Ni asili ya Uislaam kutii mamlaka ila sio uchawa

Ni asili ya Uislaam kutii mamlaka ila sio uchawa

AbuuMaryam

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2015
Posts
2,649
Reaction score
4,756
Uislaam unatufundisha waumini wake kutii mamlaka hata kama aliyepata mamlaka hayo hakustahili...au ameyapata mamlaka hayo isivyostahili...madhali amekuwa KIONGOZI...NA MAMLAKA YAPO MIKONONI MWAKE...NI WAJIBU WETU SISI WAISLAAM KUTII MAMLAKA HAYO.

Hata kama kuna wakati utakuwa unaonewa...ila tumeamrishwa kutotoka nje ya utiifu wa kiongozi.

Pamoja na hayo, HATUJARUHUSIWA KUMTII KIONGOZI kwenye jambo linalohusu KUMUASI ALLAAH MUNGU WETU...

Vilevile dini yetu haitaki UNAFKI useme Nyeupe mdomoni, hali ya kuwa nyeusi MOYONI, au USIFIE MAASI YA KIONGOZI ILI KUTETEA MASLAHI YAKO BINAFSI(UISLAAM HAURUHUSU UCHAWA)...

YAANI TUMEAMBIWA NA MTUME WETU MUHAMMAD SWALALLAAHU ALAYHI WA SALLAM KUWA..."SEMA AU FANYA JAMBO ZURI LINALOHITAJIKA, UKIONA HUWEZI PIGA KIMYA."

Naamini wengi wetu tungepewa mamlaka haya haya waliopewa viongozi hawa...mngefanya hivi hivi au zaidi kwa yeyote anayehatarisha mamlaka yako.
 
Kwa tafsiri ya yanayojili Tanzania na uhalisia WA kitabu na Imani yenyewe it's total wrong .
Qur'an haiwezi kuwa wrong ili kukufurahisha wewe na wajinga wenzako.

Qur'an ndio muongozo wa waislamu, asiyefuata muongozo huo huyo siyo Muislamu.

Kule Zanzibar kuna mbunge wa c alitangazwa mshindi kwa kura za wizi, lakini wazazi wake ni Waislamu safi walimwambia asiwashirikishe kwenye dhulma aliyofanya, yule mbunge alijiuzuru kabla ya kuapishwa.

Misingi ya dini ndio iko hivi, na siyo kuchaguwa yale yanayokupendeza wewe tu.

 
Qur'an haiwezi kuwa wrong ili kukufurahisha wewe na wajinga wenzako.

Qur'an ndio muongozo wa waislamu, asiyefuata muongozo huo huyo siyo Muislamu.

Kule Zanzibar kuna mbunge wa c alitangazwa mshindi kwa kura za wizi, lakini wazazi wake ni Waislamu safi walimwambia asiwashirikishe kwenye dhulma aliyofanya, yule mbunge alijiuzuru kabla ya kuapishwa.

Misingi ya dini ndio iko hivi, na siyo kuchaguwa yale yanayokupendeza wewe tu.
Quran ina ruhusu mwanamke kuwa kiongozi?

Biblia natural imekataza mwanamke kuwa kiongozi.

Je quran?
 
Uislaam unatufundisha waumini wake kutii mamlaka hata

UCHAMBUZI WA KINA :

Uislamu upi huo? Wasiofanya mapinduzi, mabadiliko, vuguvugu, uchaguzi ? Ni wa Muslim brotherhood, Sunni, Shia au Sufi wa Abu Dhabi n.k ?

Maana tunaona Muslim Brotherhood kule Egypt, Sudan walikuwa wachochezi wa Arab spring revolution kupinga watawala waliopo madarakani na kusababisha madikteta wa Tunisia, Egypt kupinduliwa na demokrasia ya kiislamu inayohoji mienendo ya watawala kuhojiwa, kupingwa kwa maandamano, kuchagiza uchaguzi n.k

Wakati maSufi wa kule Abu Dhabi, UAE Emirati 7 zinafanya juhudi zote kufanya raia wasishiriki katika siasa, wasihoji, wasifanye midahalo kwa kifupi Sufi hawataki uchaguzi wowote bali familia ya watawala ndiyo wataamua nani arithi uongozi bila raia kushirikishwa

Tukienda nako Tehran Iran waislamu Mashia wanafanya siasa, wanafanya uchaguzi, wanafanya mapinduzi kuondoa watawala au kungoa mfumo wasioutaka .

Tukienda kule Bangladeshi tuliona nchi hii ya Sunni watu wakiandamana na kumtimua waziri mkuu kutoka Ikulu akakimbia nchi.

Pia nchini Pakistani nchi yenye Sunni wengi kuna vyama vingi, watawala hupinduliwa siasa za vyama vingi vikishindikana kuwa huru. Watawala wa zamani hufunguliwa mashtaka na kutupwa jela baada ya kuondolewa kwa nguvu ya umma Ikulu n.k


Hapa jirani Sudan nchi ya kiislamu pia wanazichapa wenyewe kwa wenyewe hata kama kuna mtawala ili wamuondoe wafanye mabadiliko.

Na nchi jirani ya kiislamu ya Zanzibar walifanya mapinduzi matukufu 1964 kumng'oa Sultani, ambaye baadaye alipewa ukimbizi kwa siku kadhaa katika nchi ya Tanganyika akapewa jumba Oysterbay jijini Dar es Salaam akisubiri taratibu za ukimbizi kukamilishwa aende Uingereza.
 
Uislaam unatufundisha waumini wake kutii mamlaka hata kama aliyepata mamlaka hayo hakustahili...au ameyapata mamlaka hayo isivyostahili...madhali amekuwa KIONGOZI...NA MAMLAKA YAPO MIKONONI MWAKE...NI WAJIBU WETU SISI WAISLAAM KUTII MAMLAKA HAYO.

Hata kama kuna wakati utakuwa unaonewa...ila tumeamrishwa kutotoka nje ya utiifu wa kiongozi.

Pamoja na hayo, HATUJARUHUSIWA KUMTII KIONGOZI kwenye jambo linalohusu KUMUASI ALLAAH MUNGU WETU...

Vilevile dini yetu haitaki UNAFKI useme Nyeupe mdomoni, hali ya kuwa nyeusi MOYONI, au USIFIE MAASI YA KIONGOZI ILI KUTETEA MASLAHI YAKO BINAFSI(UISLAAM HAURUHUSU UCHAWA)...

YAANI TUMEAMBIWA NA MTUME WETU MUHAMMAD SWALALLAAHU ALAYHI WA SALLAM KUWA..."SEMA AU FANYA JAMBO ZURI LINALOHITAJIKA, UKIONA HUWEZI PIGA KIMYA."

Naamini wengi wetu tungepewa mamlaka haya haya waliopewa viongozi hawa...mngefanya hivi hivi au zaidi kwa yeyote anayehatarisha mamlaka yako.
Sema ni asili ya watanzania kutii mamlaka usisingizie uislam. Uislam unasimamia haki popote pale ambapo dhuluma ipo bila kuangalia mamlaka za kidunia.
 
Uislaam unatufundisha waumini wake kutii mamlaka hata kama aliyepata mamlaka hayo hakustahili...au ameyapata mamlaka hayo isivyostahili...madhali amekuwa KIONGOZI...NA MAMLAKA YAPO MIKONONI MWAKE...NI WAJIBU WETU SISI WAISLAAM KUTII MAMLAKA HAYO.

Hata kama kuna wakati utakuwa unaonewa...ila tumeamrishwa kutotoka nje ya utiifu wa kiongozi.

Pamoja na hayo, HATUJARUHUSIWA KUMTII KIONGOZI kwenye jambo linalohusu KUMUASI ALLAAH MUNGU WETU...

Vilevile dini yetu haitaki UNAFKI useme Nyeupe mdomoni, hali ya kuwa nyeusi MOYONI, au USIFIE MAASI YA KIONGOZI ILI KUTETEA MASLAHI YAKO BINAFSI(UISLAAM HAURUHUSU UCHAWA)...

YAANI TUMEAMBIWA NA MTUME WETU MUHAMMAD SWALALLAAHU ALAYHI WA SALLAM KUWA..."SEMA AU FANYA JAMBO ZURI LINALOHITAJIKA, UKIONA HUWEZI PIGA KIMYA."

Naamini wengi wetu tungepewa mamlaka haya haya waliopewa viongozi hawa...mngefanya hivi hivi au zaidi kwa yeyote anayehatarisha mamlaka yako.
Kutii mamlaka juu ya utekaji kuwaua watu kuwabambikia kesi za uongo wizi wa pesa za umma, vitendo haramu vya kishetani ndio waislam mnapenda? Mnatii mamlaka kwa kubariki mauaji manyanyaso kwa wakosoaji, waislam nani kawaroga?
 
Hivi kiislamu mwanamke kuwa raisi,kiongozi mkuu juu ya jamii pana kama tunavyoona hapa nyumbani ni sahihi?
Hii JF inaanza kuwa cha hatari wabaguzi wamehamia humu, na siku serikali ikifunga huu mtandao mmiliki wake asijeanza kulialia wana uwezo w kuchuja threads wakazuia hizi za kibaguzi
 
Huko Bakwataccm kuna ibirisi wengi sana na ndiko chanzo cha utekaji kwani huwakuti bakwataccm wakakemea vitendo haramu vya kishetani vinavyofanywa na ccm wao
 
Hii JF inaanza kuwa cha hatari wabaguzi wamehamia humu, na siku serikali ikifunga huu mtandao mmiliki wake asijeanza kulialia wana uwezo w kuchuja threads wakazuia hizi za kibaguzi
watesi nao siyo wajinga wanajua Bakwataccm kuna ibirisi wengi kuna unafiki kuna uchawa kwa ccm na mambo mengi ya hovyo ambayo wangependa kuyajua hawawezi funga huku
 
Back
Top Bottom