Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,334
- 9,755
Ndugu zangu Watanzania,
Fanya shughuli mapema na kwa haraka sana huku macho na masikio yako yakitegwa na kuelekezwa visiwani Zanzibar ambako Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu ambaye ndiye mwenyekiti wa CCM Taifa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hasssan mama wa shoka chuma cha Reli, shujaa wa Afrika, jasiri muongoza njia, simba wa nyika, komandoo wa vita, nuru ya wanyonge, nyota ya matumaini ataongoza kikao cha kamati kuu ya halmashauri kuu ya CCM Taifa leo Jumatatu januari 15 visiwani Zanzibar.
Ikumbukwe ya kuwa vikao vya CCM ndio hutoa muelekeo wa nchi na mustakabali wa mambo mbalimbali hapa nchini. Ndio vikao ambavyo hufuatiliwa na vyombo vyote vikubwa Duniani kwote kutokana na umuhimu wake. Ni vikao vilivyosheheni vigogo na watu wazito hapa nchini. Ni vikao ambavyo hata sisiminzi hutulia na kuacha kukatisha eneo husika.
Tutarajie mambo makubwa na mazito na yenye maslahi kwa Taifa letu kutoka katika kikao hicho. Tutarajie mtetemeko na mtikisiko mkubwa kwa watu, kwa kuwa ndio vikao pekee vya CCM ambavyo matamko na maazimio yake huchukuliwa na kuheshimiwa na watanzania tofauti na matamko ya vile vyama vinavyopigania maslahi yake binafsi na matumbo yao kama ilivyo kwa genge la CHADEMA.
Kaeni kwa kutulia maana CCM Ndio wenye kutoa njia na mstakabali wa Taifa letu. Ndio wenye kutoa muelekeo sahihi wa kila jambo, ndio wenye kuongoza mambo nyeti na muhimu kwa njia iliyo sahihi, ndio wenye uchungu na maisha ya Watanzania, ndio wanaojuwa wapi Taifa hili linapaswa kuelekea na kupita, ndio wanaojuwa vyema watanzania wanahitaji nini na kwa wakati gani na kiasi gani. Ndio maana wakati wote huzungumzia lugha za Watanzania na kueleweka kwa urahisi na wepesi.
Mpaka sasa vyombo vya kimataifa na waandishi wake mahili na wenye uzoefu wanaendelea kumiminika na kufurika kwa wingi visiwani Zanzibar ili kuijulisha Dunia kitakachojili kutoka katika kikao hicho. Usalama ni wa kutosha ambapo hata sisiminzi wanalindwa wasikanywagwe.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia Watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya Watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627
Fanya shughuli mapema na kwa haraka sana huku macho na masikio yako yakitegwa na kuelekezwa visiwani Zanzibar ambako Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu ambaye ndiye mwenyekiti wa CCM Taifa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hasssan mama wa shoka chuma cha Reli, shujaa wa Afrika, jasiri muongoza njia, simba wa nyika, komandoo wa vita, nuru ya wanyonge, nyota ya matumaini ataongoza kikao cha kamati kuu ya halmashauri kuu ya CCM Taifa leo Jumatatu januari 15 visiwani Zanzibar.
Ikumbukwe ya kuwa vikao vya CCM ndio hutoa muelekeo wa nchi na mustakabali wa mambo mbalimbali hapa nchini. Ndio vikao ambavyo hufuatiliwa na vyombo vyote vikubwa Duniani kwote kutokana na umuhimu wake. Ni vikao vilivyosheheni vigogo na watu wazito hapa nchini. Ni vikao ambavyo hata sisiminzi hutulia na kuacha kukatisha eneo husika.
Tutarajie mambo makubwa na mazito na yenye maslahi kwa Taifa letu kutoka katika kikao hicho. Tutarajie mtetemeko na mtikisiko mkubwa kwa watu, kwa kuwa ndio vikao pekee vya CCM ambavyo matamko na maazimio yake huchukuliwa na kuheshimiwa na watanzania tofauti na matamko ya vile vyama vinavyopigania maslahi yake binafsi na matumbo yao kama ilivyo kwa genge la CHADEMA.
Kaeni kwa kutulia maana CCM Ndio wenye kutoa njia na mstakabali wa Taifa letu. Ndio wenye kutoa muelekeo sahihi wa kila jambo, ndio wenye kuongoza mambo nyeti na muhimu kwa njia iliyo sahihi, ndio wenye uchungu na maisha ya Watanzania, ndio wanaojuwa wapi Taifa hili linapaswa kuelekea na kupita, ndio wanaojuwa vyema watanzania wanahitaji nini na kwa wakati gani na kiasi gani. Ndio maana wakati wote huzungumzia lugha za Watanzania na kueleweka kwa urahisi na wepesi.
Mpaka sasa vyombo vya kimataifa na waandishi wake mahili na wenye uzoefu wanaendelea kumiminika na kufurika kwa wingi visiwani Zanzibar ili kuijulisha Dunia kitakachojili kutoka katika kikao hicho. Usalama ni wa kutosha ambapo hata sisiminzi wanalindwa wasikanywagwe.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia Watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya Watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627