Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta


Tusitoke sana nje ya mada, field ya real estate ndio ugali wangu, hasa maeneo ya oysterbay, masaki na ada estate, kwa hiyo sibahatishi price za maeneo hayo.

Kwa kuanzia tu anza kwa haohao Rupia waulize kupangisha lile hekalu lao la mwaya street masaki wanakula kiasi gani kwa mwezi...usisahau kurudi na jibu hapa jamvini!

Hapo hatujagusa mijengo ya mitaa ya coral beach, masaki, utapagawa!
 
You can have something that is enough but limited.. ! enough that is to satisfy current needs but limited as to its constant supply! I beg u not to get confused.


Double-talk
 
Last edited:
Spika Pelosi wa Marekani analipwa mshahara dola 18,000 kwa mwezi sawa na Tshs. 24,000.000 na anakatwa kodi, Spika Sitta analipwa Tshs. 16,000,000 na hakatwi kodi. Akiongezewa na marurupu mengine yawezekana kabisa anamzidi Spika Pelosi kwa mbali.

Mtumishi wa chini wa serikali Marekani anaweza akalipwa USD 2,400 kwa mwezi sawa na Tshs. 3,200,000 kwa mwezi lakini masikini wa TZ analipwa Tshs. 100,000 hadi 300,000 ! asilimia 0.1% - je mpo ?

Tutalinda hadhi ya Spika na wengineo hata kama kwa kufanya hivyo tunawaua watoto wetu kwa njaa na maradhi. Na huyo anayekubali kufanyiwa kufuru kama hii tumweleweje, awe Spika, Jaji Mkuu, Gavana au Raisi mwenyewe na Bunge tunalolichagua kuisimamia serikali kwa niaba yetu , tulieleweje ?

Kwamba Spika aliyetangulia aliweza kuuziwa nyumba zote mbili zilizokuwa za Spika (moja kwake na lingine kwa mkewe) na sasa tunalipa Tshs. 10,000,000 kama pango la Spika na huku Uchaguzi Mkuu unapiga hodi ni uenda wazimu. (NB - Maspika wetu wana bahati ya wake zao kuteuliwa mawaziri !)
 
Tatizo la hii forum watu wameshakariri ya kuwa Ufisadi ni pale tuu unapofanywa na Rostam et al.

exactly
Hao wabunge wote ni mafisadi hiyo pesa wanayojilipa ni ndefu sana tena sana
 

sio spika tu Wabunge wote,kwanza hakuna wanachokifanya huko ilipaswa maximum walipwe laki tano.Harafu mbunge wakati akiwa mbunge sharti aishi jimboni kwake
 
sio spika tu Wabunge wote,kwanza hakuna wanachokifanya huko ilipaswa maximum walipwe laki tano.Harafu mbunge wakati akiwa mbunge sharti aishi jimboni kwake
wangestaafu in less than 6 months woote!wakatafute "another gold mine".

wangebaki wachapakazi tu.
 

naomba radhi kwanza lakini VIONGOZI WETU NI MAJAMBAZI!

maelezo yako yanatoa taswira halisi ya nchi yetu.ikituhusu sisi sawa,wao tuwatunzie heshima, P*&^%FU.kwani sie sio watu!

si binadam wote ni sawa?!au ukiitwa mheshimiwa spika unaota mapembe?!
 
Tukipunguza jazba na kuamua kufikiri sana, mjadala utakua mzuri zaidi as tutaelekea kwenye kutatua moja ya matatizo ya taifa. Ila kwa mwendo huu wa Sitta this, Sitta that, sitta...hatutaishia popote.
 
ndugu yangu rufiji nakubaliana na msimamo wako in general

Mzee Vassil,

Ni jambo la kusikitisha kufikiri ya kuwa simply kwa kuwa sheria aikuvunjwa basi ufisadi aujafanyika. Ni lazima tutambue ya kuwa ufisadi mwingine sio tu unalindwa na sheria; bali, unafanyika kwa mujibu wa sheria pia.
 
Mzee Vassil,

Ni jambo la kusikitisha kufikiri ya kuwa simply kwa kuwa sheria aikuvunjwa basi ufisadi aujafanyika. Ni lazima tutambue ya kuwa ufisadi mwingine sio tu unalindwa na sheria; bali, unafanyika kwa mujibu wa sheria pia.

Hasa ukizingatia wao ndio wanatunga sheria.
 
Mzee Vassil,

Ni jambo la kusikitisha kufikiri ya kuwa simply kwa kuwa sheria aikuvunjwa basi ufisadi aujafanyika. Ni lazima tutambue ya kuwa ufisadi mwingine sio tu unalindwa na sheria; bali, unafanyika kwa mujibu wa sheria pia.

mawazo ya namna hiyo hayana msingi; Kama sheria haifai haina maana hatuitii; tunafanya juhudi kuibadilisha. Kama sheria ni dhaifu tunafanya juhudi kuipa nguvu. Mtu ambaye anatii sheria iliyopo ambayo ni sheria halali unaweza kumuita vyovyote lakini siyo fisadi kwani Ufisadi kunahusiana na kuvunja sheria.

Kwa sababu tukikubali kuwa ufisadi ni kutii sheria basi tuna matatizo mengine kabisa.

Kama tunaona kuwa sheria zilizotungwa zinatengeneza mazingira ya kuruhusu vitendo vya kifisadi kufanyika (kwa kuweka mianya mbalimbali) basi ni jukumu letu kuwaondoa watunga sheria hao na kuwaweka wale ambao watatunga sheria ambazo zitaziba mianya hiyo. Hili naamini ni la kweli zaidi.

Sheria zetu ni dhaifu mno, lakini hawa watunga sheria dhaifu wanatoka wapi? Wanawezaje kuingia madarakani? Well.. "we the people"! Hivyo basi utaona utendaji wao wa kazi unahusiana moja kwa moja na watu waliowawweka.

Kama sisi wananchi wakati wa kampeni tunakubai kanga, mashati, nyimbo na pilau tukawarudisha watu wale wale, wakati tunajua udhaifu wao kiuongozi watakapoanza kuboronga kwanini tuwanyoshee vidole wao?

Sitta hakujipachika Uspika kapigiwa kura na wenzake! Hao waliompigia kura hawakujipachika pale wamepigiwa kura na wananchi.

So.. the buck stop with the people.. that is why.. tunaongoza mapambano ya fikra, kwani bila kubadili fikra, watu hawezi kubadili kura!
 

Unaweza kutuma kainzi kakatuletee data za mishahara na malupulupu ya hao uliowataja hapo juu ili tuanze kuzichambua?
 
Kwenye hii topic sijatia neno... Labda tuangalie kwa ufupi tu...

Nyumba ya zamani ambayo imegeuzwa kuwa Club ni hii hapa:



Na nyumba mpya inayolipiwa $8,000 kwa mwezi ni hii hapa:





 


Wee mwanakijiji vipi?
Yani tenda itolewe na serikali harafu vijikapuni viombe tenda na serikali hiyohiyo tena nayo iingie ktk mchakato wa kuiombe tenda hiyo hiyo.Basi nivichekesho tupu.
 
Kwenye hii topic sijatia neno... Labda tuangalie kwa ufupi tu...

Nyumba ya zamani ambayo imegeuzwa kuwa Club ni hii hapa:


Mzee Invisible,

Hebu tusaidie kidogo kwa hiyo Nyumba ya kwanza imegeuzwa Club. . . Nadhani hii nyumba ya kwanza ilikuwa aina hadhi ya Spika. Kweli watanzania tumelala ...
 

unachanganya mambo mkubwa rufiji anaamini na mimi nakubaliana nae ni kitu kinachotokea kila siku kufanya ufisadi bila kuvunja sheria kwa hiyo mawazo ya kwamba ili mradi sheria haijavunjwa hakuna ufisadi ni potofu
 
hizi biashara ya the bucket stops with people TZ hai-aplyy hata siku moja.kwa sababu hakuna DEMOKRASIA.

wangapi wanakufa kwa kukosa dawa?matibabu?polisi akikaa kwenye nyumba ya mabati no one talks about hadhi and dignity of our constitution's guards.lakini hiyo minjemba inayotuibia kila siku mnataka iwe na hadhi.kwa lipi la maana wanalolifanya?!hizo nyumba zote mbili,ya zamani na mpya in zaidi ya mara 10 ya ile ya mtanzania wa kawaida.zinatosha!mnataka waishi kama wako DC?!kwa lipi,kwa kipi?!we are soo proud of nothing.the day we learn to be humble may be things will change.

nchi yetu yenyewe haina hadhi,tunaitwa omba-omba,all the funny names huku tuliko,kwa ajili ya poor perfomances ya hawa tunaowapa dhamana ya madaraka miaka enda miaka rudi sasa.

the only time utaona action ni pale maslahi yao miungu watu yanapoguswa.if you are out of the system TZ you are worthless.watanzania hamna anayewasikiliza.so stop telling us tutaanzwa kusikilizwa leo kwa sababu eti spika kapata skendo.may be in 40 years to come lakini sio katika bunge lile lililojaa wake,shangazi,watoto,wajomba,maswahiba wa nanihiii na nanihiii.

watanzania sie always tunaimbiwa all the crap about democracy mambo yakiwa hovyo,oh tuache sheria ifate mkondo,oh uchaguzi ulikuwa wa huru na wa haki.oh,flani kachaguliwa kwa sababu hamna wengine wenye vigezo!siku ya uchaguzi au kuwekana wao kwenye vyeo democracy goes to hell.full double standards
 
Kwenye hii topic sijatia neno... Labda tuangalie kwa ufupi tu...

Nyumba ya zamani ambayo imegeuzwa kuwa Club ni hii hapa:



Na nyumba mpya inayolipiwa $8,000 kwa mwezi ni hii hapa:







Sasa mkuu tafadhali tunaomba picha za nyumba za polisi pale Tazara (full suit) mabati juu mpaka chini. Kwa upande wangu naona wazi hii ni kufuru na ufujaji wa pesa bila huruma.
Hiyo nyumba ya mwanzo iko sehemu nzuri tu ilikuwa ni kuifanyia ukarabati kidogo na ingemtosha kufanya apate usingizi bila shida. Kulikuwa na sababu gani ya kuibadilisha hiyo nyumba kuwa Pub?. Jamani viongozi wetu tafadhali muwe na huruma na watanzania, mnachangia sana kuwaletea watanzania maisha magumu kwa kupenda maisha ya starehe.
 
8,000 x 12 x 5 = usd 480,000 in five years only housing; kweli masikini hajijui kuwa ni masikini; hata akili haifanyi kazi. Hata Raisi hana akili!

Hapa umegusa pabaya, usije ukaacha jf ikafungiwa kama zeutamu ilivyotoa picha ya rais!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…