Ni aibu kusema Tanzania kuna njaa

Ni aibu kusema Tanzania kuna njaa

Chakula cha familia yako kiwe kipaumbele cha CCM? kwa msimamo huu mtalalamika sana.Ninakutana na watanzania wanaojua majukumu yao wanaotafuta maeneo ya kumwagilia na kuvuna wanachotaka na kwa wakati wanaotaka.Nimekutana na wakulima ambao hawajawahi kusaidiwa na mtu yeyote ili waanze umwagiliaji.Baadhi yao walianza kwa kubeba maji kwa mikono yao( Ilula kando kando ya barabara kuu utawaona) wengine wakamudu kununua pampu za kuendesha kama baiskeli wakasonga mbele hadi wanatumia mashine za mafuta.

Mnasubiri umwagiliaji kwa miundombinu ya serikali.Ni sawa na hapa jiulize ukiacha mahali ulipong'ang'ania kuishi umewahi kutafuta eneo lenye mifereji iliyotengezwa tayari ukaikosa nchi nzima? Je iliyopo imetumika inavyopaswa? Au mpka usukumwe? Njaa itatusukuma.

Niliwashauri wenye nia ya dhati ya kuepuka kilimo cha mvua tu watafute Kenya Mashariki Wakamba wamefanya nini.Yapo maeneo Ukambani mvua inanyesha siku 14 tu kwa mwaka njaa wameisahau.Hawakusubiri wahisani wala Serikali.Kilichowapa maarifa ni njaa.Mkamba mmoja tu alijiuliza tumesaidiwa miaka Zaidi ya 50 njaa haiishi,je tuendelee kusubiri misaada milele? Jibu lake likawa hapana tuiondoe njaa wenyewe akawahamasisha ndugu zake na kuwahimiza namna ya kufanya.

Hawakumkubali kirahisi,matokeo ya waliokubali yaliwashawishi waliokataa.Unaposubiri kitu cha kufanya njaa haisubiri.
Kweli kaka mtu anayejitambua hasubiri serikali imfanyie kila kitu. Mwaka jana nilikwenda mkoa wa Shinyanga nikakuta watu wanalima kilimo cha mpunga kwa kumwagilia kwa kutumia diesel water pump. Nilimuuliza huyo mtu una mudu vipi gharama za mafuta akaniambia huwa anafuga kuku kila anapotaka kumwagilia huuza kuku mmoja na kupata lita zisizopunga tano ambazo zinauwezo wa kunyeshea hata heka mbili na hufanya hivyo mara mbili kwa wiki. Anasema zamani walikuwa wanalima hadi kuvuna kwa kutegemea mvua. Mabadiliko ya tabia nchi yamewafanya wajiongeze ili wasiwe wana kula hasara.
 
Kweli kaka mtu anayejitambua hasubiri serikali imfanyie kila kitu. Mwaka jana nilikwenda mkoa wa Shinyanga nikakuta watu wanalima kilimo cha mpunga kwa kumwagilia kwa kutumia diesel water pump. Nilimuuliza huyo mtu una mudu vipi gharama za mafuta akaniambia huwa anafuga kuku kila anapotaka kumwagilia huuza kuku mmoja na kupata lita zisizopunga tano ambazo zinauwezo wa kunyeshea hata heka mbili na hufanya hivyo mara mbili kwa wiki. Anasema zamani walikuwa wanalima hadi kuvuna kwa kutegemea mvua. Mabadiliko ya tabia nchi yamewafanya wajiongeze ili wasiwe wana kula hasara.


Ukisema ukweli kama huu watakuambia unaongea nadharia.Wengine wamezoea kudanganywa na kudanganya.Hongera wakweli wataelewa.
 
Kilimo cha umwagiliaji ni lini kimewahi kuwa kipaumbele cha serikali za CCM?

Acha kujitoa akili.
Hao vijana wanaomiminika mjini kutafuta ajira kwenye sekta ya sanaa!

Nchi kugeuzwa soko la bidhaa zisizozalishwa nchini!

Utitiri wa machinga na bidhaa za nje!

Vijana vijijini waliokuwa wanashinda kwenye 'mapool' na kutiana mimba!

Iko mifano mingi yenye kutoa kiini cha upungufu wa chakula nchini.
 
Hakuna suala la unafiki mmezoea kuwa na viongozi wanaotoa ahadi za uongo.
Hapa Kazi tu
Acha unafki wewe, ukweli ni kwamba Sehemu mkubwa ya nchi yetu inayojishughulisha na kilimo ilikiwa na desturi ya kuwa na vipindi 2 vya mvua Kwa mwaka,
Hadi sasa mvua hazijanyesha ipasavyo, waliojitahidi kupanda mazao wakitegemea mvua mazao yamekauka.
Wananchi wanapoongelea baa la njaa ni kutokana na mvua kutonyesha.
Acheni ujinga wenu nchi hii wakulima wengi wanategemea kilimo cha mvua
 
Mkuu mto Nile nimetolea mfano nina maana tunatakiwa tuanzishe kilimo cha umwagiliaji kutumia mito na maziwa tuliyonayo
Serikali ndo kila kitu kuwawekea sawa miundombinu ya maji wananchi wake,hakuna mahali kwenye maji ya kutosha na wananchi wakawa hawalimi wakailalamikia serikali wana njaa.hakuna sehemu kama hiyo.sehem nyingi zenye njaa zina ukame na vyanzo vya maji kwa ajili ya umwagiliaji hakuna hili sasa ni jukum la serikal iangalie nini cha kufanya kwa wananchi wake wapate maji
 
Serikali ndo kila kitu kuwawekea sawa miundombinu ya maji wananchi wake,hakuna mahali kwenye maji ya kutosha na wananchi wakawa hawalimi wakailalamikia serikali wana njaa.hakuna sehemu kama hiyo.sehem nyingi zenye njaa zina ukame na vyanzo vya maji kwa ajili ya umwagiliaji hakuna hili sasa ni jukum la serikal iangalie nini cha kufanya kwa wananchi wake wapate maji
Unajua Maelezo bila takwimu inakuwa vigumu hata kuchangia. Kiukweli nchi ina eneo la kekta milioni 40 linalofaa kwa Kilimo, asilimia 10.2 ya eneo hilo ndilo linalolimwa. Eneo linalofaa kuendelezwa miundombinu ya umwagiliaji ni hekta milioni 29.4. Eneo lenye miundombinu linakaribia hekta laki 5 tu. Maeneo haya yote kwa sasa yanategemea maji ya juu ya ardhi ambayo kama mvua isiponyesha maji hayo nayo hukauka. Kwahiyo, kinachotakiwa kwa sasa ni kuhifadhi maji kwa kukinga maji ya mvua ambayo hufurika kwenda baharini kunapokuwa na mvua nyingi.

Kwahiyo, Kilimo cha umwagiliaji kinatakiwa kuwa ni strategic ukizingatia mabadiliko ya tabia nchi kwa sasa.

Hili ni jambo linalohitaji uwekezaji mkubwa kwa maana ya rasilimali. Nayazungumza haya ili mtu asidhani kuwa ujenzi huo ni jambo la kulala na kuamka ukakuta kuna miundombinu inayotakiwa kwa umwagiliaji. Hili ni jambo la kupangilia kwa muda mrefu.

Jambo jingine ni kwa wananchi ambao wamebahatika kuwa sehemu ya hizo hekta laki 5 zenye miundombinu ya umwagiliaji kujipanga vizuri kutumia ardhi hiyo kwa tija zaidi ili kupata manufaa zaidi kwa kuzalisha chakula hata mara mbili kwa eneo kwa mwaka.

Tija kwa eneo bado iko chini hata kwenye maeneo yenye miundombinu ya umwagiliaji. Hivyo, wakulima na wadau tunayo kazi ya kufanya ili tuweze kupiga hatua zaidi tutoke kwenye Kilimo cha kujikimu na kuwa na Kilimo cha kibiashara.

Serikali haina mashamba Bali inaweka mazingira wezeshi ya upatikanaji wa pembejeo na wataalam. Wananchi tunatakiwa kujiongeza kwa kutumia fursa zilizopo kwa kulima kibiashara. Tunapokwama tunaiambia serikali nn tumekwama na tunahitaji msaada upi.

Suala la mvua kutonyesha au kuchelewa Serikali inalaumiwa kwa lipi? Kwakuwa mvua hunyesha kwa neema na rehema za mungu.

Nilitegemea wananchi waiombe Serikali kama kuna uhaba wa mbegu zinazovumilia ukame ama kuomba kupatiwa ruzuku ya aina fulani n.k.

Kwahiyo, tujenge hoja zinazoweza kutusaidia kama nchi kuondokana na tatizo, tutoe ushauri ambao utasaidia serikali na wananchi kujipanga vizuri zaidi katika Siku za usoni, kukabiliana na majanga.

Huo ndo mchango wangu kwa sasa, najua kuna wengine watakuwa na michango mizuri zaidi ya kutujenga.
 
Back
Top Bottom