Nguzo ya Taifa Stars inashikiliwa na safu ya ulinzi ya Yanga

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,129
7,898
Tukiweka ushabiki pembeni, safu ya ulinzi ya Yanga imethibitisha kwa misimu miwili sasa kuwa ni safu ngumu sana kupitika si tu katika mashindano ya ndani ila hata ya kimataifa. Kuna jinsi hawa vijana wanajua kuwajibishana ndani na nje ya uwanja kiasi kwamba kila mmoja wao anahakikisha hazembei na makosa hayatokei mbele yake.

Safu ya kiungo ya Stars bado ina shida kubwa na ushambuliaji ndiyo tatizo ni kubwa zaidi. Shida kubwa ni wale tunaowategemea ni "maji ya jioni" halafu hakuna mbadala kabisa nje, ni kama tulisahau kabisa kwa kipindi cha miaka 5 kuandaa washambuliaji wapya. Hivi Samatta mara ya mwisho kufunga goli kwa Taifa Stars ni lini?

Tunapokwenda kupambana na Morocco hivi leo, tegemeo letu kubwa ni safu ya ulinzi, kule mbele hakuleti matumaini kabisa yaani. Baada ya mechi ya leo, Kocha afikirie kuongeza wachezaji kama Chilunda ili hao kina Samatta wasijione bila wao mambo hayaendi.

Feisal akiwa kwenye ubora wake, anaenda kuwa na gemu nzuri sana.
 
Kwa mpira ule tuliocheza juzi labda team ibadilike tunaacha nafasi kubwa sana tukiwa hatuna mpira team haina muunganiko na Morocco ni wazuri kwa kutumia open space walifanya kwa Spain wakafanya kwa Portugal and they're dangerous on set pieces.
 
Tukiweka ushabiki pembeni, safu ya ulinzi ya Yanga imethibitisha kwa misimu miwili sasa kuwa ni safu ngumu sana kupitika si tu katika mashindano ya ndani ila hata ya kimataifa. Kuna jinsi hawa vijana wanajua kuwajibishana ndani na nje ya uwanja kiasi kwamba kila mmoja wao anahakikisha azembei na makosa hayatokei mbele yake.

Safu ya kiungo ya Stars bado ina shida kubwa na ushambuliaji ndiyo tatizo ni kubwa zaidi. Shida kubwa ni wale tunaowategemea ni "maji ya jioni" halafu hakuna mbadala kabisa nje, ni kama tulisahau kabisa kwa kipindi cha miaka 5 kuandaa washambuliaji wapya. Hivi Samatta mara ya mwisho kufunga goli kwa Taifa Stars ni lini?

Tunapokwenda kupambana na Morocco hivi leo, tegemeo letu kubwa ni safu ya ulinzi, kule mbele hakuleti matumaini kabisa yaani. Baada ya mechi ya leo, Kocha afikirie kuongeza wachezaji kama Chilunda ili hao kina Samatta wasijione bila wao mambo hayaendi.

Feisal akiwa kwenye ubora wake, anaenda kuwa na gemu nzuri sana.
Kama kuna mchezaji najiuliza Kwa nini kaachwa ni Chilunda. Hata kama Hana game time kubwa lakini Kwa Wachezaji wa ndani bado ni back up nzuri Kwa hao Wenye timu.
 
Kama kuna mchezaji najiuliza Kwa nini kaachwa ni Chilunda. Hata kama Hana game time kubwa lakini Kwa Wachezaji wa ndani bado ni back up nzuri Kwa hao Wenye timu.
Kama kocha anaweza kuokoteza na kuwajaribu wachezaji wanaocheza madaraja ya chini huko nje sioni kwa nini ashindwe kuwajaribu hawa kina Chilunda wa Simba na Yanga ambao hawapewi nafasi ndani ya vilabu vyetu hivi vya Kariakoo kwa sababu ya ushindani wa wachezaji wa nje na sababu zingine.
 
Kwa mpira ule tuliocheza juzi labda team ibadilike tunaacha nafasi kubwa sana tukiwa hatuna mpira team haina muunganiko na Morocco ni wazuri kwa kutumia open space walifanya kwa Spain wakafanya kwa Portugal and they're dangerous on set pieces.

Uko sahihi.....ila hawa Morocco ni hatari sana

Kazi tunayo leo..acha watufundishe mpira .....Pira Biriani ya kiarabu....Pira mandi
Kama kwa Wydad Simba iliweza kwenda nao sambamba kwa pira objective, sioni kwa nini tushindwe tukiamua kukaza. Baada ya kuondoa hofu nao, hawa waarabu wa Kaskazini wameshakuwa level yetu. Morocco walikuwa wanapaki basi kule Qatar ndiyo kilichowabeba ila hawatishi kihivyooo.

Middle yetu ikikaza, sina wasiwasi sana na defense yetu ikitulia.
 
Tukiweka ushabiki pembeni, safu ya ulinzi ya Yanga imethibitisha kwa misimu miwili sasa kuwa ni safu ngumu sana kupitika si tu katika mashindano ya ndani ila hata ya kimataifa. Kuna jinsi hawa vijana wanajua kuwajibishana ndani na nje ya uwanja kiasi kwamba kila mmoja wao anahakikisha azembei na makosa hayatokei mbele yake.

Safu ya kiungo ya Stars bado ina shida kubwa na ushambuliaji ndiyo tatizo ni kubwa zaidi. Shida kubwa ni wale tunaowategemea ni "maji ya jioni" halafu hakuna mbadala kabisa nje, ni kama tulisahau kabisa kwa kipindi cha miaka 5 kuandaa washambuliaji wapya. Hivi Samatta mara ya mwisho kufunga goli kwa Taifa Stars ni lini?

Tunapokwenda kupambana na Morocco hivi leo, tegemeo letu kubwa ni safu ya ulinzi, kule mbele hakuleti matumaini kabisa yaani. Baada ya mechi ya leo, Kocha afikirie kuongeza wachezaji kama Chilunda ili hao kina Samatta wasijione bila wao mambo hayaendi.

Feisal akiwa kwenye ubora wake, anaenda kuwa na gemu nzuri sana.
Sawa na hiyo safu yenu ya ulinzi lolote baya litukutute tufedheeke tu na mabango tutabandika Jangwani na Lumbumba🤣🤣🤣
 
Safu ya yanga hujaitaja hapo. Nimeona samata, chilunda na feisal. Safu ya ulinzi ya yanga ni ipi?
Mwamnyeto, Bacca, Job. Naweza kumuongeza Kibabage siyo sana kwa sababu ya ubora lakini kwa sababu anaweza kuwajibishwa na wenzake.

Nilichogundua ukiangalia vipaji vya wachezaji wa ulinzi wa Yanga mmoja mmoja siyo vya kutisha sana ila wakicheza pamoja wanawajibishana na ile rotation yao inafanya kila mmoja asifanye usng
 
Sawa na hiyo safu yenu ya ulinzi lolote baya litukutute tufedheeke tu na mabango tutabandika Jangwani na Lumbumba🤣🤣🤣
Sipo tena kwenye huo usimba na uyanga. Kupeana tu presha na kuumizana mioyo bila sababu
 
Kama kocha anaweza kuokoteza na kuwajaribu wachezaji wanaocheza madaraja ya chini huko nje sioni kwa nini ashindwe kuwajaribu hawa kina Chilunda wa Simba na Yanga ambao hawapewi nafasi ndani ya vilabu vyetu hivi vya Kariakoo kwa sababu ya ushindani wa wachezaji wa nje na sababu zingine.
Uko sahihi Sana Mkuu. Kama vilabu vimeshindwa kuisaidia timu ya Taifa kutengeneza Wachezaji wa nchi basi kocha wa Taifa aifanye mwenyewe. Kwani amemuona wapi Msheri Hadi amemuamini mbele ya Makaka wa Mtibwa?
 
Uko sahihi Sana Mkuu. Kama vilabu vimeshindwa kuisaidia timu ya Taifa kutengeneza Wachezaji wa nchi basi kocha wa Taifa aifanye mwenyewe. Kwani amemuona wapi Msheri Hadi amemuamini mbele ya Makaka wa Mtibwa?
Ni kweli kabisa. Ni kama alivyomuita Mwenda kwenye ile trip ya Saudi Arabia, aendelee kuwaita tu akiona wanafaa awatumie bila kujali kama kwenye vilabu vyao wanasugua benchi. Anaweza kupata timu ya wachezaji wasio na majina ila ambao bado wana njaa ya mafanikio.
 
Tukiweka ushabiki pembeni, safu ya ulinzi ya Yanga imethibitisha kwa misimu miwili sasa kuwa ni safu ngumu sana kupitika si tu katika mashindano ya ndani ila hata ya kimataifa. Kuna jinsi hawa vijana wanajua kuwajibishana ndani na nje ya uwanja kiasi kwamba kila mmoja wao anahakikisha azembei na makosa hayatokei mbele yake.

Safu ya kiungo ya Stars bado ina shida kubwa na ushambuliaji ndiyo tatizo ni kubwa zaidi. Shida kubwa ni wale tunaowategemea ni "maji ya jioni" halafu hakuna mbadala kabisa nje, ni kama tulisahau kabisa kwa kipindi cha miaka 5 kuandaa washambuliaji wapya. Hivi Samatta mara ya mwisho kufunga goli kwa Taifa Stars ni lini?

Tunapokwenda kupambana na Morocco hivi leo, tegemeo letu kubwa ni safu ya ulinzi, kule mbele hakuleti matumaini kabisa yaani. Baada ya mechi ya leo, Kocha afikirie kuongeza wachezaji kama Chilunda ili hao kina Samatta wasijione bila wao mambo hayaendi.

Feisal akiwa kwenye ubora wake, anaenda kuwa na gemu nzuri sana.
Chilunda umemuona lini akifunga?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom