Ni haki kumwabudu marehemu?

Ni haki kumwabudu marehemu?

Tatizo kubwa liko kwa imani zetu au ndani ya makanisa yetu. Tulifundishwa hadithi zaidi badala ya maandiko. Tulishaacha maandiko mbali sana tunaelea gizani
 
Wana JF.Hili swala la kumwabudu marehemu au kumwombea wakati yeye kashakufa na hana ufahamu wowote kweli ni jambo jema? Maiti haijui wala haisikii nijuavyo mimi sijui wenzangu mnajuaje? Maiti haina thamani yoyote hata fungu la mchicha la mia mbili inaizidi thamani nijuavyo mimi.Naombeni na nyie mawazo yenu kuhusu hili watu wa jf.

Sijui kama utanielewa, ni hivi marehemu anapokufa tunakuwa hatuna uhakika kaenda wapi, maana unaweza kudhani kafariki kumbe yupo, uchawi upo na Bible inatambua hilo, wapo wanaogeuzwa misukule tu, je si sahihi kuwaombea?

Suala la kuabudi sidhani kama unaelewa, hivi wewe unapoendelea kutunza picha ya Babu yako aliyefariki ni kuabudu picha hiyo? Je unapoona picha ya mtu aliyefariki hukumbuki mema yake na je kuyafata ni kuabudu? Je unapoangalia hotuba ya watu waliokufa ukajifunza toka kwao huko ni kuabudu?

Kifupi kuabudu ni kuwa na picha ya mtu usiyemjua na wewe ukawa umeitundika.
 
JEKI

Ninapo maanisha kuabudu ni kwa mfano mtu anamwomba marehemu amletee mvua wakati hasikii wala hajui.Unawmombea marehemu asamehewe wakati marehemu mwenyewe hajijui na wala hajitambui.Kumbukumbu ya aliekuwa binadamu kumwona katika picha sio kumwabidu mkuu.

Mtu anamwomba marehemu eti amwombee kwa Mungu wakati marehemu mwenyewe hasikii na wala hajijui hiyo ni akili kweli mkuu? Ni sawa na kuimbia jiwe ikuombee kwa Mungu.
 
Last edited by a moderator:
Wana JF.Hili swala la kumwabudu marehemu au kumwombea wakati yeye kashakufa na hana ufahamu wowote kweli ni jambo jema? Maiti haijui wala haisikii nijuavyo mimi sijui wenzangu mnajuaje? Maiti haina thamani yoyote hata fungu la mchicha la mia mbili inaizidi thamani nijuavyo mimi.Naombeni na nyie mawazo yenu kuhusu hili watu wa jf.

Nambea ufiwe halafu uje hapa JF ujibu swali lako, au ufe mwenyewe pichu yako Na mjadala utajifunga!
 
Natumaini utaanza wewe kisha mimi niko nyuma yako.

Hivi Mkuu ulisema mwisho wa Dunia ungetokea kipindi cha kombe la dunia...Vipi ume fix tarehe nini.....????

Onyo:

Ogopa kufuata dini iliyoanzishwa kwa mihemko ya Mama Hellena White....Ni hatari kwa afya ya Roho na mwili
 
Ninapo maanisha kuabudu ni kwa mfano mtu anamwomba marehemu amletee mvua wakati hasikii wala hajui.Unawmombea marehemu asamehewe wakati marehemu mwenyewe hajijui na wala hajitambui.

Kumbukumbu ya aliekuwa binadamu kumwona katika picha sio kumwabidu mkuu.Mtu anamwomba marehemu eti amwombee kwa Mungu wakati marehemu mwenyewe hasikii na wala hajijui hiyo ni akili kweli mkuu? Ni sawa na kuimbia jiwe ikuombee kwa Mungu.

Anhaa, ndo nikakuuliza mtu akifa unajuaje kafa? je unaamini juu ya uchawi na watu kupotea kwa miujiza? au watu kugeuzwa misukule? je huoni hao bado ni wazima sema wamefichwa kimazingara?
 
Anhaa, ndo nikakuuliza mtu akifa unajuaje kafa? je unaamini juu ya uchawi na watu kupotea kwa miujiza? au watu kugeuzwa misukule? je huoni hao bado ni wazima sema wamefichwa kimazingara?

Wewe unajuaje mtu hajafa kafichwa?
 
Ndugu ibada ya wafu haikubaliki kwasababu mtu akiisha kufa kifuatacho ni hukumu tu hata mkeshe na Jerez's letu mkiomba haimuongezei hata tone,someni biblia na kuielewa.
 
Ndugu ibada ya wafu haikubaliki kwasababu mtu akiisha kufa kifuatacho ni hukumu tu hata mkeshe na jeneza lenu mkiomba haimuongezei hata tone,someni biblia na kuielewa.
kwaleo ninahayo tu
 
Ndugu ibada ya wafu haikubaliki kwasababu mtu akiisha kufa kifuatacho ni hukumu tu hata mkeshe na Jerez's letu mkiomba haimuongezei hata tone,someni biblia na kuielewa.

Unaamini life after death....

Hebu soma Muhubiri 12:7.....

Ukishasoma ni-mention tuelezane jambo......

.Na ili mjadala uwe mtamu tafadhali tumia Biblia kamili ya vitabu 72
 
Huhuuuuuu eti thaman ya mchicha, kwan mchicha ukisinyaa una thaman, je maiti inawezwa kutupwa jalalani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom