Baada ya kupoteza dira na mkondo wa siasa za kidemokrasia, na dhamira halisi ya kuwepo upinzani, chadema kimepoteza uhalali wake wa kisiasa hivyo hakuna sababu kuwapo katika daftari la msajlli wa vyama vya siasa Tanzania, hivyo kifutwe!
Nasema hivyo kwa sababu chadema baada ya kukubali mtego wa CCM wa kupenyeza mamluki ndani ya chama chao wakiwamo magwiji wa usalama wa taifa wastaafu (Mabere N. Marando), pamoja na magwiji wa siasa za kipropaganda kutoka CCM (John M. Shibuda), hakina tena ile rangi yake ya siasa za upinzani.
Akina Marando wanafanya kazi yao ndani ya chadema, ya kushawishi vurugu makusudi ili kuharibu muelekeo wa chadema ulionza nao, naye ameshafanikiwa hilo, kama alivyofanya na kufanikiwa akiwa ndani ya NCCR-Mageuzi, yeye na Agustino Mrema.
Maoni yangu, chadema kifutiliwe mbali, tayari kimeshajionyesha au kimeshafanywa kijionyeshe kuwa hakitaki siasa za ushindani bali vurugu na kuleta machafuko nchini.
Mbali na kugeuzwa huko kwa hila za makusudi, chadema kimegeuka na siyo chama cha matumaini kwa wantanzania kama kinavyojidai, au kinavyodanganya wananchi, kwani ndani ya dhamira za baadhi ya viongozi wao ni kukifanya chama kuwa mtaji wa kukuza vitega uchumi vyao na kujipatia fedha tu.
Chama kinachojiita, au kinacholazimisha kuwa ni chama rasmi cha upinzani bungeni hali ya kuwa hakiwakilishi jiografia ya upinzani wa Tanzania, hakiwezi kuwa na uhalali wa kusimama na kujiita chama cha kitaifa, hivyo kifutwe!
Wakati bunge la Tanzania lina vyama vingi na wabunge wa vyama kutoka maeneo tofauti, chadema kama chama rasmi cha upinzani bungeni kinawakilisha majimbo kinayoyaongoza tu, katika serikali yao kivuli, wakati wananchi wa maeneo mengine ambao wamechaguwa upinzani pia hawana uwakilishi wowote ndani ya serikali kivuli ya chadema.
Kwa maana hiyo basi chadema wamepoteza uhalali wa kuwa chama cha kitaifa, hivyo Kifutwe!