Ni aibu kusema Tanzania kuna njaa

Ni aibu kusema Tanzania kuna njaa

Mleta huzi hafai kuwa mwanasiasa na hafai kuwa msemaji Wa serikali kwa sababu hana nyota ya maneno; Pia yupo mbali na (NFRA) ambayo lipoti yao inasema mpaka mwaka Wa Jana kipindi kama hiki kulikua na tani 450000/=
na mwaka leo ni tani 90000/=
Pia mwaka Wa Jana mbali ya kua na Chakula cha akiba cha kulizisha mvua ilikua inanyesha maeneo mengi kipindi kama hiki = sasa wewe unasema unaungana + ungana nae tuu ila ukweli utabaki ukweli maana ng'ombe wanakufa kwa ajili ya njaa tunaona na isitoshe watu wengi wanashindia vitu vya asili na vyombo vya habari vimenyimwa Uhuru wake! Nilisha enda kwa RC nikamuelezea hali halisi kuhusu njaa alichonijibu, Rc yoyote adi Dc atakaetangaza kwake kuna njaa na kazi hana!!
Ukiwa mkweli sana utatolewa ngekewa kama Mramba
Ukishiba mkumbuke mwenye njaa.......
 
Kwahiyo ikichukua kodi ndiyo nini.wee unadhani hizo zinazowavuruga kina mtatiro ni karatasi?ile ndio kodi yako.
Wananchi wako ndo kipaumbele cha kwanza.unapowaambia wakalime.kuna mahindi yanayokuwa kwa siku 3.?mvua hamna mahindi yatakuwa na nini?
Naijua njaa.ndo maana nawatetea.
 
Pamoja na matatizo ya hali za hewa kubadilika, lazima tukubali kuna watu wanapata matatizo kwa sababu ya uvivu. Imekuwa mara nyingi tukidai aliyeshiba hajui mwenye njaa, lakini huwa najiuliza tumewahi kufuatilia na kujua walifikaje hapo nasi tukaiga. Kuna jamii nimewahi Kuishi nazo wao wanaamini kushindwa sio kukosa "ability" kama tuaminivyo sisi, bali kushindwa ni kukosa kufanya juhudi, wao daima hujitahidi kupambana na kufanya juhudi ili kufikia malengo na kuboresha maisha yao. Hii hali ya kutaka kuonewa huruma na kuvuta huruma imeshapelekea baadhi yetu kuacha kujituma na kujibidisha na kulahumu kutokusaidiwa, iwe anaelekeza msaada hutoke serkalini au kwa ndugu. kuna baadhi hata katika family level ukweli mnajua yapo haya na yamewavuta nyuma kimaendeleo. I said nijudge tu huwezavyo, ila sio wote wenye matatizo katika jamii yetu wasingeweza kujikwamua, anyway, tunatofautiana kufikiri maana tufikirivyo tunakuwainfluenced na background zetu.
Ni kweli kabisa watanzania ni wavivu karibu kila eneo hiyo ni factor mojawapo inayotufanya tuendelee taratibu sana huyu ni Super president anatutoa kuliko oza kutupeleka kwenye uturi tutafika tu. Kuna taarifa kuwa baadhi ya waathirika wa tetemeko walizibomoa nyumba zao zaidi ili fungu la fidia liwe kubwa. Magufuli gooooo goooo gooooo!
 
Ni kweli kabisa watanzania ni wavivu karibu kila eneo hiyo ni factor mojawapo inayotufanya tuendelee taratibu sana huyu ni Super president anatutoa kuliko oza kutupeleka kwenye uturi tutafika tu. Kuna taarifa kuwa baadhi ya waathirika wa tetemeko walizibomoa nyumba zao zaidi ili fungu la fidia liwe kubwa. Magufuli gooooo goooo gooooo!
Hivi Yale mahindi yaliyopo kwenye ghala la kuhifadhia chakula.serikali wanayatoa wapi?kwani serikali ina shamba?
 
Ni kweli mkuu aliyeshiba hawezi kumjua mwenye njaa.
Watu wafanye kazi mkuu, hivi unadhani hata serikali ikiamua kutoa misaada ya chakula kila kaya inapata kiasi gani? Hakitazidi debe tano, sasa hizo debe tano zikiisha wanaenda wapi?
Watanzania kwa bahati mbaya tulizoea vibaya sana akili za utegemezi na kulaumu laumu kila kitu.
Magufuli kaza Uzi tu, next time watu watalima chakula kitaozea kwenye maghala

Njaa ya familia yako sio hoja ya msingi sana kwa serikali, watu wanafanya uzembe kila kitu ili mwishoni walaumu serikali.

"Poor minded people will always blame politicians for their own problems "
Fanyeni kazi watanzania, acheni maneno ya wanasiasa, hata kama chakula kimepungua serikali haiwezi kuwalisha ninyi nyote, tuna uchumi gani wa kulisha nchi nzima hata kwa wiki mbili? Wanasiasa wanawadanganya oooh serikali haiwajali wananchi wake wakati wa njaa sasa hao wakiingia madarakani wataweza kuilisha nchi hii hata wiki mbili in case kuna njaa?
Ni kweli sisi bado ni maskini wa vipato, tusikubali kua maskini wa akili, kukaa tunalaumu laumu kila kitu, igeni mifano ya wachaga wao wanachakarika, wakati nyie wengine mnalialia wao magari yanaongozana kwenda Moshi kusheherekea Christmas sasa wao wako Tanzania gani? Au wote ni wapiga dili?

Fanyeni kazi bhana
 
Mie binafsi nakubaliana na kauli ya Mheshimiwa Rais Magufuli kuwa hapa nchini hakuna njaa. Tanzania ni moja wapo za nchi ambazo mwenyezi Mungu ameipa kila aina ya neema lakini watu wake hawataki kuitumia ipasavyo kwa sababu ya kutotaka kufanya kazi haswa za kilimo.
Leo nchi kama Misri yenye idadi ya watu karibu Milioni 100 wanaishi kwa kutegemea kilimo cha umwagiliaji kutoka mto Nile inakuwaje hapa Tanzania tuna maziwa na mito mengi mbali mbali na mvua kunyesha mara kwa mara tunashindwa kuwa na chakula na kusingizia njaa?
Sasa hivi tuna kiongozi asiyekuwa mnafiki anachowaambia watanzania ni ukweli mtupu na inatakiwa mkubaliane na ushauri wake kwamba kuna wafanyabiashara na wanasiasa wanajaribu kutengeneza hili suala la njaa kwa manufaa ya kujipatia umaarufu wa kisiasa na faida ya kibiashara.
Daahhh kuna watu matairi kwelikweli
 
Wananchi wako ndo kipaumbele cha kwanza.unapowaambia wakalime.kuna mahindi yanayokuwa kwa siku 3.?mvua hamna mahindi yatakuwa na nini?
Naijua njaa.ndo maana nawatetea.
Acha nikubaliane na wewe.. kwahiyo unataka serikali ifanyeje? ndiyo njaa ipo na mvua hakuna na kodi wanachukua japo tunakwepakwepa nini kifanyike?
 
Kauli ya Raid imetolewa muda muafaka ili tujipange vuzuri katika kilimo kwa kutumia vema mvua zinazonyesha kuzalisha mazao ya chakula. Kauli hiyo pia imesaidia sana wataalam hasa Mafisa ugani ambao kazi yao no kutoa utaalam was kilimo ili uzalishaji uwe na tija. Baadhi ya wakulima wamekuwa hawazingatii ushauri wa unaotolewa kuhusu Kilimo bora na hivyo kulima tu kwa mazoea. Utaalamu ukizingatiwa kwa kutumia mbegu bora, mbolea, kupanda kwa nafasi, kupalilia na kuzuia wadudu waharibifu uzalishaji kwa eneo (productivity) utaongezeka sana na hivyo kujihakikishia usalama was chakula na kuuza ziada inayopatikana. Jambo lingine mujimu in Kilimo kinachozingatia hifadhi ya mazingira (climate smart agriculture) ili kuhifadhi ardhi ya Kilimo na kutunza vyanzo vya maji. Mabadiliko ya tabianchi (climate change) yanatokana na shughuli za kibinadam ambazo zimeathiri upatikanaji wa mvua za kutosha na hata zikinyesha zinachelewa na zinakuwa na mtawanyiko mbaya. Kilimo cha umwagiliaji nacho kinategemea maji ya mito na maziwa ambayo kina chake kinazidi kupungua kutokana na uharibifu was mazingira katika vyanzo vya maji na mvua kidogo. Hivyo kuna mambo ambayo Watanzania tunatakiwa kujifunza kutokana na kauli ya Mheshimiwa Rais. Mfano, ufugaji wa mifugo mingi kuzidi uwezo wa eneo kuhimili (carrying capacity); kuzungusha mifugo kila mahali na hata kwenye hifadhi, vyanzo vya main, mashamba, nk tabia hii tuikemee kwasababu haiwezi kusaidia nchi. Ukataji was miti holela nalo ni janga kubwa ambalo hatunabudi kulikemea na kuhifadhi uoto wa asili. Hivyo ndivyo tunatakiwa kutafakazi kauli ya Mheshimiwa Rais kwa kuwa na mtazamo chanja.
 
Tanzania kuna njaa kweli kweli. Huo ndio ukweli. Bora tuseme ukweli ili tupone, kuliko kuficha aibu huku tukiangamia.

Achana na porojo za yule 'Mfalme' asiyependa kuusikia ukweli unaomuumbua.
Ila Rais sio wa kuitibu njaa yako
 
Chakula cha familia yako kiwe kipaumbele cha CCM? kwa msimamo huu mtalalamika sana.Ninakutana na watanzania wanaojua majukumu yao wanaotafuta maeneo ya kumwagilia na kuvuna wanachotaka na kwa wakati wanaotaka.Nimekutana na wakulima ambao hawajawahi kusaidiwa na mtu yeyote ili waanze umwagiliaji.Baadhi yao walianza kwa kubeba maji kwa mikono yao( Ilula kando kando ya barabara kuu utawaona) wengine wakamudu kununua pampu za kuendesha kama baiskeli wakasonga mbele hadi wanatumia mashine za mafuta.

Mnasubiri umwagiliaji kwa miundombinu ya serikali.Ni sawa na hapa jiulize ukiacha mahali ulipong'ang'ania kuishi umewahi kutafuta eneo lenye mifereji iliyotengezwa tayari ukaikosa nchi nzima? Je iliyopo imetumika inavyopaswa? Au mpka usukumwe? Njaa itatusukuma.

Niliwashauri wenye nia ya dhati ya kuepuka kilimo cha mvua tu watafute Kenya Mashariki Wakamba wamefanya nini.Yapo maeneo Ukambani mvua inanyesha siku 14 tu kwa mwaka njaa wameisahau.Hawakusubiri wahisani wala Serikali.Kilichowapa maarifa ni njaa.Mkamba mmoja tu alijiuliza tumesaidiwa miaka Zaidi ya 50 njaa haiishi,je tuendelee kusubiri misaada milele? Jibu lake likawa hapana tuiondoe njaa wenyewe akawahamasisha ndugu zake na kuwahimiza namna ya kufanya.

Hawakumkubali kirahisi,matokeo ya waliokubali yaliwashawishi waliokataa.Unaposubiri kitu cha kufanya njaa haisubiri.
Unaongea mashudu na wewe! Population ya peasants yote ihamie kwenye maeneo yenye maji? Uko sawia kichwani? Umefikiria kuhusu capacity ya hayo maeneo kuwa accommodate hao wakulima wote? Umetathimini athari za kimazingira zitakazojitokeza baada ya hapo? Na baada ya hizo athari kinafuata Nini? Miundombinu SII barabara tu na ndege, kwa wenye maono, kiongozi mzuri Ni Yule anaefikiri kuhusu Uhai wa Watu Wake na hivyo kuweka mazingira yatakayofanikisha maono hayo! Nyerere alikuwa mkweli haswa, hajawahi kuwa na maneno ya Shombo, alitafuta suluhisho kwa wananchi wake, aliifahamu vizuri nchi yake na aliwafahamu vizuri wananchi wake! Hakusubiri kupewa taarifa za kumpotosha, Wala za kumchonganisha na wananchi wake! Itoshe tu kusema, huyo anaedai anasema ukweli, Ni Muongo kwa kuwa anasema uongo!
 
Tupige porojo hapa mtandaoni, lakini njaa ya hatari ipo. Njombe debe la mahindi halijawahi fika Tsh 16,000/. Uliza sasa hivi ni sh ngapi. Sembe Njombe imefikia Tsh 30,000/ kilo 25. Hatujawahi fika huku. Njombe mvua imeanza January hii kunyesha kwa zamu/mgao, miaka ya nyuma January wakulima huwa wanapalilia na February kiazi kinatoka.

Morogoro mvua haijanyesha kwa wakati, Iringa kadharika, Mby kule bonde la Usangu ni kilio. Waulize wafugaji wa Chalinze wakwambie mifugo ilivyokufa kwa kukosa maji. Kuna watu walijiandaa kulima vizuri, mvua haijaja.

Nije kwenye suala la maji; kuna watu wana kesi ya kuharibu pump kule Manyara, kuna watu vitunguu vyao eka 200 zimekauka baada ya pump zao kuchukuliwa ili wasitumie maji kule Moshi. Sheria ya maji ni ngumu kwa wakulima wadogo maana hawana uwezo wa kuchimba visima virefu.
 
Watu wafanye kazi mkuu, hivi unadhani hata serikali ikiamua kutoa misaada ya chakula kila kaya inapata kiasi gani? Hakitazidi debe tano, sasa hizo debe tano zikiisha wanaenda wapi?
Watanzania kwa bahati mbaya tulizoea vibaya sana akili za utegemezi na kulaumu laumu kila kitu.
Magufuli kaza Uzi tu, next time watu watalima chakula kitaozea kwenye maghala
Mnataka watu wafanye kazi gani?kwani hawajalima?.
8b4bdfa98b02389a7ade559ac85648e4.jpg
 
Subiri baba yako akujengee '''''
Ndio maana mnaambiwa mnaongoza nchi kinyume na maumbile! Nini sababu ya nyie kuwa Serikali? Mbona hayo majibu hamkuyatoa kwa wasafiri WA ndege? Au baba yao ndo aliwanunulia hizo Pangaboi? Ustawi WA nchi na wananchi haukuzwi kwa UBAGUZI na kejeli za wenye shibe kwa wenye njaa!
 
Tanzania kuna njaa kweli kweli. Huo ndio ukweli. Bora tuseme ukweli ili tupone, kuliko kuficha aibu huku tukiangamia.

Achana na porojo za yule 'Mfalme' asiyependa kuusikia ukweli unaomuumbua.

Kwa sasa kila kona ya nchi kuna malalamiko ya UKAME na kukosa mvua! Magufuli amepita Kagera,Mwanza,Shinyanga,Simiyu, Bariadi kote kumekauka! Sasa Rais mzima na akili zake anapokomaa kuwa hakuna njaa anamdanganya nani kama siyo kujidanganya???
Magufuli anataka wafe watu wangapi kwa njaa ndo aamini kuna njaa Tanzania???? Anaposema watu wafanye kazi tu ili wasife na njaa anamaanisha nini? Hivi kama HAKUNA MVUA HATA UKIFANYA KAZI YA KULIMA UTAKOJOLEA HAYO MAZAO ILI YASTAWI? Lakini pia hata kama mvua zitaanza kunyesha leo, ni zao gani utapanda/lima leo halafu kesho uvune kwa chakula?Kuna muda wa kupanda,kuotesha,palizi,kukomaa, kuvuna na kueeka ghalani tayari kwa chakula. Hii ni process inayochukua miezi kadhaa say 3-6 months!
This president is a problem to Tanzania! Year 2020 is not far,let Tanzanians judge him accordingly!
 
Pamoja na yote uliyoyaandika kuhusu uvivu wa watanzania nk. lakini bado hauwezi kuondoa Ukweli huu, Tanzania kuna njaa, na watanzania wengi wanataabika kwa njaa, na wengi wanaangamia.
Juhudi la haraka za makusudi zinahitajika kufanyika sasa ili kuwanusuru.
Serikali kamwe haipaswi kulikwepa jukumu hili. Tanzania ni mali ya watanzania wote.

Kama kuna Pesa za kununua ndege kadhaa ambazo zaidi ya Asilimia 99 ya watanzania hawata weza kuzipanda maishani mwao, kwanini kukosekane pesa za kununulilia chakula ili kuwanusuru mamilioni ya watanzania waliopo katika hatari ya kuangamia?
Endapo Serikali itakua ikitoa chakula kila linapokuja baa la njaa Wananchi watabweteka anachotaka Rais ni kila mmoja atafute njia ya kukabiliana na janga hili linalokuja "Hii ndio Tanzania mpya inayojengwa"
 
Back
Top Bottom