Ndoa zina matukio jamani

Ndoa zina matukio jamani

Hata wenye pesa zao na wanatoka out kila siku wanayo matatizo mengi ya kutosha.

Yaani watu mkishaoana tu mnaanza kuwa maadui sijui tatizo nini.
Wa kwangu hajawahi kuwa adui sema mboga moja inakinai sana mkuu, papa moja inachosha sanaaa🤣
 
Inakuwa inachosha kwa sababu ya kukosa ubunifu mkuu, kama kweli unataka kuifurahia ndoa kuna namna nyingi za kufanya. Pesa iwepo ili ndoa isiwe karaha, mazingira yabadilishwe ili kuleta ladha mpya nk.

Japo kweli kuna kila haja ya kula wali nyama, then pilau na kuna wakati makande ni matamu kwa hamu.🤣🤣
Umeonaa sasa...pamoja na yoteee....sometimes tunahitaji Jambo jipyaa😂😂😂
 
Na wanaharamu watakuwa wengi sana kwa kufunika...siku wakijaa hao utalipuka Sana ...maajabu sasa unageuziwa kibao kwamba "kumbe mwenzangu Una Mambo moyoni husemi, sipendi kama unaumia si uniambie Mimi ni binadamu nakosea" kumbe anajua afanyalo ...huu ndo utapeli wa hisia, bwana dronedrake kaliona hili
Daah mkuu umeongea ukweli asee, hakuna watu wanaokwaza kama wanaosema hiyo kauli eti kumbe mwenzangu una mambo yako moyoni huyasemi, mara sijui una gubu na visirani

Yani mtu anajua kabisa anachokifanya anakukosea makusudi na anajua kabisa umekwazika, ila anataka upotezee tu kana kwamba wewe una moyo wa chuma vile na huwa wanatumia hiyo kauli kama defensive mechanism, kwamba yeye anayekukosea hana tatizo ila wewe unayeweka vitu moyoni ndio una tatizo

Na mara nyingi watu wa aina hiyo, ni wale ambao akikukosea hataki umchane ukweli kama amekukosea vinginevyo atachukia na kukuita mlalamishi, na atasema una gubu na visirani hivyo anataka ukaushe na umfurahie hata kama ni kinafiki tu
 
Tafuta mtu anajielewa kidogo amalize mambo kimyakimya🤣🤣
😂😂😂😂Kaka nimekuelewaa...kikubwaa nizingatiee neno"kimyakimya"..😂😂...huyu mwanaumee atanikata masikio
 
Ni kweli shida ni bwana harusi ambaye bado hajajitambua na hajielewi. We unamuona yuko sawa na timamu kiakili huyo?! Huoni kama binti kaolewa na Zwazwa?! 😀😀😀

Chagueni kwa makini, sio kila mwanaume ni chovyachovya... wachaneni na hawa vijana wa mjini wafuga ndevu na wachora tattoo... majority hawajielewi!
Halafu hilo group ndio linalo pendwa na linaongoza kwa kutengeneza single mother.

Yaani hilo group ulilo litaja na waume walio kwenye ndoa, wanaongoza kupendwa na dada zetu siku hizi na hawa shauriku mpaka wayakute.
 
Back
Top Bottom