Hapa tatizo si Ndugai bali tatizo ni ufinyu wenu wa kutumia terms za English.
Nilileta majuzi thread kuonyesha ufinyu wa kiingereza Bungeni wabunge waliporopoka na kusema kwamba Wenje katukana aliposema neno IMPOTENCY. Bonyeza thread hiyo
hapa.
Kumbe siku ile tunashangilia na kuwakemea wabunge kumbe baadhi yetu wengi humu JF hawajui terms hizi za English.
Ukiisoma ile thread utaona nilitumia Dictionary ifuatayo kumtetea Wenje kwamba hakutukana:{
Oxford Advanced Learner's Dictionary, Seventh Edition, ISBN: 9780194316613, pg.749}. Ukurasa huo limefafanuliwa vizuri neno IMPOTENCY.
Leo natumia dictinary hiyohiyo lakini ukurasa wa 1060. Neno "Parochial" limefafanuliwa kama ifuatavyo:
1: connected with church parish
2: (disapproving): only concerned with small issues that happen in your local area and not interested in more important things.
Hizi nido maana mbili za neno "Parochial". Hivyo, alivyolitumia Job Ndugai pamoja na kwamba simpendi kwa jinsi anavyonyanyasa wapinzani, yuko sahihi kwa sababu ametuma definition ya pili kama inavyofafanuliwa na hii dictionary.
Mimi ninaamini, Ndugai kwa kujua ama kutokujua amelitumia makusidu hilo neno akijua baadhi ya watanzania watakuja juu tena hasa katika kipindi hiki ambapo kuna utata wa udini.
Na kwa kufanya hivyo, kawanasa
wengi ambao English kwao ni mgogoro. Hii inathibitisha kwamba English ni janga la taifa.
Kama mnabisha kwamba English si janga la kitaifa, hebu angalia wana-JF wachache tu wafuatao walivyomkebehi Ndugai, bila kujijua ufinyu wa lugha walioutumbukia:
***********
Nieleweka na nadhani nimeeleweka. Simtetei Job Ndugai. Netetea English translation iliyotumika.
Cc:
Alfu Lela Ulela,
Dr. Ntinkuntina