushinda VITA tuliyoisimamia kwa urahisi mkubwa na baadaye, majambazi hayo yatarudi na kutushughulikia wenyewe (kama walivyowakamata MAC na Mike), watafungia magazeti na mitandao yote na ikibidi wataua watu na NAWAHAKIKISHIA hawatafanya makosa tena ya KUJIAMINI MNO na kutudharau tena (kusema kelele za chura) kama walivyofanya kwa RICHMOND na EPA, sasa wameshajua JF, Mwanahalisi, Thisday, RaiaMwema ni kiboko kwa hiyo wameingia kwa KASI, NGUVU, ARI na PESA 'mpya' na ndugu zangu HISTORIA ITATUHUKUMU, MUNGU ATATULAANI kwa kusema, "Muliniomba nafasi nikawapa, nikawachanganya, mukaichezea kwa kugombana wenyewe kwa wenyewe tena hadharani". Tumeingiliwa ndani ya nyumba, sasa tunagombana wenyewe na wezi WANAPETA. Tumebadili mwelekeo, sasa FISADI ni MBOWE NA SITTA huku kwa upande mwingine LOWASSA (akifananishwa na Ali Hassan Mwinyi), KARAMAGI, ROSTAM (akifafanishwa na Amir Jamal) ni MASHUJAA.

MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU WALAANI MAFISADI NA MAKUWADI WAO


ORODHA YA KWANZA YA LIST OF SHAME kama ilivyowekwa hapa JF.

 
.......simpendi Sitta kwasababu ya

Mabovu yake (Kuanzia Ustawishaji Dododma na TIC)
Kujiona yeyeni Bora Kuliko wenzake
Ubabe wake nknk nk nk nk

Kwanini, hapo mwanzo nilisema hii Hoja IENDE KWENYE VIBWEKA/VITUKO VYA WAKUBWA.................ni kwa sababu....irregardless ya Agenda 21

........mtu unaingia JF vuuu...............mara ooohhh Spika anatumia Millioni 5 katika safari zake za ndani.......mara ohhh akienda Safari zake za nje anatumia Millioni 15........mara oooohhh sijui alikopa wapi na mara alikopa wapi.............halafu Hoja yake imekuja kumezwa sasa na vimada wake so and so....wanatumia magari ya serikali fulani fulani (yakatajwa)

1.Kuna Miiko ya Viongozi (nashukuru kuna mjumbe mmoja hapo juu ameweka baadhi)
2.Kuna Mapato na matumizi ya viongozi ambayo yako clearly defined

Mtoa mada agekuja na kwa kusema Spika akisafiri safari za ndani/Nje anatakiwa kutumia Kiasi X yeye akatumia X+.......hapo ningemuelewa...and there must be a justification kwa matumizi hayo

Kwa std tulizo jiwekea hapa JF ya kujadili akina Mar Chifupa (RIP), Mengi, Mbowe na wengineo kuhus affairs zao ndio maana nili-conclude kuwa hiii mada inafaa kuwa hapa ilipo.

Pengine tukiipata HIYO MVUA.........wengine tunasubiri hiyo mvua.....kwani hatuwi disguised na just a tone la mvua.
 
Yaani ina maana hata Mh. Cheyo naye alikubali kulamba huo uchafu? Maana naamini yeye alikuwa Mwenyekiti wa hiyo Kamati kama sitakuwa nime-overlook.
 
Can two, three, four etc. wrongs make a right??????
 
jamani haya yote ni sehemu ya mapambano ya kifikra na tuelewe kabisa kuwa katika mapambano haya yasiyo na sheria basi kila silaha inaonekana kutumiwa! Tatizo ninaloliona ni watu kuanza kutumia "nuclear option" ili siyo tu kushinda vita bali pia kumuangamiza adui yao.

Lowassa, Karamagi, na Msabaha na baada ya muda si mrefu Hosea na Mwanyika wote waliangushwa/wataangushwa kutokana na kazi zao; kwambe wameshindwa kutelekeza wajibu wao. Hakuangushwa mtu kwa sababu ya alilala na nani, na hakuangushwa mtu kwa sababu ya ana vimada wangapi. Kama tunataka kuzungumzia maadili ya ngono hili ni jambo muhimu na even kabla ya hili nilishaanza kuandika makala kuhusu "ufisadi wa ngono, nao ni ufisadi". Hili tunaweza kulizungumza lakini tukianza kurusha majina, tujue kabisa "kipimo kile kile tupimiacho, ndicho kitakachotumiwa dhidi yetu au dhidi ya rafiki zetu".

Tusijefurahia mkuki kwa nguruwe lakini siku ukigeuzwa kuwa ni kwa binadamu watu tuanze kubadilisha principles.

Sasa ukisoma habari nyingine kule kwenye KLH News jinsi "Lowassa alivyozidiwa Kete" utaona ni kwanini kuna watu wana kisasi na spika.

Kwa hiyo badala ya kudandia tu, tukumbuke kuwa kuna watu wanaweza kuja na madazi mazito ilimradi wafanye damage hata kama madai hayo si ya kweli; kama yule jamaa aliyedai kuwa Mbowe ni mbakaji watoto na ana kesi kadhaa mahakamana "tangu miaka ya tisini" na hadi hivi sasa jamaa huyo ameshindwa kuwa muungwana na kuiondoa na kuomba radhi.

Na kama kuna mtu anafikiria haya mambo yanamlenga Sitta tu afikirie tena, wenye kuleta habari hii wana target zao na hapo kwa Sitta siyo mwisho.

Hata hiyvo kama nilivyozungumza wakati ya mada ile ya "picha" kuwa viongozi wenyewe wasipokemeana wakidhani wanaumbuana wajue kabisa kuwa kikigeuzwa upande wao wasilie faulu!
 
Mkuu halisi

Umesomeka Mkuu!

Nafikiri wakati mwingine ni kukumbushana, make ukiwa Vitani na Risasi zinatoka kila upande unaweza kusahau kama mwenzako ametangulia.
 
duh.. hili linaweza kuwauma kama tumewashtukia.. itabidi waanzishe JF yao..
 
mhh ,minjemba hii hata haya hawana ,hao wote watatu wa wawizi inakuwaje?.kwa nini tusimwambie mwenye mzigo wake unamalizwa.Ahh lakini ya nini we acha tunyamaze tu, maana ufisadi wa huyo mwenye mzigo wake naye hatuujui labda na yeye ana play boy wake maana hawa wenzetu kwa sababu ya mihela ya bure wanaishi kama wazungu,kila mtu kivyake,mpaka watoto wao huwezi kuamini wanavyoishi ukibahatika kuokota jamani umeukata.
tutaishia kusema tu hatuwawezi,wenyewe wanaitana mashujaa, sasa sisi ninani kwao.
NAOMBA NIJIBU HAYO UNAYOSEMA NIKWELI? MAANA HAINGII AKILINI KAMA SUGAR DADY HUYU ANAFANANA NA HAYO UNAYOTUPA.HALAFU UNASEMA HILO NI TONE LA MAJI TU 'INATISHA! IKIWA KATIKA KIKOMBE CHA KAHAWA ITAKUWAJE.
HE HAYA KWAHERI
TUMUACHIE MUNGU SIJUI ITAKUWAJE SIKU MTU APATE MSHTUKO WA MOYO YUPO NYUMBA NDOGO.

SEFF
 
TUHUMA za ufisadi zilizosambazwa katika mtandao wa intaneti zikimlenga Spika wa Bunge, Samuel Sitta, zimesababisha Ofisi ya Bunge kuanzisha uchunguzi dhidi ya kiongozi huyo wa juu wa mamlaka hiyo ya dola.
Taarifa za kuanza kwa uchunguzi huo zilitangazwa na Katibu wa Bunge, Damian Foka wakati alipofanya mahojiano na gazeti hili, ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana.

Kwa mujibu wa Foka, madai ambayo atayafanyia uchunguzi ni yale yanayomhusisha Spika na tuhuma za kuwasilisha katika ofisi ya Mhasibu Mkuu wa Bunge risiti za kughushi za matumizi yake.

“Ofisi za Bunge hazina taarifa za Spika kughushi risiti, nipeni muda niwasiliane na wakuu wa vitengo husika, ili tutafute ukweli kuhusu tuhuma hizo, na iwapo tutabaini lolote tutatoa majibu. Ile ni ofisi ya umma na mali zake zinatakiwa zitumike kwa matumizi yanayopaswa na si vinginevyo,” alisema Foka.

Pamoja na hilo, Foka alikiri madai yaliyoandikwa katika mtandao wa intaneti yanayoeleza kuwa, Sitta aliwasilisha risiti ya shilingi milioni mbili aliyonunulia dawa kutoka katika duka moja la dawa lililopo Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Aidha, alisema baada ya kuwasilisha risiti hiyo, alimwelekeza alete pia cheti cha daktari kilichokuwa kikionyesha kuwa alitakiwa kutumia dawa zenye gharama hizo kutokana na matatizo yake ya kiafya katika kipindi cha wiki moja.

“Ni kweli kuwa mwezi uliopita, Spika Sitta alilipwa shilingi milioni mbili katika kipindi cha wiki moja kwa ajili ya kununulia dawa katika duka la dawa la Oysterbay,” alisema Foka.

Alisema malipo hayo ni halali kwa sababu Ofisi ya Bunge ina taarifa kuhusu matatizo ya kiafya ya Spika Sitta ambayo hata hivyo hakutaka kuyaweka bayana kwa madai kuwa maradhi ya mtu ni siri yake na daktari wake.

Hata hivyo taarifa ambazo gazeti hili linazo zinaeleza kuwa, Spika amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya miguu ambayo kimsingi ndiyo aliyokuwa akiyatibu kupitia dawa alizonunua katika duka hilo la dawa.

Kuhusu madai kwamba Spika amekuwa akijihusisha katika matumizi mabaya yasiyotambulika kisheria na kikanuni kwa madaraka yake, ya magari mawili ya Bunge aliyopewa kwa shughuli zake binafsi, Foka alisema hana taarifa hizo na kuongeza kuwa uwezekano wa kuwepo kwa jambo hilo ni mdogo.

Wakati Foka akitoa taarifa hizo, maofisa kadhaa wa Bunge waliozungumza na Tanzania Daima wanaeleza kuwa, siku chache zilizopita ofisi ya Katibu wa Bunge ilipata kumhoji Sitta kuhusu kuwapo kwa madai hayo yanayomhusisha na matumizi yasiyofaa ya magari ya umma.

Foka pia alikanusha madai kwamba Ofisi ya Bunge imekuwa ikilipa gharama za umeme na maji kwa baadhi ya watu walio na uhusiano wa karibu na Spika, ambao kimsingi hawastahili kupata malipo hayo.

Pia alikanusha madai kuwa, kamati moja ya kudumu ya Bunge iligundua kuwepo mapungufu katika matumuzi ya fedha yaliyofanywa na Spika, lakini wajumbe wake walinyamazishwa na Sitta mwenyewe baada ya kuwatisha kuwa, iwapo wangeweka hadharani upungufu huo, wangekabiliwa na adhabu ya kunyimwa posho pamoja na kutopangiwa safari za nje.

Akizungumza madai kwamba Sitta amekuwa akilipwa kiasi kikubwa kwa ajili ya safari anazofanya ndani na nje ya nchi, na pia kujilimbikizia deni kubwa linalotajwa kufikia sh milioni 60, Foka alisema anachofahamu, Spika anasafiri nje na huwa analipiwa huduma ya maradhi na nusu ya asilimia 20 ya posho kama fedha za matumuzi na si zaidi ya hapo.

Naye Mkurugenzi wa Elimu ya Umma na Uhusiano wa Kimataifa wa Bunge, Jose Mwakasyuka ambaye alikuwapo wakati Foka akihojiwa, alisema mali za Bunge zipo salama na kwamba tuhuma zinazoelekezwa sasa kwa Spika zina kila dalili ya kuwepo nia ya makusudi ya kumchafua.

“Hizi tuhuma ni za kupakana matope na kuchafuliana majina, kwani tuhuma zenyewe hazimtaji nani aliyezitoa. Nadhani kuna watu wanataka waandishi waache kuandika mambo ya msingi kwa ajili ya maendeleo ya nchi na badala yake wajielekeze kwenye tuhuma dhidi ya viongozi,” alisema Mwakasyuka.

Hivi karibuni, Spika Sitta alizungumza na gazeti hili kuhusu tuhuma mbalimbali zinazoelekezwa kwake na kueleza kuwa, hawezi kuzizungumzia kwa sababu zinatolewa na wahuni wenye lengo la kumchafulia jina lake mbele ya jamii.

Mbali ya hilo, Sitta alilielekeza Tanzania Daima kuwasiliana na maofisa wa Bunge ili kupata ukweli wote kuhusu madai hayo yaliyoandikwa katika mtandao mmoja wa intaneti

SOURCE: TANZANIA DAIMA
 
Hivi huyu Sitta hajajua kwamba JF ndiyo kombora la kuangusha vigogo. Sasa achukulie mzaha haya yanayojadiliwa hapa kama atapona. Ukiingia kwa kashafa ni kashfa hizohizo zitakazokutimua!
 
Hmm! Dawa za 2 mil, huh? I can come up with a few:
A) 2nd line ARVs for HIV
B) Chemotherapeutic agents for a cancer
None of the above are anything 2 b ashamed of so Bunge better tell us what they have been doing with OUR money!
I am sure he could afford 2 buy the drugs out of his own pocket if he wanted to! Kuna waTZ wanakufa kwa kushindwa kununua dawa kama Insulin wao wanaspend govt monies on fancy remedies.
Tut tut!!
 
Hivi huyu Sitta hajajua kwamba JF ndiyo kombora la kuangusha vigogo. Sasa achukulie mzaha haya yanayojadiliwa hapa kama atapona. Ukiingia kwa kashafa ni kashfa hizohizo zitakazokutimua!
sita his days are countable now.anaandamwa na dhambi ya usaliti na siku moja itantoa nje ya ukumbi.
 
..Samuel Sitta ameoza tangu zamani sana alipokuwa DG wa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Mkuu Dodoma, maarufu kama CDA. Pengine hata kabla ya hapo.

..Hizi taarifa za ngono zilikuwepo tangu akiwa waziri ktk serikali ya Kambarage.

..Nilifikiri kwamba kwasababu ya uzee na umri basi atakuwa amepumzika ngono.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…