Ni aibu kusema Tanzania kuna njaa

Ni aibu kusema Tanzania kuna njaa

Hivi mleta mada kweli huwezi kuuona ukweli wewe mwenyewe mpaka yule 'Mfalme' aje kukuaminisha kwa zile porojo zake?

'Mfalme' anasema "Tz hakuna njaa kabisa, sitaleta chakula cha bure cha msaada, ardhi ni ya kijani, watanzania muache uvivu, muanze kulima vyakula vinavyohimili ukame!"
What does he mean?
Try to read between the lines, utaona ukweli.
Akilete chakula cha msaada kwani hata anacho???? Hahaahah
 
Kuna nafasi gani utenguzi umetokea ili uteuliwe kwa kuwa nakuona huna kazi. Kuwa na maziwa na mito mingi hakupelekei wananchi kutopatwa na njaa. Kule kwetu Mara tuko pembezoni mwa ziwa pia kuna MTO Mara lakini si maeneo yote ya Mara yako Karibu na ziwa au MTO kuwa wachote maji na waendeshe kilimo cha umwagiriaji. Inahitajika kuandaliwa mazingira kama vile kusambaza mambomba ya maji ili wananchi wajishughulishe na hicho kilimo unachodai. Pia siyo kila ardhi anastahili kwa kilimo cha umwagiriaji. Mkoa kama wa mara kuna ardhi kidogo sana kwa ajili ya kilimo. Emu chukulia familia yenye watu 10 kuwa na shamba lenye ukubwa wa ekari 5 na ardhi imechoka. Ndugu upumbavu huu unaoandika haukubaliki ni lazima serikali iwajibike kuwanusuru watu waliokumbwa na baa la njaa.
Nyie always ni kumtafutia lawama Rais Magufuli hata akiwafanyia nini kwenu ni negative. Sasa this time msipolima ama kufanya kazi mtaisoma namba.
 
Ni kweli mkuu aliyeshiba hawezi kumjua mwenye njaa.
Mkuu...
Naunga hoja ya mleta uzi.
Kiuhalisia alicho kisema Pombe, ni sahihi.
Japokua binafsi sina mahaba nae, lakini kwa hili la Tanzania kuna njaa.... Hapana aiseeee.
Na ukijiuliza kwamba wapi kuna njaa ndani ya Tanzania, hakuna atakae toa jibu sahihi
 
Kilimo cha umwagiliaji ni lini kimewahi kuwa kipaumbele cha serikali za CCM?

Acha kujitoa akili.
Mkuu.....
Upo sahihi, lakini....
Ni kweli Tanzania kuna njaa?
Kama jibu ni ndio.
Je, njaa hiyo ipo wapi?
 
Penye miti hapana wajenzi.

Magufuli anachosema kuhusu chakula kinaingia akilini.

Watanzania watie akili.
Bahati mbaya waTanganyika tunapenda sana kulalamika na kusikiliza maneno ya kuletewa, badala ya kusikiliza hoja ya kile kinacho semwa na muhusika na tuelewe nini anamaanisha.
Mnyonge tumnyonge, lakini haki yake tumpe jamani....
 
Hakuna suala la unafiki mmezoea kuwa na viongozi wanaotoa ahadi za uongo.
Hapa Kazi tu
Kuongoza nchi sio mchezo alisema ni rais wa wanyonge ambao hawana uwezo wa kununua pampu za maji angalia alichofanya Bukoba na simiyu eti rais wa wanyonge kila tatizo anafuta visingizio na njaa anawakazia wanasiasa na vyombo vya habari
 
Kuna watu Wa ajabu sana tatizo La Tanzania sio rasilimali Bali matumizi ya hizo rasilimali serikali ndio inayotakiwa kuweka mazingira mazuri mfano suala La irrigation schemes Nani anatakiwa kuzijenga? Kilimo kwanza ulikuwa Sera ya serikali walifanya nini kuboresha Kilimo kiwe cha kisasa? Leo mvua hakuna karibu nchi nzima unabishaje sasa kama hakuna njaaa bei ya unga na mchele vimepanda bado watu hawajiulizi kwa nn, so ukisema kuwa hakuna njaaa basi sema hakuna haja ya kukopa au kupewa Msaada na Morocco kwa kuwa ss na Morocco Nani ana rasilimali nyingi? Mbona bado tunaomba Msaada kwenye nchi jangwa? Naona tunakimbia kivuri chetu so mleta mada umepungukiwa kidogo akiri au huyajui mazingira ya Tanzania kwa maana hujatembea ndani ya nchi hii zaidi ya kukaa town mchele unaenda kununua kisutu. Kwa kifupi Kilimo cha umwagiliaji nchi hii ni kwa wachache yaani hata 2% hawafiki waliobaki ni Kilimo mvua au wanaolima mbogamboga pembezoni mwa mto napo serikali hairuhusu. Kilimo cha umwagiliaji kinahitaji uwekezaji Wa miundo mbinu ndugu zetu wengi ni maskini usichukulie poa.
 
Siku zote binadam hana shukurani yule mlikuwa mnamwita Dhaifu sasa wasasa anawasafishia nchi ni mbaya pia what kind of Presidential material you want?
Suala la first lady kila kiongozi ana hulka yake kama Mheshimiwa hataki kumhusisha mambo ya siasa ni dhambi?
Rais Magufuli kama mwanadamu hakosi mapungufu lakini mnyonge mnyongeni haki yake mpe
Kiongozi ye yote bora huchukua mema ya watangilizi wake. Huangalia maeneo ya kuboresha. Hawalaumu watangulizi wake. Hujifunza kutoka kwa watangulizi wake.
Umesema vema kuwa Magufuli ana udhaifu wake kama ilivyo kwa watangulizi wake.
Kwamba nchi hii ilikuwa imeoza ni maneno yanayokosa hekima na busara. Kumbuka Magufuli amekuwa waziri kwa miaka 20. Hivyo chunga maneno yako, indirectly unamsema yeye pia.
 
Mie binafsi nakubaliana na kauli ya Mheshimiwa Rais Magufuli kuwa hapa nchini hakuna njaa. Tanzania ni moja wapo za nchi ambazo mwenyezi Mungu ameipa kila aina ya neema lakini watu wake hawataki kuitumia ipasavyo kwa sababu ya kutotaka kufanya kazi haswa za kilimo.

Leo nchi kama Misri yenye idadi ya watu karibu Milioni 100 wanaishi kwa kutegemea kilimo cha umwagiliaji kutoka mto Nile inakuwaje hapa Tanzania tuna maziwa na mito mengi mbali mbali na mvua kunyesha mara kwa mara tunashindwa kuwa na chakula na kusingizia njaa?

Sasa hivi tuna kiongozi asiyekuwa mnafiki anachowaambia watanzania ni ukweli mtupu na inatakiwa mkubaliane na ushauri wake kwamba kuna wafanyabiashara na wanasiasa wanajaribu kutengeneza hili suala la njaa kwa manufaa ya kujipatia umaarufu wa kisiasa na faida ya kibiashara.
Meli mbovu, nyumba za serikali, barabara mbovu zimeshatolewa ufafanuzi? Mijitu ya Geita bn mtoto wa kiume kujipendekeza ni aibu sn
 
Mkuu...
Naunga hoja ya mleta uzi.
Kiuhalisia alicho kisema Pombe, ni sahihi.
Japokua binafsi sina mahaba nae, lakini kwa hili la Tanzania kuna njaa.... Hapana aiseeee.
Na ukijiuliza kwamba wapi kuna njaa ndani ya Tanzania, hakuna atakae toa jibu sahihi

Kwa sasa kinatumika chakula cha akiba cha msimu uliopita kilicholimwa msimu huu kimekauka sasa subiri muda kidogo tu utajua ndio maana unahisi hakuna njaa njaaa itakuwepo soon viashiria nenda kanunue unga utajua bei imeongezekaje, then uwe unaangalia taarifa za habari wananchi wanalia au nao wamenunuliwa? Mfano mdogo tu kisiwani ukerewe
 
Hivi huu ukame umeikumba nchi nzima hata ile mikoa big five kwa uzalishaji wa chakula imekumbwa nayo na ukame kama ni hivyo basi nchi yetu inageuka kuwa jangwa kama Sudan au Somalia, basi kama si hivyo basi mikoa isiyo na njaa isaidie kusambaza vyakula kwenye mikoa inayokumbwa na njaa hata kwa kuuziana ili kupunguza tatizo.
 
Unajua humu kuna watu watetea masilahi ya chama na watetea masilahi ya nchi na watu wake.
Km nyie tu hizo ajira za watu mezifugia kabati na kumkaanda uhakiki usioisha ili msiajiri watu.
WW MTOA THREAD UNASHAMBA? UNAFANYA KILIMO CHA UMWAGILIAJI?
MUNGU WENU WA SISIEM NAYE ANAJISHUGHULISHA NA KILIMO CHA UMWAGILIAJI?
Tatizo ukiwa msukule wa chama fulan huwez kuona ya mbele. Watu wanaishi chin ya dola moja ataweza kununua vifaa vya umwagiliaji? Kaz kuimba hapa kaz tu km misukule. KAM NYIE KUAJIRI TU MESHINDWA HUYO MTANZANIA ANAYEUSHI CHIN YA DOLA ATAWEZA?
 
Mie binafsi nakubaliana na kauli ya Mheshimiwa Rais Magufuli kuwa hapa nchini hakuna njaa. Tanzania ni moja wapo za nchi ambazo mwenyezi Mungu ameipa kila aina ya neema lakini watu wake hawataki kuitumia ipasavyo kwa sababu ya kutotaka kufanya kazi haswa za kilimo.

Leo nchi kama Misri yenye idadi ya watu karibu Milioni 100 wanaishi kwa kutegemea kilimo cha umwagiliaji kutoka mto Nile inakuwaje hapa Tanzania tuna maziwa na mito mengi mbali mbali na mvua kunyesha mara kwa mara tunashindwa kuwa na chakula na kusingizia njaa?

Sasa hivi tuna kiongozi asiyekuwa mnafiki anachowaambia watanzania ni ukweli mtupu na inatakiwa mkubaliane na ushauri wake kwamba kuna wafanyabiashara na wanasiasa wanajaribu kutengeneza hili suala la njaa kwa manufaa ya kujipatia umaarufu wa kisiasa na faida ya kibiashara.
Lini tutasaidia nchi nyingine kwenye ishu ya misaada maana kwa sasa hatutaki kuomba tena misaada toka kwa wenzetu
 
Jamani baa la njaa ni janga kama majanga mengine. Janga halina uhusiano na kufanya au kutofanya kazi. Wewe umelima vizuri, mvua hazikunyesha ipaswavyo, sasa unasemacwatu hawafanyi kaxi? Kivipi? Janga linajali km unafanya au hufanyi kazi?
 
Back
Top Bottom