Elitwege
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 5,154
- 10,809
KUAPISHWA KWA RAIS MLISUSA, RAIS ALIPOZINDUA BUNGE MKASUSA, SHEREHE ZA KITAIFA MNASUSA, MAENDELEO YA NCHI MNAPINGA, KULIKONI MSHIRIKI SHEREHE ZA UHURU?
Nimepokea kwa mshangao mkubwa kuhusu tamko la Kamati kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwa viongozi wake wa kitaifa wakiongozwa na Mwenyekiti Freeman Aikael Mbowe, watahudhuria sherehe za kitaifa za Uhuru wa Tanganyika 09th Dec,2019 zinazotarajiwa kufanyika kikanda kwa mara ya kwanza Mkoani Mwanza.
Nasema, nimepokea tamko hilo kwa mshangao kwa sababu, kwanza sikuamini iwapo ni kweli limetolewa na Kamati kuu ya Chadema, lakini pia sikuamini kwamba kuna wakati shetani anaweza kujigeuza kuwa malaika. Hii ni kwa sababu shetani kamwe hajawahi kuzaliwa upya bali shetani ni yule yule, na kinachobadilika kwake huwa ni mbinu za uadui anazozitumia pindi anapotaka kumwangamiza mwanadamu. Kuna wakati anaweza kujigeuza kuwa katika umbo la nyoka, simba, chui na wakati mwingine hata kudiriki kuonyesha kwamba anayo tabia ya matendo mema sawa na malaika wakati si kweli.
Ni jambo la kushangaza kwamba, Chadema waliosusia sherehe za kuapishwa kwa Rais Magufuli tarehe 05th Nov,2015 pale Uwanja wa Uhuru na kueleza kwamba, hawamtambuwi kama Rais aliyechaguliwa kidemokrasia kwa kushinda kupitia uchaguzi, leo ndiyo wanasema wako tayari kuhudhuria sherehe za Uhuru, kwa maana wawe karibu au waketi jukwaa moja na Rais wasiyemtambua? Hili halikubaliki.
Ji jambo la kushangaza kwamba, Chadema waliosusia hotuba ya Rais wakati akizindua Bunge tarehe 20th Nov,2015 Jijini Dodoma, ambapo kupitia hotuba ile ndipo watanzania tumeweza kuona mwelekeo wa taifa tulilonalo kwa sasa na siku za usoni, eti leo ndiyo wanadai wako tayari kuhudhuria sherehe za Uhuru wa Tanganyika (Tanzania)? Hii haikubaliki.
Ni jambo la kushangaza kwamba, Chadema waliosusia sherehe za kitaifa kwa miaka minne mfululizo ikiwemo ya Uhuru ambayo ni miongoni mwa tunu za kitaifa, leo ndiyo bila aibu wanasema wapo tayari kushirikiana na Rais? Haiwezekani.
Ni jambo ya kushitua kwamba, Chadema ambao wanapinga kila kitu yakiwemo maendeleo yanayofanywa na serikali ya awamu ya tano kwa miaka minne mfululizo kama vile miradi mikubwa ya kiuchumi, ununuzi wa ndege, elimu bure, maji, afya, umeme vijijini, mikopo vyuo vikuu, barabara, fly over, mazao ya wakulima, eti leo ndiyo wanataka kuwa karibu na Rais? Haiwezekani.
Ni jambo la kufikirisha kwamba, Chadema waliodiriki hata kumzushia Rais wa nchi kifo kutokana na uadui walioujenga kwake, na hawajamwomba radhi kwa kitendo hicho, eti leo ndiyo wanataka wakakae jukwaa moja na Rais? Haiwezekani.
Ni jambo la kushangaza kwamba, Chadema wanaoshiriki ndani na nje ya nchi kulihujumu taifa dhidi ya vita vya uchumi ikiwemo kushirikiana na mabeberu kukamata rasilimali zetu (ndege) ili kudhoofisha jitihada za nchi kujikomboa kiuchumi, eti leo ndiyo wanataka wakakae jukwaa moja na Mzalendo wa nchi, mtetezi wa taifa, mtetezi wa wanyonge. Hii haikubaliki.
Ni jambo la kushangaza kwamba, Chadema kupitia Tundu Lissu walivyozunguka dunia nzima kuishitaki serikali, kuombea nchi mabaya ikiwemo kunyimwa misaada ya maendeleo kutoka nchi wahisani, mikopo pamoja na kuitangaza nchi vibaya kuhusu kukiuka haki za binadamu na utawala bora, eti leo ndiyo wanataka kukaa jukwaa moja na Rais wanayemwita dikiteta. Hilo haliwezekani.
Ni jambo la kushangaza kwamba, Chadema wanaokesha na kushinda mitandaoni wakimtukana Rais wa nchi kwa utovu wa nidhamu uliovuka kiwango cha maadili, ndiyo sasa wanataka kukaa jukwaa moja na Rais wanayemtukana kutwa mara tatu kama vile wanatoa dozi kwa mgonjwa wakati Mwenyekiti wao Mbowe yupo na jajawahi kukemea uovu huo. Hii haikubaliki.
Kwa maoni yangu ili tamko la Chadema kushiriki sherehe za uhuru liweze kueleweka kwa Watanzania kwamba lina nia njema, viongozi wa Chadema wangeanza kutekeleza masharti yafuatayo:-
Kwanza, wamtambuwe Rais Magufuli kwamba ni Rais halali aliyechaguliwa kidemokrasia na si vinginevyo.
Pili, watambuwe na kuunga mkono jitihada zinazofanywa na serikali ya Chama cha Mapinduzi hususani katika swala la kufufua uchumi wa nchi, kuwaletea wananchi maendeleo.
Washiriki kwa vitendo vita dhidi ya rushwa, ufisadi pamoja na kushiriki vita vya uchumi kwa kutoshirikiana na mabeberu wa nje.
Waache kumtukana Rais ikiwa ni pamoja na kumwomba msamaha, kuwaomba msamaha watanzania kutokana na uovu waliofanya kwa nchi hii.
Watamke hadharani kwamba, kuanzia sasa watafanya siasa za ushindani kwa njia ya kistaarabu, kwa kuheshimiana, kwa kushindanisha sera na hoja badala ya matusi na kwamba kiongozi wao au mwanachama wao atakayekwenda kinyume, Chama kitamchukulia hatua za kinidhamu mara moja.
#MUHIMU: Iwapo Chadema haitatimiza masharti haya, kwa unyenyekevu mkubwa, naviomba vyombo vya dola visiruhusu viongozi wa Chama hiki kumsogelea Rais wetu mahali popote atakapokuwa. Kama mbwai na iwe mbwai tu, hakuna namna.
Nimepokea kwa mshangao mkubwa kuhusu tamko la Kamati kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwa viongozi wake wa kitaifa wakiongozwa na Mwenyekiti Freeman Aikael Mbowe, watahudhuria sherehe za kitaifa za Uhuru wa Tanganyika 09th Dec,2019 zinazotarajiwa kufanyika kikanda kwa mara ya kwanza Mkoani Mwanza.
Nasema, nimepokea tamko hilo kwa mshangao kwa sababu, kwanza sikuamini iwapo ni kweli limetolewa na Kamati kuu ya Chadema, lakini pia sikuamini kwamba kuna wakati shetani anaweza kujigeuza kuwa malaika. Hii ni kwa sababu shetani kamwe hajawahi kuzaliwa upya bali shetani ni yule yule, na kinachobadilika kwake huwa ni mbinu za uadui anazozitumia pindi anapotaka kumwangamiza mwanadamu. Kuna wakati anaweza kujigeuza kuwa katika umbo la nyoka, simba, chui na wakati mwingine hata kudiriki kuonyesha kwamba anayo tabia ya matendo mema sawa na malaika wakati si kweli.
Ni jambo la kushangaza kwamba, Chadema waliosusia sherehe za kuapishwa kwa Rais Magufuli tarehe 05th Nov,2015 pale Uwanja wa Uhuru na kueleza kwamba, hawamtambuwi kama Rais aliyechaguliwa kidemokrasia kwa kushinda kupitia uchaguzi, leo ndiyo wanasema wako tayari kuhudhuria sherehe za Uhuru, kwa maana wawe karibu au waketi jukwaa moja na Rais wasiyemtambua? Hili halikubaliki.
Ji jambo la kushangaza kwamba, Chadema waliosusia hotuba ya Rais wakati akizindua Bunge tarehe 20th Nov,2015 Jijini Dodoma, ambapo kupitia hotuba ile ndipo watanzania tumeweza kuona mwelekeo wa taifa tulilonalo kwa sasa na siku za usoni, eti leo ndiyo wanadai wako tayari kuhudhuria sherehe za Uhuru wa Tanganyika (Tanzania)? Hii haikubaliki.
Ni jambo la kushangaza kwamba, Chadema waliosusia sherehe za kitaifa kwa miaka minne mfululizo ikiwemo ya Uhuru ambayo ni miongoni mwa tunu za kitaifa, leo ndiyo bila aibu wanasema wapo tayari kushirikiana na Rais? Haiwezekani.
Ni jambo ya kushitua kwamba, Chadema ambao wanapinga kila kitu yakiwemo maendeleo yanayofanywa na serikali ya awamu ya tano kwa miaka minne mfululizo kama vile miradi mikubwa ya kiuchumi, ununuzi wa ndege, elimu bure, maji, afya, umeme vijijini, mikopo vyuo vikuu, barabara, fly over, mazao ya wakulima, eti leo ndiyo wanataka kuwa karibu na Rais? Haiwezekani.
Ni jambo la kufikirisha kwamba, Chadema waliodiriki hata kumzushia Rais wa nchi kifo kutokana na uadui walioujenga kwake, na hawajamwomba radhi kwa kitendo hicho, eti leo ndiyo wanataka wakakae jukwaa moja na Rais? Haiwezekani.
Ni jambo la kushangaza kwamba, Chadema wanaoshiriki ndani na nje ya nchi kulihujumu taifa dhidi ya vita vya uchumi ikiwemo kushirikiana na mabeberu kukamata rasilimali zetu (ndege) ili kudhoofisha jitihada za nchi kujikomboa kiuchumi, eti leo ndiyo wanataka wakakae jukwaa moja na Mzalendo wa nchi, mtetezi wa taifa, mtetezi wa wanyonge. Hii haikubaliki.
Ni jambo la kushangaza kwamba, Chadema kupitia Tundu Lissu walivyozunguka dunia nzima kuishitaki serikali, kuombea nchi mabaya ikiwemo kunyimwa misaada ya maendeleo kutoka nchi wahisani, mikopo pamoja na kuitangaza nchi vibaya kuhusu kukiuka haki za binadamu na utawala bora, eti leo ndiyo wanataka kukaa jukwaa moja na Rais wanayemwita dikiteta. Hilo haliwezekani.
Ni jambo la kushangaza kwamba, Chadema wanaokesha na kushinda mitandaoni wakimtukana Rais wa nchi kwa utovu wa nidhamu uliovuka kiwango cha maadili, ndiyo sasa wanataka kukaa jukwaa moja na Rais wanayemtukana kutwa mara tatu kama vile wanatoa dozi kwa mgonjwa wakati Mwenyekiti wao Mbowe yupo na jajawahi kukemea uovu huo. Hii haikubaliki.
Kwa maoni yangu ili tamko la Chadema kushiriki sherehe za uhuru liweze kueleweka kwa Watanzania kwamba lina nia njema, viongozi wa Chadema wangeanza kutekeleza masharti yafuatayo:-
Kwanza, wamtambuwe Rais Magufuli kwamba ni Rais halali aliyechaguliwa kidemokrasia na si vinginevyo.
Pili, watambuwe na kuunga mkono jitihada zinazofanywa na serikali ya Chama cha Mapinduzi hususani katika swala la kufufua uchumi wa nchi, kuwaletea wananchi maendeleo.
Washiriki kwa vitendo vita dhidi ya rushwa, ufisadi pamoja na kushiriki vita vya uchumi kwa kutoshirikiana na mabeberu wa nje.
Waache kumtukana Rais ikiwa ni pamoja na kumwomba msamaha, kuwaomba msamaha watanzania kutokana na uovu waliofanya kwa nchi hii.
Watamke hadharani kwamba, kuanzia sasa watafanya siasa za ushindani kwa njia ya kistaarabu, kwa kuheshimiana, kwa kushindanisha sera na hoja badala ya matusi na kwamba kiongozi wao au mwanachama wao atakayekwenda kinyume, Chama kitamchukulia hatua za kinidhamu mara moja.
#MUHIMU: Iwapo Chadema haitatimiza masharti haya, kwa unyenyekevu mkubwa, naviomba vyombo vya dola visiruhusu viongozi wa Chama hiki kumsogelea Rais wetu mahali popote atakapokuwa. Kama mbwai na iwe mbwai tu, hakuna namna.