samurai
JF-Expert Member
- Oct 16, 2010
- 11,478
- 24,262
Hivi mkuu Rose,kweli kabisa hata ukitumia akili ya kawaida tu ya kuzaliwa nayo ambayo Mungu anatunuku kila mtoto wake,huwezi ona kuwa ni nani mwenye njama za kuivuruga CDM? Kweli mkuu hulioni hilo hata kwa haya haya macho ya nyama?
Pamoja na yote kuzungumzwa na kuwekwa hadharani kwa ushahidi kadha wa kadha kwa pande zote zinazohitilafiana katika CDM,bado hujaweza kujua tu nani ni nani na anafanya nini kwa manufaa ya nani na yapi?
Ni vyema sana tukawa tunarudi nyuma kujaribu kuona kulitokea nini katika jambo fulani kwa kipindi cha nyuma,maana bila kujua historia ya jambo lolote lile,ni vigumu sana kuweza kutambua jambo hilo kwa undani.
mkuu joel,, naona hiyo comment yako iko kijasusi sana, maana CDM watasema ni ZZK na wenzake.. ila mimi kwa mtazamo wangu ni wana-CDM wenyewe wanaua chama chao.
namaanisha nini ZZK ni mbunge kupitia CDM kigoma, anawashutumu wana CDM wenzake suala ni demokrasia ndani ya chama na wana-CDM wenzie wanamshutumu ZZK suala ni USALITI.
Kesi iko mahakama kuu wakili wa ZZK ni MSANDO kutoka CDM (tena diwani) kwa hiyo hapa tunapata picha kumbe hata MSANDO Halidhiki na hili, mwishoni tunaona kuna wengi wako kimya wanamawazo kama ZZK Ndani ya CDM.
MWIGAMBA alikuwa mwenyekiti wa chama ngazi ya mkoa, akashutumiwa na wana-CDM suala ni USALITI yeye anasema alikuwa akipigania demokrasia.
Marehemu chacha wangwe (rasta) alikuja na mawazo kama ya ZZK akaitwa naye msaliti akaenda zake.
KAFULILA,kabourou, arfi walikuwa wana -CDM wengine hadithi ni ileile kama ya ZZK.
Hawa wote ni wanachama ndani ya CDM, sio kutoka chama kingine.
CCM kama adui wa CDM hawezi kuwa salama kama adui yuko fit (tunasema adui mwombee njaa), hatutakiwi kuishutumu CCM katika hili ila kinachotakiwa CDM ni kumaliza shida yao na wao wamwombee njaa adui (CCM).
NI MTAZAMO TU.