Tundu Lissu anaendelea kushikiliwa gerezani si kwa sababu watawala waliomweka huko wanataka aendelee kuwa gerezani.
Kubaki gerezani kwa Tundu Lissu sasa hivi kunawatesa sana watawala, laiti kama wangekuwa na njia ya kumwondoa huko bila ya kuonekana kuwa wameshindwa kumdhibiti wangefanya hivyo haraka ili swala lake lisiendelee kuwatesa wao, hata kuliko linavyomtesa Tundu Lissu mwenyewe.
Wamejaribu kila njia ya kumtumia ili wajijengee sifa na kujisafisha mbele za waTanzania lakini imeshindikana kwa kukosa ushirikiano toka kwa mfungwa huyo.
Tundu Lissu akisema anataka kutoka gerezani kesho, ni rahisi kwake kuwaeleza tu watawala waovu kuwa atashirikana nao kwenye juhudi zao za kujisafisha; kama vile kushawishi waTanzania wakubali uwepo wa maridhiano FEKI.
Tundu Lissu anaendelea kubaki gerezani kwa sababu hataki kushiriki katika unajisi wa taifa hili na wananchi wake.
Kwa sababu hiyo, Tundu Lissu anastahili kutambuliwa kuwa mzalendo wa nchi hii.
Amekataa kuuza utu wake na wa waTanzania ili ajiokoe nafsi yake mwenyewe.
Kwa hiyo, ni jukumu letu sote kutambua mchango muhimu anaoutoa Tundu Lissu kwa taifa hili.
Na katika pumzi hiyo hiyo, napenda vile vile kuwapongeza waTanzania wengine wote wanaoendelea katika mapambano haya ya kuliokoa taifa letu kutoka wa watu waovu hawa. Namtambua kwa nafasi yake adimu sana Mzee Jaji Warioba.
Historia ya taifa hili itawatambua watu hawa waliosimama kidete kukataa kushiriki katika hujuma dhidi ya taifa letu..
Kubaki gerezani kwa Tundu Lissu sasa hivi kunawatesa sana watawala, laiti kama wangekuwa na njia ya kumwondoa huko bila ya kuonekana kuwa wameshindwa kumdhibiti wangefanya hivyo haraka ili swala lake lisiendelee kuwatesa wao, hata kuliko linavyomtesa Tundu Lissu mwenyewe.
Wamejaribu kila njia ya kumtumia ili wajijengee sifa na kujisafisha mbele za waTanzania lakini imeshindikana kwa kukosa ushirikiano toka kwa mfungwa huyo.
Tundu Lissu akisema anataka kutoka gerezani kesho, ni rahisi kwake kuwaeleza tu watawala waovu kuwa atashirikana nao kwenye juhudi zao za kujisafisha; kama vile kushawishi waTanzania wakubali uwepo wa maridhiano FEKI.
Tundu Lissu anaendelea kubaki gerezani kwa sababu hataki kushiriki katika unajisi wa taifa hili na wananchi wake.
Kwa sababu hiyo, Tundu Lissu anastahili kutambuliwa kuwa mzalendo wa nchi hii.
Amekataa kuuza utu wake na wa waTanzania ili ajiokoe nafsi yake mwenyewe.
Kwa hiyo, ni jukumu letu sote kutambua mchango muhimu anaoutoa Tundu Lissu kwa taifa hili.
Na katika pumzi hiyo hiyo, napenda vile vile kuwapongeza waTanzania wengine wote wanaoendelea katika mapambano haya ya kuliokoa taifa letu kutoka wa watu waovu hawa. Namtambua kwa nafasi yake adimu sana Mzee Jaji Warioba.
Historia ya taifa hili itawatambua watu hawa waliosimama kidete kukataa kushiriki katika hujuma dhidi ya taifa letu..