Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 372,000
- 861,690
Ndugu Watanzania!
Usiku huu nimepokea ujumbe kutoka kwa mtu ambaye ni mmoja wa ndugu wa Mhe. Balozi Humphrey Polepole. Nimebadilisha initials au utambulisho wake kwa sababu za kiusalama. Suala la Polepole lina simanzi isiyoisha, hivyo hatuwezi kupuuzia minong'ono yoyote kuhusu wapi alipo.
Kwa kuwa hakuna mamlaka iliyowahi kusema kuwa inamshikilia, umma umebaki kukisia na kuokoteza taarifa ikiyumkini inaweza kutokea taarifa iliyobeba ukweli. Kwa sababu hiyo hiyo ni vigumu kwa askofu kwenda kumuulizia au kumtafuta Polepole katika mamlaka yoyote ile.
Hata hivyo, nauweka ujumbe huo hapa kwa ajili kuleta hamasa ya maombi ili kumuombea hata kumpazia sauti zaidi yumkini wanaomshikilia wanaweza kuzidiwa au kuogopa kelele nyingi.
Tukikata tamaa na kuacha kupiga kelele juu ya Balozi Humphrey Polepole hata wengine kama Dioniz Kipanya, Deusdedith Soka, Kaswahili, Chaula, Mbise, Mlay, nk tutarajie watu wengi zaidi kuendelea kutekwa na kupotezwa katika siku za kwenye kipanda uso.
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Itunge, Dar es Salaam; 5 Agosti 2026; Saa 7:35 usiku
UJUMBE KUTOKA NDUGU WA POLEPOLE!
Nakusalimu Baba Askofu Mwamakula!
Nisamehe nakuandikia usiku. Nimeona taarifa mtandaoni, ina viashiria kuna ukweli katika hili. Ikupendeze na iwe ni vyema kwako ninaomba uende Ukonga ili kusudi ukamuone Mhe. Balozi Humphrey Polepole, kwa maelekezo ya ujumbe wa mitandaoni kuwa Polepole yupo Ukonga!
Ni mimi K. L. P.,
Ndugu yake na Humphrey Polepole.
5 Septemba 2026
Usiku huu nimepokea ujumbe kutoka kwa mtu ambaye ni mmoja wa ndugu wa Mhe. Balozi Humphrey Polepole. Nimebadilisha initials au utambulisho wake kwa sababu za kiusalama. Suala la Polepole lina simanzi isiyoisha, hivyo hatuwezi kupuuzia minong'ono yoyote kuhusu wapi alipo.
Kwa kuwa hakuna mamlaka iliyowahi kusema kuwa inamshikilia, umma umebaki kukisia na kuokoteza taarifa ikiyumkini inaweza kutokea taarifa iliyobeba ukweli. Kwa sababu hiyo hiyo ni vigumu kwa askofu kwenda kumuulizia au kumtafuta Polepole katika mamlaka yoyote ile.
Hata hivyo, nauweka ujumbe huo hapa kwa ajili kuleta hamasa ya maombi ili kumuombea hata kumpazia sauti zaidi yumkini wanaomshikilia wanaweza kuzidiwa au kuogopa kelele nyingi.
Tukikata tamaa na kuacha kupiga kelele juu ya Balozi Humphrey Polepole hata wengine kama Dioniz Kipanya, Deusdedith Soka, Kaswahili, Chaula, Mbise, Mlay, nk tutarajie watu wengi zaidi kuendelea kutekwa na kupotezwa katika siku za kwenye kipanda uso.
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Itunge, Dar es Salaam; 5 Agosti 2026; Saa 7:35 usiku
UJUMBE KUTOKA NDUGU WA POLEPOLE!
Nakusalimu Baba Askofu Mwamakula!
Nisamehe nakuandikia usiku. Nimeona taarifa mtandaoni, ina viashiria kuna ukweli katika hili. Ikupendeze na iwe ni vyema kwako ninaomba uende Ukonga ili kusudi ukamuone Mhe. Balozi Humphrey Polepole, kwa maelekezo ya ujumbe wa mitandaoni kuwa Polepole yupo Ukonga!
Ni mimi K. L. P.,
Ndugu yake na Humphrey Polepole.
5 Septemba 2026