Ngoma za mashetani

Ngoma za mashetani

Unajua wewe ni ngumi mkononi sister

Yaani hapo unataka kulianzisha. Haya basi mimi nimemsamehe, usianze kuzikusanya hasira sasa😀😀😀
bwana shemeji umeniwahi kuuliza hili swali

kwanza, samahani bwana kwa kutokupa taarifa ila nilichokuahidi ndicho nilichotekeleza

heshima yako bwana shemeji, habari za wikiend?
 
Hiyo inaitwa chano. Inakua na vitu vitamu kama miwa, asali, ndizi kusukari, halua, mkate wa kumimina na vitu kama juice ambavyo huwekwa kwenye sinia

Wanasema hicho ni chakula cha hao mashetani ambao huja kupitia miili ya binadamu na kuja kula hivo vitu. Katika baadhi ya makabila na koo jambo hili linafanyika kila mwaka na wanapiga na hizo ngoma za kuwaalika hao viumbe

Inasemekana kua hiyo ni aina ya matambiko kama matambiko mengine yanayofanywa kwa aina tofauti kwenye makabila mengi hapa nchini au Afrika kwa ujumla

Kuna wakati Tanga zinapopigwa hizi ngoma huwa wanatembea barabarani mchana kweupe, wanaume wakiwa vifua wazi na wanawake manyonyo nje!

Wanaoshiriki mambo haya wanadai inawafanya wakae vizuri katika maisha yao kwa mwaka mzima. Yaani ni matambiko ya kuondoa mikosi ya kuumwa, kuharibikiwa na mambo ya kazi au biashara, kuvurugikiwa na mahusiano ya kifamilia kama vile ndoa n.k

Jambo la kushangaza kama nilivosema awali ni kwamba hata waliowasomi na wenye exposure kubwa kwenye hizo koo ikiwemo waliowahi kuishi Ulaya na Amerika wanaamini na kushiriki hayo mambo!
Huku ni kudanganyana na imani potofu. Nilipokuwa mdogo zilikuwa zinapigwa ngoma hizi na walikuwa wanatengeneza hicho chano na kupeleka porini kwenye njia ya panda ili hao mashetani waje wale.
Mimi na wenzangu tulikuwa tunasubiri waondoke na kula vyakula vyote vitamu vilivyowekwa na hatujadhurika.
Siku hizi kwa ukali wa maisha ngoma hizi zimepungua sana almost hazipo.
 
Huku ni kudanganyana na imani potofu. Nilipokuwa mdogo zilikuwa zinapigwa ngoma hizi na walikuwa wanatengeneza hicho chano na kupeleka porini kwenye njia ya panda ili hao mashetani waje wale.
Mimi na wenzangu tulikuwa tunasubiri waondoke na kula vyakula vyote vitamu vilivyowekwa na hatujadhurika.
Siku hizi kwa ukali wa maisha ngoma hizi zimepungua sana almost hazipo.
Dah mkuu! Mlikua mnajipigia ile mikate ya kumimina na tende na halua😀😀😀

Yaani kisha hamkudhurika wala nini, badala yake mlijiongezea afya tu😀😀😀
 
Kuwa msomi hakukuzuii kuamini unachoamini
Halafu hivi usomi mnaumaanishaje nyinyi vichwani kwenu hasa?
Utaskia ooh yule kaka ulaya,kasoma ana madegree bla bla blaaaah
Kwahiyo matambiko ndo yanawapima akili na usomi wao? au kuishi ulaya ndio ustaarabu? mbona wao wana maparade yao na mavitu ya ajabu ajabu tu huko kwao mnakoona ndo pameendelea

wasomi hawarogi? hawatambiki?
Acheni hizo bwana kila mtu anaamini anachoamini na haimzuii kuitwa au kuwa mstaarabu
 
Tena hiyo ni israfu, huwez weka chakula hivo kuna watu chungu nzima slice ya mkate wanaitafta nimewahi baatika nazi kuzikuta, nyembe nywele, miwa, mtama, mikaa chungu sjabahatika mkate
Dah mkuu! Mlikua mnajipigia ile mikate ya kumimina na tende na halua😀😀😀

Yaani kisha hamkudhurika wala nini, badala yake mlijiongezea afya tu😀😀😀
 
Back
Top Bottom