Ndugai amefuata utaratibu wa kujiuzulu Uspika kwa mujibu wa Katiba. Mbatia hayupo sahihi na kesi yake haina mashiko

Peter Madukwa

JF-Expert Member
Sep 20, 2012
3,135
2,471
Kumekuwa na mjadala kutoka baadhi ya watu mbalimbali mtandaoni juu ya kujiuzulu kwa aliyekuwa Spika Mh Job Ndugai.

Ulianza mjadala kwamba kwanini ktk barua yake ameandika herufi kubwa pekee? KIMSINGI kilichosambaa mtandaoni siyo barua bali ni TAARIFA KATIKA VYOMBO VYA HABARI ambayo ni sawasawa tu na TANGAZO. Katika uandishi TANGAZO/TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NI KAWAIDA SANA KUANDIKWA KWA HERUFI KUBWA PEKEE. Barua za kujiuzulu zimewasilishwa katika bunge na katika Chama cha Mapinduzi.

Jambo la Pili nimeona Ndg James Mbatia amesema anakusudia kupeleka kesi mahakamani kupinga utaratibu uliotumika ktk kujiuzulu kwa spika. Kwamba kwa maelezo ya Mbatia ni kiwa Spika alitakiwa aende bungeni kujiuzulu kupitia ktk kamati ya bunge na bunge lenyewe.

Kimsingi hoja yake siyo sahihi. Kwa maoni yangu Mh Spika amefuata utaratibu wa kikatiba na ametimiza matakwa ya kisheria katika mchakato wa kujiuzulu.

Ukisoma katiba ya JMT sura ya 11 ibara ya 149(1)(c) imeeleza wazi kuwa endapo Spika au Naibu spika anataka kujiuzulu anatakiwa kuwasilisha taarifa hiyo katika bunge. Katiba haijatoa masharti kuwa taarifa hiyo iwe ktk mkutano, kamati au kwa barua original au nakala ya barua? Katiba imetaka tu kuwa Spika atoe taarifa katika Bunge.

Mh Spika Job Ndugai katika kujiuzulu ametoa taarifa katika bunge na chama cha mapinduzi na kwamba KWA KUWA BUNGE LIMEKIRI KUPOKEA TAARIFA YA KUJIUZULU KWA SPIKA (KAMA TAARIFA YA KATIBU WA BUNGE INAVYOJIELEZA) Basi tuhitimishe kwa kusema Spika amewasilisha taarifa yake ktk bunge na amefuata taratibu za kisheria za kujiuzulu kwa spika.

Kwa lugha rahisi Spika amejiuzulu kisheria na uchaguzi wa Spika mwingine utafanyika mwezi Februari kama ilivyotangazwa na BUNGE katika taarifa yake ya vyombo vya Habari.

Screenshot_20220107-141947.jpg

BARUA RASMI YA KUJIUZULU KUTOKA KWA SPIKA KWENDA KWA KATIBU WA BUNGE AMBAPO NAKALA IMEELEKEZWA KWA KATIBU MKUU WA CCM.
Barua ya Ndugai_1.jpg

UPDATES: Tarehe 28.1.2022

Mahakama imetupilia mbali kesi ya kikatiba ya kupinga kujiuzulu kwa SPIKA.
 
Watu wanasema lile sio bunge la CCM ni bunge la wananchi sasa kwanini Ndugai amwandikie Chongolo.


Umeelewa au bado?

Kikubwa ni Bunge kupata taarifa ya kujiuzulu kwake.

Suala la kukitaarifu chama kilichomdhamini ni hiyari yake na wala siyo kosa na haiathiri ukweli kuwa bunge limepewa taarifa ya kujiuzulu kwa spika na bunge lenyewe limekiri
 
Nafasi ya U spika inahudumia Watanzania regardless tofauti zetu za kiitikadi,means hawezi akawa anawajibika katika system's za kichama ,speaker alitakiwa awasiliane na Bunge sio political party ndio maana halipwi na political party,tatizo ni KATIBA na mbaya zaidi ccm wamejimilikisha nchi yetu,yaani wanaiona ni sehemu ya Lumumba na wengineo wote ni wakimbizi,Tanzania it belongs to all of us na wote tunawajibika kwa ustawi wake.
 
Kwani Ndugai mwenyewe anasemaje? Au amekataa kujiuzulu kwake? Ngoja tusubiri siku ya kwanza ya kikao kama atavaa lile joho au atakaa kule kwa maamuma.
 
Nafasi ya U spika inahudumia Watanzania regardless tofauti zetu za kiitikadi,means hawezi akawa anawajibika katika system's za kichama ,speaker alitakiwa awasiliane na Bunge sio political party ndio maana halipwi na political party,tatizo ni KATIBA na mbaya zaidi ccm wamejimilikisha nchi yetu,yaani wanaiona ni sehemu ya Lumumba na wengineo wote ni wakimbizi,Tanzania it belongs to all of us na wote tunawajibika kwa ustawi wake.
Ungeongea kiswahili tu bado tungekuelewa
 
Nafasi ya U spika inahudumia Watanzania regardless tofauti zetu za kiitikadi,means hawezi akawa anawajibika katika system's za kichama ,speaker alitakiwa awasiliane na Bunge sio political party ndio maana halipwi na political party,tatizo ni KATIBA na mbaya zaidi ccm wamejimilikisha nchi yetu,yaani wanaiona ni sehemu ya Lumumba na wengineo wote ni wakimbizi,Tanzania it belongs to all of us na wote tunawajibika kwa ustawi wake.
Jambo la msingi ni bunge kupewa taarifa ya kujiuzulu kwa spika na bunge limesema limepata taarifa hiyo.
 
Angetolea hili suala lissu ufafanuzi nadhani ningeelewa vizuri. Maana naona kama masuala haya ya mabunge Ana utaalam nayo. Wengineo tunaongea tuu kwa kucopy visheria nusunusu.
 
Kikubwa ni Bunge kupata taarifa ya kujiuzulu kwake.

Suala la kukitaarifu chama kilichomdhamini ni hiyari yake na wala siyo kosa na haiathiri ukweli kuwa bunge limepewa taarifa ya kujiuzulu kwa spika na bunge lenyewe limekiri
Hivi unafahamu tofauti ya haya kwenye kutuma barua au mail yoyote?
To:
CC:

Kwenda kwa:
Nakala kwa:

Aliyewekwa kwenye TO (kwenda kwa), ndiye anayelengwa kushughurika na kilichoandikwa kwenye barua au taarifa husika. Huyu wa kwenye CC (Nakala kwa) ni kumpa taarifa tu
 
Yawezekana unajua kusoma na kuandika vizuri ila umekosa analytical thinking.

Kwa fikra zako, na kwa uelewa tu wa kawaida, hivi tuseme umeajiriwa na kampuni fulani, kabla ya kuajiriwa ulidhaminiwa na Baba yako, unaweza kujiuzulu kazi kwa kumwandikia barua baba yako, na anakala ukampelekea mwajiri wako?

Katiba ipo wazi, spika akitaka kujiuzulu anapeleka taarifa Bungeni, huko kwenye chama chake, hakuna mahali popote katiba imetamka. Unaacha kitu kilichotamkwa kikatiba, unaenda kufanya upuuzi halafu unasema katiba imefuatwa!
 
Kikubwa ni Bunge kupata taarifa ya kujiuzulu kwake.

Suala la kukitaarifu chama kilichomdhamini ni hiyari yake na wala siyo kosa na haiathiri ukweli kuwa bunge limepewa taarifa ya kujiuzulu kwa spika na bunge lenyewe limekiri
Mbatia ni mnufaika wa ubunge wa viti maalumu.
 
Kikubwa ni Bunge kupata taarifa ya kujiuzulu kwake.

Suala la kukitaarifu chama kilichomdhamini ni hiyari yake na wala siyo kosa na haiathiri ukweli kuwa bunge limepewa taarifa ya kujiuzulu kwa spika na bunge lenyewe limekiri
Tukisema vyuo vya Tanzania vinatoa Premature mnakasirika. Kwa akili yako Ndugai angeweza kupiga Simu tu ikawa taarifa?
 
Mbatia anatembelea matukio kutafuta kiki,
Katiba imekanyagwa mara nyingi sana huko nyuma,hakuwahi kujitokeza kufungua kesi,
Leo hii ameona Nini?

Acha upumbavu wewe!
Hivi kukanyagwa katiba huko nyuma na kama mtu hakufungua kesi ndio kunahalalisha katiba iendelee kukanyagwa, na kwamba akitokea mtu akifungua kesi iwe ni kutafuta kiki?
Wakati mwingine kuna mijitu inakuwa inawaza kwa kutumia makalio… na mfano mzuri ni wewe!
 
Yawezekana unajua kusoma na kuandika vizuri ila umekosa analytical thinking.

Kwa fikra zako, na kwa uelewa tu wa kawaida, hivi tuseme umeajiriwa na kampuni fulani, kabla ya kuajiriwa ulidhaminiwa na Baba yako, unaweza kujiuzulu kazi kwa kumwandikia barua baba yako, na anakala ukampelrkra mwajiri wako?

Katiba ipo wazi, spika akitaka kujiuzulu anapeleka taarifa Bungeni, huko kwenye chama chake, hakuna mahali popote katiba imetamka. Unaacha kitu kilichotamkwa kikatiba, unaenda kufanya upuuzi halafu unasema katiba imefuatwa!
huyu Madukwa Peter hajui aliongealo..!!!
 
Back
Top Bottom