Ni haki kumwabudu marehemu?

Ni haki kumwabudu marehemu?

Ukijua maana ya neno IMANI utakuwa umshapata jibu lako......kwani nilianza na neno......kwa watu wa IMANI..

Hata kama ni imani je ni sahihi kumwabudu marehemu au kumwombea maana marehemu hajui na hajijui kabisaa.
 
Marehemu tuletee mvua,marehemu leo tunakuchinjia mbuzi umle,marehemu tuombee huko uliko.Huu ni ujinga uliopita kipimo.Utaiambiaje mzoga ukuombee,ukuletee mvua,umchinjie mbuzi wakati hawezi kula?
 
hata kama ni imani je ni sahihi kumwabudu marehemu au kumwombea maana marehemu hajui na hajijui kabisaa.

Jaribu kuelewa bandiko langu..na uchukue muda kulitafakali kwa umakini........nimesema kwa wenye imani au kwa wenye kuamnini kuwa kuna maisha baada ya kifo.... wao wana mtazamo tofauti kuhusu kifo.....

kwa wao kifo ni kama mfano wa mtu aliyesafiri lakini harudi tena na kama kawaida ya waungwana hutakiana heri ya safari....na kuhusu kumwabudu mimi binafsi hilo swala silifahamu isipokuwa kumwombea....lakini lazima ujue kuwa kila jamii ina mtazamo tofauti kuhusu au mtu

aliyekufa.....inawezekana ikawa kwako wewe kifo likawa ni jambo la kawaida........lakini kwa wenzako ikawa ni issue sensitive sana......
 
Kinachofanyika wakati wa msiba ni kutukumbusha sie tulio hai kumkumbuka mungu wakati tunavuta pumzi ila pamoja na kwamba marehemu hana thamani kama ulivyoainisha

lakini kwa heshima na kutambua mchango wake alivyokuwa hai ndio maana kuna taratibu za kuonyesha heshima kwa mwili wa marehemu hata kama hajui kinachoendelea, assume mzazi anafariki ni kweli pale ameshakwenda lakini bado heshima kwa mwili wake inatakiwa,

ni sawa tu na watu wanaipigia salute bendera ya Taifa
 
Jodoki Kalimilo

Heshima katika mwili ila sio kumwabudu au kumwomba atuombee au kumsihi atuletee mvua au eti anataka achinjiwe mbuzi.
 
Last edited by a moderator:
Naomba twende kwa mfano ili tuelewane.
Maiti ya mama yako na mchicha wa 2000, kipi unadhani ni bora kitupwe jalalani kiliwe na mbwa?!

we kwani huelewi nini hapa?..acha kukurupuka hebu rudia tena kusoma alichokiandika mtoa mada.. hamaanishi mfu anatakiwa kutupwa jalalani, kwani kumzika mtu ndio kumuabudu? issue hapa ni kumuhusisha mfu kwenye maisha ya kawaida baada ya kifo,

mf. kumuomba mfu akusaidie katika maisha yako ya kila siku hiyo ndio mifano ya ibada za wafu
 
umetoka nje mada mkuu hata hivyo asante kwa kuchangia.
Sijatoka nje ya mada. Swali lako linauliza, "Ni haki kumwabudu marehemu?". Nimekupa vifungu vya katiba vinavyoruhusu mtu kuwa muumini wa mafundisho ya imani yake ili mradi havunji sheria. Huyo anaamini katika 'kumwabudu' marehemu. Hajavunja sheria za nchi. Sasa hapo kwa nini isiwe haki?
 
Sijatoka nje ya mada. Swali lako linauliza, "Ni haki kumwabudu marehemu?". Nimekupa vifungu vya katiba vinavyoruhusu mtu kuwa muumini wa mafundisho ya imani yake ili mradi havunji sheria. Huyo anaamini katika 'kumwabudu' marehemu. Hajavunja sheria za nchi. Sasa hapo kwa nini isiwe haki?

Sijagusia sheria za nchi bali nime base katika swala la kwanini marehemu aombewe au aombwe,je kuna faida?
 
Hebu weka na aya uliyosoma kwenye Biblia yako.

Mhubiri 9:4-5.... Kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote, wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahauliwa. Mapenzi yao na machukio yao, na husuda yao, imepotea yote pamoja; wala hawana sehemu tena katika jambo lo lote lililofanyika chini ya jua.
 
Kuenzi fikra na busara hiyo ni sawa.Lakini kumuombea huko aliko si sawa kwa maana yuko chini ya ardhi na analiwa na wadudu.

Hii inategemeana unavyoamini !

Je, Mtu ni ule mwili tuliozika kwa heshima pale kaburini au ni Roho aliekuako ktk mwili ule na sasa ameondoka yuko kwa Baba ambae ndiye Asili yake ?

Na je Huyu Mtu alifuata kweli maelekezo ya Mungu pale alipoishi hapa Duniani pakiwa ndiyo mahali pekee ambapo Mtu binafsi anaweza kufanya bidii ya kuweka mahusiano mazuri na Mungu?

Tunayo nafasi ya kujipatia Neema sisi wenyewe na Yeye kwa kumwombea kwa Mungu ili amrehemu. Tunayo pia nafasi ya kunufaika na maombi yake iwapo yupo kwa Mungu.

Huu ni Ushirika wa Watakatifu.
 
Ninachoamini mimi ni kuwa Binadamu akiwepo duniani ndipo unapoweza kumuomba chochote na hata Kumuombea.

-Pia binadamu anapokuwa duniani ndipo anapokuwa na fursa ya kuamua na kukata shauri aishije na Atakapokufa tu ndipo atakapohukumiwa kulingana na aliyoyatenda duniani. "Duniani ndipo penye bonde la kukata maneno"

-Akishakufa ndugu yangu huwezi kumwombea akabadilishiwa hukumu na Muumba wake,au akifa na maovu yake eti awekwe peponi.tunajifariji tuu kwa kuonesha kumjali. Kata shauri ukiwa bado una pumzi ya bure.

-
 
Wana JF.Hili swala la kumwabudu marehemu au kumwombea wakati yeye kashakufa na hana ufahamu wowote kweli ni jambo jema? Maiti haijui wala haisikii nijuavyo mimi sijui wenzangu mnajuaje? Maiti haina thamani yoyote hata fungu la mchicha la mia mbili inaizidi thamani nijuavyo mimi.Naombeni na nyie mawazo yenu kuhusu hili watu wa jf.

-Ni kweli mkuu maiti haijui wala haisikii chochote NA PIA si jambo jema kuombea maiti.

-Na pia roho yake itakuwa salama huko inapokwenda ikiwa tu alikufa ktk kutenda mema na kuomba peke yake na si kwa kuombewa kamwe!!!
 
gkileo

Mkuu mzoga wa binadamu haijui kitu na wala haielewi kitu na hakuna aliekufa kisha akararudi akatuambia haya yote uyasemayo kwanba alikuwa kwa Mungu na kuendelea na maisha mengine,

Huo ni uvumi tu wa mwanadamu kwahiyo tunarudi palepale kwamba maiti a.k.a mzoga wa binadamu haijui chochote wala kutambua na tunapowaomba au kuwaombea tunapoteza mda wetu bureee bila faida.
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom