Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,503
- 51,098
Huhitaji kuvaa miwani ya uoni mkubwa kuweza kuona dhahiri shahiri kuwa nchi yetu imefeli, tena imefeli kila idara.
Hakuna jambo lenye nafuu katika nchi yetu. Kila kitu ni bora liende, nchi inaporomoka kwenye korongo na ni kama hakuna anayejali.
1. Miaka zaidi ya 60 bila ya umeme wa uhakika.
Najiuliza hawa viongozi wetu waliopewa dhamana, wanajisikiaje wanapoamka asubuhi na kwenda kazini. Kisha wakakaa katika viti vyao vya kunesanesa. Kitu gani hasa kinachoweza kuwapa ufahari wa kiuongozi wakati wameshindwa kutatua changamoto ya hili jambo kwa zaidi ya miaka 60 ya kuongoza Taifa hili. Nchi imeshapitia marais 6, wa chama kilekile lakini Umeme wa uhakika hata katika jiji kubwa nchini ni shida. Hawa watu kimsingi wamefeli hawatufai
2. Maji ya uhakika ni ndoto
Nchi yenye vyanzo vya maji vingi kuliko nchi yoyote ndani ya Afrika lakini ni miongoni mwa nchi zenye shida ya maji kwelikweli katika bara hili. Hili linakufanya ujiulize, hawa viongozi wetu wenye dhamana ya kukusanya kodi kimsingi wamezifanyia nini jambo la maana kodi zetu?. Wamegeuka mabingwa wa misafara mikubwa ya magari, mabingwa wa kusafiri nje na kutumia pesa nyingi kujilipa maposho makubwamakubwa. Huo ndiyo uwezo wao na fikra zao zilipoishia. Hawana uwezo kabisa wa kutatua matatizo ya msingi ya wananchi.
3. Shida katika Upatikanaji wa bidhaa muhimu.
Leo nchi ina shida ya sukari. Na hili siyo tatizo la leo wala jana, limekuwa likikirudia mara kwa mara na serikali imefeli kulipatia suluhisho. Kama hiki chama na serikali yake vingekuwa na uwezo, hili jambo lingekuwa limekwishakuwa historia. Lakini unaona wazi kuwa hata kitu kidogo kama hiki wamefeli. Tangu enzi za sokoine eti tumeshindwa kudeal na issue ndogo kama hii ya sukari.
4. Kila indicator inaonyesha wazi kuwa CCM imefeli, Samia amefeli na Taifa limegeuka a failed state.
a) Alichoweza ni kutengeneza sheria ya viongozi na "wapenzi" wao kulipana posho. Hii sijui inamsaidia nini mtanzania au inamhusu nini kumlipa la azizi wa kiongozi. Ni ubinafsi tu na kutokujali matatizo halisi ya wananchi
b) Wanachoweza ni kupiga sound na uwongouwongo mwingi. Kila mwaka wanasema ikifika mwaka kadhaa tatizo la umeme au maji litakuwa historia, lakini kwa miaka zaidi ya 60 tatizo liko palepale. Sasa hawa watu wamekuwa wanabaishaji, hawana chochote wanachiweza kudeliver zaidi ya ujanjaujanja tu, hamna chochote
c) Hawaumii na wala hawajali chochote kuhusu hali ngumu za maisha ya watu.
Unaposikia kiongozi anatoa kejeli kwa wananchi kuwa Ukosefubwa Sukari ni fursa ya kuacha kutumia sukari. Halafu kiongozi huyo hakemewi achilia mbali kuendelea kubaki katika nafasi yake ujue Uongozi mzima umeoza yaani Rotten to the core. Hawajali chochote tena zaidi ya kujijali wao binafsi na matumbo yao. Yaani wamegeuka kama genge hivi la maslahi binafsi. They Don't care
d) Uwezo na fikra za watawala wetu sasa siyo kutengeneza uwezo na utajiri wa watu bali kuuza na kugawa rasilimali zetu.
Uwezo wa kuondoa wananchi katika lindi la umasikini haupo, bali akili za watawala wetu sasa zimegeuka kwenye kuuza rasilimali zetu kwa bei chee ili wapate hela za kufanya vimiradi uchwara vya kuendelea kuwalaghai wananchi kuwa wanafanya kazi. Leo bandari imeuzwa kihuni, misitu imegawiwa gizani, madini walishauza, gesi imeshakwenda. Tumebaki na nini sisi zaidi ya suruali na sketi zetu?
MWISHO
No doubt Taifa letu ni failed state. Hakuna chochote tunachofanya kwa ufanisi, kwa uwezo au hata kwa akili. Kiufupi tuna viongozi incapable, Incompetent, Corrupt, visionless and Selfish. Bila kubadili mifumo ya uongozi katika nchi yetu tutaendelea kuwa Petty people, dispised people na kuonekana mbele ya mataifa na watu wa ulimwengu kama Imbecile na stupid.
Namna ya kuanzia kwenye kujikwamua na tatizo letu ni complete overhaul ya mifumo ya uendeshaji nchi, itakayoweka misingi ya uwajibikaji weledi na ufanisi katika kuendesha nchi.
Hii ndiyo hoja ya Uhitaji wa KATIBS BORA. Nje ya hapo tukiendelea na Ujingaujinga huu hatufiki popote!
Hakuna jambo lenye nafuu katika nchi yetu. Kila kitu ni bora liende, nchi inaporomoka kwenye korongo na ni kama hakuna anayejali.
1. Miaka zaidi ya 60 bila ya umeme wa uhakika.
Najiuliza hawa viongozi wetu waliopewa dhamana, wanajisikiaje wanapoamka asubuhi na kwenda kazini. Kisha wakakaa katika viti vyao vya kunesanesa. Kitu gani hasa kinachoweza kuwapa ufahari wa kiuongozi wakati wameshindwa kutatua changamoto ya hili jambo kwa zaidi ya miaka 60 ya kuongoza Taifa hili. Nchi imeshapitia marais 6, wa chama kilekile lakini Umeme wa uhakika hata katika jiji kubwa nchini ni shida. Hawa watu kimsingi wamefeli hawatufai
2. Maji ya uhakika ni ndoto
Nchi yenye vyanzo vya maji vingi kuliko nchi yoyote ndani ya Afrika lakini ni miongoni mwa nchi zenye shida ya maji kwelikweli katika bara hili. Hili linakufanya ujiulize, hawa viongozi wetu wenye dhamana ya kukusanya kodi kimsingi wamezifanyia nini jambo la maana kodi zetu?. Wamegeuka mabingwa wa misafara mikubwa ya magari, mabingwa wa kusafiri nje na kutumia pesa nyingi kujilipa maposho makubwamakubwa. Huo ndiyo uwezo wao na fikra zao zilipoishia. Hawana uwezo kabisa wa kutatua matatizo ya msingi ya wananchi.
3. Shida katika Upatikanaji wa bidhaa muhimu.
Leo nchi ina shida ya sukari. Na hili siyo tatizo la leo wala jana, limekuwa likikirudia mara kwa mara na serikali imefeli kulipatia suluhisho. Kama hiki chama na serikali yake vingekuwa na uwezo, hili jambo lingekuwa limekwishakuwa historia. Lakini unaona wazi kuwa hata kitu kidogo kama hiki wamefeli. Tangu enzi za sokoine eti tumeshindwa kudeal na issue ndogo kama hii ya sukari.
4. Kila indicator inaonyesha wazi kuwa CCM imefeli, Samia amefeli na Taifa limegeuka a failed state.
a) Alichoweza ni kutengeneza sheria ya viongozi na "wapenzi" wao kulipana posho. Hii sijui inamsaidia nini mtanzania au inamhusu nini kumlipa la azizi wa kiongozi. Ni ubinafsi tu na kutokujali matatizo halisi ya wananchi
b) Wanachoweza ni kupiga sound na uwongouwongo mwingi. Kila mwaka wanasema ikifika mwaka kadhaa tatizo la umeme au maji litakuwa historia, lakini kwa miaka zaidi ya 60 tatizo liko palepale. Sasa hawa watu wamekuwa wanabaishaji, hawana chochote wanachiweza kudeliver zaidi ya ujanjaujanja tu, hamna chochote
c) Hawaumii na wala hawajali chochote kuhusu hali ngumu za maisha ya watu.
Unaposikia kiongozi anatoa kejeli kwa wananchi kuwa Ukosefubwa Sukari ni fursa ya kuacha kutumia sukari. Halafu kiongozi huyo hakemewi achilia mbali kuendelea kubaki katika nafasi yake ujue Uongozi mzima umeoza yaani Rotten to the core. Hawajali chochote tena zaidi ya kujijali wao binafsi na matumbo yao. Yaani wamegeuka kama genge hivi la maslahi binafsi. They Don't care
d) Uwezo na fikra za watawala wetu sasa siyo kutengeneza uwezo na utajiri wa watu bali kuuza na kugawa rasilimali zetu.
Uwezo wa kuondoa wananchi katika lindi la umasikini haupo, bali akili za watawala wetu sasa zimegeuka kwenye kuuza rasilimali zetu kwa bei chee ili wapate hela za kufanya vimiradi uchwara vya kuendelea kuwalaghai wananchi kuwa wanafanya kazi. Leo bandari imeuzwa kihuni, misitu imegawiwa gizani, madini walishauza, gesi imeshakwenda. Tumebaki na nini sisi zaidi ya suruali na sketi zetu?
MWISHO
No doubt Taifa letu ni failed state. Hakuna chochote tunachofanya kwa ufanisi, kwa uwezo au hata kwa akili. Kiufupi tuna viongozi incapable, Incompetent, Corrupt, visionless and Selfish. Bila kubadili mifumo ya uongozi katika nchi yetu tutaendelea kuwa Petty people, dispised people na kuonekana mbele ya mataifa na watu wa ulimwengu kama Imbecile na stupid.
Namna ya kuanzia kwenye kujikwamua na tatizo letu ni complete overhaul ya mifumo ya uendeshaji nchi, itakayoweka misingi ya uwajibikaji weledi na ufanisi katika kuendesha nchi.
Hii ndiyo hoja ya Uhitaji wa KATIBS BORA. Nje ya hapo tukiendelea na Ujingaujinga huu hatufiki popote!