Ni kwanini waliotajwa kutafuna mabilioni ya pesa ya walipa kodi na CAG, hawachukuliwi hatua za kisheria?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,160
Ni jambo lilizoeleka kwa mkaguzi mkuu na mdhibiti wa pesa za Serikali (CAG) kuibuka na ripoti kila mwaka, inayoonyesha namna mabilioni ya pesa ya walipa zinavyotafunwa na "wajanja" wachache walioko Serikalini, pasipo kuchukuliwa hatua zozote.

Lakini tunashuhudia magereza yetu, yakiwa yamefurika wafungwa, wakiwa wamehukumiwa kwa vijikesi, vidogo vidogo, kama vile wizi wa kuku!

Ndiyo hapo ninapouliza, hivi kuna sababu gani ya kutusomea hadharani ripoti hizo za CAG, kama Serikali yetu, haina dhamira ya dhati kuwachukulia hatua za kisheria?

Tumeshuhudia, makamu Mwenyekiti wa CCM, Abdrahman Kinana, eti akisema, atamshairi Rais Samia, aweze kuwachukulia hatua za kisheria, wale wote waliotajwa kwenye ripoti hiyo ya CAG!

Hivi umewahi kuona wapi watu waliotenda makosa makubwa kama hayo ya kutafuna mabilioni ya pesa ya walipa kodi wa nchi hii, eti mpaka Rais ashauriwe Ili achukue hatua za kisheria?

Mbona hawa wanaotuhumia kwa vijikesi vidogo vidogo, kama vile wezi wa vibasikeli, wakiwa wamejazana magerezani, wakiwa wameshahukumiwa tayari, kutumikia vifungo vyao, je na hao Rais ameshauriwa kabla ya kupelekwa mahakamani na kuhukumiwa' vifungo vyao??

Huu mtindo unaotumika na Serikali hii ya CCM, ni wa hatari Sana, unaofanya upendeleo wa wazi kabisa na "kubariki" kwa kuwaona wale wezi wa mabilioni ya Serikali, kama mashujaa na kuachiwa watembee kifua mbele, wakati wezi wa vitu vidogo vidogo, kama wale wanaowakwapua vipochi kwa abiria kwenye daladala, ndiyo wahukumiwe vifungo mahakamani na watuhumiwa wengine hata wakipoteza Maisha yao kwa "kuhukumiwa' vipigo na wananchi wenye hasira kali!

Ndiyo maana nchi hii kodi zinakuwa nyingi mno, kama vile tozo mbalimbali, kwenye miamala ya simu, ambazo zinawakamua watanzania wanyonge, kumbe pesa hizo, zinaliwa na watanzania wachache, tuliowaamini na kuwakabidhi madaraka ya juu, Katika nchi hii!

Tunaomba viongozi wetu wa Serikali hii ya CCM, wawe "serious" na wachukue hatua mara moja na tuone watuhumiwa wote waliotajwa na CAG kukwapua mabilioni ya pesa ya walipa kodi wa nchi hii wanafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zao.
 
Hilo ombi likitokea kukubaliwa na hatimaye kufanyiwa kazi ndio utakuwa mwisho wangu wakuja hapa Jamiiforums kuchachafya nisiyoyajua.

Lakini kwa sasa, niulize tu, hiyo Serikali yenye uthubutu wa kufanya hivyo itaongozwa na Chama gani?
ACT, pwaa
CHADEMA, pwaa
CCM, pwaa
...na vile vyama vingine, vivuli, vya hao juu...only time will tell.

Ninayojua hizi Ripoti zikitokea hakuna 'kuu' linalotokea zaidi ya kuimarishwa kwa Vyama vya Kisiasa. Porojo, mihemeko, na vijembe.

Hata Kipanya ana Vijembe! Madenge naye yumo, huko twitani ndiyo usiseme, hata miye Nimo!

CAG,wala, na sintoshangaa nikasikia eti anajiuzulu, kabadilishwa na fedheha wakati hao waliotajwa(kama wametajwa) wanaendelea kupiga ramli za 'kusingiziwa' 'kuonewa'.. kadhalika na kadhalika

Binafsi nitajiuzulu kuingia hapa Jamiiforums na kwenda kuwekeza kilimo cha mihogo Chanika pale tu kuna mtu au watu watafikishwa mahakamani, na kumaliza mchakato huo, halafu kupigwa miaka stahiki Keko. Nitajiuzulu.
 
Matokeo yake ripoti ya CAG siku hizi imekuwa kama mchezo wa kuigiza, inasomwa kwa mbembwe kuonesha tulivyopigwa halafu wapigaji wanalindwa, huu umasikini wa hili taifa utaendelea kuwepo kwa miaka sana mingi ijayo.

Tukiibiwa mapesa mengi na marafiki zao wanakaa kimya, lakini tukiibiwa kidogo na wasio rafiki zao ndio wanawatoa sadaka, hili taifa chini ya utawala wa CCM linaongozwa kisanii sana.
 
Hawa CAG wakaguzi na wathibiti wanaweza kuwa ndio washirika wakuu wa upigaji. Wako zaidi kisiasa kutokana na uongozi wa muda huo.

Ukitaka kuondoa upigaji kwa dhati toa sheria ya Viongozi kutoshtakiwa, waweze kuwajibishwa kama raia wengine wote. Bunge, mahakama, polisi viwe vyombo huru, vipewe meno na kutenda haki. Kiufupi ni kudai Katiba Mpya.
 
Wizi ni wizi,hata wizi wa kuku ni wizi mbaya sana.
Je mtu baki mwenye kipato kidogo sana anategemea kuku wake wawili apate mayai kwa matumizi yake,anakuja kipanga anawaiba wote,unataka tumchekee kipanga?
Tukemee aina yote ya wizi,mara nyingi wezi uanza kama wadokozi hadi kufikia mafisadi.
 
Matokeo yake ripoti ya CAG siku hizi imekuwa kama mchezo wa kuigiza, inasomwa kwa mbembwe kuonesha tulivyopigwa halafu wapigaji wanalindwa, huu umasikini wa hili taifa utaendelea kuwepo kwa miaka sana mingi ijayo.

Tukiibiwa mapesa mengi na marafiki zao wanakaa kimya, lakini tukiibiwa kidogo na wasio rafiki zao ndio wanawatoa sadaka, hili taifa chini ya utawala wa CCM linaongozwa kisanii sana.
Linaongozwa kisanii, hata baada ya Makamu Mwenyekiti wa CCM, Abdrahman Kinana, kuwaeleza wananchi kuwa atamwambia Rais Samia, kuwa sasa ni mwisho wa hao watuhumiwa, kuendelea kulindwa?
 
Linaongozwa kisanii, hata baada ya Makamu Mwenyekiti wa CCM, Abdrahman Kinana, kuwaeleza wananchi kuwa atamwambia Rais Samia, kuwa sasa ni mwisho wa hao watuhumiwa, kuendelea kulindwa?

Wachukuliwe hatua wezi wa awamu zote tukianzia na ya kwanza hadi hii ya sita.

Ama sivyo ni upuuzi mtupu usio na tija yoyote.

Tuanze na Kinana mwenyewe na Ujangili uliotukuka. Wapigaji wa Tanesco sasa hivi. CAG anakague matumizi ya kodi/ tozo zote za sasa.
 
Matokeo yake ripoti ya CAG siku hizi imekuwa kama mchezo wa kuigiza, inasomwa kwa mbembwe kuonesha tulivyopigwa halafu wapigaji wanalindwa, huu umasikini wa hili taifa utaendelea kuwepo kwa miaka sana mingi ijayo.
Siku hizi tu? Mkuu miaka nenda rudi, sasa hivi wanafikia Season 40 episode 2 na Muvii zingine za Ukweli.😅
Tukiibiwa mapesa mengi na marafiki zao wanakaa kimya, lakini tukiibiwa kidogo na wasio rafiki zao ndio wanawatoa sadaka, hili taifa chini ya utawala wa CCM linaongozwa kisanii sana.
Mkuu, "rushwa inanuka" marashi ya Asali!
 
Wizi ni wizi,hata wizi wa kuku ni wizi mbaya sana.
Je mtu baki mwenye kipato kidogo sana anategemea kuku wake wawili apate mayai kwa matumizi yake,anakuja kipanga anawaiba wote,unataka tumchekee kipanga?
Tukemee aina yote ya wizi,mara nyingi wezi uanza kama wadokozi hadi kufikia mafisadi.
sblandes
Sijasema kuwa wale wezi wa kuku, wasipelekwe mahakamani kujibu tuhuma zao, ila ninachouliza, kama kweli nchi yetu inaendeshwa Katika mfumo wa kisheria, ni kwanini wezi wa kuku wafikishwe mahakamani na wale wa mabilioni ya shilingi ya walipa kodi, waachiwe huru mitaani??🥺
 
Ni jambo lilizoeleka kwa mkaguzi mkuu na mdhibiti wa pesa za Serikali (CAG) kuibuka na ripoti kila mwaka, inayoonyesha namna mabilioni ya pesa ya walipa zinavyotafunwa na "wajanja" wachache walioko Serikalini, pasipo kuchukuliwa hatua zozote.

Lakini tunashuhudia magereza yetu, yakiwa yamefurika wafungwa, wakiwa wamehukumiwa kwa vijikesi, vidogo vidogo, kama vile wizi wa kuku!

Ndiyo hapo ninapouliza, hivi kuna sababu gani ya kutusomea hadharani ripoti hizo za CAG, kama Serikali yetu, haina dhamira ya dhati kuwachukulia hatua za kisheria?

Tumeshuhudia, makamu Mwenyekiti wa CCM, Abdrahman Kinana, eti akisema, atamshairi Rais Samia, aweze kuwachukulia hatua za kisheria, wale wote waliotajwa kwenye ripoti hiyo ya CAG!

Hivi umewahi kuona wapi watu waliotenda makosa makubwa kama hayo ya kutafuna mabilioni ya pesa ya walipa kodi wa nchi hii, eti mpaka Rais ashauriwe Ili achukue hatua za kisheria?

Mbona hawa wanaotuhumia kwa vijikesi vidogo vidogo, kama vile wezi wa vibasikeli, wakiwa wamejazana magerezani, wakiwa wameshahukumiwa tayari, kutumikia vifungo vyao, je na hao Rais ameshauriwa kabla ya kupelekwa mahakamani na kuhukumiwa' vifungo vyao??

Huu mtindo unaotumika na Serikali hii ya CCM, ni wa hatari Sana, unaofanya upendeleo wa wazi kabisa na "kubariki" kwa kuwaona wale wezi wa mabilioni ya Serikali, kama mashujaa na kuachiwa watembee kifua mbele, wakati wezi wa vitu vidogo vidogo, kama wale wanaowakwapua vipochi kwa abiria kwenye daladala, ndiyo wahukumiwe vifungo mahakamani na watuhumiwa wengine hata wakipoteza Maisha yao kwa "kuhukumiwa' vipigo na wananchi wenye hasira kali!

Ndiyo maana nchi hii kodi zinakuwa nyingi mno, kama vile tozo mbalimbali, kwenye miamala ya simu, ambazo zinawakamua watanzania wanyonge, kumbe pesa hizo, zinaliwa na watanzania wachache, tuliowaamini na kuwakabidhi madaraka ya juu, Katika nchi hii!

Tunaomba viongozi wetu wa Serikali hii ya CCM, wawe "serious" na wachukue hatua mara moja na tuone watuhumiwa wote waliotajwa na CAG kukwapua mabilioni ya pesa ya walipa kodi wa nchi hii wanafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zao.
Wahusika ni wanaccm na wanaotakiwa kuwachukulia hatua ni wanaccm.
 
sblandes
Sijasema kuwa wale wezi wa kuku, wasipelekwe mahakamani kujibu tuhuma zao, ila ninachouliza, kama kweli nchi yetu inaendeshwa Katika mfumo wa kisheria, ni kwanini wezi wa kuku wafikishwe mahakamani na wale wa mabilioni ya shilingi ya walipa kodi, waachiwe huru mitaani??🥺
La hasha, every point counts.
 
Linaongozwa kisanii, hata baada ya Makamu Mwenyekiti wa CCM, Abdrahman Kinana, kuwaeleza wananchi kuwa atamwambia Rais Samia, kuwa sasa ni mwisho wa hao watuhumiwa, kuendelea kulindwa?
Kuna ukweli na hayo, yaani tuamini kuwa Mh Raisi hajawajua, na kwamba kama kamanda wa juu wa CCM basi akimdokeza Mwenyekiti wake fulani ameng'oa... basi watalundikana kwenye basi la magereza .

Naweza hata kuthubutu kusema basi wapunguze na Mahakama zisizo na tija hizo fedha za kuendeshea wazirudishe hazina kufunika hiyo mitungi ya Asali. Manake wanaingiliwa wajibu wao kuonekana butu. Bunge ndio wala usitheme, wana uzi wao wa kudai 'walipitishwa' na hivyo hawana uwezo wa kunyoosha vidole! Usanii wa aina yake hapa kwetu, nao Buree-wote- hao hao na Jersey za Kijjani!
 
Sheria za Tanzania ni principle based na sio rule based. Kosa likifanyika tunaweza kuliacha kama hakuna maslahi.
 
Kiuahalisia hawa wakaguzi /wathibiti wetu inabidi nao kuthibitiwa,kukaguliwa na kuhojiwa na Bunge letu. Bunge lenyewe liliondolewa spika na likabaki kimya kabisa.

Naona wanaidhalilisha tu hii ofisi sababu hawaonekani wakiwa serious zaidi ya kutumika kisiasa, maigizo.
 
Ni jambo lilizoeleka kwa mkaguzi mkuu na mdhibiti wa pesa za Serikali (CAG) kuibuka na ripoti kila mwaka, inayoonyesha namna mabilioni ya pesa ya walipa zinavyotafunwa na "wajanja" wachache walioko Serikalini, pasipo kuchukuliwa hatua zozote.

Lakini tunashuhudia magereza yetu, yakiwa yamefurika wafungwa, wakiwa wamehukumiwa kwa vijikesi, vidogo vidogo, kama vile wizi wa kuku!

Ndiyo hapo ninapouliza, hivi kuna sababu gani ya kutusomea hadharani ripoti hizo za CAG, kama Serikali yetu, haina dhamira ya dhati kuwachukulia hatua za kisheria?

Tumeshuhudia, makamu Mwenyekiti wa CCM, Abdrahman Kinana, eti akisema, atamshairi Rais Samia, aweze kuwachukulia hatua za kisheria, wale wote waliotajwa kwenye ripoti hiyo ya CAG!

Hivi umewahi kuona wapi watu waliotenda makosa makubwa kama hayo ya kutafuna mabilioni ya pesa ya walipa kodi wa nchi hii, eti mpaka Rais ashauriwe Ili achukue hatua za kisheria?

Mbona hawa wanaotuhumia kwa vijikesi vidogo vidogo, kama vile wezi wa vibasikeli, wakiwa wamejazana magerezani, wakiwa wameshahukumiwa tayari, kutumikia vifungo vyao, je na hao Rais ameshauriwa kabla ya kupelekwa mahakamani na kuhukumiwa' vifungo vyao??

Huu mtindo unaotumika na Serikali hii ya CCM, ni wa hatari Sana, unaofanya upendeleo wa wazi kabisa na "kubariki" kwa kuwaona wale wezi wa mabilioni ya Serikali, kama mashujaa na kuachiwa watembee kifua mbele, wakati wezi wa vitu vidogo vidogo, kama wale wanaowakwapua vipochi kwa abiria kwenye daladala, ndiyo wahukumiwe vifungo mahakamani na watuhumiwa wengine hata wakipoteza Maisha yao kwa "kuhukumiwa' vipigo na wananchi wenye hasira kali!

Ndiyo maana nchi hii kodi zinakuwa nyingi mno, kama vile tozo mbalimbali, kwenye miamala ya simu, ambazo zinawakamua watanzania wanyonge, kumbe pesa hizo, zinaliwa na watanzania wachache, tuliowaamini na kuwakabidhi madaraka ya juu, Katika nchi hii!

Tunaomba viongozi wetu wa Serikali hii ya CCM, wawe "serious" na wachukue hatua mara moja na tuone watuhumiwa wote waliotajwa na CAG kukwapua mabilioni ya pesa ya walipa kodi wa nchi hii wanafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zao.
Wala rushwa wakubwa ni viongozi wa CCM unategemea nini?
 
Back
Top Bottom