Watu wafanye kazi mkuu, hivi unadhani hata serikali ikiamua kutoa misaada ya chakula kila kaya inapata kiasi gani? Hakitazidi debe tano, sasa hizo debe tano zikiisha wanaenda wapi?
Watanzania kwa bahati mbaya tulizoea vibaya sana akili za utegemezi na kulaumu laumu kila kitu.
Magufuli kaza Uzi tu, next time watu watalima chakula kitaozea kwenye maghala
Njaa ya familia yako sio hoja ya msingi sana kwa serikali, watu wanafanya uzembe kila kitu ili mwishoni walaumu serikali.
"Poor minded people will always blame politicians for their own problems "
Fanyeni kazi watanzania, acheni maneno ya wanasiasa, hata kama chakula kimepungua serikali haiwezi kuwalisha ninyi nyote, tuna uchumi gani wa kulisha nchi nzima hata kwa wiki mbili? Wanasiasa wanawadanganya oooh serikali haiwajali wananchi wake wakati wa njaa sasa hao wakiingia madarakani wataweza kuilisha nchi hii hata wiki mbili in case kuna njaa?
Ni kweli sisi bado ni maskini wa vipato, tusikubali kua maskini wa akili, kukaa tunalaumu laumu kila kitu, igeni mifano ya wachaga wao wanachakarika, wakati nyie wengine mnalialia wao magari yanaongozana kwenda Moshi kusheherekea Christmas sasa wao wako Tanzania gani? Au wote ni wapiga dili?
Fanyeni kazi bhana