Ndugulile: Magufuli hajui sheria, anakurupuka tu...

Nani kasema Mnyika haungwi mkono na wabunge wa CCM katika suala la uthibiti wa bei?
 
hakika wabunge wa dar mmeonesha uzalendo kwa kuweka vyama venu pembeni na kupigania watanzania wote.hongereni sana

Katika matukio yote yaliyotokea wameona hili ndio la kuonyesha uzalendo?
Naomba unikumbushe walichukua hatua gani wakati wa mafuriko
na bei ya umeme tumesikia itapanda sijui wametoa tamko gani?
 
[h=6]Majuuzi mafuriko ya Dsm mko kimya, Mahosipitalini mfano Muhimbili,Mwananyamala, Amana na TMK huduma haziko sawa, mko kimya.... Hizi gharama za maisha zinavoenda juu namna hii mmeona kivuko tu? Nauli za daladala, mabasi ya mikoani na hapo mmekaa kimya tuuu... Mi na hofu na chanzo cha huu msukumo na huu umoja wa ghafla[/h]
 
Baada ya kuzomewa Kigamboni, Dk Magufuli alifanya mkutano na waandishi wa habari na kusisitiza kwamba, “Kuanzia Januari, Mosi, mwaka huu Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa), imeongeza viwango vya nauli katika vivuko vyote vya Serikali nchini.”

Alisema kwa muda wa miaka 14 iliyopita Kivuko cha Kigamboni kimekuwa kikitoza nauli ya Sh100 kwa mtu mmoja, wakati vivuko vingine vyote nchini, vimepandisha nauli zaidi ya mara mbili tangu mwaka 1997 kuendana na gharama za uendeshaji.

“'Kwa mfano, Kivuko cha Pangani ambako umbali wa uvushaji hauzidi ule wa Magogoni kilikuwa kinatoza Sh 200 na hali ya uchumi kwa wananchi ni ya chini kuliko Dar es Salaam. Kivuko cha Kilombero kilikuwa kikitoza Sh200 ikilinganishwa na Sh100 zilizokuwa zikitozwa hapa Magogoni.”

Dk Magufuli alitaja sababu zilizochangia kupandisha nauli hizo kwamba ni pamoja na ongezeko la mishahara ya watumishi serikalini kwa zaidi ya asilimia 100, ongezeko alilosema la zaidi ya asilimia 400 la bei ya mafuta ya dizeli na mafuta ya kulainishia mitambo ambayo hutumika kuendeshea vivuko hivyo.

Alitaja sababu nyingine kwamba ni pamoja na: “Ongezeko la bei za vipuri na kodi zake linalowiana na kushuka kwa thamani ya shilingi na ongezeko la bei kwa jumla.”

Alisema upandishaji wa nauli hizo ulifanywa kwa kuzingatia taratibu za kisheria na hatimaye kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali toleo Na. 367 la Novemba 4, mwaka jana kwa mujibu wa sheria za uendeshaji wa vivuko vya Serikali.

“Sura 173 Kifungu cha 11(b), mwenye mamlaka ya kupanga nauli za vivuko vya Serikali ni Waziri mwenye dhamana na vivuko vya Serikali. Hata hivyo, kabla ya kufikia uamuzi huu, kumekuwa na jitihada za aina mbalimbali katika kuimarisha mapato ya vivuko. Machi, 2009, Wakala wa Ufundi na Umeme wakishirikiana na
Jeshi la Polisi pamoja na Askari kutoka Kikosi cha Wanamaji waliendesha zoezi la kudhibiti mapato ya Kivuko.”

Alisema hilo liliwahi kufanywa na na Kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart mnamo Aprili 17 hadi 20, mwaka jana kwa makubaliano na Temesa. “Zoezi hilo liliendeshwa tena Septemba 16 hadi 20, 2010 na
Wizara kwa ushirikiano na Jeshi la Polisi.”

Alisema Julai, 2011, Temesa iliamua kubadili wakata tiketi na kuajiri wengine akisisitiza kuwa Serikali imechukua hatua mbalimbali kupambana na matukio ya watumishi wasio waaminifu. Hatua nyingine ni ile ya Temesa kuondoa askari wa kuajiriwa na badala yake kuingia mikataba na kampuni za ulinzi.

“Kwa sasa katika Kivuko cha Magogoni, Kampuni ya ulinzi ya Suma JKT ndiyo inayotumika kufanya kazi hiyo,” alisema.

Alisema juhudi hizo zimesaidia kuongeza mapato kwa siku kutoka Sh5.5 milioni mwaka 2009 hadi Sh9 milioni kwa sasa katika Kivuko cha Magogoni na kusisitiza kwamba wizara itaendeleza hatua hizi kwa lengo la kubana uvujaji wa mapato na matumizi yasiyo ya lazima kwa vivuko vyote.

Magufuli alisema kwa utaratibu, watumiaji wote wa huduma za vivuko wanatakiwa walipie huduma hiyo na kuongeza: “Tunaomba utaratibu huu uzingatiwe isipokuwa kwa wanafunzi waliovaa sare za shule. Tunasisitiza watumiaji wa vivuko waheshimu sheria na taratibu zote za vivuko kwa ajili ya usalama wao na ufanisi wa huduma.”
 
Naomba mwenye uelewa na haya mambo atusaidie, Energy and Water Utilities Regulatory Authority inaingiaje hapa? Au ile WATER inamaanisha na boti, vivuko, kambale nk.
Nadhani mkuu utakuwa umechanganya na Surface and Marine Transport Regulatory Authority (SUMATRA) Ambayo ndo inahusika na hayo mambo
 
Majuuzi mafuriko ya Dsm mko kimya, Mahosipitalini mfano Muhimbili,Mwananyamala, Amana na TMK huduma haziko sawa, mko kimya.... Hizi gharama za maisha zinavoenda juu namna hii mmeona kivuko tu? Nauli za daladala, mabasi ya mikoani na hapo mmekaa kimya tuuu... Mi na hofu na chanzo cha huu msukumo na huu umoja wa ghafla


Hapo ni 2015 tu hakuna lingine.

Mbunge anayekaa kulia kwa sh 200 kuwa ni kubwa wakati kajipitishia 200,000 na bado anadai ni ndogo ni mnafiki.

Mbona dala dala imepanda mara kadhaa hawakusema.
 
TO THE CONTRARY, HAKIKA WAMEONESHA UHAINI KWA KUWEKA PEMBENI UKWELI WA UTAWALA BORA, HUKU WAKITAFUTA KUWAPLEASE MASKINI WA KIGAMBONI TEMPORARILY, WAMEJITENGA NA UKWELI MCHUNGU WA KIUCHUMI NA KUAMUA KUJITAFUTIA UMAARUFU RAHISI TOKA KWA WAPIGA KURA:shock: HAIWEZEKANI GHARAMA ZA MAISHA, USAFIRI NA USAFIRISHAJI ZIPANDE KILA MWAKA CONSISTENTLY KARIBU KILA ENEO LA NCHI HII ISIPOKUWA KWENYE KIVUKO CHA KIGAMBONI. VIVUKO MAENEO MENGI YA NCHI HII KWA MUDA MREFU SASA VINATOZA GHARAMA ZAIDI SHS MIA MBILI, KWA NINI KIGAMBONI IWE TOFAUTI, AU KUNA HIDDEN AGENDA KATIKA HILI NA MNAMFANYA MAGUFULI KAMA SCAPEGOAT, WE THE ENLIGHTENED TANGANYIKANS WILL NOT REST UNTIL YOU PROVIDE ALL THE FACTS ON THE TABLE CONCERNING THIS SAGA.

hakika wabunge wa dar mmeonesha uzalendo kwa kuweka vyama venu pembeni na kupigania watanzania wote.hongereni sana
 
Mtemvu suala la kujipandishia POSHO bungeni linatukera sisi wapigakura wako zaidi ya hili la kupandisha nauli ferry,kwa akilizenu nyie wabunge wa CCM hamna linalowafananisha na sisi wapiga kura wenu mbona mpaka leo hamajazungumzia Bei juu ya mchele,petrol nauli za mabasi ,daladala mbona kwanini msingemuuliza maghufuli pungufu ni kiasi gani ilii mtulipie toka kwenye posho zenu nasi tukapanada bure,nyie ni CCM,Maghufuri no CCM, Kivuko kililtetwa na serikali ya CCM,nanyi wakazi wenzangu wa kigamboni kwanini tusiandamane ili tujengewe Daraja badala ya kutumia kulilia sh 100.kwanza mie nashangaa kama kuna sehemu ndani ya nchi yetu watu bado wanatumia shs 100 kwa usafiri .Mtemvu kuna kitu kipo nyuma yenu na si gharama za ferry zilizotangazwa na Maghufuri.Mnyika waache hao wabunge wewe ni msomi tunaamini Maghufuri hajakurupuka.TUTAWASIDIA WABUNGE NA WANAKIGAMBONI MTAKAPO ANDAMANA KWA MAISHA YA KUWA MAGUMU SIO HILI LA MIA YA FERRY.
 
Kweli Wadaganyika hata uwezo wa kufikiri umepungua kwa kiasi kikubwa na kubaki kushabikia tu. Ndiyo maana hata wakati wa kampeni tunadanganyika kirahisi. Uzalendo wameshindwa kuonyesha kwenye hili tatizo kubwa kabisa la foleni Dar, watu wanalala saa nne na kuamka saa tisa kuwahi usafiri na humo kwenye daladala unakaa zaidi ya saa mbili hujafika ofisini, watu wenye magari yao wanaunguza shilingi ngapi kwenye hizi foleni?. Leo hii mtu anajitokeza kinafiki anaonekana anatetea raia. Amkeni WTz mtaendelea kuliwa na kupumbazwa kila mwaka.
 
Kwako ni ndogo lakini kwa wenzako ni kubwa sana. Fikiri mtu anayefanya shughuli zake K'koo na anakaa Tungi au Mjimwema. Tungi-Kigamboni,300/=; Pantoni-200/=; Kivukoni-K'koo 300/=. Jumla kwenda na kurudi ni 1600 per day. Assume ni siku moja kwa wiki havuki, kwa mwezi atatumia 41,600/=. Sasa hebu tia akili.
Watu wa kigamboni acheni kudekadeka nauli ya 200 ipo sahihi na kauli ya Magufuli ipo sahihi. Kama mnapinga ongezeko la nauli unganeni na wabunge wenu kupinga mfumuko wa bei ya chakula kama mchele, sukuri, unga na pia ongezeko la ada za shule etc sio kushupalia kitu kidogo kupiga mbizi
 
EWURA???
Mbunge amechemka big time...
Mbunge anajiumbua mwenyewe kwanini hatukumsikia akipinga ongezeko la Posho na marupurupu ya wabunge ache kutuzingua nauli ipo sawa asiweza apige mbizi mbona sisi wakazi wa mbezi mwisho tunalipa nauli ya daladala 1500 kila jioni na wabunge hawapingi shilingi mia mbili mbunge anatufa umaarufu wa kujulikana kwanza tulikuwa hatumfahamu aibue hoja zake binafsi na sio kudandia hoja za waziri mtendaji
 
Ni kweli kipo chini ya wizara yake lakini nafikiri SUMATRA ndio wanamamlaka ya kupanga bei wakishirikisha wadau. Suala linalomwandama Mgufuri hapa ni kauli ameshindwa kuwasilisha hoja yake kwa maskini lakini nauli kuwa 200 sifikirii kwamba ni tatizo kubwa. Hii inatufundisha viongozi wanatakiwa wachunge midomo yao kwani siku moja tu unaweza ukaharibu sifa zako zote

Hivi kwa nini watanzania tunapenda kuitwa masikini? Kigamboni kuna masikini gani pale? embe dodo karibu zote mjini zinatoka huko na bei ya moja usipime! Sh. 200/= tu? ifike wakati tuukatae umasikini bana!
 
Mombasa kenya kuna ferry nzuri sana na watu huvushwa bure miaka nenda rudi.Kenya ni nchi ya kibepari ambayo kwao kutafuta faida na pesa ni kitu kikubwa.Wao na ubepari wao na uroho wao wamewezaji kuvusha maelfu ya watu kwa ferry kila siku bila kuwatoza pesa? Siri yao ni nini wajuzi mtujuze kama hamjui nendeni mkajifunze Mombasa kwenye ferry zao mtuletee taarifa
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Mie niliamini ungetujuza siri ya wao kuvusha watu bure badala yake taarifa yako haijakamilika. Ungetusaidia zaidi au ungeikamilisha taarifa yako kwa kutoa sababu za Kenya kuvusha watu bure. Arguments zako zingewasaidia Wabunge wa Mkoa wa Dar kujustify kauli zao.
 
hiyo ni strategy ya kuwaondoa kigamboni ili bush aingie kilaini

Mi nadhani wabunge wa DSM hawana hoja. Meya aliwaambia wanafikiri kwa kutumia MA...:rant::ballchain:lio yao lakini hakuna aliyelalamika . Sasa hili la nauli limewasibu nini? Hawaoni hali halisi ya uendeshaji wa kivuko ni ngumu? Wamwacha Magufuri achape mzigo
 
Mombasa kenya kuna ferry nzuri sana na watu huvushwa bure miaka nenda rudi.Kenya ni nchi ya kibepari ambayo kwao kutafuta faida na pesa ni kitu kikubwa.Wao na ubepari wao na uroho wao wamewezaji kuvusha maelfu ya watu kwa ferry kila siku bila kuwatoza pesa? Siri yao ni nini wajuzi mtujuze kama hamjui nendeni mkajifunze Mombasa kwenye ferry zao mtuletee taarifa
Nimejiuliza hilo swali mara nyingi bila kupata majibu maana ferry Mombasa zina hali nzuri sana, usafiri ni bure na hata wafanyakazi wa ferry wanafanya kazi zao za kwa umakini mkubwa, sijui hapa bongo tatizo ni nini maana basi hata kama wameamua wananchi kuchangia huduma ingekuwa kidogo sana ili angalau kila mtu aweze kutumia.
 
Viongozi wa sasa wa Tanzania hawajawahi kujifunza jambo lenye manufaa kwa wananchi.

Ukisikia wanasema kuna kitu wamejifunza kwa wenzetu ujue wao wachache wananufaika.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Back
Top Bottom