Ni nini sababu ya binadamu kuletwa Duniani?

Ni nini sababu ya binadamu kuletwa Duniani?

Hukutengenezewa kama upungufu, ni zawadi, kwamba uwe na free will. changamoto tu ni kuwa will power haina mipaka, na unaweza ukafanya jambo hata kinyume na aliyekupa huo uwezo wa kuchagua. Hasa ndo kinachokutesa.

Hasira ya Mungu ipo kwasababu uliumbwa ukiwa mkamilifu. Kwa hiyo mapungufu uliyonayo ni ya kujitakia tu, ni kama unavyolea mtoto wako alaf afanye kitu tofauti na unavyo mwelekeza utakasirika
Mweh
 
Habari wanaJf
Nimekuwa nikijiuliza swali moja la msingi sana lakini majibu thabiti nimekuwa nikikosa kabisa...

Kwa wale wanaoamini kuhusu uwepo wa Mungu naomba wanijuze kwanini tumeletwa hapa duniani ambako tunaishi maisha mafupi na kupita, je Mungu hakuona namna nyingine ya kutufanya tufike huko kwenye maisha ya milele kunakosemwa na vitabu vyake bila kupitia hapa duniani kwenye shida na karaha?
Kulikuwa na haja ipi kutupitisha kwenye mateso hali ya kuwa ipo sehemu salama tunaelekea? ( Kwanini alitupitisha duniani?)

Hata wale wasioamini uwepo wa Mungu nao naomba wanisaidie kujua juu ya hili swali langu...kama hakuna maisha baada ya haya kwanini tupitishwe hii sehemu yenye taabu na mateso mengi tena kwenye maisha mafupi..kwanini tumetolewa huko tulikokuwa na kuletwa hapa duniani ambako kuishi kwetu ni muda mfupi na tisingebaki huko huko kama tulikuwa na maisha kabla?

Nini sababu ya sisi binadamu kuletwa/kupitishwa hapa duniani?
Swali lako kwa wasioamini mungu ni batili kwa sababu wao hawaamini unapitishwa duniani na yoyote na wala hawaamini wametolewa popote huko walikokuwa.
 
evolution.................................... hakuna cha Mungu hapa it is purely science..................
Kupitia hiyo science itueleze ni kwanini tumekuja duniani tena kuishi maisha ya muda mfupi sana
Pia kama ipo sehemu tunaelekea kwanini kusingetumika njia nyingine tofauti na kifo?
 
Kwani wewe una upungufu gan ambao una uhakika hauwezi kuushinda?
Je ni watu wote tunao huo?
(Ingekuwa hivyo basi ingekuwa technical error za uumbaji), lakin kile kinachokusumbua wewe mwenzako anakiweza na vice versa, hii ina maana hata wewe ungeamua ungeweza tu kama hao binadamu wenzako.
Kwanini nihangaike kuushinda wakati ndivyo nilivyoumbwa? Mateso yote ya kazi gani? Tungeumbwa perfect hapa tungekuwa tunasifu na kuabudu kwa raha zote. Na hata hizo amri kumi za mungu zisingekuwepo maana tusingekuwa na uwezo wa kuzitenda kwa jinsi tulivyoumbwa kikamilifu.
 
Upo hapa kwa naturally chance tu , na wewe ndio upo hapa kuyapa maisha maana .
Hakuna mahali kwingine kwenye kuleta maana zaidi ya hapa duniani kwenye mateso na karaha?
 
Back
Top Bottom