Nenda Lugola, Bodaboda watakukumbuka

Nenda Lugola, Bodaboda watakukumbuka

Full 8

JF-Expert Member
Joined
Nov 11, 2010
Posts
313
Reaction score
272
Duniani kila kitu kina pande mbili, wema na ubaya, mbele na nyuma bila kusahau juu na chini.

Siko hapa kuongelea mabaya ya Kangi Lugola maana atayaongelea mwingine. Mimi naongelea jambo moja tu ambalo ni miongoni mwa mazuri mengi aliyoyafanya katika kipindi kifupi cha uongozi wake.

Bodaboda wasinyanyaswe, bodaboda kama haijahusika kwenye jinai isikae kituoni n.k.

Ni wazi kuwa katika kipindi cha Kangi, bodboda wamepata nafuu sana. Uonevu wa kukamatwa na askari wa barabarani ulipungua sana.

Pia, bodaboda walifanya kazi zao kwa uhuru mkubwa n kupata faida mara kutokana na kutotoa rushwa na faini za kubambikiwa kwa askari wa barabarani.

Lakini pia bodaboda waliweza kufanya kazi kwa uhuru na amani kwani walisajiliwa, wakapewa mafunzo na leseni za udereva. Mafunzo haya yamechangia kwa kiasi fulani kupunguza ajali barabarani.

Naimani waziri ajaye atafanikisha pendekezo la wadau la kuwa na faini tofauti kati ya dereva wa gari na bodaboda hasa ukizingatia vipato havilingani na zaidi lengo la adhabu ni kufunza. Hivyo, kuhekimisha madereva wa bodaboda kutasaidia sana kupunguza ajali kuliko kuwaadhibu kwa faini kubwa.

Ni hayo tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila wakuu tukitafakari vyema hivi kweli mpk hawa wakuu kwenda kusaini huo mkataba wa takribani 1t ikulu isijue kweli kwanza waliendaje bila kibali maana tuliambiwa hakuna mtumishi kwenda nje bila kibali cha ikulu

Nadhani hapa tumelishwa taarifa mbaya ili tuwaone hawa wakuu hawafai na kwa kuwa wana kiapo hawawezi kusema
 
Ila wakuu tukitafakari vyema hivi kweli mpk hawa wakuu kwenda kusaini huo mkataba wa takribani 1t ikulu isijue kweli kwanza waliendaje bila kibali maana tuliambiwa hakuna mtumishi kwenda nje bila kibali cha ikulu

Nadhani hapa tumelishwa taarifa mbaya ili tuwaone hawa wakuu hawafai na kwa kuwa wana kiapo hawawezi kusema

Tujaribu kulitafakari hili kwa kina naona kama kuna mchele mchele hapa.

Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Ila wakuu tukitafakari vyema hivi kweli mpk hawa wakuu kwenda kusaini huo mkataba wa takribani 1t ikulu isijue kweli kwanza waliendaje bila kibali maana tuliambiwa hakuna mtumishi kwenda nje bila kibali cha ikulu

Nadhani hapa tumelishwa taarifa mbaya ili tuwaone hawa wakuu hawafai na kwa kuwa wana kiapo hawawezi kusema
Kuna jambo bado lipo GIzan.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nliiandika humu.wee Lugora achana kunyanyasa walokole mitume na manabii akajitia mjuaji na hajali Kiko wapi aende zake huko na amwambie Sophia Mjema mkuu wa wilaya ya Ilala anayejifanya babe pamoja na kuonywa .Ajiandae na ujuaji wake wa kuegemea kwa Lugora Ajiandae
 
Back
Top Bottom