Ni kweli USA supremacy ina collapse?

Ni kweli USA supremacy ina collapse?

Hill liko wazi ila je kuna viashiria vinavyoonesha kuwa itadondoka ndani ya muda mfupi ujao kama wadau wengi wanavyodai au bado sana ..kwa wewe unavyoona
Suala la U.S.A kuanguka sio suala la muda mfupi [miaka 5- 10 ijayo] ni suala la [miaka 50- 100 ijayo ] lakini dalili za kutikisika kwa dola la kimarekani zinaonekana hasa hasa katika kutikisika kwa dola na kupungua kwa nguvu ya ushawishi kwa baadhi ya mataifa . haya mambo ya kuanguka dola huanza taratibu taratibu inayochukua miaka na miaka mpaka kuanguka kabisa.
 
Suala la U.S.A kuanguka sio suala la muda mfupi [miaka 5- 10 ijayo] ni suala la [miaka 50- 100 ijayo ] lakini dalili za kutikisika kwa dola la kimarekani zinaonekana hasa hasa katika kutikisika kwa dola na kupungua kwa nguvu ya ushawishi kwa baadhi ya mataifa . haya mambo ya kuanguka dola huanza taratibu taratibu inayochukua miaka na miaka mpaka kuanguka kabisa.
Mrithi unamuona nani? Binafsi simuoni Russia wala China...
 
Yeah hiyo Empire inaelekea mwisho. Empire yoyote lazima iwe na wanaume kamili. But now that country has become a Gay country.
Racial discrimination inazidi kukua.
Uchumi wao ni WA makaratasi... Wako kwenye bubble Debt... Italipuka muda wowote.
Plus The elites wameshaitumia USA vya kutosha it time now wanamove kwenye next phase "NEW WORLD ORDER" And since it's new then they will put a new Wolrd Police Country.......
 
Marekani ushawishi wake upo kwenye hela yake tu, kile china na urusi wanachokifanya walitaka kufanya marais kadhaa wakaambulia kitanzi. Marais hao ambao walijaribu nikiwa na akili timamu ni ghadafi maana alitaka kuanzisha golden ruby, saddam hussein alitaka kuanzisha kuuza mafuta kwa pesa yake kilichofuata ni wote hatunao kwa sasa.
Hii sasa akiponyoka kwa mrusi nitakuwa sina matumaini tena ya yeye kuanguka. Kwa sasa china na mrusi wana swift ya kwao. Marekani dola yake anamimashine inaprint usiku na mchana. Jaribu nchi ingine ujinga huo utaona kitakachotokea. Alijaribu mwamba mmoja zimbabwe huko, ilibidi atumie hela ya southafrica kujinasua.
Siipendi marekani kutoka moyoni japo natamani kuishi marekani
Ha ha ha ha ha ha umemaliza mkuu

Leo Russia anapigana anatumia rasilimali zake nyingi, China anatafutwa vibaya saana huko Taiwan.

US yeye amekaa tu kwake anamwaga pesa na vifaa, tena hatoi bure, pengine anatumia fedha za warusi wanazozishikilia.
 
Habari wakuu,

Kulingana na upepo unavyoenda sasa inasemekana ushawishi wa Marekani kisiasa na kiuchumi unakwenda kuanguka kwa kasi. Binafsi sio mtaalam wa siasa za kimataifa hivyo nilikua naomba wadau wenye uelewa wa haya mambo wanisaidie kama hii inshu ni kweli au ni porojo tu za vijiwe vya kahawa.

NB: Tafadhali wakuu naomba tuweke ushabiki pembeni tujadili facts.

Karibuni wakuu
Hicho kitu ndio kinatokea kaka,na China ndio nchi inayopora ushawishi wa USA kiuchumi na kisiasa.
Tukianza na kiuchumi,taktiban mataifa 138 ulimwenguni yamekua yakipata financial aid ikiwemo mikopo na ruzuku kutoka China,kuna ripoti itokayo IMF ilijadiliwa 2020 ikionesha kuwa taifa lililokopesha mataifa mengi ulimwenguni ni China hususan mataifa ya Africa,Asia,south and Central America ambako world population ndipo ilipoelemea,kiviwanda China anachangia 64% ya bidhaa za viwandani mengine kaka yanajulikana.
Kisiasa kaka ntarudi kuelezea navyojua mm kwa upeo wangu.
 
Hicho kitu ndio kinatokea kaka,na China ndio nchi inayopora ushawishi wa USA kiuchumi na kisiasa.
Tukianza na kiuchumi,taktiban mataifa 138 ulimwenguni yamekua yakipata financial aid ikiwemo mikopo na ruzuku kutoka China,kuna ripoti itokayo IMF ilijadiliwa 2020 ikionesha kuwa taifa lililokopesha mataifa mengi ulimwenguni ni China hususan mataifa ya Africa,Asia,south and Central America ambako world population ndipo ilipoelemea,kiviwanda China anachangia 64% ya bidhaa za viwandani mengine kaka yanajulikana.
Kisiasa kaka ntarudi kuelezea navyojua mm kwa upeo wangu.
Shukrani mkuu nasubiri
 
Mrithi unamuona nani? Binafsi simuoni Russia wala China...
Mrithi hatabirikagi kirahisi boss alafu ata kipindi marekani anaanza kupanda juu mataifa mengine hayakuisi ata atakuja kuwa super power ivi mbinu alizotumia Marekani kuwa juu ndyo izoizo China anazitumia siku Marekani akija kujiingiza kwenye vita kubwa ndyo utakuwa mwisho wake atabaki kuwa mropokaji kama uingereza ndyo maana ata yeye hataki kujiingiza kwenye vita na mataifa makubwa kama yeye
 
Suala la U.S.A kuanguka sio suala la muda mfupi [miaka 5- 10 ijayo] ni suala la [miaka 50- 100 ijayo ] lakini dalili za kutikisika kwa dola la kimarekani zinaonekana hasa hasa katika kutikisika kwa dola na kupungua kwa nguvu ya ushawishi kwa baadhi ya mataifa . haya mambo ya kuanguka dola huanza taratibu taratibu inayochukua miaka na miaka mpaka kuanguka kabisa.
Inaweza ikatikisika na ikaja kukaa vyema tena. Nakubaliana na wewe kuwa kudondoka kwa US sio suala la leo wala kesho.

Toka miaka ya 60, 80 na 2001 au 2002 iliwahi tabiriwa kufikia 2010 China atakuwa super power, leo tupo 2020 na bado dalili za US kuanguka hazipo ila ni ushabiki tu.

China azidi kujijenga zaidi ktk teknolojia, wazawa kuwekeza zaidi nchini kwao na kukuza pesa yake, huenda hii ikasaidia mno kumpiku US.
 
Habari wakuu,

Kulingana na upepo unavyoenda sasa inasemekana ushawishi wa Marekani kisiasa na kiuchumi unakwenda kuanguka kwa kasi. Binafsi sio mtaalam wa siasa za kimataifa hivyo nilikua naomba wadau wenye uelewa wa haya mambo wanisaidie kama hii inshu ni kweli au ni porojo tu za vijiwe vya kahawa.

NB: Tafadhali wakuu naomba tuweke ushabiki pembeni tujadili facts.

Karibuni wakuu
tukirudi hapo hapo kwenye uchumi watu watakwambia China anategemea soko la USA ili auze bidhaa zake huo ni uongo,China anaendelea kwa uwekezaji wa makampuni ya USA huo ni uongo.
China takriban asilimia 70 ya viwanda ni vya wazawa na vina mikono ya serikali,pia China ndio jamii yenye top skilled labours duniani hiivyo ht USA aseme anaondoa uwekezaji CHINA haitoumia wala kuathirika kwasababu asilimia 70 ya viwanda vya wazawa,1992 China ikiwa inatangazwa kuwa taifa linalokua kwa kasi kiuchumi ilikua ishajenga viwanda takriban 45000 ambavyo vyote vya kizawa,hivyo uwekezaji waUSA China hauna nguvu.
kisoko China yenyewe ni soko,maana ina watu wanaokadiriwa kuwa ni robo ya dunia idadi yake pia Africa,Asia,South Ametrica ikiwemo na mataifa ya Ulaya kote China ana soko lake.Hivyo USA akigoma China kuuza bidhaa kwake wala halina athari kubwa kama watu wadhaniavyo.
Fuatilia ule mkasa wa trade war 2018 pindi Trump alipoipandishia China ushuru nayo China ikajibu kwa kupandisha mara tatu yake USA weakarudi mezani kuyamaliza.WATU PIA TUNASAHAU KUWA China ana treasury bill ya zaidi ya $3 trillions kwa USA pia tunasahau kuwa China ina reserve ya dollar inayoshindana na USA mwenye dollar yake.
 
tukirudi hapo hapo kwenye uchumi watu watakwambia China anategemea soko la USA ili auze bidhaa zake huo ni uongo,China anaendelea kwa uwekezaji wa makampuni ya USA huo ni uongo.
China takriban asilimia 70 ya viwanda ni vya wazawa na vina mikono ya serikali,pia China ndio jamii yenye top skilled labours duniani hiivyo ht USA aseme anaondoa uwekezaji CHINA haitoumia wala kuathirika kwasababu asilimia 70 ya viwanda vya wazawa,1992 China ikiwa inatangazwa kuwa taifa linalokua kwa kasi kiuchumi ilikua ishajenga viwanda takriban 45000 ambavyo vyote vya kizawa,hivyo uwekezaji waUSA China hauna nguvu.
kisoko China yenyewe ni soko,maana ina watu wanaokadiriwa kuwa ni robo ya dunia idadi yake pia Africa,Asia,South Ametrica ikiwemo na mataifa ya Ulaya kote China ana soko lake.Hivyo USA akigoma China kuuza bidhaa kwake wala halina athari kubwa kama watu wadhaniavyo.
Fuatilia ule mkasa wa trade war 2018 pindi Trump alipoipandishia China ushuru nayo China ikajibu kwa kupandisha mara tatu yake USA weakarudi mezani kuyamaliza.WATU PIA TUNASAHAU KUWA China ana treasury bill ya zaidi ya $3 trillions kwa USA pia tunasahau kuwa China ina reserve ya dollar inayoshindana na USA mwenye dollar yake.
Sawa mkuu...unaiona China ikiipiku US ndani ya miongo kadhaa ijayo?
 
Hicho kitu ndio kinatokea kaka,na China ndio nchi inayopora ushawishi wa USA kiuchumi na kisiasa.
Tukianza na kiuchumi,taktiban mataifa 138 ulimwenguni yamekua yakipata financial aid ikiwemo mikopo na ruzuku kutoka China,kuna ripoti itokayo IMF ilijadiliwa 2020 ikionesha kuwa taifa lililokopesha mataifa mengi ulimwenguni ni China hususan mataifa ya Africa,Asia,south and Central America ambako world population ndipo ilipoelemea,kiviwanda China anachangia 64% ya bidhaa za viwandani mengine kaka yanajulikana.
Kisiasa kaka ntarudi kuelezea navyojua mm kwa upeo wangu.
Hizo nchi zote ulizotaja ambazo zina ushawishi kutoka China ni za kawaida na nyingi ni masikini. Umewahi kuuliza kama China soko lake lingekuwa kwa hizo nchi angekuwa na utajiri huu wa sasa?

Umewahi kujiuliza hivyo viwanda vya china vilivyopo, ni makampuni mangapi makubwa ni ya wachina wenyewe?

Nachotaka nikukumbushe ni kuwa, China uchumi wake anategemea mno kuuza bidhaa zake Ulaya na US, huko ndiko anakoingizia pesa. Makampuni makubwa yanayofanya china isifike ya viwanda na wao kupata ruzuku na makodi makubwa zinamilikiwa na mabeberu wa Ulaya na America.

Hivyo vitaifa ulivyovisemea haviwezi kumfanya mchina kuwa na impact kubwa ktk uchumi wake. Sasa mtazame US. US ameikamata Ulaya yooote, hapa unamzungumzia UK, FRANCE, GERMAN na ITALY. Hizi ni nchi zenye pesa haswa, nchi moja inaweza ikalipiku bara zima la Afrika kiuchumi au ikafikia nusu ya bara zima.

US uko Asia ana ushirika mkubwa mno na huyo Mchina, bado ana ushirika na TURKEY n.k nchi zenye nguvu kubwa ya kiuchumi karibia zote yeye amezishika mkononi, hapo sijakutajia Japan wala Korea Kusini au Canada.

US bado yupo sana, pengine tuanze kusema miaka 2100 huko ila sio hii 2020 au 2050.
 
Sawa mkuu...unaiona China ikiipiku US ndani ya miongo kadhaa ijayo?
Kama itaendelea na hii kasi yake basi itaipiku ila ni ngumu maana USA ni taifa linalochukua tahadhari dhidi ya mahasimu wake kwa kiasi kikubwa sana kaka,hivyo China inatakiwa kujiangalia kiundani.
 
tukirudi hapo hapo kwenye uchumi watu watakwambia China anategemea soko la USA ili auze bidhaa zake huo ni uongo,China anaendelea kwa uwekezaji wa makampuni ya USA huo ni uongo.
China takriban asilimia 70 ya viwanda ni vya wazawa na vina mikono ya serikali,pia China ndio jamii yenye top skilled labours duniani hiivyo ht USA aseme anaondoa uwekezaji CHINA haitoumia wala kuathirika kwasababu asilimia 70 ya viwanda vya wazawa,1992 China ikiwa inatangazwa kuwa taifa linalokua kwa kasi kiuchumi ilikua ishajenga viwanda takriban 45000 ambavyo vyote vya kizawa,hivyo uwekezaji waUSA China hauna nguvu.
kisoko China yenyewe ni soko,maana ina watu wanaokadiriwa kuwa ni robo ya dunia idadi yake pia Africa,Asia,South Ametrica ikiwemo na mataifa ya Ulaya kote China ana soko lake.Hivyo USA akigoma China kuuza bidhaa kwake wala halina athari kubwa kama watu wadhaniavyo.
Fuatilia ule mkasa wa trade war 2018 pindi Trump alipoipandishia China ushuru nayo China ikajibu kwa kupandisha mara tatu yake USA weakarudi mezani kuyamaliza.WATU PIA TUNASAHAU KUWA China ana treasury bill ya zaidi ya $3 trillions kwa USA pia tunasahau kuwa China ina reserve ya dollar inayoshindana na USA mwenye dollar yake.
Twende taratibu

Unasema China hategemei soko la US na ulaya kuuza bidhaa zake, si ndio?

Unaweza ukaleta hapa Balanc of Trade baina ya US na China? Pia tutazame BoT ya China na Ulaya?

Naomba tuongee kwa facts ili sasa tujue ni nani muongo.
 
Uchumi makubwa ndiyo sauti ya Mmarekani. Unadhani huo ushawishi ulikuja tu. Uwezo wa Marekani kiuchumi ulisababisha uwezo kijeshi na kisiasa duniani.

Bila uchumi mkubwa na imara ushawishi ungetoka wapi.

Jaribuni kuchambua hoja kikomavu.
Mkuu haitaji rocket science kujua hili,ajaribu tu kufikiria kwenye ukoo yule mwenye utajili wakutisha na yule wakawaida ni nani mwenye ushawishi?.Sasa sijui mtu anakuaje na uchumi mkubwa afu asiwe na ushawishi!
 
Mkuu haitaji rocket science kujua hili,ajaribu tu kufikiria kwenye ukoo yule mwenye utajili wakutisha na yule wakawaida ni nani mwenye ushawishi?.Sasa sijui mtu anakuaje na uchumi mkubwa afu asiwe na ushawishi!
Ha ha ha ha upo sahihi, mwenye pesa ndie mwenye kauli kaka.
 
Hizo nchi zote ulizotaja ambazo zina ushawishi kutoka China ni za kawaida na nyingi ni masikini. Umewahi kuuliza kama China soko lake lingekuwa kwa hizo nchi angekuwa na utajiri huu wa sasa?

Umewahi kujiuliza hivyo viwanda vya china vilivyopo, ni makampuni mangapi makubwa ni ya wachina wenyewe?

Nachotaka nikukumbushe ni kuwa, China uchumi wake anategemea mno kuuza bidhaa zake Ulaya na US, huko ndiko anakoingizia pesa. Makampuni makubwa yanayofanya china isifike ya viwanda na wao kupata ruzuku na makodi makubwa zinamilikiwa na mabeberu wa Ulaya na America.

Hivyo vitaifa ulivyovisemea haviwezi kumfanya mchina kuwa na impact kubwa ktk uchumi wake. Sasa mtazame US. US ameikamata Ulaya yooote, hapa unamzungumzia UK, FRANCE, GERMAN na ITALY. Hizi ni nchi zenye pesa haswa, nchi moja inaweza ikalipiku bara zima la Afrika kiuchumi au ikafikia nusu ya bara zima.

US uko Asia ana ushirika mkubwa mno na huyo Mchina, bado ana ushirika na TURKEY n.k nchi zenye nguvu kubwa ya kiuchumi karibia zote yeye amezishika mkononi, hapo sijakutajia Japan wala Korea Kusini au Canada.

US bado yupo sana, pengine tuanze kusema miaka 2100 huko ila sio hii 2020 au 2050.
Kwa kiasi fulani hujakosea ila wacha nikukumbushe kitu kaka,UCHUMI WA CHINA UMEKUA BAADA YA KUPANUA WIGO WAKE WA KIBIASHARA TAMBUA HILO,NA KUUZA KWAKE BIDHAA ULAYA SIYO KWA HURUMA BALI KWA UBORA WA TEKNOLOJIA ALONAYO,kipindi USA na hayo mataifa unayoyataja yakiinyanyapaa Afrika mwenzako China aliikumbatia Africa kwa kuleta bidhaa zinazoendana na uchumi wa watu wa Africa,pia umesahau kama construction companies zinazoijenga asilimia zaidi 60 ya dunia ni Chinese construction companies,reli,injini za treni,madaraja n.k mataifa mengi hukimbilia Chinese construction companies hilo pia huongeza pato la nchi usisahau hilo.
UARABUNI kuna pesa kuliko huko ulaya na bidhaa za kichina zimejaa uarabuni kuliko bidhaa za wazungu,mfuatilie mchina vizuri ni mfanyabiashara mzuri na mjanja kaka.
 
Back
Top Bottom