Ni adhabu Gani uliyowahi kupewa ukiwa shuleni mpaka ukatamani upigwe yaishe

Ni adhabu Gani uliyowahi kupewa ukiwa shuleni mpaka ukatamani upigwe yaishe

Godoro la kioo

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2025
Posts
364
Reaction score
727
Wakuu kama kichwa kinavyojieleza

Naomba leo tujikumbushe kidogo adhabu tulizowahi kupewa mpaka ukatamani Bora akuchape tu yaishe

1) Binafsi nakumbuka kipindi tukiwa shuleni siku Moja tulichelewa kufika

Basi siku hiyo ilikuwa zamu ya mwalimu mmoja hivi

Yule mwalimu akatuambia Mimi sitoweza kuwapiga Cha kufanya chukueni hii ndoo

Akatupatia ndoo ya Lita ishirini, Kisha akasema, pangeni mstari mmoja akae kule bombani (Bomba la maji) na mwingine akae huku mwisho karibu na ndoo

Sasa zoezi lililokuwepo ni unakinga maji kwa mikono yote miwili Kisha unampatia mwenzako na yeye anampatia mwenzake yeye Tena anampatia mwenzake hivyo hivyo mpaka ndoo ijae

Changamoto iliyokuwepo ni kwamba unakinga maji kitendo Cha kumpatia mwenzako tayar mengine yamemwagika yamebakia machache

Nakumbuka hiyo siku wengi tulilia mpaka mwalimu akaja kutusamehe


2) Nilipewa swali nikakosea jibu basi yule mwalimu alivyokuwa katili akaniambia weka miguu juu kichwa chini halafu pale chini akaweka jiwe Ili kama nikichoka na nikadondoka basi kichwa kidondokee lile jiwe sitosahau


3)Nilipitiwa na usingizi wakati wa kipindi baada ya kuniona akaniita akaniambia chukua ndoo hii hapa

Zoezi lililopo hapo ni unaenda unachota maji unakunywa halafu unatoka unakimbia Yale maji unayatemea kwenye ndoo

Changamoto ni kwamba ndoo ilikuwa mbali kiasi kwamba ukija kuifikia Ile ndoo tayari Yale maji umeshayameza
Inabidi urudi Tena. Siyo Siri nilitamani kulia


Ila shule basi tu
 
Tulipewa adhabu tukiwa wanafunzi watatu kufyeka kiwanja cha mpira nyasi zote ziwe sawa,kisha tukate miti tuchimbie kuzunguka kiwanja kizima iwe kama mabenchi! Mbona tulijuta?
 
Mkuu, mlifanyiwa kitendo cha kinyama sana.

Huenda hayo ungefanyiwa sasa; tunavyoongea hapa sasa hiv, wewe mochwari, mwalimu nyuma ya nondo.
 
Mm niliambiwa nichague adhabu, nikaleta vikombe idadi sawa na waalimu, nikaanza kumwagia bao kwenye kila kikombe, nilivyofika kikombe cha 45 nikafukuzwa shule sasa hv mm ni saidia fundi huku nabeba zege
 
kuchuchumaa kisha unapitisha mikono chini ya mapaja halafu unashika masikio na kuanza kunesanesa....dah ukitoka hapo kutembea ni shida
imagine mabinti na makalio yao makubwa wabinuke ? Si ni trela tosha? Bahati nzuri mimi nimesoma memkwa adhabu za kipuuzi hatukuwahi kupewa
 
Wakuu kama kichwa kinavyojieleza

Naomba leo tujikumbushe kidogo adhabu tulizowahi kupewa mpaka ukatamani Bora akuchape tu yaishe

1) Binafsi nakumbuka kipindi tukiwa shuleni siku Moja tulichelewa kufika

Basi siku hiyo ilikuwa zamu ya mwalimu mmoja hivi

Yule mwalimu akatuambia Mimi sitoweza kuwapiga Cha kufanya chukueni hii ndoo

Akatupatia ndoo ya Lita ishirini, Kisha akasema, pangeni mstari mmoja akae kule bombani (Bomba la maji) na mwingine akae huku mwisho karibu na ndoo

Sasa zoezi lililokuwepo ni unakinga maji kwa mikono yote miwili Kisha unampatia mwenzako na yeye anampatia mwenzake yeye Tena anampatia mwenzake hivyo hivyo mpaka ndoo ijae

Changamoto iliyokuwepo ni kwamba unakinga maji kitendo Cha kumpatia mwenzako tayar mengine yamemwagika yamebakia machache

Nakumbuka hiyo siku wengi tulilia mpaka mwalimu akaja kutusamehe


2) Nilipewa swali nikakosea jibu basi yule mwalimu alivyokuwa katili akaniambia weka miguu juu kichwa chini halafu pale chini akaweka jiwe Ili kama nikichoka na nikadondoka basi kichwa kidondokee lile jiwe sitosahau


3)Nilipitiwa na usingizi wakati wa kipindi baada ya kuniona akaniita akaniambia chukua ndoo hii hapa

Zoezi lililopo hapo ni unaenda unachota maji unakunywa halafu unatoka unakimbia Yale maji unayatemea kwenye ndoo

Changamoto ni kwamba ndoo ilikuwa mbali kiasi kwamba ukija kuifikia Ile ndoo tayari Yale maji umeshayameza
Inabidi urudi Tena. Siyo Siri nilitamani kulia


Ila shule basi tu
Una uhakika ni shule? Sio JKT,
 
Kulima heka moja kwa kutumia vidole, kung'oa nyasi zisizohitajika eneo kubwa kuzunga library, kung'oa kisiki kikongwe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom